1 Nyakati 16 – NEN & BPH

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

1 Nyakati 16:1-43

Sanduku Lawekwa Ndani Ya Hema

116:1 2Sam 6:17-19Wakaleta Sanduku la Mungu na kuliweka ndani ya hema ambalo Daudi alikuwa amelisimamisha kwa ajili yake, na wakatoa sadaka za kuteketezwa na sadaka za amani mbele za Mungu. 216:2 Kut 39:43; Hes 6:23-27Baada ya Daudi kumaliza kutoa hizo sadaka za kuteketezwa na hizo sadaka za amani, akawabariki watu katika jina la Bwana. 3Kisha akamgawia kila Mwisraeli mwanaume na mwanamke mkate, andazi la tende na andazi la zabibu kavu.

416:4 1Nya 15:1-2Akawaweka pia baadhi ya Walawi ili wahudumu mbele ya Sanduku la Bwana kufanya maombi, kumshukuru na kumsifu Bwana, Mungu wa Israeli: 5Asafu ndiye alikuwa mkuu wao, akisaidiwa na Zekaria, Yeieli, Shemiramothi, Yehieli, Matithia, Eliabu, Benaya, Obed-Edomu na Yeieli. Hawa ndio wangepiga zeze na vinubi, Asafu angepiga matoazi, 6nao Benaya na Yahazieli makuhani, ndio wangepiga tarumbeta mara kwa mara mbele ya Sanduku la Agano la Mungu.

Zaburi Ya Daudi Ya Shukrani

(Zaburi 105:1-15; 96:1-13; 106:1, 47-48)

716:7 2Sam 23:1; Za 47:7Siku ile, kitu cha kwanza Daudi alichofanya ni kumkabidhi Asafu na wenzake zaburi hii ya shukrani kwa Bwana:

816:8 Za 107:1; 118:1; 2Fal 19:19Mshukuruni Bwana, liitieni jina lake;

wajulisheni mataifa yale aliyoyatenda.

916:9 Za 100:1; Kut 15:1; Za 7:17; 95:1-2Mwimbieni yeye, mwimbieni yeye sifa;

waambieni matendo yake yote ya ajabu.

1016:10 Za 34:3; Isa 45:25Lishangilieni jina lake takatifu;

mioyo ya wale wamtafutao Bwana na ifurahi.

1116:11 Za 27:8; Mit 8:17; Amo 5:6-14Mtafuteni Bwana na nguvu zake;

utafuteni uso wake siku zote.

1216:12 Za 78:43; 103:2Kumbuka matendo ya ajabu aliyoyafanya,

miujiza yake na hukumu alizozitamka,

13enyi wazao wa Israeli mtumishi wake,

enyi wana wa Yakobo, wateule wake.

1416:14 Isa 29:9; 4:4Yeye ndiye Bwana Mungu wetu;

hukumu zake zimo duniani pote.

15Hulikumbuka agano lake milele,

neno ambalo aliamuru, kwa vizazi elfu,

1616:16 Mwa 17:2; Neh 9:8; Ebr 6:13-18; Za 105:8-10; Mwa 15:18; 26:3agano alilolifanya na Abrahamu,

kiapo alichomwapia Isaki.

1716:17 Mwa 35:9-12Alilithibitisha kwa Yakobo kuwa amri,

kwa Israeli liwe agano la milele:

1816:18 Mwa 13:14-17“Nitakupa wewe nchi ya Kanaani

kuwa sehemu utakayoirithi.”

1916:19 Mwa 34:30; Ebr 11:13; Kum 7:7Walipokuwa wachache kwa idadi,

wachache sana na wageni ndani yake,

20walitangatanga kutoka taifa moja hadi jingine,

kutoka ufalme mmoja hadi mwingine.

2116:21 Mwa 20:3; Kut 7:15-18; Za 9:5; Mwa 12:17Hakuruhusu mtu yeyote awaonee;

kwa ajili yao aliwakemea wafalme, akisema:

2216:22 Mwa 20:7; Za 105; 15; 1Yn 2:27“Msiwaguse niliowatia mafuta;

msiwadhuru manabii wangu.”

2316:23 Za 47:1; 96:1Mwimbieni Bwana dunia yote;

tangazeni wokovu wake siku baada ya siku.

2416:24 Isa 12:4Tangazeni utukufu wake katikati ya mataifa,

matendo yake ya ajabu miongoni mwa mataifa yote.

2516:25 Za 18:3; 76:7; 89:7; Kut 18:11; Isa 40:25-26; Za 24:8Kwa kuwa Bwana ni mkuu,

mwenye kustahili kusifiwa kuliko wote;

yeye ni wa kuogopwa kuliko miungu yote.

