1 Nyakati 16 – NEN & NIVUK

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

1 Nyakati 16:1-43

Sanduku Lawekwa Ndani Ya Hema

116:1 2Sam 6:17-19Wakaleta Sanduku la Mungu na kuliweka ndani ya hema ambalo Daudi alikuwa amelisimamisha kwa ajili yake, na wakatoa sadaka za kuteketezwa na sadaka za amani mbele za Mungu. 216:2 Kut 39:43; Hes 6:23-27Baada ya Daudi kumaliza kutoa hizo sadaka za kuteketezwa na hizo sadaka za amani, akawabariki watu katika jina la Bwana. 3Kisha akamgawia kila Mwisraeli mwanaume na mwanamke mkate, andazi la tende na andazi la zabibu kavu.

416:4 1Nya 15:1-2Akawaweka pia baadhi ya Walawi ili wahudumu mbele ya Sanduku la Bwana kufanya maombi, kumshukuru na kumsifu Bwana, Mungu wa Israeli: 5Asafu ndiye alikuwa mkuu wao, akisaidiwa na Zekaria, Yeieli, Shemiramothi, Yehieli, Matithia, Eliabu, Benaya, Obed-Edomu na Yeieli. Hawa ndio wangepiga zeze na vinubi, Asafu angepiga matoazi, 6nao Benaya na Yahazieli makuhani, ndio wangepiga tarumbeta mara kwa mara mbele ya Sanduku la Agano la Mungu.

Zaburi Ya Daudi Ya Shukrani

(Zaburi 105:1-15; 96:1-13; 106:1, 47-48)

716:7 2Sam 23:1; Za 47:7Siku ile, kitu cha kwanza Daudi alichofanya ni kumkabidhi Asafu na wenzake zaburi hii ya shukrani kwa Bwana:

816:8 Za 107:1; 118:1; 2Fal 19:19Mshukuruni Bwana, liitieni jina lake;

wajulisheni mataifa yale aliyoyatenda.

916:9 Za 100:1; Kut 15:1; Za 7:17; 95:1-2Mwimbieni yeye, mwimbieni yeye sifa;

waambieni matendo yake yote ya ajabu.

1016:10 Za 34:3; Isa 45:25Lishangilieni jina lake takatifu;

mioyo ya wale wamtafutao Bwana na ifurahi.

1116:11 Za 27:8; Mit 8:17; Amo 5:6-14Mtafuteni Bwana na nguvu zake;

utafuteni uso wake siku zote.

1216:12 Za 78:43; 103:2Kumbuka matendo ya ajabu aliyoyafanya,

miujiza yake na hukumu alizozitamka,

13enyi wazao wa Israeli mtumishi wake,

enyi wana wa Yakobo, wateule wake.

1416:14 Isa 29:9; 4:4Yeye ndiye Bwana Mungu wetu;

hukumu zake zimo duniani pote.

15Hulikumbuka agano lake milele,

neno ambalo aliamuru, kwa vizazi elfu,

1616:16 Mwa 17:2; Neh 9:8; Ebr 6:13-18; Za 105:8-10; Mwa 15:18; 26:3agano alilolifanya na Abrahamu,

kiapo alichomwapia Isaki.

1716:17 Mwa 35:9-12Alilithibitisha kwa Yakobo kuwa amri,

kwa Israeli liwe agano la milele:

1816:18 Mwa 13:14-17“Nitakupa wewe nchi ya Kanaani

kuwa sehemu utakayoirithi.”

1916:19 Mwa 34:30; Ebr 11:13; Kum 7:7Walipokuwa wachache kwa idadi,

wachache sana na wageni ndani yake,

20walitangatanga kutoka taifa moja hadi jingine,

kutoka ufalme mmoja hadi mwingine.

2116:21 Mwa 20:3; Kut 7:15-18; Za 9:5; Mwa 12:17Hakuruhusu mtu yeyote awaonee;

kwa ajili yao aliwakemea wafalme, akisema:

2216:22 Mwa 20:7; Za 105; 15; 1Yn 2:27“Msiwaguse niliowatia mafuta;

msiwadhuru manabii wangu.”

2316:23 Za 47:1; 96:1Mwimbieni Bwana dunia yote;

tangazeni wokovu wake siku baada ya siku.

2416:24 Isa 12:4Tangazeni utukufu wake katikati ya mataifa,

matendo yake ya ajabu miongoni mwa mataifa yote.

2516:25 Za 18:3; 76:7; 89:7; Kut 18:11; Isa 40:25-26; Za 24:8Kwa kuwa Bwana ni mkuu,

mwenye kustahili kusifiwa kuliko wote;

yeye ni wa kuogopwa kuliko miungu yote.

