2 Samweli 1 – NEN & CARST

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

2 Samweli 1:1-27

Daudi Afahamishwa Kifo Cha Sauli

11:1 1Sam 26:10; 1Nya 10:13; Yos 22:8; 1Sam 30:17; Mwa 14:7; Hes 13:29; 1Sam 11:11; 1Fal 20:29-30Baada ya kifo cha Sauli, Daudi alipokuwa amerudi kutoka kuwashinda Waamaleki, Daudi alikaa siku mbili huko Siklagi. 21:2 2Sam 4:10; Ay 2:12; Eze 27:30; 1Sam 20:41; Mwa 37:7; 37:29; 44:13; Hes 14:6; Yos 7:6; Ay 1:20; Mdo 14:14Siku ya tatu akaja mtu mwenye nguo zilizoraruka na mavumbi kichwani mwake kutoka kwenye kambi ya Sauli. Alipomjia Daudi, akajitupa chini ili kumpa heshima.

3Daudi akamuuliza, “Wewe umetoka wapi?”

Akamjibu, “Nimetoroka kutoka kambi ya Waisraeli.”

41:4 1Sam 4:16Daudi akamuuliza, “Ni nini kilichotokea? Niambie.”

Akasema, “Watu walikimbia kutoka vitani. Wengi wao walianguka na kufa. Naye Sauli na Yonathani mwanawe wamekufa.”

5Ndipo Daudi akamwambia huyo kijana aliyemletea taarifa, “Je, umefahamuje kwamba Sauli na Yonathani mwanawe wamekufa?”

61:6 1Sam 28:4; 31:2-4; 1Nya 10:1-3Yule kijana akasema, “Nilijipata huko Mlima Gilboa, naye Sauli alikuwa huko akiegemea mkuki wake, na magari ya vita na wapanda farasi wa upande wa adui wakawa wamemkaribia sana. 7Alipogeuka na kuniona, akaniita, nami nikasema, ‘Je, nifanye nini?’

81:8 1Sam 15:2; 27:8; 30:13, 17“Akaniuliza, ‘Wewe ni nani?’

“Nikamjibu, ‘Mimi ni Mwamaleki.’

91:9 Amu 9:54“Kisha akaniambia, ‘Nikaribie mimi na uniue! Niko katika maumivu makali ya kifo, lakini bado ningali hai.’

101:10 Amu 9:54; 2Fal 11:12“Kwa hiyo nikamkaribia nikamuua, kwa sababu nilijua kwamba baada ya kuanguka hangeweza kupona. Nami nikachukua lile taji lililokuwa kichwani mwake na utepe uliokuwa mkononi mwake nami nimevileta hapa kwa bwana wangu.”

111:11 Mwa 37:29; Hes 14:6; Yos 7:6; 2Sam 3:31; 13:31; Ezr 9:3; 2Nya 34:27; Yoe 2:13Ndipo Daudi pamoja na watu wote waliokuwa pamoja naye wakazishika nguo zao na kuzirarua. 12Wakaomboleza, wakalia pia na kufunga mpaka jioni kwa ajili ya Sauli na Yonathani mwanawe, kwa ajili ya jeshi la Bwana na nyumba ya Israeli, kwa sababu wameanguka kwa upanga.

131:13 1Sam 14:48Daudi akamwambia yule kijana aliyemletea taarifa, “Wewe ni mwenyeji wa wapi?”

Akamjibu, “Mimi ni mwana wa mgeni, Mwamaleki.”

141:14 1Sam 12:3; 26:9; 24:6; Hes 12:8; Za 105:15Daudi akamuuliza, “Kwa nini hukuogopa kuinua mkono wako ili kumwangamiza mpakwa mafuta wa Bwana?”

151:15 2Sam 4:10-12; Amu 8:20; 1Sam 22:17-18; 1Fal 2:25, 34, 46Kisha Daudi akamwita mmoja wa watu wake na kumwambia, “Nenda ukamuue!” Kwa hiyo akampiga, naye akafa. 161:16 Law 20:9; Mt 27; 24:25; Mdo 18:6; 1Sam 26:9; Lk 19:22Kwa maana Daudi alikuwa amemwambia, “Damu yako iwe juu ya kichwa chako mwenyewe. Kinywa chako mwenyewe kimeshuhudia dhidi yako uliposema, ‘Nilimuua mpakwa mafuta wa Bwana.’ ”

Ombolezo La Daudi Kwa Ajili Ya Sauli Na Yonathani

171:17 Mwa 50:10; Eze 32:2; 2Nya 35:25Daudi akafanya maombolezo haya kuhusu Sauli na Yonathani mwanawe, 181:18 Yos 10:13; 1Sam 31:3naye akaagiza kwamba watu wa Yuda wafundishwe ombolezo hili la upinde (ambalo limeandikwa katika Kitabu cha Yashari):

191:19 2Sam 23:8; Za 29:1; 45:3; 2Sam 3:38“Walio fahari yako, ee Israeli, wameuawa juu ya mahali pako palipoinuka.

Jinsi wenye nguvu walivyoanguka!

201:20 Mik 1:10; Yos 13:3; 1Sam 31:8; 18:6; Amu 16:23; Kut 15:20; Amu 11:34“Msilisimulie hili katika Gathi,

msilitangaze hili katika

barabara za Ashkeloni,

binti za Wafilisti wasije wakafurahia,

binti za hao wasiotahiriwa

wasije wakashangilia.

211:21 Mwa 27:28; Isa 18:4; Kum 11:17; 1Fal 8:35; 17:1; 18:1; 2Nya 6:26; Ay 36:27; 38:28; Za 65:10; 147:8; Isa 5:6; Yer 5:24; 14:4; 12:4; Eze 31:5; Isa 21:5“Enyi milima ya Gilboa,

msipate umande wala mvua,

wala mashamba yazaayo sadaka ya nafaka.

