1 Yohana 3 – NEN & NIRV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

1 Yohana 3:1-24

13:1 Yn 3:16; 15:21Tazameni ni pendo kuu namna gani alilotupa Baba, kwamba sisi tuitwe wana wa Mungu! Na ndivyo tulivyo. Kwa sababu hii ulimwengu haututambui, kwa kuwa haukumtambua yeye. 23:2 Rum 8:29; 2Pet 1:4; Za 17:15Wapendwa, sasa tu wana wa Mungu, lakini bado haijadhihirika tutakavyokuwa, lakini twajua ya kwamba yeye atakapodhihirishwa, tutafanana naye, kwa maana tutamwona kama alivyo. 33:3 2Kor 7:1; 2Pet 3:13, 14Kila mmoja mwenye matumaini haya ndani yake hujitakasa, kama vile yeye alivyo mtakatifu.

43:4 1Yn 5:17; Mt 7:23; Rum 4:15Kila mtu atendaye dhambi afanya uasi, kwa kuwa dhambi ni uasi. 53:5 2Kor 5:21; 1Yn 1:2; Isa 53:5, 6, 11; 1Tim 1:15; Ebr 1:3; 9:26; 1Pet 2:24Lakini mwajua ya kuwa yeye alidhihirishwa ili aziondoe dhambi, wala ndani yake hamna dhambi. 63:6 1Yn 5:18; 3Yn 1; 1Yn 2:4Kila mtu akaaye ndani yake hatendi dhambi. Kila mtu atendaye dhambi hakumwona yeye wala hakumtambua.

73:7 1Yn 2:1; 2:26; 2:29Watoto wapendwa, mtu yeyote asiwadanganye. Kila mtu atendaye haki ana haki, kama yeye alivyo na haki. 83:8 Yn 1:13; Za 119:3; 1Pet 1:23Yeye atendaye dhambi ni wa ibilisi, kwa sababu ibilisi amekuwa akitenda dhambi tangu mwanzo. Kwa kusudi hili Mwana wa Mungu alidhihirishwa, ili aziangamize kazi za ibilisi. 93:9 Yn 1:13; 1Yn 3:6; Za 119:3; 1Yn 5:18; 1Pet 1:23Yeyote aliyezaliwa na Mungu hatendi dhambi, kwa sababu uzao wa Mungu wakaa ndani yake, wala hawezi kutenda dhambi kwa sababu amezaliwa na Mungu. 103:10 1Yn 3:1, 2; Yn 1:12; 1Yn 3:8; 4:8; 2:9Kwa jinsi hii tunaweza kujua dhahiri watoto wa Mungu na pia watoto wa ibilisi. Yeyote asiyetenda haki hatokani na Mungu, wala yeye asiyempenda ndugu yake.

Mpendane Ninyi Kwa Ninyi

113:11 1Yn 1:5; Yn 15:12Hili ndilo neno mlilolisikia tangu mwanzo: Kwamba imetupasa tupendane sisi kwa sisi. 123:12 Mwa 4:8; Mt 5:37; Za 38:20; Mit 29:10Msiwe kama Kaini aliyekuwa wa yule mwovu akamuua ndugu yake. Basi kwa nini alimuua? Ni kwa sababu matendo yake Kaini yalikuwa mabaya na ya ndugu yake yalikuwa ya haki. 133:13 Yn 15:18, 19; 17:14Ndugu zangu, ninyi msistaajabu kama ulimwengu ukiwachukia. 143:14 Yn 5:24; 1Yn 2:9Sisi tunajua ya kwamba tumepita mautini kuingia uzimani, kwa sababu tunawapenda ndugu. Kila asiyempenda ndugu yake akaa mautini. 153:15 Mt 5:21, 22; Gal 5:20, 21; Yn 3:16Yeyote amchukiaye ndugu yake ni muuaji, nanyi mwajua ya kwamba muuaji hana uzima wa milele ndani yake.

