1 Samweli 27 – NEN & NUB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

1 Samweli 27:1-12

Daudi Miongoni Mwa Wafilisti

1Daudi akasema moyoni mwake, “Katika mojawapo ya siku hizi nitaangamizwa kwa mkono wa Sauli. Jambo lililo bora ni kutorokea kwenye nchi ya Wafilisti. Hivyo Sauli atakata tamaa ya kunisaka popote katika Israeli, nami nitakuwa nimeponyoka mkononi mwake.”

227:2 1Sam 30:9; 2:3; 21:10; 1Fal 2:39; 1Sam 25:13Hivyo Daudi akaondoka na hao watu mia sita waliokuwa pamoja naye na kwenda kwa Akishi mwana wa Maoki mfalme wa Gathi. 327:3 1Sam 25:43; 30:3Daudi na watu wake wakakaa huko Gathi pamoja na Akishi. Kila mtu alikuwa pamoja na jamaa yake, naye Daudi pamoja na wakeze wawili: yaani Ahinoamu wa Yezreeli, na Abigaili wa Karmeli, mjane wa Nabali. 4Sauli alipokuwa ameambiwa kwamba Daudi alikuwa amekimbilia Gathi, hakuendelea kumsaka tena.

5Ndipo Daudi akamwambia Akishi, “Kama nimepata kibali machoni pako, unipe sehemu katika mojawapo ya miji katika nchi nikae huko. Kwa nini mtumwa wako akae pamoja nawe katika mji huu wa kifalme?”

627:6 Yos 15:31; 19:5; 1Sam 30:1; 1Nya 12:30; Neh 11:28Hivyo siku hiyo Akishi akampa Daudi mji wa Siklagi, nao Siklagi umekuwa mali ya wafalme wa Yuda tangu wakati huo. 727:7 1Sam 29:3Daudi akaishi katika nchi ya Wafilisti muda wa mwaka mmoja na miezi minne.

827:8 Yos 12:5; Kut 17:14, 16; 1Sam 14:48; 30:1; 2Sam 1:8; 8:12; Mwa 16:5; Kut 15:22; Yos 13:2; Amu 1:29; Mwa 25:18Basi Daudi na watu wake wakapanda na kuwashambulia Wageshuri, Wagirizi na Waamaleki. (Tangu zamani haya mataifa yalikuwa yameishi kwenye eneo lililotanda kuanzia Telemu katika njia iteremkayo Shuri hadi kufikia nchi ya Misri.) 927:9 1Sam 15:3Kila mara Daudi aliposhambulia eneo, hakubakiza hai mwanaume wala mwanamke, lakini alichukua kondoo na ngʼombe, punda na ngamia, na nguo. Kisha akarudi kwa Akishi.

1027:10 1Sam 30:29; Amu 1:16; 1Nya 2:9, 25; Za 14:3; Mit 29:25Akishi alipomuuliza, “Je leo umeshambulia wapi?” Daudi humjibu, “Dhidi ya Negebu ya Yuda,” au wakati mwingine husema, “Dhidi ya Negebu ya Yerameeli,” au “Dhidi ya Negebu ya Wakeni.” 11Daudi hakumwacha hai mwanaume au mwanamke ili apate kuletwa Gathi, kwa maana Daudi aliwaza, “Wanaweza kujulisha habari zetu na kusema, ‘Hivi ndivyo alivyofanya Daudi.’ ” Hii ndiyo ilikuwa desturi yake wakati wote aliishi katika nchi ya Wafilisti. 1227:12 Mwa 34:30; 1Sam 29:6Akishi akamsadiki Daudi na kuwaza moyoni mwake, akasema, “Daudi amekuwa kitu cha kuchukiza kabisa kwa watu wake, Waisraeli, hivi kwamba atakuwa mtumishi wangu milele.”

Swedish Contemporary Bible

1 Samuelsboken 27:1-12

David hos filistéerna

1Men David tänkte för sig själv: ”Endera dagen får Saul tag i mig i alla fall. Det är bäst jag flyr bort till filistéerna. Då kommer Saul att ge upp och sluta jaga mig överallt i Israel och då kan jag komma utom räckhåll för honom.” 2Han tog med sig sina sexhundra män och gick till kungen i Gat, Akish, Maoks son. 3Han och hans män bosatte sig med sina familjer i Gat hos Akish. David hade med sig sina båda hustrur, Achinoam från Jisreel och Navals änka Avigajil från Karmel. 4När Saul fick reda på att David hade flytt till Gat, slutade han att jaga honom.

5En dag sa David till Akish: ”Om du ser välvilligt på mig, låt mig då få bosätta mig i någon av städerna ute på landsbygden i stället för att bo här i huvudstaden hos dig, min herre!” 6Kungen gav honom då Siklag som än i dag tillhör judakungarna 7och David bodde där bland filistéerna i ett år och fyra månader.

8David och hans män anföll och plundrade geshuréerna, girséerna och amalekiterna, folk som sedan lång tid tillbaka levde nära Shur längs vägen till Egypten. 9De lät inte en enda människa, vare sig man eller kvinna, komma undan med livet i behåll i de byar de plundrade och de tog med sig alla får, oxar, åsnor och kameler och alla kläder de kom över. Sedan återvände han till Akish. 10När Akish frågade: ”Vart gick ert plundringståg i dag?”, brukade David svara: ”Mot Judas del av Negev”, eller: ”Mot Jerachmeels”, eller: ”Mot keniternas.”27:10 Samtliga dessa ställen beboddes av Davids vänner. Se 30:27-31. 11Han lämnade ju inga överlevande kvar som kunde komma till Gat och berätta vad David egentligen hade gjort.

Så gick David till väga under hela den tid han bodde bland filistéerna. 12Och kung Akish trodde på David och tog för givet att Israels folk vid det här laget måste hata honom bittert. Därför tänkte han: ”Nu måste David stanna här och tjäna mig för alltid!”