2 Samweli 1 – NEN & CCB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

2 Samweli 1:1-27

Daudi Afahamishwa Kifo Cha Sauli

11:1 1Sam 26:10; 1Nya 10:13; Yos 22:8; 1Sam 30:17; Mwa 14:7; Hes 13:29; 1Sam 11:11; 1Fal 20:29-30Baada ya kifo cha Sauli, Daudi alipokuwa amerudi kutoka kuwashinda Waamaleki, Daudi alikaa siku mbili huko Siklagi. 21:2 2Sam 4:10; Ay 2:12; Eze 27:30; 1Sam 20:41; Mwa 37:7; 37:29; 44:13; Hes 14:6; Yos 7:6; Ay 1:20; Mdo 14:14Siku ya tatu akaja mtu mwenye nguo zilizoraruka na mavumbi kichwani mwake kutoka kwenye kambi ya Sauli. Alipomjia Daudi, akajitupa chini ili kumpa heshima.

3Daudi akamuuliza, “Wewe umetoka wapi?”

Akamjibu, “Nimetoroka kutoka kambi ya Waisraeli.”

41:4 1Sam 4:16Daudi akamuuliza, “Ni nini kilichotokea? Niambie.”

Akasema, “Watu walikimbia kutoka vitani. Wengi wao walianguka na kufa. Naye Sauli na Yonathani mwanawe wamekufa.”

5Ndipo Daudi akamwambia huyo kijana aliyemletea taarifa, “Je, umefahamuje kwamba Sauli na Yonathani mwanawe wamekufa?”

61:6 1Sam 28:4; 31:2-4; 1Nya 10:1-3Yule kijana akasema, “Nilijipata huko Mlima Gilboa, naye Sauli alikuwa huko akiegemea mkuki wake, na magari ya vita na wapanda farasi wa upande wa adui wakawa wamemkaribia sana. 7Alipogeuka na kuniona, akaniita, nami nikasema, ‘Je, nifanye nini?’

81:8 1Sam 15:2; 27:8; 30:13, 17“Akaniuliza, ‘Wewe ni nani?’

“Nikamjibu, ‘Mimi ni Mwamaleki.’

91:9 Amu 9:54“Kisha akaniambia, ‘Nikaribie mimi na uniue! Niko katika maumivu makali ya kifo, lakini bado ningali hai.’

101:10 Amu 9:54; 2Fal 11:12“Kwa hiyo nikamkaribia nikamuua, kwa sababu nilijua kwamba baada ya kuanguka hangeweza kupona. Nami nikachukua lile taji lililokuwa kichwani mwake na utepe uliokuwa mkononi mwake nami nimevileta hapa kwa bwana wangu.”

111:11 Mwa 37:29; Hes 14:6; Yos 7:6; 2Sam 3:31; 13:31; Ezr 9:3; 2Nya 34:27; Yoe 2:13Ndipo Daudi pamoja na watu wote waliokuwa pamoja naye wakazishika nguo zao na kuzirarua. 12Wakaomboleza, wakalia pia na kufunga mpaka jioni kwa ajili ya Sauli na Yonathani mwanawe, kwa ajili ya jeshi la Bwana na nyumba ya Israeli, kwa sababu wameanguka kwa upanga.

131:13 1Sam 14:48Daudi akamwambia yule kijana aliyemletea taarifa, “Wewe ni mwenyeji wa wapi?”

Akamjibu, “Mimi ni mwana wa mgeni, Mwamaleki.”

141:14 1Sam 12:3; 26:9; 24:6; Hes 12:8; Za 105:15Daudi akamuuliza, “Kwa nini hukuogopa kuinua mkono wako ili kumwangamiza mpakwa mafuta wa Bwana?”

151:15 2Sam 4:10-12; Amu 8:20; 1Sam 22:17-18; 1Fal 2:25, 34, 46Kisha Daudi akamwita mmoja wa watu wake na kumwambia, “Nenda ukamuue!” Kwa hiyo akampiga, naye akafa. 161:16 Law 20:9; Mt 27; 24:25; Mdo 18:6; 1Sam 26:9; Lk 19:22Kwa maana Daudi alikuwa amemwambia, “Damu yako iwe juu ya kichwa chako mwenyewe. Kinywa chako mwenyewe kimeshuhudia dhidi yako uliposema, ‘Nilimuua mpakwa mafuta wa Bwana.’ ”

Ombolezo La Daudi Kwa Ajili Ya Sauli Na Yonathani

171:17 Mwa 50:10; Eze 32:2; 2Nya 35:25Daudi akafanya maombolezo haya kuhusu Sauli na Yonathani mwanawe, 181:18 Yos 10:13; 1Sam 31:3naye akaagiza kwamba watu wa Yuda wafundishwe ombolezo hili la upinde (ambalo limeandikwa katika Kitabu cha Yashari):

191:19 2Sam 23:8; Za 29:1; 45:3; 2Sam 3:38“Walio fahari yako, ee Israeli, wameuawa juu ya mahali pako palipoinuka.

Jinsi wenye nguvu walivyoanguka!