Kwa maana huko ndiko ngao ya mwenye nguvu iliponajisiwa,

ngao ya Sauli haitapakwa tena mafuta.

221:22 Isa 34:3, 7; 49:26; Kum 32:42; 1Sam 18:4Kutokana na damu ya waliouawa,

kutokana na miili ya wenye nguvu,

ule upinde wa Yonathani haukugeuka nyuma.

Upanga wa Sauli haukurudi bure.

231:23 Kum 28:49; Amu 14:18; Yer 4:13“Sauli na Yonathani,

maishani walipendwa na kuneemeka,

na katika kifo hawakutengana.

Walikuwa wepesi kuliko tai,

walikuwa na nguvu kuliko simba.

241:24 Amu 5:30“Enyi binti za Israeli,

lieni kwa ajili ya Sauli,

ambaye aliwavika nguo

nyekundu na maridadi,

ambaye aliremba mavazi yenu

kwa mapambo ya dhahabu.

25“Tazama jinsi mashujaa

walivyoanguka vitani!

Yonathani ameuawa

mahali pako palipoinuka.

261:26 Yer 22:18; 34:5; 1Sam 20:42; 18:1; 19:2; 20:17Nahuzunika kwa ajili yako,

Yonathani ndugu yangu,

kwangu ulikuwa mpendwa sana.

Upendo wako kwangu ulikuwa wa ajabu,

wa ajabu zaidi kuliko ule wa wanawake.

271:27 1Sam 2:4“Tazama jinsi mashujaa walivyoanguka!

Silaha za vita zimeangamia!”

Священное Писание (Восточный перевод), версия для Таджикистана

2 Царств 1:1-27

Довуд узнаёт о смерти Шаула

1После смерти Шаула Довуд вернулся, победив амаликитян. Он пробыл в Циклаге два дня. 2На третий день из лагеря Шаула пришёл человек в разорванной одежде, а вся его голова была в пыли1:2 Такой внешний вид был знаком глубокой скорби.. Придя к Довуду, он поклонился ему, пав лицом на землю.

3– Откуда ты пришёл? – спросил его Довуд.

– Я спасся из стана исроильтян, – ответил он.

4– Что случилось? – спросил Довуд. – Расскажи мне.

Человек сказал:

– Народ бежал с поля боя. Многие пали. И Шаул, и его сын Ионафан мертвы.

5Довуд сказал юноше, который принёс ему это известие:

– Откуда ты знаешь, что Шаул и его сын Ионафан мертвы?

6– Я случайно оказался на горе Гильбоа, – сказал юноша, – и там был Шаул, который опирался на своё копьё, а колесницы и всадники приближались к нему. 7Обернувшись назад и увидев меня, он позвал меня, и я сказал: «Что мне сделать?» 8Он спросил меня: «Кто ты?» – «Амаликитянин», – ответил я. 9Тогда он сказал мне: «Подойди и убей меня! У меня агония, но я ещё жив». 10Я подошёл и убил его, потому что знал, что после своего поражения он не сможет жить. Я взял венец, который был у него на голове, и браслет с его руки и принёс их сюда, к моему господину.

11Тогда Довуд и все, кто был с ним, разорвали на себе одежду. 12Они рыдали, плакали и постились до вечера о Шауле, о его сыне Ионафане, о войске Вечного1:12 Вечный – на языке оригинала: «Яхве». Под этим именем Всевышний открылся Мусо и народу Исроила (см. Исх. 3:13-15). См. пояснительный словарь. и об Исроиле, потому что все они пали от меча. 13Довуд сказал юноше, который принёс ему известие:

– Откуда ты?

– Я сын чужеземца, амаликитянина, – ответил он.

14Довуд сказал ему:

– Как же ты не побоялся поднять руку на помазанника Вечного?

15Довуд позвал одного из своих людей и сказал ему:

– Подойди и убей его!

И тот убил его. 16А Довуд сказал, повернувшись к амаликитянину:

– Твоя кровь на твоей голове. Ты сам свидетельствовал против себя, когда сказал: «Я убил помазанника Вечного».

Плач Довуда о Шауле и Ионафане

17Довуд оплакивал Шаула и его сына Ионафана этой горестной песней 18и приказал научить жителей Иудеи этой «Песне лука» (она записана в «Книге Праведного»1:18 Букв.: «Книга Иашара». Эта древняя книга, не вошедшая в состав Священного Писания, не сохранилась до наших времён.):

19«Слава твоя, о Исроил, сражена на твоих высотах.

Как пали могучие!

20Не объявляйте об этом в Гате,

не разглашайте на улицах Ашкелона,

чтобы не радовались дочери филистимлян,

чтобы не ликовали дочери необрезанных.

21О горы Гильбоа,

пусть не будет вам ни росы, ни дождя,

ни щедрых полей.

Ведь там осквернён был щит могучих,

щит Шаула – не натираемый больше маслом.

22Без крови сражённых,

без плоти могучих

лук Ионафана не возвращался назад,

меч Шаула не возвращался даром.

23Шаул и Ионафан –

столь любимы и чтимы при жизни,

и в смерти не разлучились.

Были они быстрее орлов,

львов сильнее.

24О дочери Исроила,

оплакивайте Шаула,

который одевал вас в роскошные алые наряды,

который украшал ваши платья золотым убранством.

25Как пали могучие в бою!

Ионафан сражён на высотах твоих, Исроил.

26Я скорблю по тебе, Ионафан, мой брат,

ты был мне очень дорог.

Твоя любовь была для меня прекрасна,

прекраснее любви женщин.

27Как пали могучие!

Погибло оружие брани!»