1 Wafalme 18 – NEN & CARST

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

1 Wafalme 18:1-46

Eliya Na Obadia

118:1 Lk 4:25; Kum 28:12Baada ya muda mrefu, katika mwaka wa tatu, neno la Bwana likamjia Eliya kusema, “Nenda ukajionyeshe kwa Ahabu na mimi nitanyesha mvua juu ya nchi.” 218:2 Law 26:26Kwa hiyo Eliya akaenda kujionyesha kwa Ahabu.

Wakati huu njaa ilikuwa kali sana katika Samaria, 318:3 1Fal 16:9; Neh 7:2naye Ahabu alikuwa amemwita Obadia ambaye alikuwa msimamizi wa jumba lake la kifalme. (Obadia alimcha Bwana sana. 418:4 1Fal 21:23; Yer 26:24Wakati Yezebeli alipokuwa akiwaua manabii wa Bwana, Obadia alikuwa amewachukua manabii mia moja na kuwaficha katika mapango mawili, hamsini kwenye kila moja na akawa akiwapa chakula na maji.) 518:5 Yer 14:3; Mwa 47:4Ahabu alikuwa amemwambia Obadia, “Nenda katika nchi yote kwenye vijito vyote na mabonde. Huenda tunaweza kupata majani ya kuwalisha farasi na nyumbu wapate kuishi ili tusilazimike kuwaua hata mmoja wa wanyama wetu.” 6Kwa hiyo wakagawanya nchi waliyokusudia kutafuta majani, Ahabu akaenda upande mmoja na Obadia upande mwingine.

718:7 2Fal 1:8; Zek 13:4Wakati Obadia alipokuwa akitembea njiani, Eliya akakutana naye. Obadia akamtambua, akamsujudia hadi nchi na kusema, “Je, hivi kweli ni wewe, bwana wangu Eliya?”

8Eliya akamjibu, “Ndiyo, nenda ukamwambie bwana wako Ahabu, ‘Eliya yuko hapa.’ ”

9Obadia akamuuliza, “Ni kosa gani nimefanya, hata ukaamua kumkabidhi mtumishi wako mkononi mwa Ahabu ili aniue? 1018:10 1Fal 17:3Hakika kama Bwana Mungu wako aishivyo, hakuna taifa hata moja au ufalme ambapo bwana wangu hajamtuma mtu kukutafuta. Kila wakati taifa au ufalme walipodai kwamba haupo huko, aliwafanya waape kwamba hawakuweza kukupata. 11Lakini sasa unaniambia niende kwa bwana wangu na kusema, ‘Eliya yuko hapa.’ 1218:12 2Fal 2:16; Eze 3:14; Mdo 8:39Sijui ni wapi Roho wa Bwana ataamua kukupeleka wakati nitakapokuacha. Kama nikienda kumwambia Ahabu na asikupate, ataniua. Hata hivyo mimi mtumishi wako nimemwabudu Bwana tangu ujana wangu. 13Je, hukusikia, bwana wangu, nilifanya nini wakati Yezebeli alipokuwa akiua manabii wa Bwana? Niliwaficha manabii wa Bwana mia moja katika mapango mawili, hamsini katika kila moja, nami nikawapatia chakula na maji. 14Nawe sasa unaniambia niende kwa bwana wangu na kumwambia, ‘Eliya yuko hapa.’ Yeye ataniua!”

15Eliya akasema, “Kama Bwana Mwenye Nguvu Zote aishivyo, yeye ninayemtumikia, hakika nitajionyesha kwa Ahabu leo.”

Eliya Juu Ya Mlima Karmeli

16Basi Obadia akaenda kukutana na Ahabu na kumwambia, naye Ahabu akaenda kukutana na Eliya. 1718:17 Yos 7:25; 1Fal 21:20Ahabu alipomwona Eliya, akamwambia, “Je, ni wewe, mtaabishaji wa Israeli?”

