1 Yohana 2 – NEN & NIRV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

1 Yohana 2:1-29

Kristo Mwombezi Wetu

12:1 1The 2:11; Ebr 7:25; 1Tim 2:5Watoto wangu wapendwa, nawaandikia haya ili msitende dhambi. Lakini kama mtu yeyote akitenda dhambi, tunaye Mwombezi kwa Baba: ndiye Yesu Kristo, Mwenye Haki. 22:2 1Yn 4:10; Rum 3:25; Mt 1:21; Yn 3:17Yeye ndiye dhabihu ya upatanisho kwa ajili ya dhambi zetu, wala si kwa ajili ya dhambi zetu tu, bali pia kwa ajili ya dhambi za ulimwengu wote.

32:3 Yn 14:15; 1Yn 2:5; 3:24; 4:13; 5:2; 2:4Basi katika hili twajua ya kuwa tumemjua, tukizishika amri zake. 42:4 1Yn 1:6, 8; 2:3; Tit 1:16; 1Yn 3:6; 4:7, 8Mtu yeyote asemaye kuwa, “Ninamjua,” lakini hazishiki amri zake, ni mwongo, wala ndani ya mtu huyo hamna kweli. 52:5 Yn 14:15, 21, 23; 1Yn 4:12Lakini mtu yeyote anayelitii neno lake, upendo wa Mungu umekamilika ndani yake kweli kweli. Katika hili twajua kuwa tumo ndani yake. 62:6 Mt 11:29; 2Pet 2:21Yeyote anayesema anakaa ndani yake hana budi kuenenda kama Yesu alivyoenenda.

Amri Mpya

72:7 1Kor 10:14; 1Yn 2:24; 3:11, 23; 4:2Wapendwa, siwaandikii ninyi amri mpya bali ile ya zamani, ambayo mmekuwa nayo tangu mwanzo. Amri hii ya zamani ni lile neno mlilosikia. 82:8 Yn 13:34; Ebr 10:25; Yn 1:9; Efe 5:8; 1The 5:5Lakini nawaandikia amri mpya, yaani, lile neno lililo kweli ndani yake na ndani yenu, kwa sababu giza linapita na ile nuru ya kweli tayari inangʼaa.

92:9 1Yn 2:11; Law 19:17; 1Yn 3:10; 4:20, 21; 1:5Yeyote anayesema yumo nuruni lakini anamchukia ndugu yake bado yuko gizani. 102:10 1Yn 3:14; 2:11; Za 119:165; Rum 14:13, 15; Yn 11:9Yeye ampendaye ndugu yake anakaa nuruni, wala hakuna kitu chochote ndani yake cha kumkwaza. 112:11 Yn 11:9; 11:10; 12:35; 1Yn 1:6; Yn 12:35Lakini yeyote amchukiaye ndugu yake, yuko gizani na anaenenda gizani, wala hajui anakokwenda, kwa sababu giza limempofusha macho.

122:12 1Yn 2:9; 3:23Nawaandikia ninyi, watoto wadogo,

kwa sababu dhambi zenu

zimesamehewa kwa ajili ya Jina lake.

132:13 Mt 5:37; Yn 1:1; 16:33; 1Yn 2:14; 2:13Nawaandikia ninyi, akina baba,

kwa sababu mmemjua

yeye aliye tangu mwanzo.

Nawaandikia ninyi vijana

kwa sababu mmemshinda yule mwovu.

Nawaandikia ninyi watoto wadogo,

kwa sababu mmemjua Baba.

142:14 Efe 6:10; Yn 5:38; 1Yn 1:10Nawaandikia ninyi akina baba,

kwa sababu mmemjua

yeye aliye tangu mwanzo.

Nawaandikia ninyi vijana,

kwa sababu mna nguvu,

na neno la Mungu linakaa ndani yenu,

nanyi mmemshinda yule mwovu.

Msiupende Ulimwengu

152:15 Rum 12:2; Yak 4:4Msiupende ulimwengu wala mambo yaliyo ulimwenguni. Kama mtu yeyote akiupenda ulimwengu, upendo wa Baba haumo ndani yake. 162:16 Efe 2:8; Mit 27:20Kwa maana kila kitu kilichomo ulimwenguni, yaani tamaa ya mwili, tamaa ya macho na kiburi cha uzima, havitokani na Baba bali hutokana na ulimwengu. 172:17 Ebr 12:27; Mt 12:50; 1Kor 7:31; Yak 1:10; 4:14; 1Pet 1:24Nao ulimwengu unapita, pamoja na tamaa zake, bali yeye afanyaye mapenzi ya Mungu adumu milele.

Onyo Dhidi Ya Wapinga Kristo

182:18 1Yn 4:1; 2Yn 7Watoto wadogo, huu ni wakati wa mwisho! Kama mlivyosikia kwamba mpinga Kristo anakuja, hivyo basi wapinga Kristo wengi wamekwisha kuja. Kutokana na hili twajua kwamba huu ni wakati wa mwisho. 192:19 Mk 1:24; Yer 31:34Walitoka kwetu, lakini hawakuwa wa kwetu hasa. Kwa maana kama wangelikuwa wa kwetu, wangelikaa pamoja nasi, lakini kutoka kwao kulionyesha kwamba hakuna hata mmoja wao aliyekuwa wa kwetu.

