2 Nyakati 31 – NEN & BPH

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

2 Nyakati 31:1-21

Sehemu Za Ibada Za Kipagani Zaondolewa

131:1 2Fal 18:4; Isa 36:7; 2Nya 13:14Baada ya mambo haya yote kumalizika, Waisraeli ambao walikuwako huko wakaenda kwenye miji ya Yuda, wakayavunja yale mawe ya kuabudia na kuzikatakata zile nguzo za Ashera. Wakabomoa mahali pa juu pa kuabudia miungu pamoja na madhabahu zake kila mahali katika Yuda na Benyamini na katika Efraimu na Manase. Baada ya kuviharibu hivi vyote, Waisraeli wakarudi katika miji yao wenyewe na kwenye milki zao.

231:2 2Nya 29:9; Za 71:22; 1Nya 23:28-32; 15:2Hezekia akawapanga makuhani na Walawi katika migawanyo, kila mgawanyo kulingana na wajibu wao, kama ni makuhani au Walawi, ili kutoa sadaka za kuteketezwa na sadaka za amani, kuhudumu, kushukuru na kuimba sifa katika malango ya makao ya Bwana. 331:3 1Nya 29:3; Eze 45:17; Hes 28:1; 29:40Mfalme akatoa matoleo kutoka mali zake mwenyewe kwa ajili ya sadaka za kuteketezwa za asubuhi na za jioni na sadaka za kuteketezwa kwa siku za Sabato, kwa Sikukuu za Mwezi Mwandamo na kwa ajili ya sikukuu zilizoamriwa kama ilivyoandikwa katika Sheria ya Bwana. 431:4 Neh 13:10-12; Mal 2:7; 1Kor 9:13; Hes 18:8Akawaagiza watu wanaoishi Yerusalemu watoe sehemu iliyo haki ya makuhani na Walawi ili waweze kujitoa kikamilifu kutimiza wajibu wao katika Sheria ya Bwana. 531:5 Neh 13:12; Eze 44:30; Kum 12:17; 1Kor 15:20; Kut 22:29; 23:19; Hes 18:12; Eze 20:40; Yak 1:18; Mit 3:9Mara tu baada ya kutolewa tangazo hilo, Waisraeli wakatoa kwa ukarimu malimbuko ya nafaka zao, divai mpya, mafuta na asali pamoja na vyote vilivyotoka mashambani. Wakaleta kiasi kikubwa cha fungu la kumi la kila kitu. 631:6 Law 27:30; Neh 13:10-12; Kum 14:28; Rut 3:7Watu wa Israeli na Yuda walioishi katika miji ya Yuda wakaleta pia fungu la kumi la makundi yao ya ngʼombe na makundi ya kondoo na mbuzi pia na fungu la kumi la vitu vitakatifu vilivyowekwa wakfu kwa ajili ya Bwana Mungu wao na kuvikusanya katika malundo. 731:7 Kut 23:16Wakaanza kufanya haya katika mwezi wa tatu na kumaliza katika mwezi wa saba. 831:8 Za 144:13-15; Mwa 14:19; 2Sam 6:18; Kum 33:29; 1Fal 8:55-56; 2Nya 6:3; Za 33:12; 144:15Wakati Hezekia na maafisa wake walipokuja na kuona yale malundo, wakamsifu Bwana na kuwabariki watu wake Israeli.

9Hezekia akawauliza makuhani na Walawi kuhusu yale malundo, 1031:10 2Sam 8:17; Kut 36:5; Hag 2:19; Mal 3:10-12naye Azaria aliyekuwa kuhani mkuu, kutoka jamaa ya Sadoki, akajibu, “Tangu watu walipoanza kuleta sadaka zao katika Hekalu la Bwana tumekuwa na chakula cha kutosha na vingi vya kuweka akiba kwa sababu Bwana amewabariki watu wake, hivyo tumekuwa na kiasi kingi kilichobaki.”

