2 Wakorintho 1 – NEN & NIRV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

2 Wakorintho 1:1-24

Salamu

11:1 1Kor 1:11; Efe 1:1; Kol 1:1; 2Tim 1:1; Mdo 16:1; 1Kor 10:32; Mdo 18:1; 18:12Barua hii ni kutoka kwangu mimi Paulo, mtume wa Kristo Yesu kwa mapenzi ya Mungu, na Timotheo ndugu yetu,

Kwa kanisa la Mungu lililoko Korintho, pamoja na watakatifu wote walioko Akaya yote:

21:2 Rum 1:7; 1Kor 1:3; Gal 1:3; Flp 1:2; Kol 1:2; Flp 3:1; 1The 1:1Neema na amani itokayo kwa Mungu Baba yetu na kwa Bwana Yesu Kristo iwe nanyi.

Mungu Wa Faraja Yote

31:3 Efe 1:3; 1Pet 1:3; Rum 15:5Ahimidiwe Mungu na Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo, Baba wa huruma na Mungu wa faraja yote. 41:4 Isa 49:13; 51:12; 66:13; 2Kor 7:6-13Yeye hutufariji katika taabu zetu, ili tuweze kuwafariji walio katika taabu yoyote kwa faraja ambayo sisi wenyewe tumepokea kutoka kwa Mungu. 51:5 Rum 8:17; 2Kor 4:10; Gal 6:17; Flp 3:10; Kol 1:24; 1Pet 4:13Kama vile mateso ya Kristo yanavyozidi ndani ya maisha yetu, hivyo ndivyo faraja yetu inavyofurika kwa njia ya Kristo. 61:6 2Kor 4:15; 4:17Kama tunataabika, ni kwa ajili ya faraja na wokovu wenu; kama tukifarijiwa, ni kwa ajili ya faraja yenu, iwaleteayo saburi ya mateso yale yale yanayotupata. 71:7 2Kor 1:5; Rum 8:17; 2Tim 2:12Nalo tumaini letu kwenu ni thabiti, kwa sababu tunajua kwamba kama vile mnavyoshiriki mateso yetu, ndivyo pia mnavyoshiriki katika faraja yetu.

81:8 Rum 11:25; 1Kor 15:32; Mdo 2:9Ndugu wapendwa, hatutaki mkose kujua kuhusu zile taabu tulizopata huko Asia. Kwa maana tulilemewa na mizigo sana, kiasi cha kushindwa kuvumilia, hata tulikata tamaa ya kuishi. 91:9 Yer 17:5-7; Yn 5:21Kwa kweli, mioyoni mwetu tulihisi tumekabiliwa na hukumu ya kifo, ili tusijitegemee sisi wenyewe bali tumtegemee Mungu afufuaye wafu. 101:10 Rum 15:31; 1Tim 4:10Yeye aliyetuokoa kwenye hatari kubwa ya kifo na atatuokoa tena. Kwake yeye tumeweka tumaini letu kwamba ataendelea kutuokoa. 111:11 Rum 15:30; Flp 1:19; 2Kor 4:15; 9:11Kama vile mlivyoungana kusaidiana nasi katika maombi, hivyo wengi watatoa shukrani kwa niaba yetu kwa ajili ya baraka za neema tulizopata kwa majibu ya maombi ya wengi.

Paulo Aahirisha Ziara

121:12 Mdo 23:11; 1The 2:10; 2Kor 2:17; 1Kor 1:17; 2:1-13Basi haya ndiyo majivuno yetu: Dhamiri yetu inatushuhudia kwamba tumeenenda katika ulimwengu na hasa katika uhusiano wetu na ninyi, katika utakatifu na uaminifu utokao kwa Mungu. Hatukufanya hivyo kwa hekima ya kidunia bali kwa neema ya Mungu. 13Kwa maana hatuwaandikii mambo ambayo hamwezi kusoma au kuyaelewa. Natumaini kwamba, 141:14 1Kor 1:8kama vile mlivyotuelewa kwa sehemu, mtakuja kuelewa kwa ukamilifu ili mweze kujivuna kwa ajili yetu, kama na sisi tutakavyojivuna kwa ajili yenu katika siku ya Bwana Yesu.

151:15 1Kor 4:19; Rum 1:11-13; 15:29Kwa kuwa nilikuwa na uhakika wa mambo haya, nilitaka nije kwenu kwanza, ili mpate faida mara mbili. 161:16 1Kor 16:5-7; Mdo 16:9; 3Yn 6; Mdo 19:2Nilipanga kuwatembelea nikiwa safarini kwenda Makedonia na kurudi tena kwenu nikitoka Makedonia, ili mnisafirishe katika safari yangu ya kwenda Uyahudi. 171:17 2Kor 10:2-3; 11:18Nilipopanga jambo hili, je, nilikuwa kigeugeu? Au ninafanya mipango yangu kwa hali ya mwili, ili niseme, “Ndiyo, ndiyo” na “Siyo, siyo” wakati huo huo?

