2 Wafalme 8 – NEN & NRT

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

2 Wafalme 8:1-29

Ardhi Ya Mshunami Yarudishwa

18:1 2Fal 4:8-37; Kum 28:22Wakati huu, Elisha alikuwa amemwambia yule mwanamke ambaye mwanawe alikuwa amefufuliwa, “Ondoka wewe na jamaa yako ukaishi mahali popote unapoweza kwa kitambo kidogo, kwa sababu Bwana ameamuru njaa katika nchi hii ambayo itadumu kwa miaka saba.” 2Yule mwanamke akafanya kama vile yule mtu wa Mungu alivyosema. Yeye na jamaa yake wakaondoka na kwenda kuishi katika nchi ya Wafilisti kwa miaka saba.

3Baada ya miaka saba, yule mwanamke akarudi kutoka nchi ya Wafilisti, akaenda kwa mfalme kumsihi kwa ajili ya nyumba yake na shamba lake. 4Mfalme alikuwa anazungumza na Gehazi, mtumishi wa mtu wa Mungu, naye alikuwa amesema, “Hebu niambie mambo yote makuu yaliyofanywa na Elisha.” 58:5 2Fal 4:35Wakati Gehazi alipokuwa akimweleza mfalme jinsi Elisha alivyomfufua mtu, yule mwanamke ambaye mwanawe alikuwa amefufuliwa na Elisha akaja ili amsihi mfalme kwa ajili ya nyumba yake na shamba lake.

Gehazi akasema, “Huyu ndiye huyo mwanamke, bwana wangu mfalme, na huyu ndiye mwanawe ambaye Elisha alimfufua.” 6Mfalme akamuuliza yule mwanamke kuhusu mambo hayo, naye akamweleza.

Ndipo akaamuru afisa ashughulikie shauri lake na kumwambia, “Mrudishie huyu mwanamke kila kitu kilichokuwa mali yake, pamoja na mapato yote yaliyotokana na shamba lake tangu siku alipoondoka nchini hadi sasa.”

Hazaeli Anamuua Ben-Hadadi

78:7 2Sam 8:5; 2Fal 6:27Elisha akaenda Dameski, naye Ben-Hadadi mfalme wa Aramu alikuwa mgonjwa. Mfalme alipoambiwa, “Mtu wa Mungu ametoka mbali akapanda hadi hapa,” 88:8 1Fal 19:15; 1Sam 9:7mfalme akamwambia Hazaeli. “Chukua zawadi na uende kumlaki huyo mtu wa Mungu. Muulize Bwana kupitia yeye, kwamba, ‘Je, nitapona ugonjwa huu?’ ”

9Hazaeli akaenda kumlaki Elisha, akiwa amechukua zawadi ya kila kitu kizuri kilichopatikana Dameski, mizigo iliyobebwa na ngamia arobaini. Akaingia ndani na kusimama mbele yake, akasema, “Mwanao Ben-Hadadi mfalme wa Aramu amenituma niulize, ‘Je, nitapona ugonjwa huu?’ ”

10Elisha akajibu, “Nenda ukamwambie, ‘Hakika utapona’; lakini Bwana amenifunulia kwamba kweli atakufa.” 118:11 Lk 19:41; Amu 3:25Elisha akamkazia Hazaeli macho kwa nguvu mpaka akaona aibu. Kisha mtu wa Mungu akaanza kulia.

128:12 1Fal 19:17; 2Fal 15:16Hazaeli akauliza “Kwa nini bwana wangu analia?”

Elisha akajibu, “Kwa sababu najua mabaya utakayowatendea Waisraeli. Utachoma moto ngome zao, utawaua vijana wao kwa upanga, kuwatupa chini kwa nguvu watoto wachanga, na kuwatumbua wanawake wenye mimba.”

138:13 1Sam 17:43; 1Fal 19:15Hazaeli akasema, “Itawezekanaje mtumishi wako, aliye mbwa tu, kufanya tendo la ajabu namna hiyo?”

Elisha akamjibu, “Bwana amenionyesha kuwa utakuwa mfalme wa Aramu.”

14Kisha Hazaeli akamwacha Elisha na kumrudia bwana wake. Ben-Hadadi akamuuliza, “Elisha alikuambia nini?” Hazaeli akajibu, “Aliniambia kwamba hakika utapona.” 158:15 2Fal 1:17Lakini kesho yake Hazaeli akachukua nguo nzito, akailoweka ndani ya maji, akaitandaza juu ya uso wa mfalme, hivyo akafa. Kisha Hazaeli akaingia mahali pake kuwa mfalme wa Aramu.

