1 Wafalme 10 – NEN & CCB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

1 Wafalme 10:1-29

Malkia Wa Sheba Amtembelea Solomoni

(2 Nyakati 9:1-12)

110:1 2Nya 20:9; Dan 9:20Malkia wa Sheba aliposikia habari za umaarufu wa Solomoni na uhusiano wake na jina la Bwana, akaja kumjaribu kwa maswali magumu. 210:2 Ezr 9:2; Kut 34:13; Neh 13:27; Kum 30:8-10Alifika Yerusalemu akiwa na msafara mkubwa sana: pamoja na ngamia waliobeba vikolezi, kiasi kikubwa cha dhahabu na vito vya thamani; alikuja kwa Solomoni na kuzungumza naye kuhusu yote ambayo alikuwa nayo moyoni mwake. 310:3 2Fal 11:17; 2Nya 34:31; Kut 34:16; Kum 7:2-3; Ezr 9:4; Za 119:53, 120; Isa 66:2Solomoni akamjibu maswali yake yote, hakukuwa na jambo lolote lililokuwa gumu kwa mfalme asiweze kumwelezea. 410:4 1Nya 28:10; Isa 35:3-4Malkia wa Sheba alipoona hekima yote ya Solomoni na jumba la kifalme alilokuwa amejenga, 510:5 Neh 5:12; 13:25chakula kilichokuwa mezani pake, jinsi maafisa wake walivyokaa, wahudumu katika majoho yao, wanyweshaji wake na sadaka za kuteketezwa alizotoa katika hekalu la Bwana, alipatwa na mshangao.

610:6 Kum 9:18; Yn 3:7; Za 102:4Akamwambia mfalme, “Taarifa niliyosikia kwenye nchi yangu mwenyewe kuhusu mafanikio na hekima yako ni kweli. 7Lakini sikuamini mambo haya hadi nilipokuja na kuona kwa macho yangu mwenyewe. Naam, sikuambiwa hata nusu yake; katika hekima na mali umezidi sana ile taarifa niliyoisikia. 810:8 Law 27:28; Yos 6:19Heri watu wako! Heri hawa maafisa wako wasimamao mbele yako daima na kusikia hekima yako! 910:9 1Sam 12:18; Ezr 1:5Ahimidiwe Bwana Mungu wako, ambaye amependezwa sana nawe na kukuweka juu ya kiti cha ufalme cha Israeli. Kwa sababu ya upendo wake Bwana wa milele ajili ya Israeli, amekufanya mfalme, ili kudumisha haki na uadilifu.”

10Naye akampa mfalme talanta 12010:10 Talanta 120 za dhahabu ni sawa na tani 4.5. za dhahabu, kiasi kikubwa sana cha vikolezi na vito vya thamani. Haikuwahi kamwe kuletwa tena vikolezi vingi hivyo kuletwa kama vile malkia wa Sheba alivyompa Mfalme Solomoni.

1110:11 Kum 24:1; Mit 28:13; Mal 2:10-16; Yer 3:13; Isa 1:16-17; Rum 12:2(Meli za Hiramu zilileta dhahabu kutoka Ofiri; tena kutoka huko zilileta shehena kubwa ya miti ya msandali na vito vya thamani. 1210:12 Yos 6:5Mfalme akatumia miti ya msandali kuwa nguzo ya Hekalu la Bwana na kwa jumba la kifalme, pia kwa kutengeneza vinubi na zeze kwa ajili ya waimbaji. Kiasi hicho kingi cha msandali hakijawahi kuingizwa au kuonekana humo tangu siku ile.)

13Mfalme Solomoni akampa malkia wa Sheba kila kitu alichotamani na kukiomba, kando na vile mfalme alivyokuwa amempa kwa ukarimu wake wa kifalme. Kisha malkia akaondoka na kurudi katika nchi yake, yeye na watumishi wake.

