2 Nyakati 32 – NEN & BPH

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

2 Nyakati 32:1-33

Senakeribu Aitishia Yerusalemu

(2 Wafalme 18:13-37; 19:14-19, 35-37; Isaya 36:1-22; 37:8-38)

132:1 2Fal 18:13-19; Isa 37:9Baada ya yale yote aliyokuwa amefanya Hezekia kwa uaminifu mkubwa, Senakeribu mfalme wa Ashuru akaja na kuvamia Yuda. Akaizunguka miji yenye ngome kwa jeshi, akifikiri kuiteka iwe yake. 232:2 Isa 22:7; Yer 1:15Hezekia alipoona kuwa Senakeribu amekuja na kwamba alikusudia kufanya vita juu ya Yerusalemu, 3akafanya shauri na maafisa wake na mashujaa wake juu ya kuzuia maji kutoka chemchemi zilizo nje ya mji, nao wakamsaidia. 432:4 2Fal 20:20; Nah 3:14Umati mkubwa wa watu ukakusanyika na kuzuia chemchemi zote na vijito vilivyotiririka katika nchi yote, wakisema: “Kwa nini wafalme wa Ashuru waje na kukuta maji tele?” 532:5 2Nya 25:23; Isa 22:9-10; 1Fal 9:24; 2Sam 5:9; 1Nya 11:8Hezekia akafanya kazi kwa bidii kukarabati sehemu zote zilizokuwa zimebomoka za ukuta na kujenga minara juu yake. Akajenga ukuta mwingine nje ya ule uliokuwepo na kuimarisha Milo32:5 Milo maana yake Boma la Ngome. katika Mji wa Daudi. Akatengeneza pia silaha nyingi na ngao.

632:6 2Nya 30:22; Isa 40:2Akaweka maafisa wa jeshi juu ya watu, wakawakutanisha mbele yake katika uwanja kwenye lango la mji, naye akawatia moyo kwa maneno haya: 732:7 Kum 31:6; 1Nya 22:13; 28:10; 2Nya 20:15; Hes 14:9; 2Fal 6:16; Za 55:18“Kuweni hodari na wenye moyo mkuu. Msiogope, msifadhaike wala msikate tamaa kwa sababu ya mfalme wa Ashuru na hili jeshi kubwa lililo pamoja naye, kwa kuwa aliye pamoja nasi ni mkuu kuliko aliye pamoja naye. 832:8 Ay 40:9; Isa 41:10-14; 52:10; 1Sam 17:45; 2Nya 13:12; 1Nya 5:22; Rum 8:31; Yer 17:5; 1Yn 4:4; Kum 20:1-4; 31:6-8; Mit 18:10; Amo 5:14Kwake uko mkono wa mwili tu, bali kwetu yuko Bwana Mungu wetu kutusaidia na kutupigania vita vyetu.” Nao watu wakatiwa moyo kutokana na maneno aliyowaambia Hezekia mfalme wa Yuda.

932:9 2Fal 18:17; Yos 10:3Hatimaye Senakeribu mfalme wa Ashuru na majeshi yake yote walipokuwa wameuzunguka Lakishi, akawatuma maafisa wake kwenda Yerusalemu wakiwa na ujumbe huu kwa Hezekia mfalme wa Yuda, na kwa watu wote wa Yuda waliokuwako humo, kusema:

1032:10 Eze 29:16“Hili ndilo asemalo Senakeribu mfalme wa Ashuru: Je, mmeweka tumaini lenu wapi, hata mnaendelea kukaa katika Yerusalemu, hali mmezungukwa na jeshi? 1132:11 Isa 37:10Hezekia asemapo, ‘Bwana Mungu wetu atatuokoa kutokana na mkono wa mfalme wa Ashuru,’ anawapotosha ninyi, naye atawaacha mfe kwa njaa na kiu. 12Je, si Hezekia mwenyewe aliyeondoa mahali pa juu pa kuabudia miungu pamoja na madhabahu zake, akiwaambia Yuda wa Yerusalemu, ‘Ni lazima mwabudu mbele ya madhabahu moja na kuteketeza dhabihu juu yake’?

