1 Wakorintho 1 – NEN & KJV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

1 Wakorintho 1:1-31

Salamu

11:1 Rum 1:1; Efe 1:1; 2Kor 1:1; 2Tim 1:1; Mdo 18:17Paulo, niliyeitwa kwa mapenzi ya Mungu kuwa mtume wa Kristo Yesu, na Sosthene ndugu yetu.

21:2 1Kor 10:32; Mdo 2:21; 18:1; Rum 1:17Kwa kanisa la Mungu lililoko Korintho, kwa wale waliotakaswa katika Kristo Yesu na walioitwa kuwa watakatifu, pamoja na wale wote ambao kila mahali wanaliitia Jina la Kristo Yesu Bwana wetu, aliye Bwana wao na wetu pia:

31:3 Rum 1:7; 1Kor 1:2; Efe 1:2; 1Pet 1:2Neema na amani itokayo kwa Mungu Baba yetu na kwa Bwana Yesu Kristo iwe nanyi.

Shukrani

41:4 Rum 1:8Ninamshukuru Mungu siku zote kwa ajili yenu kwa sababu ya neema yake mliyopewa katika Kristo Yesu. 51:5 2Kor 8:7; 1Kor 12:8; 2Kor 9:11Kwa kuwa katika Kristo mmetajirishwa kwa kila hali, katika kusema kwenu na katika maarifa yenu yote, 61:6 2The 1:10; 1Tim 2:6; Ufu 1:2kwa sababu ushuhuda wetu kumhusu Kristo ulithibitishwa ndani yenu. 71:7 Rum 1:11; 1Kor 12:1-3; Mt 16:27; Lk 17:30; Ufu 1:7; 1The 1:10; 2:19; Tit 2:13; Yak 5:7-8; 1Pet 1:13; 2Pet 3:12Kwa hiyo hamkupungukiwa na karama yoyote ya kiroho wakati mnangoja kwa shauku kudhihirishwa kwa Bwana wetu Yesu Kristo. 81:8 1The 3:13; 5:2; Amo 5:18; 1Kor 5:5; Flp 1:6; 2:16Atawafanya imara mpaka mwisho, ili msiwe na hatia siku ile ya Bwana wetu Yesu Kristo. 91:9 Rum 8:28; 1Yn 1:3; Isa 49:7; Kum 7:9; 1Kor 10:13; 1The 3:3; 1Tim 2:13; Ebr 10:23; 11:11Mungu ambaye mmeitwa naye ili mwe na ushirika na Mwanawe Yesu Kristo, Bwana wetu ni mwaminifu.

Mgawanyiko Ndani Ya Kanisa

101:10 Rum 7:1; 15:5; 1Kor 11:18Nawasihi ndugu zangu, katika Jina la Bwana wetu Yesu Kristo, kwamba mpatane nia zenu ninyi kwa ninyi, ili pasiwepo na matengano katikati yenu na kwamba mwe na umoja kikamilifu katika nia na katika kusudi. 111:11 Mdo 11:14Ndugu zangu, nimepata habari kutoka kwa baadhi ya watu wa nyumbani mwa Kloe kwamba kuna magomvi katikati yenu. 121:12 1Kor 3:4-22; Mdo 18:24; Yn 1:42; 1Kor 3:22; 9:5Maana yangu ni kwamba: Mmoja wenu husema, “Mimi ni wa Paulo”; mwingine, “Mimi ni wa Apolo”; mwingine, “Mimi ni wa Kefa,”1:12 Yaani Petro. na mwingine, “Mimi ni wa Kristo.”

13Je, Kristo amegawanyika? Je, Paulo ndiye alisulubishwa kwa ajili yenu? Je, mlibatizwa kwa jina la Paulo? 141:14 Mdo 18:8; 19:29; Rum 16:23Nashukuru kwamba sikumbatiza mtu yeyote isipokuwa Krispo na Gayo. 15Kwa hiyo hakuna mtu yeyote anayeweza kusema kwamba alibatizwa kwa jina langu. 161:16 Mdo 11:14; 1Kor 16:15(Naam, niliwabatiza pia watu wa nyumbani mwa Stefana. Lakini zaidi ya hao sijui kama nilimbatiza mtu mwingine yeyote.) 171:17 Yn 4:2; Mdo 2:38; 1Kor 2:1-13Kwa maana Kristo hakunituma ili kubatiza bali kuhubiri Injili; sio kwa maneno ya hekima ya kibinadamu, ili msalaba wa Kristo usije ukakosa nguvu yake.

Kristo Ni Hekima Na Nguvu Ya Mungu

181:18 1Kor 2:14; 2Kor 2:15; 4:3; 2The 2:10; Mdo 2:47; Rum 1:16Kwa maana ujumbe wa msalaba kwa wale wanaopotea ni upuzi, lakini kwetu sisi tunaookolewa ni nguvu ya Mungu. 191:19 Isa 29:14; Ay 5:12, 13; Yer 8:9Kwa maana imeandikwa:

“Nitaiharibu hekima ya wenye hekima,

na kubatilisha akili ya wenye akili.”

