1 Samweli 26 – NEN & NUB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

1 Samweli 26:1-25

Daudi Amwacha Sauli Hai Tena

126:1 1Sam 23:19; Za 54; 1Sam 23:24Hao Wazifu wakamwendea Sauli huko Gibea na kusema, “Je, Daudi hakujificha katika kilima cha Hakila, kinachotazamana na Yeshimoni?”

226:2 1Sam 24:2; 13:2Hivyo Sauli akashuka kwenda katika Jangwa la Zifu, akiwa na watu wake 3,000 wa Israeli waliochaguliwa, kumsaka Daudi huko. 326:3 1Sam 12:19Sauli akapiga kambi yake kando ya barabara juu ya kilima cha Hakila kinachotazamana na Yeshimoni, lakini Daudi alikuwa anaishi huko jangwani. Alipoona kuwa Sauli amemfuata huko, 4Daudi akatuma wapelelezi na akapata habari kwa hakika kwamba Sauli alikuwa amewasili.

526:5 1Sam 17:55; 14:50Ndipo Daudi akaondoka, akaenda hadi mahali Sauli alikuwa amepiga kambi. Akaona mahali Sauli na Abneri mwana wa Neri, jemadari wa jeshi, walipokuwa wamelala. Sauli alikuwa amelala ndani ya kambi, jeshi likiwa limemzunguka.

626:6 Mwa 10:15; 2Sam 2:18; 10:10; 16:9; 18:2; 19:21; 23:18; 1Nya 11:20; 19:11; 2:16; Amu 7:10-11Basi Daudi akamuuliza Ahimeleki Mhiti, na Abishai mwana wa Seruya, nduguye Yoabu, akisema, “Ni nani atakayeshuka pamoja nami kambini kwa Sauli?”

Abishai akajibu, “Nitakwenda pamoja nawe.”

7Hivyo Daudi na Abishai wakaenda kwenye jeshi wakati wa usiku, tazama Sauli, alikuwa amelala ndani ya kambi na mkuki wake umekitwa ardhini karibu na kichwa chake. Abneri na askari walikuwa wamelala kumzunguka Sauli.

826:8 1Sam 24:18Abishai akamwambia Daudi, “Leo Mungu amemtia adui yako mikononi mwako. Sasa niruhusu nimchome mpaka ardhini kwa pigo moja la mkuki wangu; sitamchoma mara mbili.”

926:9 Mwa 26:11; 1Sam 9:16; 2Sam 1:14; 19:21; Mao 4:20; 1Sam 24:5Lakini Daudi akamwambia Abishai, “Usimwangamize! Ni nani awezaye kutia mkono juu ya mpakwa mafuta wa Bwana na asiwe na hatia?” 1026:10 Mwa 16:5; 1Sam 25:38; Rum 12:19; Za 37:13; 31:6; 2Sam 1:1; Za 94:1, 2, 23; Mit 20:22; Lk 18:7; Rum 12:19; Ebr 10:30; Ufu 18:8; Kum 31:14; Ay 7:1; 14:5Daudi akasema, “Hakika kama vile Bwana aishivyo, Bwana mwenyewe atampiga; au wakati wake utafika, naye atakufa, au atakwenda vitani na kuangamia. 1126:11 Law 19:8; 1Sam 24:6, 12; Mit 24:29; Rum 12:17, 19; Yak 5:5-11; 1Pet 3:9Lakini Mungu na apishie mbali nisije nikainua mkono juu ya mpakwa mafuta wa Bwana. Sasa chukua huo mkuki na hilo gudulia la maji vilivyo karibu na kichwa chake, tuondoke.”

1226:12 Amu 4:21; Mwa 2:21; Es 6:1; Isa 29:10Hivyo Daudi akachukua huo mkuki na hilo gudulia la maji vilivyokuwa karibu na kichwa cha Sauli, nao wakaondoka. Hakuna yeyote aliyeona au kufahamu habari hii, wala hakuna hata mmoja aliyeamka usingizini. Wote walikuwa wamelala, kwa sababu Bwana alikuwa amewatia kwenye usingizi mzito.

