1 Nyakati 28 – NEN & CCB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

1 Nyakati 28:1-21

Maandalizi Ya Daudi Ya Kujenga Hekalu

128:1 1Nya 11:10; 29:6; Kut 18:25; 1Nya 27:16; Yos 23:2; 24:1; 1Nya 23:2; Kum 1:15Daudi akawaita maafisa wote wa Israeli wakusanyike huko Yerusalemu: yaani, maafisa walio juu ya makabila, majemadari wa vikosi katika utumishi wa mfalme, majemadari wa maelfu na majemadari wa mamia, maafisa wanaosimamia mali zote na mifugo ya mfalme na wanawe, wakiwemo maafisa wa jumba la kifalme, mashujaa na askari wote walio hodari.

228:2 1Sam 10:7; 1Nya 17:2; Za 132:7; Isa 60:13; Ebr 2:11; Kum 17:20; 1Nya 11:1-3; Za 22:22; 2Sam 7:2; 1Fal 8:17; 2Nya 6:7-8Mfalme Daudi akainuka na kusema: “Nisikilizeni ndugu zangu nanyi watu wangu. Nilikuwa na nia ya kujenga nyumba ili iwe mahali pa kukaa Sanduku la Agano la Bwana kwa ajili ya kuwa mahali pa kuwekea miguu ya Mungu wetu, nami nikafanya maandalizi ya kuijenga. 328:3 2Sam 7:5; 1Nya 22:8; 1Fal 5:3; 1Nya 17:4Lakini Mungu akaniambia, ‘Wewe hutajenga nyumba kwa Jina langu, kwa sababu wewe umepigana vita na umemwaga damu.’

428:4 1Nya 17:23-27; 2Nya 6:6; 1Sam 16:1-13; Mwa 49:10; Hes 24:17-19“Hata hivyo, Bwana, Mungu wa Israeli, alinichagua mimi kutoka jamaa yangu yote niwe mfalme juu ya Israeli milele. Alimchagua Yuda kuwa kiongozi na kutoka nyumba ya Yuda akaichagua jamaa yangu na kutoka wana wa baba yangu ikampendeza kunifanya niwe mfalme juu ya Israeli yote. 528:5 1Nya 3:1; 2Sam 12:24; 1Nya 22:9; 14:4-7Miongoni mwa wanangu wote, naye Bwana amenipa wengi, amemchagua Solomoni mwanangu ili kukikalia kiti cha enzi cha ufalme wa Bwana juu ya Israeli. 628:6 2Sam 7:13; 1Nya 22:9-10Aliniambia, ‘Solomoni mwanao ndiye atakayejenga nyumba yangu na nyua zangu, kwa maana nimemchagua yeye kuwa mwanangu, nami nitakuwa baba yake. 728:7 1Nya 22:13; 1Fal 9:4; 11:11Nitaufanya imara ufalme wake milele kama akiendelea kuzishika amri zangu na sheria zangu, kama afanyavyo hivi leo.’

828:8 Kum 6:1; 4:1; 17:14-20“Hivyo basi ninawaagiza mbele za Israeli yote na kusanyiko hili la Bwana naye Mungu wetu akiwa anasikia: Kuweni na bidii kuzifuata amri za Bwana Mungu wenu, ili mpate kumiliki nchi hii nzuri na kuwaachia wana wenu kuwa urithi milele.

928:9 1Nya 29:19; 2Nya 6:30; Za 40:16; Yer 29:13; Kum 4:31; Yos 24:20; Za 9:10; Yer 9:24; Yn 17:3; 2Fal 20:3; Za 101:2; 1Sam 16:7; 1Fal 8:39; 1Nya 29:17; Ufu 2:23; 2Nya 15:2; Mt 7:7; Yak 4:8-10“Nawe Solomoni mwanangu, mjue Mungu wa baba yako, ukamtumikie kwa kujitoa kwa moyo wote na kwa nia ya kumkubali, kwa maana Bwana huuchunguza kila moyo na kujua kila kusudi la kila fikira. Ukimtafuta, ataonekana kwako; bali kama ukimwacha, yeye atakukataa milele. 1028:10 1Nya 22:16; Mit 4:23Angalia basi, kwa maana Bwana amekuchagua wewe ili ujenge Hekalu kuwa mahali patakatifu. Uwe hodari ukafanye kazi hiyo.”

1128:11 Kut 25:9; Ebr 8:9; 1Fal 6:2Ndipo Daudi akampa Solomoni mwanawe kielelezo kwa ajili ya ukumbi wa Hekalu, nyumba zake, vyumba vyake vya hazina, ghorofa zake, vyumba vyake vya ndani na mahali pa kufanyia upatanisho. 1228:12 1Nya 12:18; 26:12-20Akampa vielelezo vya yote Roho alikuwa ameviweka moyoni mwake kwa ajili ya kumbi za Hekalu la Bwana na vyumba vyote vilivyolizunguka, kwa ajili ya hazina za Hekalu la Mungu na kwa hazina za vitu vilivyowekwa wakfu. 13Mfalme pia akampa Solomoni maelekezo kwa ajili ya migawanyo ya huduma za makuhani na Walawi, pia kwa ajili ya kazi zote za huduma katika Hekalu la Bwana. Akampa pia maelezo kuhusu vifaa vyote vya kutumika katika huduma ya Hekalu. 14Akamwagizia uzito wa dhahabu kwa ajili ya vitu vyote vya dhahabu vya kutumika katika huduma mbalimbali, uzito wa fedha kwa ajili ya vitu vyote vya fedha vya kutumika katika huduma mbalimbali. 1528:15 Kut 25:31Uzito wa dhahabu kwa ajili ya vinara vya dhahabu na taa zake, kukiwa na uzito kwa ajili ya kila kinara na taa zake, pamoja na uzito wa fedha kwa ajili ya kila kinara cha fedha na taa zake, kulingana na matumizi ya kila kinara; 1628:16 Kut 25:23; 1Fal 7:48; 2Nya 4:8uzito wa dhahabu kwa ajili ya meza ya mikate iliyowekwa wakfu, uzito wa fedha kwa ajili ya meza ya fedha; 1728:17 Kut 27:3uzito wa dhahabu safi kwa ajili ya nyuma, mabakuli ya kunyunyizia na vikombe, masinia; uzito wa dhahabu kwa ajili ya kila bakuli la dhahabu; uzito wa fedha kwa ajili ya kila bakuli la fedha; 1828:18 Kut 30:1-10; 25:22; Eze 10:2; Za 68:17; 1Fal 6:23; Za 18:10na uzito wa dhahabu safi kwa ajili ya madhabahu ya kufukizia uvumba. Pia alimpa kielelezo kwa ajili ya gari, yaani, wale makerubi wa dhahabu waliokunjua mbawa zao na kuweka kivuli juu ya Sanduku la Agano la Bwana.