201:20 Mik 1:10; Yos 13:3; 1Sam 31:8; 18:6; Amu 16:23; Kut 15:20; Amu 11:34“Msilisimulie hili katika Gathi,

msilitangaze hili katika

barabara za Ashkeloni,

binti za Wafilisti wasije wakafurahia,

binti za hao wasiotahiriwa

wasije wakashangilia.

211:21 Mwa 27:28; Isa 18:4; Kum 11:17; 1Fal 8:35; 17:1; 18:1; 2Nya 6:26; Ay 36:27; 38:28; Za 65:10; 147:8; Isa 5:6; Yer 5:24; 14:4; 12:4; Eze 31:5; Isa 21:5“Enyi milima ya Gilboa,

msipate umande wala mvua,

wala mashamba yazaayo sadaka ya nafaka.

Kwa maana huko ndiko ngao ya mwenye nguvu iliponajisiwa,

ngao ya Sauli haitapakwa tena mafuta.

221:22 Isa 34:3, 7; 49:26; Kum 32:42; 1Sam 18:4Kutokana na damu ya waliouawa,

kutokana na miili ya wenye nguvu,

ule upinde wa Yonathani haukugeuka nyuma.

Upanga wa Sauli haukurudi bure.

231:23 Kum 28:49; Amu 14:18; Yer 4:13“Sauli na Yonathani,

maishani walipendwa na kuneemeka,

na katika kifo hawakutengana.

Walikuwa wepesi kuliko tai,

walikuwa na nguvu kuliko simba.

241:24 Amu 5:30“Enyi binti za Israeli,

lieni kwa ajili ya Sauli,

ambaye aliwavika nguo

nyekundu na maridadi,

ambaye aliremba mavazi yenu

kwa mapambo ya dhahabu.

25“Tazama jinsi mashujaa

walivyoanguka vitani!

Yonathani ameuawa

mahali pako palipoinuka.

261:26 Yer 22:18; 34:5; 1Sam 20:42; 18:1; 19:2; 20:17Nahuzunika kwa ajili yako,

Yonathani ndugu yangu,

kwangu ulikuwa mpendwa sana.

Upendo wako kwangu ulikuwa wa ajabu,

wa ajabu zaidi kuliko ule wa wanawake.

271:27 1Sam 2:4“Tazama jinsi mashujaa walivyoanguka!

Silaha za vita zimeangamia!”

Chinese Contemporary Bible (Simplified)

撒母耳记下 1:1-27

大卫得知扫罗的死讯

1大卫战胜了亚玛力人之后便回到洗革拉,在那里住了两天。那时扫罗已经死了。 2第三天,有一个衣服撕裂、头蒙灰尘的人从扫罗军营中跑到大卫面前,俯伏下拜。 3大卫问他:“你从哪里来?”那人答道:“我是从以色列军营逃出来的。” 4大卫说:“请告诉我那边的情况。”他说:“以色列军溃逃,伤亡惨重,扫罗和他儿子约拿单都死了!” 5大卫又问报信的青年:“你怎么知道扫罗和他儿子约拿单死了?” 6青年说:“我偶然到基利波山,看见扫罗在那里扶枪而立,敌人的战车骑兵紧紧追来。 7他回头看到我,便呼唤我。我说,‘我在这里。’ 8他问我是什么人。我告诉他我是亚玛力人。 9扫罗说他痛苦难当,却又死不掉,要我杀了他。 10我知道他身受重伤,必死无疑,就把他杀了,并取下他头上的王冠和臂上的镯子带来献给我主。”

11大卫就撕裂衣服,他的随从也撕裂衣服。 12他们因扫罗、他的儿子约拿单和耶和华的子民——以色列同胞阵亡而悲哀痛哭,禁食直到黄昏。 13大卫又问报信的青年:“你是哪里的人?”他答道:“我是寄居在以色列亚玛力人。” 14大卫说:“你怎么敢下手杀耶和华所膏立的王? 15-16你是咎由自取!因为你亲口承认自己杀了耶和华所膏立的王。”大卫随即命令一个年轻的随从杀死他,随从便杀死了他。

大卫的哀歌

17大卫作了一首挽歌哀悼扫罗和他儿子约拿单18并吩咐人教导犹大人唱这首弓歌。这首歌记在《雅煞珥书》上,歌词说:

19以色列啊,

你荣耀的王伏尸山上,

伟大的勇士竟然倒下!

20不要在迦特宣告,

不要在亚实基伦的街上传扬,

免得非利士的妇女幸灾乐祸,

免得未受割礼之人的女子欢喜雀跃。

21基利波山啊,愿你没有雨露,

你的田地不长献祭用的五谷,

因为在那里勇士的盾牌污迹斑斑,

扫罗的盾牌没有抹油。

22约拿单的弓射敌无数,

扫罗的剑不杀强敌不收回。

23扫罗约拿单深受爱戴,

生死不分离。

他们比鹰更敏捷,

比狮子还强壮。

24以色列的女子啊,

扫罗哀哭吧!

他曾使你们衣服华美,

穿金戴银。

25“勇士竟战死沙场!

约拿单竟伏尸山上!

26我的兄弟约拿单啊,

我为你悲伤,

你对我情深义重,

你对我的爱胜过女人的恋情。

27“伟大的勇士竟然倒下!

兵器竟然长埋!”