1818:18 1Fal 16:33Eliya akamjibu, “Mimi sijaitaabisha Israeli. Lakini wewe na jamaa ya baba yako ndio mnaofanya hivyo. Mmeziacha amri za Bwana na mkafuata Mabaali. 1918:19 2Fal 10:19; Yos 19:26Sasa waite watu kutoka Israeli yote tukutane nao juu ya Mlima Karmeli. Nawe uwalete hao manabii wa Baali mia nne na hamsini na hao manabii mia nne wa Ashera, walao chakula mezani mwa Yezebeli.”

2018:20 2Fal 2:25; 4:25Ndipo Ahabu akatuma ujumbe katika Israeli yote na kuwakusanya manabii hao juu ya mlima Karmeli. 2118:21 Yos 24:15; 2Fal 17:41; Mt 6:24Eliya akasimama mbele ya watu na kusema, “Mtasitasita katika mawazo mawili hadi lini? Ikiwa Bwana ndiye Mungu, mfuateni yeye; lakini ikiwa Baali ni Mungu, basi mfuateni yeye.”

Lakini watu hawakusema kitu.

2218:22 1Fal 19:10; Yer 2:8Kisha Eliya akawaambia, “Ni mimi peke yangu nabii wa Bwana aliyebaki, lakini Baali ana manabii mia nne na hamsini. 23Leteni mafahali wawili. Wao na wajichagulie mmoja, wamkate vipande vipande na waweke juu ya kuni lakini wasiiwashie moto. Nitamwandaa huyo fahali mwingine na kumweka juu ya kuni lakini sitawasha moto. 2418:24 1Sam 7:8; Law 9:24Kisha mliitie jina la mungu wenu, nami nitaliitia jina la Bwana Mungu yule ambaye atajibu kwa moto, huyo ndiye Mungu.”

Kisha watu wote wakasema, “Hilo unalosema ni jema.”

25Eliya akawaambia manabii wa Baali, “Chagueni mmoja kati ya hawa mafahali na mwe wa kwanza kumwandaa, kwa kuwa ninyi mko wengi sana. Liitieni jina la mungu wenu, lakini msiwashe moto.” 2618:26 Za 115:4-5; 1Kor 8:4; 12:2Kwa hiyo wakamchukua yule fahali waliyepewa, nao wakamwandaa.

Kisha wakaliitia jina la Baali kutoka asubuhi hadi adhuhuri, wakapiga kelele, “Ee Baali, utujibu!” Lakini hapakuwa na jibu; hakuna aliyejibu. Nao wakacheza kuizunguka madhabahu waliyoijenga.

27Wakati wa adhuhuri, Eliya akaanza kuwadhihaki, akisema, “Pigeni kelele zaidi! Hakika yeye ni mungu! Labda amezama katika mawazo mazito, au ana shughuli nyingi, au amesafiri. Labda amelala usingizi mzito, naye ni lazima aamshwe.” 2818:28 Law 19:28Kwa hiyo wakapiga kelele zaidi na kama ilivyokuwa desturi yao wakajichanja wenyewe kwa visu na vyembe, mpaka damu ikachuruzika. 2918:29 Kut 29:41; 2Fal 19:12; Isa 16:12Adhuhuri ikapita, nao wakaendelea na utabiri wao wa kiwazimu mpaka wakati wa dhabihu ya jioni. Lakini hapakuwa na jibu, hakuna aliyejibu, hakuna aliyeangalia.