1928:19 1Fal 6:38; Kut 25:9; 25:40; 26:30Daudi akasema, “Hii yote, ninayo kwa maandishi kutoka mkononi mwa Bwana ulio juu yangu, naye amenipa ufahamu kwa ajili ya habari zote za kielelezo hiki.”

2028:20 2Nya 29:11; Hag 2:4; Kum 4:31; Yos 24:20; 1Fal 6:14; Ebr 13:5; Kum 31:7; Yos 1:5-7; 1Nya 22:13; 1Kor 16:13Daudi pia akamwambia Solomoni mwanawe, “Uwe hodari na moyo mkuu, ukafanye kazi hii. Usiogope wala usifadhaike, kwa maana Bwana aliye Mungu, Mungu wangu yu pamoja nawe. Hatakuacha wala hatakupungukia mpaka kazi hii yote kwa ajili ya utumishi wa Hekalu la Bwana itakapokamilika. 2128:21 1Nya 25:1; Kut 35:25–36:5Migawanyo ya makuhani na Walawi iko tayari kwa ajili ya kazi yote katika Hekalu la Mungu, naye kila mtu mwenye moyo wa kupenda mwenye ustadi katika aina yoyote ya ufundi atakusaidia katika kazi yote. Maafisa na watu wote watatii kila agizo lako.”

Chinese Contemporary Bible (Simplified)

历代志上 28:1-21

大卫对所罗门的嘱咐

1大卫以色列的众首领到耶路撒冷。于是,各支派的首领、各班将领、千夫长、百夫长、负责王和王子的财产及牲畜的官员、宫廷侍臣、显贵和勇士都来了, 2大卫王站起来说:“我的弟兄,我的人民啊,请听我说。我本想建造一座殿宇安放耶和华的约柜,作我们上帝的脚凳,我已准备好建造的材料。 3但上帝对我说,‘你不可为我的名建造殿宇,因为你是个战士,曾流过人的血。’ 4以色列的上帝耶和华从我父亲家中拣选我做以色列的王,直到永远。因为祂拣选了犹大支派做首领;在犹大支派中,祂拣选了我父亲家;在我父亲的众子中,祂喜悦我,立我做以色列的王。 5耶和华赐给我许多儿子,祂在我众子中拣选了所罗门,让他坐以色列的王位,治理耶和华的国。 6耶和华对我说,‘你儿子所罗门必建造我的殿宇和庭院,因为我拣选他做我的儿子,我也必做他的父亲。 7倘若他像今天一样继续坚守我的诫命和典章,我必使他的国度永远稳固。’ 8现在,当着耶和华的会众——全体以色列人的面,趁着我们的上帝在垂听,你们要谨遵你们的上帝耶和华的一切诫命,以便你们可以拥有这片佳美之地,并且把它传给你们的子孙作永远的产业。

9“我儿所罗门啊,你要认识你父亲的上帝耶和华,诚心乐意地事奉祂,因为祂洞察人心,知道人一切的心思意念。倘若你寻求祂,祂必让你寻见;倘若你背弃祂,祂必永远丢弃你。 10现在你要谨慎,因为耶和华拣选你来建造殿宇作圣所。你要坚定不移地去做。”

11大卫将殿的走廊、房舍、库房、楼房、内室和安放施恩座的圣所的图样都交给所罗门12又将心里构想的耶和华殿的院子、四周的房屋、殿的库房和圣物库房的图样都交给他。 13大卫还让他知道祭司和利未人的班次、耶和华殿里各样的工作及一切所需的器皿, 14制造各种金器银器所需金银的分量—— 15金灯台和金灯的分量,银灯台和银灯的分量——按每座灯台的用途酌定金银的分量, 16放供饼的金桌子的分量,银桌子的分量, 17纯金的叉子、碗、瓶的分量,每个金碗和银碗的分量, 18纯金香坛的分量,以及在施恩座上展开翅膀遮盖耶和华约柜的基路伯天使的样式。 19大卫说:“以上这一切都是耶和华亲手指示我的,让我明白工作的细节。”

20大卫又对儿子所罗门说:“你要坚定勇敢地去做!不要惧怕,也不要惊慌,因为我的上帝耶和华必不撇下你,也不丢弃你,祂必与你同在,直到圣殿的一切工作完毕。 21你看,在上帝殿里司职的各班祭司和利未人已准备就绪,又有各种能工巧匠乐意在各种工作上帮你,众首领和百姓都听你调遣。”