181:18 1Kor 1:9Hakika kama Mungu alivyo mwaminifu, maneno yetu kwenu hayajawa “Ndiyo na Siyo.” 191:19 Mt 4:3; Mdo 15:22; 16:1Kwa kuwa Yesu Kristo, Mwana wa Mungu, ambaye tulimhubiri kwenu: Mimi, Silvano1:19 Yaani Sila. na Timotheo, hakuwa “Ndiyo” na “Siyo,” bali kwake yeye siku zote ni “Ndiyo.” 201:20 Rum 15:9Kwa maana ahadi zote za Mungu zilizo katika Kristo ni “Ndiyo.” Kwa sababu hii ni kwake yeye tunasema “Amen” kwa utukufu wa Mungu. 211:21 1Kor 16:13; 1Yn 2:20-27Basi ni Mungu atufanyaye sisi pamoja nanyi kusimama imara katika Kristo. Ametutia mafuta 221:22 Mwa 38:18; Hag 2:23; 2Kor 5:5kwa kututia muhuri wake na kutupa Roho wake mioyoni mwetu kuwa rehani kwa ajili ya kututhibitishia kile kijacho.

231:23 Rum 1:9; 1Kor 4:21; 2Kor 2:1-3; 13:2-10Mungu ni shahidi wangu kwamba ilikuwa ni kwa ajili ya kuwahurumia ninyi sikurudi Korintho. 241:24 1Pet 5:3; Rum 11:20; 1Kor 1:5-11Si kwamba tunatawala imani yenu, bali twatenda kazi pamoja nanyi kwa ajili ya furaha yenu, kwa sababu ni kwa imani mwasimama imara.

New International Reader’s Version

2 Corinthians 1:1-24

1I, Paul, am writing this letter. I am an apostle of Christ Jesus just as God planned. Timothy our brother joins me in writing.

We are sending this letter to you, the members of God’s church in Corinth. It is also for all God’s holy people everywhere in Achaia.

2May God our Father and the Lord Jesus Christ give you grace and peace.

Praise to the God Who Gives Comfort

3Give praise to the God and Father of our Lord Jesus Christ! He is the Father who gives tender love. All comfort comes from him. 4He comforts us in all our troubles. Now we can comfort others when they are in trouble. We ourselves receive comfort from God. 5We share very much in the sufferings of Christ. So we also share very much in his comfort. 6If we are having trouble, it is so that you will be comforted and renewed. If we are comforted, it is so that you will be comforted. Then you will be able to put up with the same suffering we have gone through. 7Our hope for you remains firm. We know that you suffer just as we do. In the same way, God comforts you just as he comforts us.

8Brothers and sisters, we want you to know about the hard times we had in Asia Minor. We were having a lot of trouble. It was far more than we could stand. We even thought we were going to die. 9In fact, we felt as if we were under the sentence of death. But that happened so that we would not depend on ourselves but on God. He raises the dead to life. 10God has saved us from deadly dangers. And he will continue to do it. We have put our hope in him. He will continue to save us. 11You must help us by praying for us. Then many people will give thanks because of what will happen to us. They will thank God for his kindness to us in answer to the prayers of many.

Paul Changes His Plans

12Here is what we take pride in. Our sense of what is right and wrong tells us how we have acted. We have lived with honor and godly honesty. We have depended on God’s grace and not on the world’s wisdom. We lived that way most of all when we were dealing with you. 13We are writing only what you can read and understand. And here is what I hope. 14Up to this point you have understood some of the things we have said. But now here is what I hope for when the Lord Jesus returns. I hope that your pride in us will be the same as our pride in you. When this happens, you will understand us completely.

15Because I was sure of this, I wanted to visit you first. Here is how I thought you would be helped twice. 16I planned to visit you on my way to Macedonia. I would have come back to you from there. Then you would have sent me on my way to Judea. 17When I planned all this, was I ready to change my mind for no good reason? No. I don’t make my plans the way the world makes theirs. In the same breath the world says both, “Yes! Yes!” and “No! No!”

18But just as sure as God is faithful, our message to you is not “Yes” and “No.” 19Silas, Timothy and I preached to you about the Son of God, Jesus Christ. Our message did not say “Yes” and “No” at the same time. The message of Christ has always been “Yes.” 20God has made a great many promises. They are all “Yes” because of what Christ has done. So through Christ we say “Amen.” We want God to receive glory. 21He makes both us and you remain strong in the faith because we belong to Christ. He anointed us. 22He put his Spirit in our hearts and marked us as his own. We can now be sure that he will give us everything he promised us.

23I call God to be my witness. May he take my life if I’m lying. I wanted to spare you, so I didn’t return to Corinth. 24Your faith is not under our control. You remain strong in your own faith. But we work together with you for your joy.