1332:13 2Fal 18:33-35; Za 115:4-8“Je, hamjui yale mimi na baba zangu tuliyoyafanya kwa mataifa yote ya nchi zingine? Je, miungu ya mataifa hayo iliweza kuokoa nchi zao kutoka mkononi mwangu? 14Ni yupi miongoni mwa miungu yote ya mataifa haya ambayo baba zangu waliyaangamiza ameweza kuwaokoa watu wake mkononi mwangu? Inawezekanaje basi Mungu wenu kuwaokoa mkononi mwangu? 1532:15 Isa 37:10; Dan 3:15; Kut 5:2; Yn 19:10-11Sasa basi, msikubali Hezekia awadanganye na kuwapotosha namna hii. Msimwamini, kwa kuwa hakuna mungu wa taifa lolote wala wa ufalme wowote aliyeweza kuwaokoa watu wake kutoka mkononi mwangu au mkononi mwa baba zangu. Sembuse huyo mungu wenu atawaokoaje kutoka mkononi mwangu!”

16Maafisa wa Senakeribu wakaendelea kunena dhidi ya Bwana aliye Mungu na dhidi ya mtumishi wake Hezekia. 1732:17 Isa 37:14; Za 74:22; 2Fal 19:12Mfalme pia aliandika barua akimtukana Bwana, Mungu wa Israeli na kusema haya dhidi yake: “Kama vile miungu ya mataifa ya nchi nyingine ilivyoshindwa kuwaokoa watu wao mkononi mwangu, vivyo hivyo Mungu wa Hezekia hataweza kuwaokoa watu wake kutoka mkononi mwangu.” 1832:18 2Fal 18:28Kisha wakawaita kwa Kiebrania watu wa Yerusalemu waliokuwa juu ya ukuta ili kuwatisha na kuwatia hofu ili waweze kuuteka mji. 1932:19 Za 115:4; Yer 1:16; Za 135:15-18; Isa 10:10; Kum 4:28; 2Fal 19:18; Yer 10:3; Hos 8:5-6Wakanena juu ya Mungu wa Yerusalemu kama vile walivyonena juu ya miungu ya mataifa mengine ya dunia ambayo ni kazi ya mikono ya wanadamu.

20Mfalme Hezekia na nabii Isaya mwana wa Amozi wakalilia mbingu katika maombi kuhusu jambo hili. 2132:21 Mwa 19:13; Isa 37:38; Yer 41:2Naye Bwana akamtuma malaika ambaye aliangamiza wanajeshi wote, na viongozi na maafisa katika kambi ya mfalme wa Ashuru. Kwa hiyo, mfalme wa Ashuru akarudi nchini mwake kwa aibu. Naye alipokwenda katika hekalu la mungu wake, baadhi ya watoto wake wakamuua kwa upanga.

2232:22 Za 18:48-50; Isa 31:5Hivyo Bwana akamwokoa Hezekia na watu wa Yerusalemu kutoka mkononi mwa Senakeribu mfalme wa Ashuru na kutoka mikononi mwa wengine wote. Bwana akawastarehesha kila upande. 2332:23 1Sam 10:27; Za 76:11; 1Nya 29:25; 2Nya 17:5Watu wengi wakaleta sadaka Yerusalemu kwa ajili ya Bwana na zawadi za thamani kwa ajili ya Hezekia mfalme wa Yuda. Tangu hapo na kuendelea, Hezekia aliheshimiwa sana na mataifa yote.

Kiburi Cha Hezekia, Mafanikio Na Kifo

(2 Wafalme 20:1-3, 12-19; Isaya 38:1-3; 39:1-8)

2432:24 Isa 38:1Katika siku hizo, Hezekia akaugua, naye akawa karibu kufa. Akamwomba Bwana, ambaye alimjibu na kumpa ishara. 2532:25 2Fal 14:10; Kum 32:6; 2Nya 26:16; 19:2; 24:18; Kum 8:12; Za 116:12; Lk 17:17; 2Fal 14:10; Hab 2:4; 1Tim 3:6; 1Pet 5:5-6Lakini moyo wa Hezekia ukajaa majivuno na hakuonyesha itikio kwa wema aliotendewa, kwa hiyo ghadhabu ya Bwana ikawa juu yake na juu ya Yuda na Yerusalemu. 2632:26 Yer 26:18-19; 2Nya 34:27-28; 2Fal 19:20; Isa 39:8Ndipo Hezekia akatubu kwa ajili ya kiburi cha moyo wake, kama walivyofanya watu wa Yerusalemu, kwa hiyo ghadhabu ya Bwana haikuja juu yao katika siku za Hezekia.

