1 Nyakati 17 – NEN & NIVUK

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

1 Nyakati 17:1-27

Ahadi Ya Mungu Kwa Daudi

(2 Samweli 7:1-17)

117:1 Mdo 7:46; 1Nya 15:1Baada ya Daudi kuingia rasmi katika jumba lake la kifalme, akamwambia nabii Nathani, “Hebu tazama, mimi ninakaa kwenye nyumba nzuri iliyojengwa kwa mierezi, wakati Sanduku la Agano la Bwana liko ndani ya hema.”

217:2 1Nya 22:7; 2Nya 6:7Nathani akamjibu Daudi, “Lolote ulilo nalo moyoni mwako litende, kwa maana Mungu yu pamoja nawe.” 3Usiku ule neno la Mungu likamjia Nathani, kusema:

417:4 1Nya 28:3“Nenda ukamwambie mtumishi wangu Daudi, ‘Hili ndilo asemalo Bwana: Wewe hutanijengea mimi nyumba ili nikae humo. 517:5 2Sam 6:21; Kut 40:2; 1Fal 8:4, 16Mimi sijakaa ndani ya nyumba tangu siku ile niliyowatoa Israeli kutoka Misri mpaka leo. Nimehama kutoka hema moja hadi jingine na kutoka mahali pamoja hadi pengine. 6Je, popote nilipokwenda pamoja na Waisraeli wote, wakati wowote nilimwambia kiongozi yeyote niliyemwagiza kuwachunga watu wangu, kwa nini hujanijengea nyumba ya mierezi?’ 

717:7 2Sam 6:21“Sasa basi, mwambie mtumishi wangu Daudi, ‘Hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote: Nilikuchukua machungani na kutoka kuandama kondoo ili uwatawale watu wangu Israeli. 8Nimekuwa pamoja nawe popote ulipokwenda, nami nimekuondolea mbali adui zako wote mbele yako. Basi nitalifanya jina lako kuwa kuu kama majina ya watu walio wakuu sana duniani. 917:9 2Nya 15:2; Isa 49:17; Yer 31:12; Eze 34:14Nami nitawapatia watu wangu Israeli mahali na nitawapa ili wawe na mahali pao wenyewe pa kuishi na wasisumbuliwe tena. Watu waovu hawatawaonea tena, kama walivyofanya mwanzoni, 1017:10 Amu 2:16na ambavyo wamefanya siku zote tangu nilipowachagua viongozi kwa ajili ya watu wangu Israeli. Pia nitawatiisha adui zenu wote.

“ ‘Pamoja na hayo ninakuambia kwamba Bwana atakujengea nyumba: 11Wakati wako utakapokuwa umekwisha, nawe ukawa umekwenda kukaa na baba zako, nitamwinua mzao wako aingie mahali pako kuwa mfalme, mmoja wa wana wako mwenyewe, nami nitaufanya imara ufalme wake. 1217:12 1Fal 5:5; 2Nya 7:18; 13:5Yeye ndiye atakayejenga nyumba kwa ajili yangu, nami nitakifanya imara kiti cha ufalme wake milele. 1317:13 2Kor 6:18; 2Sam 7:14-15; Ebr 1:5; Lk 1:32; 1Nya 28:6; 22:10Mimi nitakuwa baba yake, naye atakuwa mwanangu. Kamwe sitaondoa upendo wangu kwake, kama nilivyouondoa kwa yeye aliyekutangulia. 1417:14 1Fal 2:12; 2Nya 9:8; Za 132:11; Yer 33:17; Za 2:6; 89:36; Isa 9:7; Eze 37:25; Dan 2:44; 7:14-27; Mt 21:1-11; Lk 1:33; Ebr 1:8Nitamweka juu ya nyumba yangu na ufalme wangu milele; kiti chake cha enzi nitakifanya imara milele.’ ”

15Nathani akamwarifu Daudi maneno yote ya maono haya.

Maombi Ya Daudi

(2 Samweli 7:18-29)

1617:16 2Sam 7:18; 2Fal 19:14; Ay 7:14-17; Mwa 32:10; Za 144:3Ndipo Mfalme Daudi akaingia ndani, akaketi mbele za Bwana, akasema:

“Mimi ni nani, Ee Bwana Mungu, na jamaa yangu ni nini, hata umenileta mpaka hapa nilipo? 17Kana kwamba hili halitoshi machoni pako, Ee Mungu, umenena pia kuhusu siku zijazo za nyumba ya mtumishi wako. Umeniangalia kama mtu aliyetukuka kuliko watu wote, Ee Bwana Mungu.

1817:18 Za 139:1; Yn 21:17“Daudi aweza kukuambia nini zaidi kuhusu kumheshimu mtumishi wako? Kwa maana wewe unamjua mtumishi wako, 1917:19 2Sam 7:16-17, 25; 2Fal 20:6; Mt 11:26; Efe 1:11Ee Bwana Mungu. Kwa ajili ya mtumishi wako, tena sawasawa na mapenzi yako, umefanya jambo hili kubwa sana na kujulisha ahadi hizi zote zilizo kubwa sana.

