1 Samweli 15 – NEN & CCBT

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

1 Samweli 15:1-35

Bwana Anamkataa Sauli Asiwe Mfalme

115:1 1Sam 9:16Samweli akamwambia Sauli, “Mimi ndiye ambaye Bwana alinituma nikutie mafuta uwe mfalme juu ya watu wake Israeli, basi sasa sikiliza ujumbe kutoka kwa Bwana. 215:2 Mwa 14:7; 1Sam 14:48; 2Sam 1; 8; Kut 17:8-14; Kum 25:17Hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote asemalo: ‘Nitawaadhibu Waamaleki kwa kile walichowatendea Israeli walipowavizia wakati walipanda kutoka Misri. 315:3 Mwa 14:23; Yos 6:17; 1Sam 22:17; 22:19; 27:9; 28:8; Es 3:13; 9:5; Law 27:28; Kut 20:5; Isa 14:21; Mwa 3:17; Yos 7:24Basi sasa nenda ukawashambulie Waamaleki na kuwaangamiza kabisa pamoja na kila kitu kilicho mali yao. Usiwahurumie; waue wanaume na wanawake, watoto na wanyonyao, ngʼombe na kondoo, ngamia na punda.’ ”

415:4 Yos 15:24Ndipo Sauli akawaita watu na kuwapanga huko Telaimu, askari wa miguu 200,000 pamoja na watu 10,000 kutoka Yuda. 5Sauli akaenda katika mji wa Amaleki na kuwavizia bondeni. 615:6 Mwa 15:19; Hes 24:22; Amu 1:16; 1Sam 30:29; Mwa 18:25; 19:12; Mdo 2:40; Ufu 18:4; Kut 18:10; Hes 10:29Kisha akawaambia Wakeni, “Ondokeni, waacheni Waamaleki ili nisije nikawaangamiza ninyi pamoja nao, kwa kuwa ninyi mliwatendea mema Waisraeli wote wakati walipanda kutoka Misri.” Basi Wakeni wakaondoka, wakawaacha Waamaleki.

715:7 1Sam 14:48; Mwa 16:7; 25:17-18; Kut 15:22Ndipo Sauli akawashambulia Waamaleki toka Havila mpaka Shuri, hadi mashariki ya Misri. 815:8 Kut 17:8-16; Hes 24:7; Yos 8:23; 1Fal 20:34; Es 3:1; 1Sam 30:1Akamchukua Agagi, mfalme wa Waamaleki akiwa hai, nao watu wake wote akawaangamiza kabisa kwa upanga. 915:9 Mit 15:27; 1Tim 6:10Lakini Sauli na hilo jeshi wakamhifadhi hai Agagi na kondoo na ngʼombe walio wazuri, mafahali na wana-kondoo walionona kila kitu kilichokuwa kizuri. Hivi vitu hawakuwa radhi kuviangamiza kabisa, bali kila kitu kilichodharauliwa na kilicho dhaifu wakakiangamiza kabisa.

10Kisha neno la Bwana likamjia Samweli kusema: 1115:11 Mwa 6:6; Kut 32:14; Yos 22:16; Ay 21:14; 34:27; Za 28:5; Isa 5:12; 53:6; Yer 48:10; Eze 18:24; 1Sam 8:6; Yos 22:16; 1Fal 9:6; Za 36:3; Sef 1:6; Mt 24:13“Ninasikitika kwamba nimemfanya Sauli kuwa mfalme, kwa sababu ameacha kunifuata mimi na hakutimiza maagizo yangu.” Samweli akafadhaika, naye akamlilia Bwana usiku ule wote.

1215:12 Yos 15:55; Hes 32:42Asubuhi na mapema Samweli akaamka kwenda kukutana na Sauli, lakini akaambiwa, “Sauli amekwenda Karmeli. Huko amesimamisha mnara kwa heshima yake mwenyewe naye ameendelea na kuteremkia Gilgali.”

1315:13 Mwa 14:19; Amu 17:2; Rut 3:2; Lk 8:11Samweli alipomfikia, Sauli akamwambia, “Bwana akubariki! Nimetimiza yale Bwana aliniagiza.”

14Lakini Samweli akasema, “Nini basi huu mlio wa kondoo masikioni mwangu? Huu mlio wa ngʼombe ninaousikia ni kitu gani?”

1515:15 Mwa 3:12; Mit 28:13Sauli akajibu, “Askari wamewaleta kutoka kwa Waamaleki, waliwaacha wale kondoo na ngʼombe wazuri ili kuwatoa dhabihu kwa Bwana, Mungu wako, lakini tuliwaangamiza kabisa wengine wote.”

16Samweli akamwambia Sauli, “Ngoja! Nami nitakuambia lile Bwana aliloniambia usiku huu.”

Sauli akajibu, “Niambie.”