163:16 Yn 10:11; 15:13; Flp 2:17; 1The 2:8Kwa namna hii twaweza kulijua pendo la Mungu: Kwa sababu Yesu Kristo aliutoa uhai wake kwa ajili yetu. Nasi imetupasa kuutoa uhai kwa ajili ya hao ndugu. 173:17 Yak 2:15, 16; 1Yn 4:20Ikiwa mtu anavyo vitu vya ulimwengu huu na akamwona ndugu yake ni mhitaji lakini asimhurumie, upendo wa Mungu wakaaje ndani ya mtu huyo? 183:18 1Yn 2:1; Eze 33:1; Rum 12:9Watoto wapendwa, tusipende kwa maneno au kwa ulimi bali kwa tendo na kweli. 193:19 Yn 18:37; 1Yn 1:8Basi hivi ndivyo tutakavyoweza kujua ya kuwa sisi tu wa kweli na hivyo twaithibitisha mioyo yetu mbele za Mungu 203:20 1Kor 4:4kila mara mioyo yetu inapotuhukumu. Kwa maana Mungu ni mkuu kuliko mioyo yetu, naye anajua kila kitu.

213:21 Efe 3:12; 1Kor 10:14; 1Yn 5:14Wapendwa, kama mioyo yetu haituhukumu, tunao ujasiri mbele za Mungu, 223:22 Mt 7:7; Ebr 13:21lolote tuombalo, twalipokea kutoka kwake, kwa sababu tumezitii amri zake na kutenda yale yanayompendeza. 233:23 Yn 6:23; 13:34Hii ndiyo amri yake: kwamba tuliamini Jina la Mwanawe, Yesu Kristo, na kupendana sisi kwa sisi kama yeye alivyotuamuru. 243:24 1Yn 4:15; 1The 4:8Wale wote wanaozishika amri zake hukaa ndani yake na yeye ndani yao. Hivi ndivyo tunavyojua kwamba anakaa ndani yetu. Nasi twajua hili kwa njia ya Roho yule aliyetupa.

New International Reader’s Version

1 John 3:1-24

1See what amazing love the Father has given us! Because of it, we are called children of God. And that’s what we really are! The world doesn’t know us because it didn’t know him. 2Dear friends, now we are children of God. He still hasn’t let us know what we will be. But we know that when Christ appears, we will be like him. That’s because we will see him as he really is. 3Christ is pure. All who hope to be like him make themselves pure.

4Everyone who sins breaks the law. In fact, breaking the law is sin. 5But you know that Christ came to take our sins away. And there is no sin in him. 6No one who remains joined to him keeps on sinning. No one who keeps on sinning has seen him or known him.

7Dear children, don’t let anyone lead you astray. The person who does what is right is holy, just as Christ is holy. 8The person who does what is sinful belongs to the devil. That’s because the devil has been sinning from the beginning. But the Son of God came to destroy the devil’s work. 9Those who are God’s children will not keep on sinning. God’s very nature remains in them. They can’t go on sinning. That’s because they are God’s children. 10Here is how you can tell the difference between God’s children and the devil’s children. Anyone who doesn’t do what is right isn’t God’s child. And anyone who doesn’t love their brother or sister isn’t God’s child either.

More Instructions About Loving and Hating One Another

11From the beginning we have heard that we should love one another. 12Don’t be like Cain. He belonged to the evil one. He murdered his brother. And why did he murder him? Because the things Cain had done were wrong. But the things his brother had done were right. 13My brothers and sisters, don’t be surprised if the world hates you. 14We know that we have left our old dead way of life. And we have entered into new life. We know this because we love one another. Anyone who doesn’t love still lives in their old condition. 15Anyone who hates their brother or sister is a murderer. And you know that no murderer has eternal life.

16We know what love is because Jesus Christ gave his life for us. So we should give our lives for our brothers and sisters. 17Suppose someone sees a brother or sister in need and is able to help them. And suppose that person doesn’t take pity on these needy people. Then how can the love of God be in that person? 18Dear children, don’t just talk about love. Put your love into action. Then it will truly be love.

19Here’s how we know that we hold to the truth. And here’s how we put our hearts at rest, knowing that God is watching. 20If our hearts judge us, we know that God is greater than our hearts. And he knows everything. 21Dear friends, if our hearts do not judge us, we can be bold with God. 22And he will give us anything we ask. That’s because we obey his commands. We do what pleases him. 23God has commanded us to believe in the name of his Son, Jesus Christ. He has also commanded us to love one another. 24The one who obeys God’s commands remains joined to him. And he remains joined to them. Here is how we know that God lives in us. We know it because of the Holy Spirit he gave us.