3018:30 1Fal 19:10Kisha Eliya akawaambia watu wote, “Sogeeni karibu nami.” Watu wote wakamkaribia, naye akakarabati madhabahu ya Bwana, ambayo ilikuwa imevunjwa. 3118:31 2Fal 17:34; Mwa 17:5Eliya akachukua mawe kumi na mawili, moja kwa ajili ya kila kabila la wana wa Yakobo, ambaye neno la Bwana lilimjia, likisema, “Jina lako litakuwa Israeli.” 3218:32 Kol 3:17; Kum 18:7Kwa mawe hayo, akajenga madhabahu katika jina la Bwana, na akachimba handaki kuizunguka, ukubwa wa kutosha vipimo viwili vya mbegu. 3318:33 Mwa 22:9Akapanga kuni, akamkata yule fahali vipande vipande na kuvipanga juu ya kuni. Kisha akawaambia, “Jazeni mapipa manne maji na kuyamwaga juu ya sadaka ya kuteketezwa na juu ya kuni.”

34Akawaambia, “Fanyeni hivyo tena.” Nao wakafanya hivyo tena.

Akaagiza, “Fanyeni kwa mara ya tatu.” Nao wakafanya hivyo kwa mara ya tatu. 35Maji yakatiririka kuizunguka madhabahu na hata kujaza lile handaki.

3618:36 Kut 29:39, 41; Yos 4:24; Hes 16:28Wakati wa kutoa dhabihu ya jioni, nabii Eliya akasogea mbele na kuomba, akisema: “Ee Bwana, Mungu wa Abrahamu, na Isaki na Israeli, ijulikane leo kwamba wewe ndiye Mungu katika Israeli na ya kwamba mimi ni mtumishi wako na nimefanya mambo haya yote kwa neno lako. 3718:37 Yos 4:24Unijibu mimi, Ee Bwana, nijibu mimi, ili watu hawa wajue kwamba wewe, Ee Bwana, ndiwe Mungu, na kwamba unaigeuza mioyo yao ikurudie tena.”

3818:38 Law 9:24; 1Nya 21:26; Ay 1:16Kisha moto wa Bwana ukashuka na kuiteketeza ile dhabihu, zile kuni, yale mawe, ule udongo, na pia kuramba yale maji yaliyokuwa ndani ya handaki.

3918:39 Law 9:24; Za 46:10Wakati watu wote walipoona hili, wakaanguka kifudifudi na kulia, “Bwana: yeye ndiye Mungu! Bwana: yeye ndiye Mungu!”

4018:40 Amu 4:7; Kut 22:20Kisha Eliya akawaamuru, “Wakamateni hao manabii wa Baali. Msimwache hata mmoja atoroke!” Wakawakamata, naye Eliya akawaleta mpaka Bonde la Kishoni na kuwachinja huko.

41Eliya akamwambia Ahabu, “Nenda, ukale na kunywa, kwa kuwa kuna sauti ya mvua kubwa.” 4218:42 Yak 5:18; Isa 5:18Hivyo Ahabu akaondoka ili kula na kunywa. Lakini Eliya akapanda kileleni mwa Karmeli, akasujudu na akaweka kichwa chake katikati ya magoti yake.

43Akamwambia mtumishi wake, “Nenda ukatazame kuelekea bahari.” Akaenda na kutazama.

Akasema, “Hakuna kitu chochote huko.”

Mara saba Eliya akasema, “Nenda tena.”

4418:44 Yos 6:15; Lk 12:54Mara ya saba, mtumishi akaleta taarifa, “Wingu dogo kama mkono wa mwanadamu linainuka kutoka baharini.”

Hivyo Eliya akasema, “Nenda ukamwambie Ahabu, ‘Tandika gari lako na ushuke kabla mvua haijakuzuia.’ ”

4518:45 Ay 37:13; Hos 1:4Wakati ule ule anga likawa jeusi kwa mawingu, upepo ukainuka na mvua kubwa ikanyesha, naye Ahabu akaenda zake Yezreeli. 4618:46 Amu 3:10; 2Fal 4:29Nguvu za Bwana zikamjia Eliya, naye akajikaza viuno, akakimbia mbele ya Ahabu njia yote hadi maingilio ya Yezreeli.