Fahari Ya Solomoni

(2 Nyakati 9:13-28)

1410:14 Kum 16:18; Hes 25:4; 2Nya 30:8; 2Fal 23:26; 2Nya 28:11-13; 29:10; 30:8; Za 78:38; Isa 12:1Uzito wa dhahabu ambayo Solomoni alipokea kwa mwaka ulikuwa talanta 666,10:14 Talanta 666 za dhahabu ni sawa na tani 25. 1510:15 Neh 11:16mbali na mapato kutoka kwa wafanyabiashara na wachuuzi, na kutoka kwa wafalme wote wa Kiarabu na watawala wa nchi.

16Mfalme Solomoni akatengeneza ngao kubwa 200 kwa dhahabu iliyofuliwa; kila ngao ilikuwa na dhahabu yenye uzito wa shekeli 60010:16 Shekeli 600 za dhahabu ni sawa na kilo 3.5. 17Akatengeneza pia ngao ndogo 300 za dhahabu iliyofuliwa, kila ngao ikiwa na uzito wa mane tatu10:17 Mane tatu za dhahabu ni sawa na kilo 1.7. za dhahabu. Mfalme akaziweka katika Jumba la Kifalme la Msitu wa Lebanoni.

1810:18 Ezr 5:2; 2:2; Amu 3:6; Zek 6:1Kisha mfalme akatengeneza kiti kikubwa cha kifalme kwa kutumia pembe za ndovu na kukifunika kwa dhahabu safi. 1910:19 2Fal 10:15; Law 5:15; 6:4-6; 1Nya 29:24; 2Nya 30:8; Gal 2:9; Mit 22:26Kiti hicho kilikuwa na ngazi sita na egemeo la nyuma lilikuwa la mviringo kwa juu. Pande zote za kiti kulikuwa na mahali pa kuegemeza mikono, na simba wawili wakisimama kando ya hiyo mikono. 2010:20 1Nya 24:14Simba kumi na wawili walisimama kwenye ngazi sita, mmoja katika kila upande wa kila ngazi. Hakuna kitu kama hicho kilichokuwa kimefanyika kwenye ufalme mwingine wowote. 2110:21 1Nya 24:8Vikombe vyote vya Mfalme Solomoni vya kunywea vilikuwa vya dhahabu na vyombo vyote vya nyumbani katika Jumba la Kifalme la Msitu wa Lebanoni vilikuwa vya dhahabu safi. Hakukuwa na kitu kilichotengenezwa kwa fedha, kwa sababu fedha ilionekana ya thamani ndogo siku za Solomoni. 2210:22 1Nya 9:12Mfalme alikuwa na meli nyingi za biashara10:22 Au: za Tarshishi (ona pia 1Fal 22:48; 2Nya 9:21; 20:36; Isa 2:16; 60:9). baharini zilizokuwa zikiandamana na meli za Hiramu. Kwa mara moja kila miaka mitatu zilirudi, zikiwa zimebeba dhahabu, fedha, pembe za ndovu na nyani wakubwa na wadogo.

2310:23 Neh 8:7; 9:4Mfalme Solomoni alikuwa mkuu zaidi kwa utajiri na hekima kuliko wafalme wote wa dunia. 2410:24 Neh 3:1; 12:10Dunia yote ikatafuta kukutana na Solomoni ili kusikia hekima ambayo Mungu alikuwa ameiweka katika moyo wake. 2510:25 Ezr 3:2; 8:3; Neh 7:13Mwaka baada ya mwaka, kila mmoja ambaye alikuja alileta zawadi: vyombo vya fedha na dhahabu, majoho, silaha na vikolezi, farasi na nyumbu.