Yehoramu Mfalme Wa Yuda

(2 Nyakati 21:1-20)

168:16 2Fal 1:17; 2Nya 21:1-4Katika mwaka wa tano wa Yoramu mwana wa Ahabu mfalme wa Israeli, wakati huo Yehoshafati akiwa mfalme wa Yuda, Yehoramu mwana wa Yehoshafati akaanza kutawala kama mfalme wa Yuda. 17Alikuwa na umri wa miaka thelathini na miwili alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu kwa miaka minane. 18Akaenenda katika njia za wafalme wa Israeli, kama nyumba ya Ahabu ilivyokuwa imefanya, kwa kuwa alimwoa binti wa Ahabu. Akatenda maovu machoni pa Bwana. 198:19 2Sam 21:17Hata hivyo, kwa ajili ya Daudi mtumishi wake, Bwana hakutaka kuiangamiza Yuda. Alikuwa ameahidi kuidumisha taa kwa ajili ya Daudi na wazao wake milele.

208:20 1Fal 22:47Wakati wa Yehoramu, Edomu waliasi dhidi ya Yuda na kujiwekea mfalme wao wenyewe. 21Basi Yehoramu akaenda Sairi pamoja na magari yake yote ya vita. Waedomu wakamzunguka yeye na majemadari wake wa magari yake ya vita, lakini akaondoka, akapenya usiku na kuwashambulia Waedomu. Hata hivyo, jeshi lake likatorokea nyumbani mwao. 228:22 Mwa 27:40; Yos 21:13Hadi leo Edomu wameasi dhidi ya Yuda. Libna pia wakaasi wakati huo huo.

23Kwa matukio mengine ya utawala wa Yehoramu na yote aliyoyafanya, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Yuda? 24Yehoramu akalala pamoja na baba zake, na akazikwa pamoja nao katika Mji wa Daudi. Naye Ahazia mwanawe akawa mfalme baada yake.

Ahazia Mfalme Wa Yuda

(2 Nyakati 22:1-6)

258:25 2Fal 9:29Katika mwaka wa kumi na mbili wa utawala wa Yoramu mwana wa Ahabu mfalme wa Israeli, Ahazia mwana wa Yehoramu mfalme wa Yuda alianza kutawala. 268:26 2Fal 8:18; 1Fal 16:23Ahazia alikuwa na umri wa miaka ishirini na miwili alipoanza kutawala, naye akatawala katika Yerusalemu kwa mwaka mmoja. Mama yake aliitwa Athalia, mjukuu wa Omri mfalme wa Israeli. 278:27 1Fal 16:30; 15:26Akaenenda katika njia za nyumba ya Ahabu, na kutenda maovu machoni pa Bwana, kama nyumba ya Ahabu ilivyokuwa imefanya, kwa kuwa alikuwa ameoa kutoka nyumba ya Ahabu.

288:28 Kum 4:43; 2Fal 9:1, 14Ahazia akaenda vitani na Yoramu mwana wa Ahabu kupigana na Hazaeli mfalme wa Aramu huko Ramoth-Gileadi. Waaramu wakamjeruhi Yoramu. 298:29 1Fal 21:29; 2Fal 10:13Hivyo Mfalme Yoramu akarudi Yezreeli ili apate kuuguza majeraha aliyojeruhiwa na Waaramu huko Ramothi8:29 Yaani Rama kwa Kiebrania. alipopigana na Hazaeli mfalme wa Aramu.

Ndipo Ahazia mwana wa Yehoramu mfalme wa Yuda akashuka kwenda Yezreeli kumtazama Yoramu mwana wa Ahabu, kwa sababu alikuwa amejeruhiwa.

New Russian Translation

4 Царств 8:1-29

Возвращение земли шунамитянки

1Елисей сказал женщине, сына которой он воскресил:

– Уходи с семьей и поселись, где сможешь, потому что Господь навел на страну голод, который будет длиться семь лет.

2Женщина собралась и сделала, как сказал Божий человек. Вместе с семьей она ушла и семь лет жила в земле филистимлян.

3Через семь лет она вернулась из земли филистимлян и пошла к царю просить о своем доме и земле. 4А царь в то время беседовал с Гиезием, слугой Божьего человека, и сказал:

– Расскажи мне о великих делах, которые совершил Елисей.

5Как раз, когда Гиезий рассказывал царю о том, как Елисей воскресил мертвого, женщина, чьего сына Елисей воскресил, пришла просить царя о своем доме и земле. Гиезий сказал:

– Вот это и есть та женщина, господин мой царь, а это ее сын, которого воскресил Елисей.