13Kisha Daudi akavuka upande mwingine na kusimama juu ya kilima mahali palipokuwa na nafasi pana kati yao. 14Daudi akalipigia kelele jeshi na Abneri mwana wa Neri, akisema, “Je, Abneri, hutanijibu?”

Abneri akajibu, “Nani wewe umwitaye mfalme?”

15Daudi akasema, “Wewe si ni mtu shujaa? Ni nani aliye kama wewe katika Israeli? Kwa nini basi hukumlinda mfalme bwana wako? Mtu mmoja alikuja kumwangamiza mfalme, bwana wako. 16Ulichokifanya si kizuri. Kwa hakika kama aishivyo Bwana, wewe na watu wako mnastahili kufa, kwa sababu hamkumlinda bwana wenu, mpakwa mafuta wa Bwana. Tazameni hapo mlipo. Uko wapi mkuki wa mfalme na gudulia la maji ambavyo vilikuwa karibu na kichwa chake?”

1726:17 1Sam 24:16Sauli akatambua sauti ya Daudi, na kusema, “Je, hiyo ni sauti yako, Daudi mwanangu?”

Daudi akajibu, “Naam, hiyo ndiyo, bwana wangu mfalme.” 1826:18 Ay 13:23; Yer 37:18; 1Sam 24:9, 11; Za 7:3Pia akaongeza, “Kwa nini bwana wangu anamfuatia mtumishi wake? Nimefanya nini, nalo kosa langu ni lipi nililolifanya niwe na hatia? 1926:19 1Sam 24:9; 2Sam 16:11; Kum 20:16; 2Sam 14:16; 20:19; 21:3; Kum 4:28; 11:28; Za 120:5; Kut 15:17; Kum 4:20; 9:26; Za 106:4, 5; Isa 19:25Sasa mfalme bwana wangu na asikilize maneno ya mtumishi wake. Kama Bwana amekuchochea dhidi yangu, basi yeye na aipokee sadaka yangu. Lakini hata hivyo, kama ni wanadamu waliofanya hivyo, walaaniwe mbele za Bwana! Wao sasa wamenifukuza kutoka sehemu yangu katika urithi wa Bwana wangu wakisema, ‘Nenda ukatumikie miungu mingine.’ 2026:20 1Sam 24:11; 24:14; Yer 4:29; 16:16; Amo 9:3Basi usiache damu yangu imwagike kwenye ardhi mbali na uso wa Bwana. Mfalme wa Israeli ametoka kutafuta kiroboto, kama vile mtu awindavyo kware katika milima.”

2126:21 Kut 9:27; Za 72:14; 1Sam 15:24; 24:17; Hes 22:34; 1Sam 15:24; 24:17; Mt 27:4Ndipo Sauli akasema, “Nimetenda dhambi. Rudi, Daudi mwanangu. Kwa kuwa uliyahesabu maisha yangu kuwa ya thamani leo, sitajaribu kukudhuru tena. Hakika nimetenda kama mpumbavu na nimekosa sana.”

22Daudi akajibu, “Mkuki wa mfalme uko hapa. Mmoja wa vijana wako na avuke kuuchukua. 2326:23 Mwa 16:5; Rut 2:21; Za 62:12; 2Sam 22:21-25; Za 18:20-24; 1Sam 24:18; Mhu 8:12; Isa 3:10-11Bwana humlipa kila mtu kwa ajili ya haki yake na uaminifu wake. Bwana alikutia katika mikono yangu leo, lakini sikuinua mkono wangu juu ya mpakwa mafuta wa Bwana. 2426:24 Za 54:7Kwa hakika kama vile maisha yako yalivyokuwa ya thamani kwangu leo, vivyo hivyo maisha yangu na yawe na thamani kwa Bwana na kuniokoa kutoka taabu zote.”

2526:25 Rut 2:12Ndipo Sauli akamwambia Daudi, “Mwanangu Daudi na ubarikiwe; utafanya mambo makubwa na hakika utashinda.”

Basi Daudi akaenda zake, naye Sauli akarudi nyumbani.