Kutambuliwa Kwa Makuhani Na Walawi

11Hezekia akatoa agizo la kutengeneza vyumba vya ghala katika Hekalu la Bwana nalo hili likafanyika. 1231:12 2Nya 35:9; Neh 13:13Kisha kwa uaminifu wakaleta sadaka zao, mafungu yao ya kumi na vitu vilivyowekwa wakfu. Konania Mlawi, ndiye alikuwa msimamizi wa vitu hivi na Shimei ndugu yake ndiye alikuwa msaidizi wake. 13Yehieli, Azazia, Nahathi, Asaheli, Yeremothi, Yozabadi, Elieli, Ismakia, Mahathi na Benaya walikuwa waangalizi chini ya Konania na Shimei ndugu yake, waliokuwa wamewekwa na Mfalme Hezekia na Azaria, afisa msimamizi wa Hekalu la Mungu.

14Kore mwana wa Imna, Mlawi, bawabu wa Lango la Mashariki, alikuwa msimamizi wa sadaka za hiari zilizotolewa kwa Mungu, akiyagawanya hayo matoleo yaliyotolewa kwa Bwana na pia zile sadaka zilizowekwa wakfu. 1531:15 2Nya 29:12; Yos 21:9-19Edeni, Miniamini, Yeshua, Shemaya, Amaria na Shekania walimsaidia kwa uaminifu katika miji ya makuhani, wakiwagawia makuhani wenzao kufuatana na migawanyo yao, wazee kwa vijana sawasawa.

1631:16 1Nya 23:3; Ezr 3:4Zaidi ya hao wakawagawia wanaume wenye umri wa miaka mitatu au zaidi ambao majina yao yalikuwa kwenye orodha ya vizazi, wale wote ambao wangeingia katika Hekalu la Bwana ili kufanya kazi zao mbalimbali za kila siku kulingana na wajibu katika mgawanyo wao. 1731:17 1Nya 23:24, 27Kuandikishwa kwa makuhani kulikuwa kwa kufuata chimbuko la nyumba za baba zao na Walawi kuanzia umri wa miaka ishirini au zaidi ilikuwa kufuatana na huduma zao, kwa migawanyo yao. 18Makuhani waliandikishwa pamoja na watoto wao wadogo, wake zao, watoto wao wa kiume na wa kike, jamii yote iliandikishwa kwa kufuata orodha ya vizazi vyao. Kwa kuwa walikuwa waaminifu katika kujitakasa.

1931:19 Law 25:34; 2Nya 31:12-15; Hes 35:2Kuhusu makuhani, wazao wa Aroni walioishi kwenye mashamba yaliyozunguka miji yao au katika miji mingine yoyote, watu walitajwa majina ili kumgawia kila mwanaume miongoni mwao na kwa wote waliokuwa katika orodha ya vizazi vya Walawi.

2031:20 2Fal 20:3; 22:2; 1The 2:10; 1Fal 15:5; Yn 1:47Hivi ndivyo Hezekia alivyofanya katika Yuda yote, akifanya lile lililo jema, sawa na la uaminifu mbele za Bwana Mungu wake. 2131:21 Kum 29:9; Mit 3:9; Yos 4:7; Mal 3:10; 1Tim 4:8Naye katika kila kitu alichofanya katika huduma kwenye Hekalu la Mungu na katika utii kwa sheria na amri, alimtafuta Mungu wake na kufanya kazi kwa moyo wake wote. Naye hivyo akafanikiwa.

Bibelen på hverdagsdansk

2. Krønikebog 31:1-21

Kong Hizkija tjente Herren af hele sit hjerte

1Da festen var forbi, var der en stor gruppe af de israelitter, som var kommet til Jerusalem, der gik ud for at gøre op med afgudsdyrkelsen. De tog rundt til alle byerne i Juda, Benjamin, Efraim og Manasse, hvor de fjernede alle afgudsaltrene, huggede Asherapælene om og nedrev afgudsofferhøjene. Først derefter gik de hjem til deres egne byer.