Священное Писание (Восточный перевод), версия для Таджикистана

3 Царств 18:1-46

Ильёс возвращается в Исроил

1Спустя долгое время, на третьем году засухи, к Ильёсу было слово Вечного:

– Иди и предстань перед Ахавом, и Я пошлю на землю дождь.

2И Ильёс пошёл, чтобы предстать перед Ахавом.

В Сомарии был страшный голод, 3и Ахав призвал Авдия, распорядителя его дворца.

(Авдий глубоко почитал Вечного. 4Когда Иезевель истребляла пророков Вечного, Авдий спрятал сто пророков в двух пещерах – по пятьдесят в каждой – и снабжал их пищей и водой.)

5Ахав сказал Авдию:

– Иди по стране ко всем источникам воды и рекам. Может быть, мы сможем найти траву, чтобы прокормить лошадей и мулов, и нам не придётся их убивать.

6Они поделили между собой землю, которую собирались обойти, и Ахав пошёл в одну сторону, а Авдий пошёл в другую. 7Когда Авдий был в пути, ему повстречался Ильёс. Авдий узнал его, пал лицом на землю и сказал:

– Ты ли это, мой господин Ильёс?

8– Я, – ответил тот. – Иди, скажи хозяину: «Ильёс здесь».

9– Чем я согрешил, – спросил Авдий, – что ты отдаёшь твоего раба в руки Ахава на казнь? 10Верно, как и то, что жив Вечный, твой Бог, – нет ни такого народа, ни царства, куда мой господин ни посылал бы искать тебя. И всякий раз, когда в том царстве или в народе говорили, что тебя там нет, он брал с них клятву, что они не смогли тебя отыскать. 11А теперь ты говоришь: «Пойди, скажи хозяину, что Ильёс здесь». 12Я уйду от тебя, а Дух Вечного унесёт тебя, не знаю куда. Я приду и скажу Ахаву, он тебя не найдёт и убьёт меня. А я, твой раб, чту Вечного с юности. 13Разве моему господину не рассказывали, что я сделал, когда Иезевель убивала пророков Вечного? Я спрятал сто пророков в двух пещерах, по пятьдесят в каждой, и снабжал их пищей и водой. 14А теперь ты говоришь мне пойти к моему хозяину и сказать: «Ильёс здесь». Да он меня убьёт!

15Ильёс сказал:

– Верно, как и то, что жив Вечный, Повелитель Сил, – я непременно предстану сегодня перед Ахавом.

Ильёс и пророки Баала на горе Кармил

16Авдий отправился навстречу Ахаву и всё рассказал ему. Тогда Ахав пошёл навстречу Ильёсу. 17Увидев его, он сказал:

– Это ты навёл беду на Исроил?

18– Не я навёл беду на Исроил, – ответил Ильёс, – а ты и дом твоего отца. Вы оставили повеления Вечного и пошли за статуями Баала. 19Пошли же людей и собери народ со всего Исроила ко мне на гору Кармил. И приведи четыреста пятьдесят пророков Баала и четыреста пророков Ашеры, которые едят со стола Иезевели.

20Ахав послал известить всех исроильтян и собрал пророков на гору Кармил. 21Ильёс вышел к народу и сказал:

– Сколько ещё вы будете пытаться усидеть на двух стульях? Если Вечный – это Бог, идите за Ним, а если Баал, то идите за ним.

Народ не отвечал ему ни слова. 22Тогда Ильёс сказал им:

– Из пророков Вечного остался я один, а у Баала пророков – четыреста пятьдесят человек. 23Пусть нам приведут двух быков. Затем пусть они выберут себе одного, разрежут его на куски и положат на дрова, но не поджигают их. Я подготовлю другого быка, положу его на дрова, но не подожгу их. 24И тогда вы призовёте имя вашего бога, а я призову имя Вечного. Бог, Который ответит огнём, и есть истинный Бог.

И весь народ сказал:

– Хорошо.