Swedish Contemporary Bible

1 Samuelsboken 26:1-25

David skonar Saul än en gång

1Männen från Sif gick nu till Saul i Giva och berättade att David gömde sig på Hakilahöjden mitt emot Jeshimon. 2Saul drog då i väg med sina 3 000 utvalda israelitiska soldater till Siföknen för att jaga honom. 3Han slog läger på Hakilahöjden längs vägen, mitt emot Jeshimon. David som befann sig i öknen förstod att Saul hade följt efter honom.

4David sände ut spejare och fick bekräftat att Saul verkligen kommit dit. 5Sedan gav han sig i väg till Sauls läger. Där såg han var kung Saul låg och sov bredvid sin härförare Avner, Ners son, längst inne i lägret, medan soldaterna låg runt omkring honom.

6”Vem av er vill följa med mig dit in till Sauls läger?” frågade David hettiten Achimelek och Avishaj, Serujas son, Joavs26:6 Joav och Avishaj var Davids systersöner. Joav blev senare ledare för hela Israels armé. bror. ”Jag går med dig”, sa Avishaj. 7Och så gick David och Avishaj till hären på natten, där de fann Saul sovande med spjutet nerstucket i marken nära huvudet. Avner och soldaterna låg runt omkring honom.

8”Gud har nu utlämnat din fiende åt dig”, sa Avishaj till David. ”Låt mig få spetsa fast honom vid marken med mitt spjut! Jag lär inte behöva mer än ett försök.” 9”Nej!” sa David. ”Du får inte döda honom, för vem kan ostraffat angripa Herrens smorde?” 10David fortsatte: ”Så sant Herren lever, Herren kommer att slå honom: antingen dör han när hans tid är inne eller genom att han faller i strid. 11Herren förbjude att jag skulle lyfta min hand mot hans smorde! Men ta Sauls spjut som står vid hans huvud och hans vattenkruka, så går vi!” 12Och så tog David spjutet och vattenkrukan vid Sauls huvud. Sedan lämnade de lägret utan att någon sett dem. Ingen av Sauls män vaknade, för Herren lät dem sova tungt.

13När David efter en stund klättrat upp på bergssluttningen på andra sidan lägret och var på betryggande avstånd, 14ropade han mot hären och Avner, Ners son: ”Avner! Svara mig!” ”Vem är det som ropar på kungen?” frågade Avner.

15David svarade: ”Du är ju en man utan like i hela Israel. Varför vakar du då inte över din herre och kung, när någon kommer för att döda honom? 16Det är verkligen illa! Så sant Herren lever borde ni dö för att ni inte vakat över er herre, Herrens smorde. Säg mig nu, var är kungens spjut och var är vattenkrukan som stod vid hans huvud?”

17Då kände Saul igen Davids röst och ropade: ”Är det du, min son David?”

David svarade: ”Ja, herre, det är det, min herre och kung! 18Varför jagar du mig? Vad har jag gjort? Har jag gjort något ont? 19Lyssna nu på mig, din tjänare, du min herre och kung! Om det är Herren som har eggat upp dig mot mig, då tar han väl emot ett offer, men om det är människor som driver dig till det, så kommer Guds förbannelse att drabba dem. De har ju drivit mig från min arvedel i Herrens land och de har velat få mig till att tillbe andra gudar. 20Låt nu inte mitt blod utgjutas långt borta från Herrens närhet. Israels kung har ju dragit ut för att jaga en loppa som man jagar rapphöns bland bergen.”

21Då bekände Saul: ”Jag har syndat. Kom tillbaka hem, min son! Jag ska inte längre försöka skada dig, för du har räddat mitt liv i dag. Jag har gjort fel och handlat dåraktigt.”

22”Här är ditt spjut, herre”, svarade David. ”Låt en av dina unga män komma hit och hämta det! 23Herren belönar var och en efter hans rättfärdighet och trohet. Herren överlämnade dig åt mig i dag, men jag lyfte inte min hand mot Herrens smorde. 24Ditt liv var dyrbart för mig i dag, så må mitt liv på samma sätt vara dyrbart för Herren och må han rädda mig ur alla mina svårigheter!”

25Då sa Saul till David: ”Du ska vara välsignad, min son David! Du ska i framtiden utföra hjältedåd och vinna stora segrar!” Sedan gick David sin väg och Saul återvände hem.