2732:27 1Nya 29:12; 2Nya 9:24Hezekia alikuwa na utajiri mwingi sana na heshima, naye akajifanyia hazina kwa ajili ya fedha yake na dhahabu na kwa ajili ya vito vyake vya thamani, vikolezi, ngao na aina zote za vyombo vya thamani. 28Akajenga pia maghala ya kuhifadhi mavuno ya nafaka, divai mpya na mafuta. Akatengeneza mabanda kwa ajili ya aina mbalimbali za mifugo, na mazizi kwa ajili ya kondoo na mbuzi. 2932:29 2Nya 29:12Akajenga vijiji na kujipatia idadi kubwa ya kondoo na mbuzi, pamoja na ngʼombe kwa kuwa Mungu alikuwa amempa utajiri mwingi sana.

3032:30 2Fal 18:17; 1Fal 1:33; Isa 22:9Ilikuwa ni Hezekia aliyeziba njia za kutolea maji za chemchemi za juu za Gihoni na kuyaelekeza maji kutiririkia upande wa magharibi wa Mji wa Daudi. Akafanikiwa katika kila kitu alichofanya. 3132:31 Isa 13:1; 39:1; 38:7; Kum 8:16; Mwa 22:1; Yn 1:12Lakini wakati wajumbe walipotumwa na watawala wa Babeli kumuuliza juu ya ishara ambayo ilitokea katika nchi, Mungu alimwacha ili kumjaribu na kujua kila kitu kilichokuwa moyoni mwake.

3232:32 Isa 36:1; 2Fal 18:1Matukio mengine ya utawala wa Hezekia na matendo yake ya kujitoa kwa moyo yameandikwa katika maono ya nabii Isaya mwana wa Amozi kwenye kitabu cha wafalme wa Yuda na Israeli. 3332:33 1Sam 2:30; Mit 10:7Hezekia akalala na baba zake na akazikwa kwenye kilima mahali yalipo makaburi ya wazao wa Daudi. Yuda wote na watu wa Yerusalemu wakamheshimu alipofariki. Naye Manase mwanawe akawa mfalme baada yake.

Bibelen på hverdagsdansk

2. Krønikebog 32:1-33

Kong Sankeribs trussel imod Jerusalem

2.Kong. 18,13–19,37

1Kong Hizkija havde således vist sin trofasthed over for Herren, men ikke så længe efter invaderede kong Sankerib af Assyrien Juda og belejrede de befæstede byer i den hensigt at indtage dem. 2Da Hizkija blev klar over, at Sankerib snart ville belejre Jerusalem, 3-4besluttede han i samråd med sine embedsmænd og officerer at tildække kilderne uden for byen, så assyrerne var afskåret fra at få vand under belejringen. Lederne gik derfor i spidsen for en stor styrke ud til kilderne og dækkede dem til, så man ikke kunne få vand derfra. 5Samtidig styrkede Hizkija sit forsvar ved at reparere bymuren, udbygge forsvarstårnene og styrke den ydre mur. Desuden udbyggede han byens store fæstningsanlæg i Davidsbyen og fremstillede en stor mængde spyd og skjolde. 6Han udnævnte en række officerer og samlede dem på den åbne plads ved byporten. Her opmuntrede han dem med følgende tale:

7„Vær ved godt mod! Lad jer ikke skræmme af assyrerkongen og hans store hær! Vi har en med os, som er langt mægtigere end ham. 8Assyrerkongen har kun militær styrke, men vi har Herren på vores side, og han vil udkæmpe slaget for os.” Det opmuntrede dem at høre.