202:20 1Yn 2:27; 2Kor 1:21; Mk 1:24; Yer 31:34; Mt 13:11; Yn 14:26Lakini ninyi mmetiwa mafuta na yeye Aliye Mtakatifu, nanyi nyote mnaijua kweli. 212:21 2Pet 1:12; Yud 5Siwaandikii kwa sababu hamuijui kweli, bali kwa sababu mnaijua, nanyi mnajua hakuna uongo utokao katika kweli. 222:22 1Yn 4:13; 2Yn 7Je, mwongo ni nani? Mwongo ni mtu yule asemaye kwamba Yesu si Kristo. Mtu wa namna hiyo ndiye mpinga Kristo, yaani, yeye humkana Baba na Mwana. 232:23 Yn 14:7; 2Yn 9Hakuna yeyote amkanaye Mwana aliye na Baba. Yeyote anayemkubali Mwana anaye na Baba pia.

242:24 2Yn 9Hakikisheni kwamba lile mlilosikia tangu mwanzo linakaa ndani yenu. Kama lile mlilosikia tangu mwanzo linakaa ndani yenu, ninyi nanyi mtakaa ndani ya Mwana na ndani ya Baba. 252:25 Mt 25:46; Yn 17:3; 1Yn 1:2; 5:11Hii ndiyo ahadi yake kwetu, yaani, uzima wa milele.

262:26 1Yn 3:7; 2Yn 7Nawaandikia mambo haya kuhusu wale watu ambao wanajaribu kuwapotosha. 272:27 1Yn 2:20; Yer 31:33, 34; Ebr 8:10, 11; Yn 14:26; 16:13Nanyi, upako mlioupata kutoka kwake unakaa ndani yenu, wala ninyi hamna haja ya mtu yeyote kuwafundisha. Lakini kama vile upako wake unavyowafundisha kuhusu mambo yote nayo ni kweli wala si uongo, basi kama ulivyowafundisha kaeni ndani yake.

Watoto Wa Mungu

282:28 Kol 3:4; 1Yn 3:2; Efe 3:12; 1The 2:19Sasa basi, watoto wapendwa, kaeni ndani yake, ili atakapofunuliwa, tuwe na ujasiri, wala tusiaibike mbele zake wakati wa kuja kwake.

292:29 1Yn 3:7; Mdo 22:14; Yn 1:13Kama mkijua kuwa yeye ni mwenye haki, mwajua kwamba kila atendaye haki amezaliwa naye.

New International Reader’s Version

1 John 2:1-29

1My dear children, I’m writing this to you so that you will not sin. But suppose someone does sin. Then we have a friend who speaks to the Father for us. He is Jesus Christ, the Blameless One. 2He gave his life to pay for our sins. But he not only paid for our sins. He also paid for the sins of the whole world.

Instructions About Loving and Hating Other Believers

3We know that we have come to know God if we obey his commands. 4Suppose someone says, “I know him.” But suppose this person does not do what God commands. Then this person is a liar and is not telling the truth. 5But if anyone obeys God’s word, then that person truly loves God. Here is how we know we belong to him. 6Those who claim to belong to him must live just as Jesus did.

7Dear friends, I’m not writing you a new command. Instead, I’m writing one you have heard before. You have had it since the beginning. 8But I am writing what amounts to a new command. Its truth was shown in how Jesus lived. It is also shown in how you live. That’s because the darkness is passing away. And the true light is already shining.

9Suppose someone claims to be in the light but hates a brother or sister. Then they are still in the darkness. 10Anyone who loves their brother and sister lives in the light. There is nothing in them to make them fall into sin. 11But anyone who hates a brother or sister is in the darkness. They walk around in the darkness. They don’t know where they are going. The darkness has made them blind.

Reasons for Writing

12Dear children, I’m writing to you

because your sins have been forgiven.

They have been forgiven because of what Jesus has done.

13Fathers, I’m writing to you

because you know the one who is from the beginning.

Young men, I’m writing to you

because you have won the battle over the evil one.

14Dear children, I’m writing to you

because you know the Father.

Fathers, I’m writing to you

because you know the one who is from the beginning.

Young men, I’m writing to you

because you are strong.

God’s word lives in you.

You have won the battle over the evil one.

Do Not Love the World

15Do not love the world or anything in it. If anyone loves the world, love for the Father is not in them. 16Here is what people who belong to this world do. They try to satisfy what their sinful desires want to do. They long for what their sinful eyes look at. They take pride in what they have and what they do. All of this comes from the world. None of it comes from the Father. 17The world and its evil desires are passing away. But whoever does what God wants them to do lives forever.

Warnings About Saying No to the Son

18Dear children, we are living in the last days. You have heard that the great enemy of Christ is coming. But even now many enemies of Christ have already come. That’s how we know that these are the last days. 19These enemies left our community of believers. They didn’t really belong to us. If they had belonged to us, they would have remained with us. But by leaving they showed that none of them belonged to us.

20You have received the Spirit from the Holy One. And all of you know the truth. 21I’m not writing to you because you don’t know the truth. I’m writing because you do know it. I’m writing to you because no lie comes from the truth. 22Who is the liar? It is anyone who says that Jesus is not the Christ. The person who says this is the great enemy of Christ. They say no to the Father and the Son. 23The person who says no to the Son doesn’t belong to the Father. But anyone who says yes to the Son belongs to the Father also.

24Make sure that you don’t forget what you have heard from the beginning. Then you will remain joined to the Son and to the Father. 25And here is what God has promised us. He has promised us eternal life.

26I’m writing these things to warn you. I am warning you about people trying to lead you astray. 27But you have received the Holy Spirit from God. He continues to live in you. So you don’t need anyone to teach you. God’s Spirit teaches you about everything. What he says is true. He doesn’t lie. Remain joined to Christ, just as you have been taught by the Spirit.

God’s Children and Sin

28Dear children, remain joined to Christ. Then when he comes, we can be bold. We will not be ashamed to meet him when he comes.

29You know that God is right and always does what is right. And you know that everyone who does what is right is God’s child.