1715:17 Kut 3:11; 1Sam 9:21Samweli akamwambia, “Ingawa zamani ulijiona mdogo machoni pako mwenyewe, Je, hukuwa kiongozi wa kabila za Israeli? Bwana alikutia mafuta kuwa mfalme juu ya Israeli. 18Naye akakutuma kwa kazi maalum, akisema, ‘Nenda ukaangamize kabisa wale watu waovu, wale Waamaleki, upigane nao vita mpaka utakapowaangamiza kabisa.’ 1915:19 Mwa 14:23; 1Sam 14:32Kwa nini hukumtii Bwana? Kwa nini ulivamia nyara na kufanya uovu machoni pa Bwana?”

2015:20 1Sam 28:18Sauli akasema, “Lakini nilimtii Bwana. Nilikamilisha ile kazi ambayo Bwana alinituma. Niliwaangamiza Waamaleki kabisa na kumleta Agagi mfalme wao. 21Askari walichukua kondoo na ngʼombe kutoka kwenye nyara, zile ambazo ni nzuri sana zimewekwa wakfu kwa Mungu, ili zitolewe dhabihu kwa Bwana Mungu wako huko Gilgali.”

2215:22 Za 40:6-8; 51:16; Mit 21:3; Isa 1:11-15; Yer 7:22; Hos 6:6; Amo 5:25; Mik 6:6-8; Mk 12:33; Mt 12:7; Ebr 10:6; Kut 19:5; Mhu 5:1; Yer 7:23; Hos 6:6; Mt 5:24; 9:13Lakini Samweli akajibu:

“Je, Bwana anafurahia sadaka za kuteketezwa na dhabihu

kama vile kuitii sauti ya Bwana?

Kutii ni bora zaidi kuliko dhabihu,

nako kusikia ni bora

kuliko mafuta ya kondoo dume.

2315:23 Kum 18:10; 1Sam 13:13Kwa maana kuasi ni kama dhambi ya uaguzi,

nao ukaidi ni kama uovu wa kuabudu sanamu.

Kwa sababu umelikataa neno la Bwana,

naye amekukataa wewe

kuendelea kuwa mfalme.”

2415:24 Kut 9:27; Hes 22:24; Za 51:4; 1Sam 13:13; Mit 29:25; Isa 51:12-13; Yer 42:11; 2Sam 12:13; Mt 27:4; Ay 31:34; Mit 29:25; Ufu 21:8Ndipo Sauli akamwambia Samweli, “Nimetenda dhambi. Nimevunja amri ya Bwana na maagizo yako. Niliwaogopa watu na kwa hiyo nikafanya walivyotaka. 2515:25 Kut 10:17Sasa ninakusihi usamehe dhambi yangu, nawe urudi pamoja nami, ili nipate kumwabudu Bwana.”

2615:26 Hes 15:31; 1Sam 13:14; 1Fal 14:10Lakini Samweli akamwambia, “Sitarudi pamoja nawe. Umelikataa neno la Bwana, naye Bwana amekukataa wewe, usiendelee kuwa mfalme juu ya Israeli!”

2715:27 1Sam 28:14; 1Fal 11:11; 14:8; 2Fal 17:21Samweli alipogeuka ili aondoke, Sauli akangʼangʼania pindo la joho lake, nalo likararuka. 2815:28 1Sam 28:17; 13:14; 2Sam 6:21; 7:15; 1Fal 11:31Samweli akamwambia, “Bwana ameurarua ufalme wa Israeli kutoka kwako leo, naye ameutia kwa mmoja wa majirani zako, aliye bora kuliko wewe. 2915:29 Tit 1:2; Hes 23:19; Ebr 7:21; 1Nya 29:11; Eze 24:14Yeye aliye Utukufu wa Israeli hasemi uongo wala hana kigeugeu; kwa kuwa yeye si mwanadamu, hata abadili nia yake.”

3015:30 Hes 22:34; Isa 29:13; Yn 12:43; 12:41-43; Rum 2:28-29Sauli akajibu, “Nimetenda dhambi. Lakini tafadhali niheshimu mbele ya wazee wa watu wangu na mbele ya Israeli; rudi pamoja nami, ili nipate kumwabudu Bwana Mungu wako.” 31Hivyo Samweli akarudi pamoja na Sauli, naye Sauli akamwabudu Bwana.

32Ndipo Samweli akasema, “Niletee Agagi mfalme wa Waamaleki.”

Agagi akaja kwake kwa ujasiri, akifikiri, “Hakika uchungu wa mauti umepita.”

3315:33 Es 9:7-10; Yer 18:21; Mwa 9:6; Kut 17:11; Amu 1:7; Yak 2:13; 1Fal 18:40Lakini Samweli akasema,

“Kama upanga wako ulivyofanya wanawake

kufiwa na watoto wao,

ndivyo mama yako atakavyokuwa

hana mtoto miongoni mwa wanawake.”

Naye Samweli akamuua Agagi mbele za Bwana huko Gilgali.