201:20 Isa 19:11-12; 1Kor 2:6-8; 3:18; 2Kor 4:4; Gal 1:4; Ay 12:17; Isa 44:25; Yer 8:9; Rum 1:22; 1Kor 3:18-19Yuko wapi mwenye hekima? Yuko wapi msomi? Yuko wapi mwanafalsafa wa nyakati hizi? Je, Mungu hakufanya hekima ya ulimwengu huu kuwa upumbavu? 211:21 1Kor 6:2; 11:32; Rum 11:14; 3:22Kwa kuwa katika hekima ya Mungu, ulimwengu kwa hekima yake haukumjua yeye, ilimpendeza Mungu kuwaokoa wale walioamini kwa upuzi wa lile neno lililohubiriwa. 221:22 Mt 12:38; Yn 2:11; 4:48Wayahudi wanadai ishara za miujiza na Wayunani wanatafuta hekima. 231:23 1Kor 2:2; Gal 3:1; Lk 2:34Lakini sisi tunamhubiri Kristo aliyesulubiwa: yeye kwa Wayahudi ni kikwazo na kwa Wayunani ni upuzi. 241:24 Rum 8:28; 1:16; Kol 2:3Lakini kwa wale ambao Mungu amewaita, Wayahudi na pia Wayunani, Kristo ndiye nguvu ya Mungu na pia hekima ya Mungu. 251:25 2Kor 13:4; 1Kor 1:18Kwa maana upumbavu wa Mungu una hekima zaidi kuliko hekima ya wanadamu, nao udhaifu wa Mungu una nguvu kuliko nguvu ya wanadamu.

261:26 Rum 8:28; 1Kor 1:20; Yn 7:48Ndugu zangu, kumbukeni mlivyokuwa mlipoitwa. Kwa kipimo cha kibinadamu, si wengi wenu mliokuwa na hekima. Si wengi mliokuwa na ushawishi, si wengi mliozaliwa katika jamaa zenye vyeo. 271:27 Yak 2:5; Rum 1:22; 1Kor 3:18-19Lakini Mungu alivichagua vitu vipumbavu vya ulimwengu ili awaaibishe wenye hekima, Mungu alivichagua vitu dhaifu vya ulimwengu ili awaaibishe wenye nguvu. 281:28 Rum 4:17; 1Kor 2:6Alivichagua vitu vya chini na vinavyodharauliwa vya dunia hii, vitu ambavyo haviko, ili avibatilishe vile vilivyoko, 291:29 Efe 2:9ili mtu yeyote asijisifu mbele zake. 301:30 Rum 16:3; Yer 5:5-6; 33:16; 2Kor 5:21; Flp 3:9; 1Kor 1:2; Rum 3:24Bali kwa yeye ninyi mmepata kuwa katika Kristo Yesu, aliyefanyika kwetu hekima itokayo kwa Mungu, yaani haki, na utakatifu na ukombozi. 311:31 Yer 9:23; Za 34:2; 44:8; 2Kor 10:17Hivyo, kama ilivyoandikwa: “Yeye ajisifuye na ajisifu katika Bwana.”

King James Version

1 Corinthians 1:1-31

1Paul, called to be an apostle of Jesus Christ through the will of God, and Sosthenes our brother, 2Unto the church of God which is at Corinth, to them that are sanctified in Christ Jesus, called to be saints, with all that in every place call upon the name of Jesus Christ our Lord, both theirs and ours: 3Grace be unto you, and peace, from God our Father, and from the Lord Jesus Christ.

4I thank my God always on your behalf, for the grace of God which is given you by Jesus Christ; 5That in every thing ye are enriched by him, in all utterance, and in all knowledge; 6Even as the testimony of Christ was confirmed in you: 7So that ye come behind in no gift; waiting for the coming of our Lord Jesus Christ: 8Who shall also confirm you unto the end, that ye may be blameless in the day of our Lord Jesus Christ. 9God is faithful, by whom ye were called unto the fellowship of his Son Jesus Christ our Lord.

10Now I beseech you, brethren, by the name of our Lord Jesus Christ, that ye all speak the same thing, and that there be no divisions among you; but that ye be perfectly joined together in the same mind and in the same judgment. 11For it hath been declared unto me of you, my brethren, by them which are of the house of Chloe, that there are contentions among you. 12Now this I say, that every one of you saith, I am of Paul; and I of Apollos; and I of Cephas; and I of Christ. 13Is Christ divided? was Paul crucified for you? or were ye baptized in the name of Paul? 14I thank God that I baptized none of you, but Crispus and Gaius; 15Lest any should say that I had baptized in mine own name. 16And I baptized also the household of Stephanas: besides, I know not whether I baptized any other. 17For Christ sent me not to baptize, but to preach the gospel: not with wisdom of words, lest the cross of Christ should be made of none effect.

18For the preaching of the cross is to them that perish foolishness; but unto us which are saved it is the power of God. 19For it is written, I will destroy the wisdom of the wise, and will bring to nothing the understanding of the prudent. 20Where is the wise? where is the scribe? where is the disputer of this world? hath not God made foolish the wisdom of this world? 21For after that in the wisdom of God the world by wisdom knew not God, it pleased God by the foolishness of preaching to save them that believe. 22For the Jews require a sign, and the Greeks seek after wisdom: 23But we preach Christ crucified, unto the Jews a stumblingblock, and unto the Greeks foolishness; 24But unto them which are called, both Jews and Greeks, Christ the power of God, and the wisdom of God. 25Because the foolishness of God is wiser than men; and the weakness of God is stronger than men. 26For ye see your calling, brethren, how that not many wise men after the flesh, not many mighty, not many noble, are called: 27But God hath chosen the foolish things of the world to confound the wise; and God hath chosen the weak things of the world to confound the things which are mighty; 28And base things of the world, and things which are despised, hath God chosen, yea, and things which are not, to bring to nought things that are: 29That no flesh should glory in his presence. 30But of him are ye in Christ Jesus, who of God is made unto us wisdom, and righteousness, and sanctification, and redemption: 31That, according as it is written, He that glorieth, let him glory in the Lord.