2Kong Hizkija inddelte nu præsterne og levitterne i skiftehold, så de til stadighed kunne ofre brændofre og takofre og forestå tilbedelsen og lovsangen ved templets indgang. 3Kongen skænkede selv offerdyrene til de daglige morgen- og aftenbrændofre, samt de dyr, der ifølge Toraen skulle bruges til sabbatshøjtiden, nymånefesten og de store årlige festhøjtider.

4Desuden befalede han, at indbyggerne i Jerusalem skulle bringe præsterne og levitterne de gaver, som ifølge Toraen tilfaldt dem, så de ikke var nødt til at arbejde, men kunne hellige sig deres foreskrevne opgaver ved templet. 5-6Folket reagerede øjeblikkeligt ved villigt at bringe en del af deres høst, det være sig korn, vin, olivenolie, honning eller andre af jordens afgrøder. De gav Herren en tiendedel af alt, hvad de ejede, og lagde det i store bunker. De israelitter, som var flyttet ned til Juda, og de indfødte judæere bragte desuden en tiendedel af deres kvæg og får, og hvad de ellers ønskede at give til Herren. 7De første gaver kom i den tredje måned, og de sidste gaver kom i den syvende måned. 8Da kong Hizkija og hans embedsmænd så de store bunker af gaver, blev de fyldt med taknemmelighed til Herren og hans folk, Israel.

9Hizkija forhørte sig nærmere hos præsterne og levitterne om bunkerne. 10Ypperstepræsten Azarja af Zadoks slægt forklarede sagen: „Lige siden folket begyndte at bringe deres gaver til tempeltjenesten, har vi haft rigeligt at spise, og alt det her er i overskud. Herren har virkelig velsignet sit folk.”

11Kongen gav nu ordre til at indrette forrådskamre i templet, 12-13hvorefter alle gaverne blev opmagasineret der. Levitten Konanja fik på kongens og ypperstepræstens foranledning opsyn med forrådet, og hans bror Shimi fik sammen med følgende mænd til opgave at hjælpe ham: Jehiel, Azazja, Nahat, Asael, Jerimot, Jozabad, Eliel, Jismakja, Mahat og Benaja.

14-15Levitten Kore, søn af Jimna, der var dørvagt ved østporten, fik til opgave at fordele de gaver, der tilfaldt præsterne. De skulle bringes ud til alle de byer, hvor der boede præster, og Kore fik hjælp af følgende pålidelige mænd: Eden, Minjamin, Jeshua, Shemaja, Amarja og Shekanja. De fordelte gaverne ligeligt mellem præsterne, gamle såvel som unge, 16i henhold til alle de mandlige medlemmer af familien fra tre år og opefter, uanset om alle var optaget i slægtsfortegnelsen. Alle præsterne fik del i gaverne, for så vidt de tilhørte et skiftehold og jævnligt arbejdede i templet. 17Præsterne var opført på listen efter deres slægtsnavn, mens alle levitter over 20 år var opført efter, hvilket skiftehold de tilhørte. 18For de præster, der brugte al deres tid i tempeltjenesten, blev alle familiens medlemmer regnet med ved udregningen af en fødevareration, inklusive småbørn, koner, sønner og døtre. 19De præster og levitter, som boede uden for byerne, fik deres ration udleveret i overensstemmelse med de officielle lister af nogle folk i byerne, som fik overdraget den opgave.31,16-19 Teksten i dette afsnit er uklar.

20Således fordelte kong Hizkija gaverne retfærdigt ud over landet, og han gjorde, hvad der var ret og rigtigt i Herrens øjne. 21Han søgte helhjertet at gøre Herrens vilje i alt, hvad han tog sig for, hvad enten det havde med tempeltjenesten eller Toraen og dens befalinger at gøre. Derfor fik han stor fremgang.