25Ильёс сказал пророкам Баала:

– Выберите одного из двух быков и приготовьте его первыми, раз вас так много. Призывайте имя своего бога, но не зажигайте огня.

26Они взяли быка, которого им дали, и подготовили его. Они призывали имя Баала с утра до полудня.

– Баал, ответь нам! – кричали они.

Но отклика не было, никто не отвечал. И они скакали вокруг сделанного ими жертвенника. 27В полдень Ильёс начал насмехаться над ними.

– Кричите громче! – говорил он. – Он же бог! Наверное, он задумался, или отошёл по нужде, или путешествует. А может быть, он спит, и его нужно разбудить.

28Они кричали громче и, по своему обычаю, резали себя мечами и копьями, пока не полилась кровь. 29Миновал полдень, а они продолжали неистовствовать до времени вечернего жертвоприношения18:29 То есть примерно до трёх часов пополудни (см. Исх. 29:38-41; Чис. 28:3-8).. Но ни отклика, ни ответа, ни отзыва не было. 30Тогда Ильёс сказал народу:

– Подойдите ко мне.

Они подошли к нему, и он восстановил разрушенный жертвенник Вечного. 31Ильёс взял двенадцать камней – по числу родов, произошедших от Якуба, которому Вечный сказал: «Твоё имя будет Исроил». 32Из этих камней он сложил жертвенник во имя Вечного и выкопал вокруг него ров вместимостью в пятнадцать литров18:32 Букв.: «две саты зерна».. 33Он разложил дрова, разрезал быка на части и положил его на дрова. 34Затем он сказал:

– Наполните четыре больших кувшина водой и вылейте её на жертву всесожжения и на дрова.

– Повторите, – сказал он.

И они повторили.

– Сделайте это в третий раз, – сказал он.

И они сделали это в третий раз.

35Вода лилась вокруг жертвенника и даже наполнила ров. 36Когда пришло время жертвоприношения, пророк Ильёс подошёл и сказал:

– Вечный, Бог Иброхима, Исхока и Якуба18:36 Букв.: «Исроила». Всевышний дал Якубу новое имя – Исроил (см. Нач. 32:27-28)., пусть откроется сегодня, что Ты – Бог в Исроиле, а я – Твой раб и совершил всё это по Твоему слову! 37Ответь мне, Вечный, ответь мне, чтобы этот народ узнал, что Ты, Вечный, – Бог, и что Ты вновь обращаешь их сердца.

38Тогда сошёл огонь Вечного и пожрал жертву всесожжения, дрова, камни и почву, и поглотил воду во рву. 39Увидев это, весь народ пал лицом на землю и закричал:

– Вечный есть Бог! Вечный есть Бог!

40А Ильёс приказал им:

– Схватите пророков Баала! Смотрите, чтобы ни один не скрылся!

Они схватили их, а Ильёс отвёл их к реке Кишон и там предал их смерти18:40 См. Втор. 13:1-5, 12-15; 17:2-7..

Конец засухи

41Ильёс сказал Ахаву:

– Иди, ешь и пей, потому что вот он, шум ливня!

42И Ахав пошёл есть и пить, а Ильёс поднялся на вершину Кармила, опустился на корточки и положил своё лицо между колен.

43– Пойди, посмотри в сторону моря, – сказал он слуге.

Тот пошёл и посмотрел.

– Ничего нет, – сказал он.

Семь раз Ильёс говорил: «Иди снова». 44На седьмой раз слуга сказал:

– С моря поднимается облако, размером не больше ладони.

Ильёс сказал:

– Пойди и скажи Ахаву: «Запрягай колесницу и поезжай, чтобы тебя не застал дождь».

45Тем временем небо потемнело от облаков, поднялся ветер, начался сильный ливень, и Ахав поехал в город Изреель. 46А на Ильёса сошла сила Вечного, и, заправив плащ под пояс, он бежал всю дорогу до Изрееля перед Ахавом.