2017:20 Kut 8:10; Kum 3:24; Isa 44:6; Kut 15:11; Kum 33:26; 1Sam 2:2; 2Sam 7:22; Za 86:8“Hakuna aliye kama wewe, Ee Bwana Mungu, wala hakuna Mungu ila wewe, kama vile tulivyosikia kwa masikio yetu wenyewe. 2117:21 Kut 6:6Naye ni nani aliye kama watu wako Israeli: taifa pekee duniani ambalo Mungu wake alitoka kwenda kulikomboa kwa ajili yake mwenyewe na kujifanyia jina kwa ajili yake mwenyewe, kwa kufanya maajabu makubwa na ya kutisha kwa kuwafukuza mataifa mbele ya watu wako, ambao uliwakomboa kutoka Misri? 2217:22 Kut 19:5-6Uliwafanya watu wako Israeli kuwa watu wako wewe mwenyewe milele, nawe, Ee Bwana Mungu, umekuwa Mungu wao.

2317:23 1Fal 8:25“Sasa basi, Bwana ahadi uliyoweka kuhusu mtumishi wako na nyumba yake na uithibitishe milele. Fanya kama ulivyoahidi, 2417:24 2Nya 6:33; Yn 12:28; Za 21:13; 72:19; Mt 6:9, 13ili ithibitike na jina lako litakuwa kuu milele. Kisha watu watasema, ‘Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote, Mungu aliye juu ya Israeli, ndiye Mungu wa Israeli.’ Nayo nyumba ya mtumishi wako Daudi itafanywa imara mbele zako.

25“Wewe, Mungu wangu, umemfunulia mtumishi wako Daudi kwamba utamjengea yeye nyumba. Hivyo mtumishi wako amekuwa na ujasiri wa kukuomba maombi haya. 2617:26 Kut 34:6; Ebr 6:18Ee Bwana, wewe ndiwe Mungu! Umemwahidi mtumishi wako mambo haya mazuri. 2717:27 Za 16:11; 21:6; Rum 11:29; Mwa 27:33; Za 72:17Basi imekupendeza kuibariki nyumba ya mtumishi wako, ili idumu milele machoni pako; kwa ajili yako, Ee Bwana, umeibariki, nayo itabarikiwa milele.”

New International Version – UK

1 Chronicles 17:1-27

God’s promise to David

1After David was settled in his palace, he said to Nathan the prophet, ‘Here I am, living in a house of cedar, while the ark of the covenant of the Lord is under a tent.’

2Nathan replied to David, ‘Whatever you have in mind, do it, for God is with you.’

3But that night the word of God came to Nathan, saying:

4‘Go and tell my servant David, “This is what the Lord says: you are not the one to build me a house to dwell in. 5I have not dwelt in a house from the day I brought Israel up out of Egypt to this day. I have moved from one tent site to another, from one dwelling-place to another. 6Wherever I have moved with all the Israelites, did I ever say to any of their leaders17:6 Traditionally judges; also in verse 10 whom I commanded to shepherd my people, ‘Why have you not built me a house of cedar?’ ”

7‘Now then, tell my servant David, “This is what the Lord Almighty says: I took you from the pasture, from tending the flock, and appointed you ruler over my people Israel. 8I have been with you wherever you have gone, and I have cut off all your enemies from before you. Now I will make your name like the names of the greatest men on earth. 9And I will provide a place for my people Israel and will plant them so that they can have a home of their own and no longer be disturbed. Wicked people will not oppress them anymore, as they did at the beginning 10and have done ever since the time I appointed leaders over my people Israel. I will also subdue all your enemies.

‘ “I declare to you that the Lord will build a house for you: 11when your days are over and you go to be with your ancestors, I will raise up your offspring to succeed you, one of your own sons, and I will establish his kingdom. 12He is the one who will build a house for me, and I will establish his throne for ever. 13I will be his father, and he will be my son. I will never take my love away from him, as I took it away from your predecessor. 14I will set him over my house and my kingdom for ever; his throne will be established for ever.” ’

15Nathan reported to David all the words of this entire revelation.

David’s prayer

16Then King David went in and sat before the Lord, and he said:

‘Who am I, Lord God, and what is my family, that you have brought me this far? 17And as if this were not enough in your sight, my God, you have spoken about the future of the house of your servant. You, Lord God, have looked on me as though I were the most exalted of men.

18‘What more can David say to you for honouring your servant? For you know your servant, 19Lord. For the sake of your servant and according to your will, you have done this great thing and made known all these great promises.

20‘There is no-one like you, Lord, and there is no God but you, as we have heard with our own ears. 21And who is like your people Israel – the one nation on earth whose God went out to redeem a people for himself, and to make a name for yourself, and to perform great and awesome wonders by driving out nations from before your people, whom you redeemed from Egypt? 22You made your people Israel your very own for ever, and you, Lord, have become their God.

23‘And now, Lord, let the promise you have made concerning your servant and his house be established for ever. Do as you promised, 24so that it will be established and that your name will be great for ever. Then people will say, “The Lord Almighty, the God over Israel, is Israel’s God!” And the house of your servant David will be established before you.

25‘You, my God, have revealed to your servant that you will build a house for him. So your servant has found courage to pray to you. 26You, Lord, are God! You have promised these good things to your servant. 27Now you have been pleased to bless the house of your servant, that it may continue for ever in your sight; for you, Lord, have blessed it, and it will be blessed for ever.’