2 Samweli 1 – NEN & CCBT

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

2 Samweli 1:1-27

Daudi Afahamishwa Kifo Cha Sauli

11:1 1Sam 26:10; 1Nya 10:13; Yos 22:8; 1Sam 30:17; Mwa 14:7; Hes 13:29; 1Sam 11:11; 1Fal 20:29-30Baada ya kifo cha Sauli, Daudi alipokuwa amerudi kutoka kuwashinda Waamaleki, Daudi alikaa siku mbili huko Siklagi. 21:2 2Sam 4:10; Ay 2:12; Eze 27:30; 1Sam 20:41; Mwa 37:7; 37:29; 44:13; Hes 14:6; Yos 7:6; Ay 1:20; Mdo 14:14Siku ya tatu akaja mtu mwenye nguo zilizoraruka na mavumbi kichwani mwake kutoka kwenye kambi ya Sauli. Alipomjia Daudi, akajitupa chini ili kumpa heshima.

3Daudi akamuuliza, “Wewe umetoka wapi?”

Akamjibu, “Nimetoroka kutoka kambi ya Waisraeli.”

41:4 1Sam 4:16Daudi akamuuliza, “Ni nini kilichotokea? Niambie.”

Akasema, “Watu walikimbia kutoka vitani. Wengi wao walianguka na kufa. Naye Sauli na Yonathani mwanawe wamekufa.”

5Ndipo Daudi akamwambia huyo kijana aliyemletea taarifa, “Je, umefahamuje kwamba Sauli na Yonathani mwanawe wamekufa?”

61:6 1Sam 28:4; 31:2-4; 1Nya 10:1-3Yule kijana akasema, “Nilijipata huko Mlima Gilboa, naye Sauli alikuwa huko akiegemea mkuki wake, na magari ya vita na wapanda farasi wa upande wa adui wakawa wamemkaribia sana. 7Alipogeuka na kuniona, akaniita, nami nikasema, ‘Je, nifanye nini?’

81:8 1Sam 15:2; 27:8; 30:13, 17“Akaniuliza, ‘Wewe ni nani?’

“Nikamjibu, ‘Mimi ni Mwamaleki.’

91:9 Amu 9:54“Kisha akaniambia, ‘Nikaribie mimi na uniue! Niko katika maumivu makali ya kifo, lakini bado ningali hai.’

101:10 Amu 9:54; 2Fal 11:12“Kwa hiyo nikamkaribia nikamuua, kwa sababu nilijua kwamba baada ya kuanguka hangeweza kupona. Nami nikachukua lile taji lililokuwa kichwani mwake na utepe uliokuwa mkononi mwake nami nimevileta hapa kwa bwana wangu.”

111:11 Mwa 37:29; Hes 14:6; Yos 7:6; 2Sam 3:31; 13:31; Ezr 9:3; 2Nya 34:27; Yoe 2:13Ndipo Daudi pamoja na watu wote waliokuwa pamoja naye wakazishika nguo zao na kuzirarua. 12Wakaomboleza, wakalia pia na kufunga mpaka jioni kwa ajili ya Sauli na Yonathani mwanawe, kwa ajili ya jeshi la Bwana na nyumba ya Israeli, kwa sababu wameanguka kwa upanga.

131:13 1Sam 14:48Daudi akamwambia yule kijana aliyemletea taarifa, “Wewe ni mwenyeji wa wapi?”

Akamjibu, “Mimi ni mwana wa mgeni, Mwamaleki.”

141:14 1Sam 12:3; 26:9; 24:6; Hes 12:8; Za 105:15Daudi akamuuliza, “Kwa nini hukuogopa kuinua mkono wako ili kumwangamiza mpakwa mafuta wa Bwana?”

151:15 2Sam 4:10-12; Amu 8:20; 1Sam 22:17-18; 1Fal 2:25, 34, 46Kisha Daudi akamwita mmoja wa watu wake na kumwambia, “Nenda ukamuue!” Kwa hiyo akampiga, naye akafa. 161:16 Law 20:9; Mt 27; 24:25; Mdo 18:6; 1Sam 26:9; Lk 19:22Kwa maana Daudi alikuwa amemwambia, “Damu yako iwe juu ya kichwa chako mwenyewe. Kinywa chako mwenyewe kimeshuhudia dhidi yako uliposema, ‘Nilimuua mpakwa mafuta wa Bwana.’ ”

Ombolezo La Daudi Kwa Ajili Ya Sauli Na Yonathani

171:17 Mwa 50:10; Eze 32:2; 2Nya 35:25Daudi akafanya maombolezo haya kuhusu Sauli na Yonathani mwanawe, 181:18 Yos 10:13; 1Sam 31:3naye akaagiza kwamba watu wa Yuda wafundishwe ombolezo hili la upinde (ambalo limeandikwa katika Kitabu cha Yashari):

191:19 2Sam 23:8; Za 29:1; 45:3; 2Sam 3:38“Walio fahari yako, ee Israeli, wameuawa juu ya mahali pako palipoinuka.

Jinsi wenye nguvu walivyoanguka!