9I mellemtiden var assyrerkongen i færd med at belejre byen Lakish. Derfra sendte han følgende budskab til kong Hizkija og Jerusalems indbyggere:

10„Kong Sankerib af Assyrien siger: Hvad får jer til at tro, at I kan modstå en belejring fra min hær? 11Hizkija vildleder jer når han siger: ‚Herren, vores Gud, vil redde os fra assyrerkongen.’ Nej, det ender bare med, at I alle dør af sult og tørst! 12Husk dog på, hvordan Hizkija ødelagde jeres guds altre og offersteder rundt omkring i landet og forlangte, at man kun måtte bringe ofre på ét alter i Jerusalem. 13Ved I ikke, hvad jeg og mine forgængere på tronen gjorde ved alle de andre folkeslag? Var nogen af deres guder i stand til at redde dem? 14Skulle jeres gud virkelig være mægtigere end alle de andre folks guder? 15Lad ikke Hizkija føre jer bag lyset. Lad være at høre på ham. Ingen gud har nogensinde formået at redde et folk, der blev angrebet af en assyrisk konge. Hvordan kan I da tro, at jeres gud kan gøre det?”

16De assyriske sendebud fortsatte med at håne Herren og hans tjener Hizkija. 17Assyrerkongen havde også skrevet et smædebrev imod Herren, Israels Gud. Det lød:

„Aldrig har nogen gud formået at redde sit folk fra min magt, og det vil heller ikke lykkes for Hizkijas Gud!”

18Sendebudene læste brevets indhold op på hebraisk i den hensigt at skræmme folket, der var samlet på bymuren, 19og de fortsatte med at håne Jerusalems Gud, som om han var en gud på lige fod med de andre folks menneskeskabte guder.

20Da råbte kong Hizkija og profeten Esajas, Amotz’ søn, til Himlens Gud om hjælp. 21Og Herren sendte en engel, der slog alle de assyriske soldater og officerer ihjel! Kong Sankerib måtte skamfuldt tage tilbage til sit land, og da han gik ind i sin guds tempel, blev han hugget ned af sine egne sønner. 22Sådan frelste Herren kong Hizkija og Jerusalems indbyggere fra assyrerkongen og deres øvrige fjender, så der fra den tid var fred til alle sider. 23Kong Hizkija blev fra da af frygtet og æret blandt de omkringboende folk, der valfartede til Jerusalem med ofre til Herren og med kostbare gaver til kongen.

Kong Hizkijas sygdom, hovmod og død

2.Kong. 20,1-21

24Senere blev Hizkija alvorligt syg og lå for døden. Da bad han til Herren, og Herren besvarede hans bøn og gjorde et mirakel for ham. 25Hizkija var dog ikke taknemmelig, men blev i stedet hovmodig. Derfor ville Herren straffe både kongen, Juda og Jerusalem, 26men kongen angrede sit hovmod. Både han og byens indbyggere ydmygede sig for Herren, og derfor udskød Herren sin straf, indtil efter Hizkija døde.

27Hizkija var en vellidt konge. Han blev så rig, at han måtte bygge skatkamre til alt sit sølv og guld, til sine ædelsten, sine sjældne krydderier og skjolde og andre kostbarheder. 28-29Han byggede forrådshuse til sit korn, sin vin og olivenolie, stalde til sine store kvægflokke og folde til sine utallige får og geder. Han byggede mange byer, for Gud gjorde ham overmåde rig. 30Han dæmmede op for Gihons øvre kilde og førte en vandledning ned vest for Davidsbyen. Alt, hvad han foretog sig, lykkedes for ham.

31Men da der kom sendebud fra Babylonien for at høre mere om det mirakel, der var sket, trak Gud sig tilbage fra ham for at prøve ham og se, hvad der gemte sig i hans hjerte.

32Resten af kong Hizkijas bedrifter og hans trofasthed over for Herren er beskrevet i profeten Esajas’ bog og i Judas og Israels kongers krønikebog. 33Da Hizkija døde, blev han begravet tæt ved vejen op til det kongelige gravsted, og hele Juda og Jerusalem ærede hans minde. Hans søn Manasse overtog tronen efter ham.