2616:26 Law 19:4; Isa 45:20; 1Kor 8:4; Za 115:4-8; Yer 10:3Kwa maana miungu yote ya mataifa ni sanamu,

lakini Bwana aliziumba mbingu.

27Fahari na enzi viko mbele yake;

nguvu na utukufu vimo patakatifu pake.

2816:28 Za 29:1-2; 8:1Mpeni Bwana, enyi jamaa za mataifa,

mpeni Bwana utukufu na nguvu,

29mpeni Bwana utukufu

unaostahili jina lake.

Leteni sadaka na mje katika nyua zake;

mwabuduni Bwana katika uzuri wa utakatifu wake.

3016:30 Za 2:11; 33:8Dunia yote na itetemeke mbele zake!

Ulimwengu ameuweka imara; hauwezi kusogezwa.

3116:31 Isa 44:23; 35:10; 49:13; Mao 5:19; Isa 52:7; Lk 2:13; Ufu 14:2Mbingu na zishangilie, nchi na ifurahi;

semeni katikati ya mataifa, “Bwana anatawala!”

3216:32 Kut 20:11; Za 98:7; 96:10Bahari na ivume, na vyote vilivyomo ndani yake;

mashamba na yashangilie, na vyote vilivyomo ndani yake.

3316:33 Isa 14:8; 55:12; Za 110:6Kisha miti ya msituni itaimba,

itaimba kwa furaha mbele za Bwana,

kwa maana anakuja kuihukumu dunia.

3416:34 Isa 12:4; Za 25:7; Ezr 3:11; Yer 33:1Mshukuruni Bwana kwa kuwa ni mwema;

upendo wake wadumu milele.

3516:35 Kum 32:15; Mik 7:7; Ezr 3:11; Yer 33:11; Za 106:47Mlilieni, “Ee Mungu Mwokozi wetu, tuokoe.

Tukusanye tena na utukomboe kutoka kwa mataifa,

ili tuweze kulishukuru jina lako takatifu,

na kushangilia katika sifa zako.”

3616:36 Kum 27:15; 1Fal 8:15; Neh 8:6; 10:27; 2Nya 8:14; Za 72:18-19Atukuzwe Bwana, Mungu wa Israeli,

tangu milele na hata milele.

Nao watu wote wakasema, “Amen,” na “Msifuni Bwana.”

37Daudi akamwacha Asafu na wenzake mbele ya Sanduku la Agano la Bwana ili wahudumu humo mara kwa mara, kulingana na mahitaji ya kila siku. 3816:38 1Nya 13:13; 26:4-10Pia akamwacha Obed-Edomu pamoja na wenzake sitini na wanane wahudumu pamoja nao. Obed-Edomu mwana wa Yeduthuni na pia Hosa walikuwa mabawabu wa lango.

3916:39 1Sam 2:35; 1Nya 21:29; 2Sam 8:17; Yos 9:3; 1Fal 3:4Daudi akamwacha kuhani Sadoki pamoja na makuhani wenzake mbele ya hema ya ibada ya Bwana katika mahali pa juu pa kuabudia huko Gibeoni 4016:40 Kut 29:38; Hes 28:1-8ili kutoa sadaka za kuteketezwa kwa Bwana kwenye madhabahu ya sadaka ya kuteketezwa mara kwa mara, asubuhi na jioni, sawasawa na kila kitu kilichoandikwa katika sheria ya Bwana ambayo alikuwa amempa Israeli. 4116:41 1Nya 15:19; 2Nya 5:13; Yak 5:11; Ezr 3:11; Neh 9:17; Za 25:10; 33:5; Yer 33:11; Yoe 2:13; Lk 3:36Waliohudumu pamoja nao walikuwa Hemani, Yeduthuni na wale wote waliochaguliwa na kutajwa kwa jina kumpa Bwana shukrani, “Kwa maana fadhili zake zadumu milele.” 4216:42 2Nya 7:6Hemani na Yeduthuni walikuwa na wajibu wa kupiga tarumbeta, matoazi na kutumia vyombo vingine kwa ajili ya nyimbo za sifa kwa Mungu. Wana wa Yeduthuni waliwekwa langoni.

4316:43 2Sam 6:19-20; Mwa 18:19; Yos 24:15Kisha watu wote wakaondoka, kila mmoja akarudi nyumbani kwake, naye Daudi akarudi nyumbani kuibariki jamaa yake.