6Царь расспросил женщину, и она рассказала ему. Тогда он назначил чиновника рассмотреть ее дело, сказав ему:

– Верни ей все, что у нее было, а также все доходы от ее земли, что были получены с того дня, как она покинула страну, до этого дня.

Предсказание Елисея об убийстве Венадада

7Елисей пришел в Дамаск, когда Венадад, царь Арама, был болен. Когда царю доложили: «Сюда пришел Божий человек», 8– он сказал Хазаилу:

– Возьми с собой подарок и иди встречать Божьего человека. Спроси через него Господа, сказав: «Выздоровею ли я от этой болезни?»

9Хазаил пошел встречать Елисея, взяв с собой в дар лучших товаров Дамаска на сорок верблюжьих поклаж. Он пришел, встал перед ним и сказал:

– Твой сын Венадад, царь Арама, послал меня спросить: «Выздоровею ли я от этой болезни?»

10Елисей сказал:

– Иди и скажи ему: «Ты обязательно выздоровеешь», но Господь открыл мне, что на самом деле он умрет.

11Елисей смотрел на него не отрываясь, пока Хазаил не смутился. Тогда Божий человек заплакал.

12– Почему мой господин плачет? – спросил Хазаил.

– Потому что я знаю, какое зло ты причинишь израильтянам, – ответил он. – Ты сожжешь их крепости, юношей их убьешь мечом, разобьешь их младенцев о землю и порубишь их беременных женщин.

13Хазаил сказал:

– Как твой слуга, который лишь пес, сможет совершить такое большое дело?

– Господь открыл мне, что ты станешь царем Арама, – ответил Елисей8:13 Здесь Елисей произносит пророчество, которое ранее было открыто Богом Илии (см. 3 Цар. 19:15-17)..

14Тогда Хазаил ушел от Елисея и вернулся к своему господину.

Венадад спросил:

– Что сказал тебе Елисей?

Хазаил ответил:

– Он сказал мне, что ты непременно выздоровеешь.

15Но на другой день он взял одеяло, намочил его водой, накрыл им лицо царя, и тот умер. А Хазаил стал царем вместо него.

Иорам – царь Иудеи

(2 Пар. 21:5-10, 20)

16На пятом году правления израильского царя Иорама, сына Ахава, когда Иосафат еще был царем Иудеи, в Иудее начал царствовать Иорам, сын Иосафата. 17Ему было тридцать два года, когда он стал царем, и правил он в Иерусалиме восемь лет. 18Он ходил путем царей Израиля, по примеру дома Ахава, потому что женился на дочери Ахава. Он делал зло в глазах Господа. 19Но ради Своего слуги Давида Господь не хотел погубить Иудею. Он обещал сохранить светильник ему и его потомкам навеки.

20Во времена Иорама Эдом восстал против правления Иудеи и поставил себе царя. 21Тогда Иорам пошел в Цаир со всеми своими колесницами. Ночью он приготовился и напал на эдомитян и на начальников их колесниц, которые окружили его, но его войско бежало домой. 22И до сих пор Эдом не покорен правлению Иудеи. Ливна восстала в то же самое время.

23Что же до прочих событий правления Иорама и его дел, то разве не записаны они в «Книге летописей царей Иудеи»? 24Иорам упокоился со своими предками и был похоронен с ними в Городе Давида. Охозия, его сын, стал царем вместо него.

Охозия – царь Иудеи

(2 Пар. 22:1-6)

25На двенадцатом году правления израильского царя Иорама, сына Ахава, над Иудеей начал царствовать Охозия, сын Иорама. 26Охозии было двадцать два года когда он стал царем, и правил он в Иерусалиме один год. Его мать звали Аталия; она была внучкой Омри, царя Израиля. 27Он ходил путем дома Ахава и делал зло в глазах Господа, по примеру дома Ахава8:27 Аталия, мать Охозии, была дочерью Ахава (см. ст. 18)., ведь он породнился с домом Ахава через брак.

28Охозия ходил с Иорамом, сыном Ахава, воевать против Хазаила, царя Арама, под Рамот Галаадский. Арамеи ранили Иорама, 29и царь Иорам вернулся в Изреель, чтобы оправиться от ран, которые ему нанесли при Рамоте8:29 Евр.: «Рама», вариант названия Рамот., когда он сражался с Хазаилом, царем Арама.

Охозия, сын Иорама, царя Иудеи, отправился в Изреель навестить Иорама, сына Ахава, потому что тот был ранен.