2616:26 Law 19:4; Isa 45:20; 1Kor 8:4; Za 115:4-8; Yer 10:3Kwa maana miungu yote ya mataifa ni sanamu,

lakini Bwana aliziumba mbingu.

27Fahari na enzi viko mbele yake;

nguvu na utukufu vimo patakatifu pake.

2816:28 Za 29:1-2; 8:1Mpeni Bwana, enyi jamaa za mataifa,

mpeni Bwana utukufu na nguvu,

29mpeni Bwana utukufu

unaostahili jina lake.

Leteni sadaka na mje katika nyua zake;

mwabuduni Bwana katika uzuri wa utakatifu wake.

3016:30 Za 2:11; 33:8Dunia yote na itetemeke mbele zake!

Ulimwengu ameuweka imara; hauwezi kusogezwa.

3116:31 Isa 44:23; 35:10; 49:13; Mao 5:19; Isa 52:7; Lk 2:13; Ufu 14:2Mbingu na zishangilie, nchi na ifurahi;

semeni katikati ya mataifa, “Bwana anatawala!”

3216:32 Kut 20:11; Za 98:7; 96:10Bahari na ivume, na vyote vilivyomo ndani yake;

mashamba na yashangilie, na vyote vilivyomo ndani yake.

3316:33 Isa 14:8; 55:12; Za 110:6Kisha miti ya msituni itaimba,

itaimba kwa furaha mbele za Bwana,

kwa maana anakuja kuihukumu dunia.

3416:34 Isa 12:4; Za 25:7; Ezr 3:11; Yer 33:1Mshukuruni Bwana kwa kuwa ni mwema;

upendo wake wadumu milele.

3516:35 Kum 32:15; Mik 7:7; Ezr 3:11; Yer 33:11; Za 106:47Mlilieni, “Ee Mungu Mwokozi wetu, tuokoe.

Tukusanye tena na utukomboe kutoka kwa mataifa,

ili tuweze kulishukuru jina lako takatifu,

na kushangilia katika sifa zako.”

3616:36 Kum 27:15; 1Fal 8:15; Neh 8:6; 10:27; 2Nya 8:14; Za 72:18-19Atukuzwe Bwana, Mungu wa Israeli,

tangu milele na hata milele.

Nao watu wote wakasema, “Amen,” na “Msifuni Bwana.”

37Daudi akamwacha Asafu na wenzake mbele ya Sanduku la Agano la Bwana ili wahudumu humo mara kwa mara, kulingana na mahitaji ya kila siku. 3816:38 1Nya 13:13; 26:4-10Pia akamwacha Obed-Edomu pamoja na wenzake sitini na wanane wahudumu pamoja nao. Obed-Edomu mwana wa Yeduthuni na pia Hosa walikuwa mabawabu wa lango.

3916:39 1Sam 2:35; 1Nya 21:29; 2Sam 8:17; Yos 9:3; 1Fal 3:4Daudi akamwacha kuhani Sadoki pamoja na makuhani wenzake mbele ya hema ya ibada ya Bwana katika mahali pa juu pa kuabudia huko Gibeoni 4016:40 Kut 29:38; Hes 28:1-8ili kutoa sadaka za kuteketezwa kwa Bwana kwenye madhabahu ya sadaka ya kuteketezwa mara kwa mara, asubuhi na jioni, sawasawa na kila kitu kilichoandikwa katika sheria ya Bwana ambayo alikuwa amempa Israeli. 4116:41 1Nya 15:19; 2Nya 5:13; Yak 5:11; Ezr 3:11; Neh 9:17; Za 25:10; 33:5; Yer 33:11; Yoe 2:13; Lk 3:36Waliohudumu pamoja nao walikuwa Hemani, Yeduthuni na wale wote waliochaguliwa na kutajwa kwa jina kumpa Bwana shukrani, “Kwa maana fadhili zake zadumu milele.” 4216:42 2Nya 7:6Hemani na Yeduthuni walikuwa na wajibu wa kupiga tarumbeta, matoazi na kutumia vyombo vingine kwa ajili ya nyimbo za sifa kwa Mungu. Wana wa Yeduthuni waliwekwa langoni.

4316:43 2Sam 6:19-20; Mwa 18:19; Yos 24:15Kisha watu wote wakaondoka, kila mmoja akarudi nyumbani kwake, naye Daudi akarudi nyumbani kuibariki jamaa yake.

Bibelen på hverdagsdansk

1. Krønikebog 16:1-43

1Guds Ark blev anbragt i det telt, som David havde ladet indrette til den. Derefter ofrede man brændofre og takofre til Gud, 2og David velsignede folket i Herrens navn. 3Så gav han hver af de tilstedeværende, både mænd og kvinder, en gave bestående af et brød, en daddelkage og en rosinkage.

