1 Wakorintho 16 – NEN & NIRV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

1 Wakorintho 16:1-24

Changizo Kwa Ajili Ya Watakatifu

116:1 Mdo 24:17; 9:13; 16:6Basi kuhusu changizo kwa ajili ya watakatifu: Kama nilivyoyaagiza makanisa ya Galatia, fanyeni vivyo hivyo. 216:2 Mdo 20:7; 2Kor 9:4-5Siku ya kwanza ya kila juma, kila mmoja wenu atenge kiasi cha fedha, kulingana na mapato yake na fedha hizo aziweke akiba, ili nitakapokuja pasiwe na lazima ya kufanya mchango. 316:3 2Kor 3:1; 8:18-19Kwa hiyo nitakapowasili, nitawapa wale mtakaowachagua barua za kuwatambulisha, ili kuwatuma wapeleke zawadi zenu huko Yerusalemu. 416:4 2Kor 8:4, 19Kama ikionekana ni vyema na mimi niende, basi hao watu watafuatana nami.

Mahitaji Binafsi

516:5 1Kor 4:19; Mdo 16:9Baada ya kupitia Makedonia nitakuja kwenu, maana ninakusudia kupitia Makedonia. 616:6 Rum 15:24; Tit 3:13Huenda nitakaa nanyi kwa muda, au hata kukaa nanyi kipindi chote cha baridi, ili mweze kunisaidia katika safari yangu, popote niendapo. 716:7 Mdo 18:21Kwa maana sitaki niwaone sasa na kupita tu; natarajia kuwa nanyi kwa muda wa kutosha, kama Bwana akipenda. 816:8 Mdo 18:19; 2:1Lakini nitakaa Efeso mpaka wakati wa Pentekoste, 916:9 Mdo 14:27; 2Kor 2:12; Kol 4:3; Ufu 3:8; Mdo 19:9kwa maana mlango mkubwa umefunguliwa kwangu kufanya kazi yenye matunda, nako huko kuna adui wengi wanaonipinga.

1016:10 Mdo 16:1; 19:22; Rum 16:21; Flp 2:20, 22; 1The 3:2Ikiwa Timotheo atakuja kwenu, hakikisheni kwamba hana hofu yoyote akiwa nanyi, kwa sababu anafanya kazi ya Bwana, kama mimi nifanyavyo. 1116:11 1Tim 4:12; 2Kor 1:16; 3Yn 6; Mdo 19:9Basi asiwepo mtu atakayekataa kumpokea. Msafirisheni kwa amani ili aweze kunijia tena. Namtarajia pamoja na ndugu.

1216:12 Mdo 18:24; 1Kor 1:12Basi kwa habari za ndugu yetu Apolo, nimemsihi kwa bidii aje kwenu pamoja na hao ndugu. Ingawa alikuwa hapendi kabisa kuja sasa, lakini atakuja apatapo nafasi.

Maneno Ya Mwisho

1316:13 1Kor 1:8; 2Kor 1:21; Gal 5:1; Flp 1:27; 1The 3:8; Tit 1:9; Efe 6:10Kesheni, simameni imara katika imani, fanyeni kiume, kuweni mashujaa kuweni hodari. 1416:14 1Kor 14:1Fanyeni kila kitu katika upendo.

1516:15 1Kor 1:6; Rum 16:5; Mdo 18; 12; 24; 17; 9:13Ninyi mnajua kwamba watu wa nyumbani mwa Stefana ndio waliokuwa wa kwanza kuamini katika Akaya, nao wamejitoa kwa ajili ya kuwahudumia watakatifu. Ndugu nawasihi, 1616:16 1The 5:12; Ebr 13:17mjitie katika kuwahudumia watu kama hawa na kila mmoja aingiaye kwenye kazi na kuifanya kwa bidii. 1716:17 2Kor 11:9; Flp 2:30Nilifurahi wakati Stefana, Fortunato na Akaiko walipofika, kwa sababu wamenipatia yale niliyopungukiwa kutoka kwenu. 1816:18 Rum 15:32; Flp 1:7; 2:29Kwa kuwa waliiburudisha roho yangu na zenu pia. Watu kama hawa wanastahili kutambuliwa.

Salamu Za Mwisho

1916:19 Mdo 2:9; 18:2; Rum 16:5Makanisa ya Asia yanawasalimu. Akila na Prisila,16:19 Prisila kwa Kiyunani ni Priska, hivyo tafsiri nyingine zimemuita Priska. pamoja na kanisa lililoko nyumbani kwao wanawasalimu sana katika Bwana. 2016:20 Rum 16:16; 2Kor 13:12; 1Pet 5:14Ndugu wote walioko hapa wanawasalimu. Salimianeni kwa busu takatifu.

2116:21 Gal 6:11; Kol 4:18; 2The 3:17Mimi, Paulo, naandika salamu hizi kwa mkono wangu mwenyewe.

2216:22 Efe 6:24; Rum 9:3; Ufu 22:20Kama mtu yeyote hampendi Bwana Yesu Kristo, na alaaniwe. Bwana wetu, njoo.16:22 Kwa Kiaramu ni Marana tha.

2316:23 Rum 16:20Neema ya Bwana Yesu iwe nanyi.

24Upendo wangu uwe nanyi nyote katika Kristo Yesu. Amen.

New International Reader’s Version

1 Corinthians 16:1-24

The Offering for the Lord’s People

1Now I want to deal with the offering of money for the Lord’s people. Do what I told the churches in Galatia to do. 2On the first day of every week, each of you should put some money away. The amount should be in keeping with how much money you make. Save the money so that you won’t have to take up an offering when I come. 3When I arrive, I will send some people with your gift to Jerusalem. They will be people you consider to be good. And I will give them letters that explain who they are. 4If it seems good for me to go also, they will go with me.

What Paul Asks for Himself

5After I go through Macedonia, I will come to you. I will only be passing through Macedonia. 6But I might stay with you for a while. I might even spend the winter. Then you can help me on my journey everywhere I go. 7I don’t want to see you now while I am just passing through. Instead, I hope to spend some time with you, if the Lord allows it. 8But I will stay at Ephesus until the day of Pentecost. 9A door has opened wide for me to do some good work here. There are many people who oppose me.

10Timothy will visit you. Make sure he has nothing to worry about while he is with you. He is doing the work of the Lord, just as I am. 11No one should treat him badly. Send him safely on his way so he can return to me. I’m expecting him to come back along with the others.

12I want to say something about our brother Apollos. I tried my best to get him to go to you with the others. But he didn’t want to go right now. He will go when he can.

13Be on your guard. Remain strong in the faith. Be brave. 14Be loving in everything you do.

15You know that the first believers in Achaia were from the family of Stephanas. They have spent all their time serving the Lord’s people. Brothers and sisters, I am asking you 16to follow the lead of people like them. Follow everyone who joins in the task and works hard at it. 17I was glad when Stephanas, Fortunatus and Achaicus arrived. They have supplied me with what you couldn’t give me. 18They renewed my spirit, and yours also. People like them are worthy of honor.

Final Greetings

19The churches in Asia Minor send you greetings.

Aquila and Priscilla greet you warmly because of the Lord’s love. So does the church that meets in their house.

20All the brothers and sisters here send you greetings.

Greet one another with a holy kiss.

21I, Paul, am writing this greeting with my own hand.

22If anyone does not love the Lord, let a curse be on that person! Come, Lord!

23May the grace of the Lord Jesus be with you.

24I give my love to all of you who belong to Christ Jesus. Amen.