3415:34 1Sam 7:17; Amu 19:14; 1Sam 10:5; 11:4Kisha Samweli akaenda Rama, lakini Sauli akapanda nyumbani kwake huko Gibea ya Sauli. 3515:35 1Sam 19:24; 16:1; Mwa 6:6Hadi siku Samweli alipofariki hakwenda kumwona Sauli tena, ingawa Samweli alimwombolezea. Naye Bwana alihuzunika kwamba alimfanya Sauli kuwa mfalme juu ya Israeli.

Chinese Contemporary Bible (Traditional)

撒母耳記上 15:1-35

掃羅王被廢

1一天,撒母耳掃羅說:「耶和華差遣我膏立你做祂以色列子民的王,所以你要聽從祂的話。 2萬軍之耶和華說,『我要懲罰亞瑪力人,因為在以色列人離開埃及的時候,他們與以色列人為敵。 3你現在要去攻打他們,徹底消滅他們和他們擁有的一切,把男女老幼、牛羊駱駝和驢全部殺掉,一個不留。』」

4於是,掃羅提拉因召集了二十萬步兵,另有從猶大來的一萬人。 5掃羅來到亞瑪力的城池,在山谷裡埋伏起來。 6他對基尼人說:「你們離開亞瑪力人吧,免得我把你們也一起消滅,因為在以色列人離開埃及的時候,你們曾善待他們。」於是,基尼人離開了亞瑪力人。 7掃羅攻打亞瑪力人,從哈腓拉直打到埃及東面的書珥8生擒了亞瑪力亞甲,殺盡了亞瑪力人。 9掃羅和他的士兵卻留下了亞甲和那些上好的牛羊、肥壯的牛犢和羊羔及一切美物,只毀滅了那些瘦弱無用的牲畜。

10那時,耶和華對撒母耳說: 11「我後悔立掃羅為王,因為他離棄了我,不遵守我的命令。」撒母耳很難過,整夜呼求耶和華。 12第二天清早,撒母耳起來去見掃羅,有人告訴他掃羅已前往迦密山,在那裡為自己立了紀念碑,然後去了吉甲13撒母耳到了掃羅那裡後,掃羅說:「願耶和華賜福給你,我已經遵守了耶和華的命令。」 14撒母耳說:「那麼,我現在聽見的牛羊叫聲是從哪裡來的?」 15掃羅答道:「這是眾人從亞瑪力人那裡帶回來的,他們留下了這些上好的牛羊要獻給你的上帝耶和華,我們毀滅了其餘的一切。」 16撒母耳掃羅說:「住口!讓我告訴你耶和華昨天晚上對我說的話。」掃羅答道:「請說。」

17撒母耳說:「雖然你從前覺得自己微不足道,但現在卻做了以色列各支派的首領。耶和華膏立你做以色列的王。 18祂差遣你去攻打那些罪惡的亞瑪力人,命你把他們全部消滅。 19你為何不聽從祂的命令?你為何急於掠奪財物,做耶和華視為邪惡的事呢?」 20掃羅答道:「我的確服從了耶和華的命令,照著耶和華的吩咐做了。我把亞瑪力亞甲帶了回來,殺盡了其餘的亞瑪力人。 21士兵們卻從本該毀滅的戰利品中取了上好的牛羊,準備在吉甲奉獻給你的上帝耶和華。」 22撒母耳說:

「耶和華喜歡燔祭和其他祭物,

還是喜歡人們聽從祂的話?

順服勝於獻祭,

聽從耶和華勝過向祂獻上公羊的脂肪。

23叛逆不亞於行巫術的罪,

頑固不化無異於拜偶像。

你拒絕耶和華的命令,

祂也拒絕你做王。」

24掃羅撒母耳說:「我犯罪了!我違背了耶和華的命令和你的指示。我因懼怕百姓,就聽從了他們。 25現在求你赦免我的罪,跟我一起回去,我好敬拜耶和華。」 26撒母耳說:「我不會跟你回去,你既然拒絕遵行耶和華的命令,祂也拒絕你做以色列的王。」 27撒母耳轉身離去,掃羅就抓住他的衣邊,結果衣邊被撕下來了。 28撒母耳對他說:「耶和華今天已經從你身上拿走了以色列國的王位,賜給了一個比你好的人。 29以色列榮耀的上帝不說謊、也不改變心意,因為祂不是多變的世人。」 30掃羅說:「我犯了罪,但求你在以色列的長老和百姓面前尊重我,求你跟我回去,我好敬拜你的上帝耶和華。」 31於是,撒母耳掃羅一起回去,掃羅就敬拜耶和華。

32撒母耳說:「把亞瑪力亞甲帶到我這裡來。」亞甲若無其事地來到他面前,心想自己一定逃過一死了。 33撒母耳對他說:「你的刀怎樣使婦人失去兒女,你的母親也要怎樣喪去她的兒子。」於是,撒母耳就在吉甲,在耶和華面前把亞甲殺死了。

34事後,撒母耳回到拉瑪掃羅也返回基比亞自己的家。 35撒母耳一直到死沒有再見掃羅,但他為掃羅哀傷。耶和華後悔立掃羅以色列王。