David etablerer lovsang til Herren

4David udpegede nogle af levitterne til at stå foran Herrens Ark og takke og lovprise Israels Gud. 5Asaf ledte lovsangen og spillede på bækken. Zekarja, Ja’aziel, Shemiramot, Jehiel, Mattija, Eliab, Benaja, Obed-Edom og Jeiel spillede på harpe og lyre, 6mens præsterne Benaja og Jahaziel blæste trompet foran Guds Pagts Ark.

7David gav fra den dag af Asaf og hans medhjælpere16,7 Teksten siger ikke, hvem der har skrevet følgende sang. Det kan være David eller Asaf, eller måske var sangen allerede kendt. ansvaret for at synge lovsange til Herren. De sang følgende sang:

8Sig tak til Herren og giv ham ære!

Forkynd hans undere for alle folkeslag!

9Syng og spil til hans ære,

tænk på alle de mirakler, han har udført.

10Glæd jer over hans herlighed.

Lad alle, der kender ham, fryde sig!

11Søg hjælp hos Herren og hans styrke,

hold jer altid nær til ham.

12Tænk på de fantastiske ting, han har gjort,

alle de undere, han har udført.

13I er jo børn af Guds tjener, Abraham,

I er de udvalgte efterkommere af Jakob.

14Han er Herren, vor Gud,

han hersker over hele jorden.

15Han holder altid sine løfter,

er trofast gennem tusind generationer.

16Han står bag sin pagt med Abraham,

det løfte han højtideligt afgav til Isak.

17Han bekræftede den over for Jakob

som en vedvarende pagt med Israels folk:

18„Jeg giver jer Kana’ans land,

det skal være jeres særlige ejendom.”

19Det sagde han, da de endnu var få,

en lille flok fremmede i Kana’ans land.

20De vandrede fra land til land,

fra det ene rige til det andet.

21Men han tillod ingen at skade dem,

han advarede konger om at holde sig væk.

22„Rør ikke mine udvalgte,

gør ikke mine profeter fortræd!”

23Lad hele jorden synge for Herren,

fortæl om hans frelse hver eneste dag.

24Lad alle folk høre om hans vældige undere,

fortæl om de forunderlige ting, han har gjort.

25For Herren er stor, og æren er hans,

ingen andre guder er værd at tilbede.

26Andre folks guder er falske guder,

men Herren har skabt både himlen og jorden.

27Han udstråler kongelig værdighed,

styrke og glæde kommer fra ham.

28Pris Herren, alle verdens folk,

erkend hans herlighed og magt.

29Giv Herren den ære, der tilkommer ham,

bring jeres gaver og træd frem for ham.

Tilbed Herren i helligt skrud,

30bøj knæ for ham, alle jordens folk.

Han skabte jorden på et sikkert fundament,

31lad himlen glæde sig og jorden juble.

Udråb blandt folkene:

„Herren har bevist, han er konge!”

32Lad havene bruse i lovprisning,

lad marken med sin afgrøde juble,

33lad lovsangen suse i skovens træer,

for Herren kommer for at dømme jorden.

34Tak Herren, for han er god.

Hans trofasthed varer til evig tid.

35Frels os, vor Gud!

Bring os tilbage fra landflygtigheden,

så vi kan give dig taknemmelighedsofre

og lovprise dit hellige navn.

36Lovet være Herren, Israels Gud.

Lad os prise ham nu og til evig tid.

Hele folket råbte „Amen” og lovpriste Herren.

37David indsatte således Asaf og hans levitiske medhjælpere til dagligt at synge og spille lovsange foran Herrens Pagts Ark. 38De blev assisteret af Obed-Edom, Jedutuns søn, og 68 levitter fra hans slægt. Obed-Edom fik også ansvaret for at holde vagt ved teltet sammen med Hosa.

39Ofringerne i den gamle helligdom på højen ved Gibeon fortsatte som hidtil. David udvalgte præsten Zadok og en gruppe af de øvrige præster til at stå for ofringerne der. 40Hver morgen og aften skulle de ofre brændofre for Herren på det alter, som var indviet til formålet, og i det hele taget nøje følge alle de forskrifter, som Herren havde pålagt Israels folk, og som var nedskrevet i lovbogen. 41Desuden blev Heman, Jedutun og flere andre udvalgt til at tage sig af lovsangstjenesten dér og synge om Herrens evige trofasthed. 42Med deres trompeter, bækkener og øvrige musikinstrumenter akkompagnerede de lovsangen til Gud. Jedutuns sønner og slægtninge skulle holde vagt.

43Da højtideligheden var overstået og folket gået hver til sit, gik David hjem for at velsigne sin familie.