2610:26 Kum 17:16Solomoni akakusanya magari ya vita na farasi. Alikuwa na magari 1,400 na farasi 12,000, ambayo aliyaweka katika miji ya magari na mengine akawa nayo huko Yerusalemu. 2710:27 Ay 27:16; 1Nya 27:28Mfalme akafanya fedha kuwa kitu cha kawaida kama mawe huko Yerusalemu, mierezi akaifanya kuwa mingi kama mikuyu vilimani. 28Farasi wa Solomoni waliletwa kutoka Misri na kutoka Kue.10:28 Yaani Kilikia ilioko Syria. Wafanyabiashara wa mfalme waliwanunua kutoka Kue. 2910:29 Hes 13:29Waliagiza magari kutoka Misri kwa bei ya shekeli 600 za fedha10:29 Shekeli 600 za fedha ni sawa na kilo 7. na farasi kwa shekeli 150.10:29 Shekeli 150 za fedha ni sawa na kilo 1.7. Pia waliwauza nje kwa wafalme wote wa Wahiti na wa Waaramu.10:29 Waaramu hapa ina maana ya Washamu.

Chinese Contemporary Bible (Simplified)

列王纪上 10:1-29

示巴女王拜访所罗门

1示巴女王听说所罗门因耶和华而名声大震,便来用难题考问他。 2她率领许多随从,用骆驼驮着香料、宝石和大量黄金到耶路撒冷晋见所罗门王,与所罗门谈论她心中的疑问。 3所罗门王解答了她所有的问题,没有一样难得住他。 4示巴女王见所罗门智慧非凡,又看见他建的宫殿、 5席上的美味、入座的群臣、侍立一旁的仆人及其服装、酒政以及他在耶和华殿里献的燔祭,感到万分惊奇。

6她对所罗门说:“我在本国听到的有关你的功业和智慧原来都是真的。 7若不是亲眼目睹,我不会相信。事实上,我听到的还不到一半!你的智慧和财富远超过我听到的传闻。 8你的臣仆能经常侍立在你面前聆听智慧之言,真有福气! 9你的上帝耶和华当受称颂!祂喜爱你,立你为以色列的王。因为祂永远爱以色列,所以立你为王,使你秉公行义。”

10示巴女王将四吨黄金、大量香料和宝石献给所罗门王。此后,再无人像示巴女王那样献给所罗门王那么多香料。

11希兰王的船只从俄斐运来黄金、大量的檀香木和宝石。 12所罗门王用这些檀香木为耶和华的殿和王宫造栏杆,又为歌乐手制作琴瑟。此后,再没有人运来或见过这样的檀香木。

13所罗门王除了厚赠示巴女王礼物以外,还满足了她的一切要求。之后,女王和随从就回示巴去了。

所罗门的财富

14所罗门每年收到的黄金约二十三吨。 15此外,还有商人、阿拉伯诸王和国中各总督送来的贡税。 16所罗门用锤好的金子打造了二百面大盾牌,每面用七公斤金子; 17又用锤好的金子打造了三百面小盾牌,每面用三点五公斤金子,全部存放在黎巴嫩林宫。

18王又造了一个象牙宝座,外面用纯金包裹。 19这宝座有六级台阶,靠背是圆形的,两旁有扶手,扶手两边各站着一头狮子。 20六级台阶上共站着十二头狮子,每级台阶两端各站一头。这宝座举世无双。 21所罗门王所有的杯子都是金的,黎巴嫩林宫里的所有器皿都是纯金的,没有一件是用银子造的,因为所罗门年间银子不算什么。 22王有他施船队和希兰的船队一起出海,每三年就运回金银、象牙、猿猴和孔雀。

23所罗门王的财富和智慧超过天下诸王。 24天下的人都纷纷来朝见他,聆听上帝赐给他的智言慧语。 25他们年年都带来礼物,有金银器皿、衣服、兵器、香料和骡马。

26所罗门组建了战车和骑兵,有一千四百辆战车、一万二千名骑兵,驻扎在屯车城和他所在的耶路撒冷27王使耶路撒冷的金银多如石头,使香柏木多如丘陵的无花果树。 28所罗门的马匹都是由王室商队从埃及古厄按定价买来的。 29他们从埃及买来车马,每辆车六百块银子,每匹马一百五十块银子,他们也把车马卖给人诸王和亚兰诸王。