201:20 Mik 1:10; Yos 13:3; 1Sam 31:8; 18:6; Amu 16:23; Kut 15:20; Amu 11:34“Msilisimulie hili katika Gathi,

msilitangaze hili katika

barabara za Ashkeloni,

binti za Wafilisti wasije wakafurahia,

binti za hao wasiotahiriwa

wasije wakashangilia.

211:21 Mwa 27:28; Isa 18:4; Kum 11:17; 1Fal 8:35; 17:1; 18:1; 2Nya 6:26; Ay 36:27; 38:28; Za 65:10; 147:8; Isa 5:6; Yer 5:24; 14:4; 12:4; Eze 31:5; Isa 21:5“Enyi milima ya Gilboa,

msipate umande wala mvua,

wala mashamba yazaayo sadaka ya nafaka.

Kwa maana huko ndiko ngao ya mwenye nguvu iliponajisiwa,

ngao ya Sauli haitapakwa tena mafuta.

221:22 Isa 34:3, 7; 49:26; Kum 32:42; 1Sam 18:4Kutokana na damu ya waliouawa,

kutokana na miili ya wenye nguvu,

ule upinde wa Yonathani haukugeuka nyuma.

Upanga wa Sauli haukurudi bure.

231:23 Kum 28:49; Amu 14:18; Yer 4:13“Sauli na Yonathani,

maishani walipendwa na kuneemeka,

na katika kifo hawakutengana.

Walikuwa wepesi kuliko tai,

walikuwa na nguvu kuliko simba.

241:24 Amu 5:30“Enyi binti za Israeli,

lieni kwa ajili ya Sauli,

ambaye aliwavika nguo

nyekundu na maridadi,

ambaye aliremba mavazi yenu

kwa mapambo ya dhahabu.

25“Tazama jinsi mashujaa

walivyoanguka vitani!

Yonathani ameuawa

mahali pako palipoinuka.

261:26 Yer 22:18; 34:5; 1Sam 20:42; 18:1; 19:2; 20:17Nahuzunika kwa ajili yako,

Yonathani ndugu yangu,

kwangu ulikuwa mpendwa sana.

Upendo wako kwangu ulikuwa wa ajabu,

wa ajabu zaidi kuliko ule wa wanawake.

271:27 1Sam 2:4“Tazama jinsi mashujaa walivyoanguka!

Silaha za vita zimeangamia!”

Chinese Contemporary Bible (Traditional)

撒母耳記下 1:1-27

大衛得知掃羅的死訊

1大衛戰勝了亞瑪力人之後便回到洗革拉,在那裡住了兩天。那時掃羅已經死了。 2第三天,有一個衣服撕裂、頭蒙灰塵的人從掃羅軍營中跑到大衛面前,俯伏下拜。 3大衛問他:「你從哪裡來?」那人答道:「我是從以色列軍營逃出來的。」 4大衛說:「請告訴我那邊的情況。」他說:「以色列軍潰逃,傷亡慘重,掃羅和他兒子約拿單都死了!」 5大衛又問報信的青年:「你怎麼知道掃羅和他兒子約拿單死了?」 6青年說:「我偶然到基利波山,看見掃羅在那裡扶槍而立,敵人的戰車騎兵緊緊追來。 7他回頭看到我,便呼喚我。我說,『我在這裡。』 8他問我是什麼人。我告訴他我是亞瑪力人。 9掃羅說他痛苦難當,卻又死不掉,要我殺了他。 10我知道他身受重傷,必死無疑,就把他殺了,並取下他頭上的王冠和臂上的鐲子帶來獻給我主。」

11大衛就撕裂衣服,他的隨從也撕裂衣服。 12他們因掃羅、他的兒子約拿單和耶和華的子民——以色列同胞陣亡而悲哀痛哭,禁食直到黃昏。 13大衛又問報信的青年:「你是哪裡的人?」他答道:「我是寄居在以色列亞瑪力人。」 14大衛說:「你怎麼敢下手殺耶和華所膏立的王? 15-16你是咎由自取!因為你親口承認自己殺了耶和華所膏立的王。」大衛隨即命令一個年輕的隨從殺死他,隨從便殺死了他。

大衛的哀歌

17大衛作了一首輓歌哀悼掃羅和他兒子約拿單18並吩咐人教導猶大人唱這首弓歌。這首歌記在《雅煞珥書》上,歌詞說:

19以色列啊,

你榮耀的王伏屍山上,

偉大的勇士竟然倒下!

20不要在迦特宣告,

不要在亞實基倫的街上傳揚,

免得非利士的婦女幸災樂禍,

免得未受割禮之人的女子歡喜雀躍。

21基利波山啊,願你沒有雨露,

你的田地不長獻祭用的五穀,

因為在那裡勇士的盾牌污跡斑斑,

掃羅的盾牌沒有抹油。

22約拿單的弓射敵無數,

掃羅的劍不殺強敵不收回。

23掃羅約拿單深受愛戴,

生死不分離。

他們比鷹更敏捷,

比獅子還強壯。

24以色列的女子啊,

掃羅哀哭吧!

他曾使你們衣服華美,

穿金戴銀。

25「勇士竟戰死沙場!

約拿單竟伏屍山上!

26我的兄弟約拿單啊,

我為你悲傷,

你對我情深義重,

你對我的愛勝過女人的戀情。

27「偉大的勇士竟然倒下!

兵器竟然長埋!」