New International Version – UK

1 Chronicles 16:1-43

Ministering before the ark

1They brought the ark of God and set it inside the tent that David had pitched for it, and they presented burnt offerings and fellowship offerings before God. 2After David had finished sacrificing the burnt offerings and fellowship offerings, he blessed the people in the name of the Lord. 3Then he gave a loaf of bread, a cake of dates and a cake of raisins to each Israelite man and woman.

4He appointed some of the Levites to minister before the ark of the Lord, to extol,16:4 Or petition; or invoke thank, and praise the Lord, the God of Israel: 5Asaph was the chief, and next to him in rank were Zechariah, then Jaaziel,16:5 See 15:18,20; Hebrew Jeiel, possibly another name for Jaaziel. Shemiramoth, Jehiel, Mattithiah, Eliab, Benaiah, Obed-Edom and Jeiel. They were to play the lyres and harps, Asaph was to sound the cymbals, 6and Benaiah and Jahaziel the priests were to blow the trumpets regularly before the ark of the covenant of God.

7That day David first appointed Asaph and his associates to give praise to the Lord in this manner:

8Give praise to the Lord, proclaim his name;

make known among the nations what he has done.

9Sing to him, sing praise to him;

tell of all his wonderful acts.

10Glory in his holy name;

let the hearts of those who seek the Lord rejoice.

11Look to the Lord and his strength;

seek his face always.

12Remember the wonders he has done,

his miracles, and the judgments he pronounced,

13you his servants, the descendants of Israel,

his chosen ones, the children of Jacob.

14He is the Lord our God;

his judgments are in all the earth.

15He remembers16:15 Some Septuagint manuscripts (see also Psalm 105:8); Hebrew Remember his covenant for ever,

the promise he made, for a thousand generations,

16the covenant he made with Abraham,

the oath he swore to Isaac.

17He confirmed it to Jacob as a decree,

to Israel as an everlasting covenant:

18‘To you I will give the land of Canaan

as the portion you will inherit.’

19When they were but few in number,

few indeed, and strangers in it,

20they16:18-20 One Hebrew manuscript, Septuagint and Vulgate (see also Psalm 105:12); most Hebrew manuscripts inherit, / 19 though you are but few in number, / few indeed, and strangers in it.’ / 20 They wandered from nation to nation,

from one kingdom to another.

21He allowed no-one to oppress them;

for their sake he rebuked kings:

22‘Do not touch my anointed ones;

do my prophets no harm.’

23Sing to the Lord, all the earth;

proclaim his salvation day after day.

24Declare his glory among the nations,

his marvellous deeds among all peoples.

25For great is the Lord and most worthy of praise;

he is to be feared above all gods.

26For all the gods of the nations are idols,

but the Lord made the heavens.

27Splendour and majesty are before him;

strength and joy are in his dwelling-place.

28Ascribe to the Lord, all you families of nations,

ascribe to the Lord glory and strength.

29Ascribe to the Lord the glory due to his name;

bring an offering and come before him.

Worship the Lord in the splendour of his16:29 Or Lord with the splendour of holiness.

30Tremble before him, all the earth!

The world is firmly established; it cannot be moved.

31Let the heavens rejoice, let the earth be glad;

let them say among the nations, ‘The Lord reigns!’

32Let the sea resound, and all that is in it;

let the fields be jubilant, and everything in them!

33Let the trees of the forest sing,

let them sing for joy before the Lord,

for he comes to judge the earth.

34Give thanks to the Lord, for he is good;

his love endures for ever.

35Cry out, ‘Save us, God our Saviour;

gather us and deliver us from the nations,

that we may give thanks to your holy name,

and glory in your praise.’

36Praise be to the Lord, the God of Israel,

from everlasting to everlasting.

Then all the people said ‘Amen’ and ‘Praise the Lord.’

37David left Asaph and his associates before the ark of the covenant of the Lord to minister there regularly, according to each day’s requirements. 38He also left Obed-Edom and his sixty-eight associates to minister with them. Obed-Edom son of Jeduthun, and also Hosah, were gatekeepers.

39David left Zadok the priest and his fellow priests before the tabernacle of the Lord at the high place in Gibeon 40to present burnt offerings to the Lord on the altar of burnt offering regularly, morning and evening, in accordance with everything written in the Law of the Lord, which he had given Israel. 41With them were Heman and Jeduthun and the rest of those chosen and designated by name to give thanks to the Lord, ‘for his love endures for ever.’ 42Heman and Jeduthun were responsible for the sounding of the trumpets and cymbals and for the playing of the other instruments for sacred song. The sons of Jeduthun were stationed at the gate.

43Then all the people left, each for their own home, and David returned home to bless his family.