1 Nyakati 15 – NEN & CCBT

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

1 Nyakati 15:1-29

Sanduku La Agano Laletwa Yerusalemu

(2 Samweli 6:12-22)

115:1 Za 132:1-5; 2Sam 6:17; 1Nya 17:1-5; Mdo 7:46Baada ya Daudi kujijengea nyumba zake katika Mji wa Daudi, akatengeneza sehemu kwa ajili ya Sanduku la Mungu, kisha akasimamisha hema kwa ajili yake. 215:2 Hes 3:6; Kum 31:9, 25; 2Nya 29:11; Hes 4:2, 15; Kum 10:5; Yos 3:3Kisha Daudi akasema, “Hakuna mtu yeyote anayeruhusiwa kulibeba Sanduku la Mungu isipokuwa Walawi peke yao, kwa sababu Bwana aliwachagua kulibeba Sanduku la Bwana na kuhudumu mbele zake milele.”

315:3 1Nya 13:5; 1Fal 8:1Daudi akawakusanya Israeli wote huko Yerusalemu ili kulipandisha Sanduku la Bwana na kulileta hadi kwenye sehemu aliyokuwa ametengeneza kwa ajili yake. 4Kisha Daudi akawakusanya pamoja wazao wa Aroni na Walawi:

515:5 Kut 6:16-18Kutoka wazao wa Kohathi,

Urieli kiongozi na ndugu zake 120,

6Kutoka wazao wa Merari,

Asaya kiongozi na ndugu zake 220.

7Kutoka wazao wa Gershoni,15:7 Namna nyingine ya kutaja Gershomu.

Yoeli kiongozi na ndugu zake 130.

815:8 Kut 6:22Kutoka wazao wa Elisafani,

Shemaya kiongozi na ndugu zake 200.

915:9 Hes 26:58; Kut 6:18Kutoka wazao wa Hebroni,

Elieli kiongozi na ndugu zake 80.

10Kutoka wazao wa Uzieli,

Aminadabu kiongozi na ndugu zake 112.

1115:11 1Nya 12:28; 1Sam 22:20Kisha Daudi akawaita makuhani Sadoki na Abiathari, pamoja na Walawi Urieli, Asaya, Yoeli, Shemaya, Elieli na Aminadabu. 1215:12 Kut 29:10; Law 11:44; Eze 48:11; Yn 17:17; Law 10:3; 2Nya 5:11; 29:5, 15; Rum 12:1-2Akawaambia, “Ninyi ndio viongozi wa jamaa za Walawi. Ninyi pamoja na Walawi wenzenu inawapasa mjitakase na kulipandisha Sanduku la Bwana, Mungu wa Israeli hadi mahali ambapo nimetengeneza kwa ajili yake. 1315:13 1Fal 8:4; 2Sam 6:3; 1Nya 13:11Ilikuwa ni kwa sababu hii, ninyi Walawi, hamkulipandisha Sanduku la Bwana mara ya kwanza, hata ikasababisha Bwana Mungu wetu kuwaka hasira dhidi yetu. Hatukumuuliza jinsi ya kufanya ili tupate kulileta jinsi alivyoagiza.” 14Kwa hiyo makuhani pamoja na Walawi wakajitakasa ili kulipandisha Sanduku la Bwana, Mungu wa Israeli. 1515:15 Kut 25:14; Hes 4:5-15Nao Walawi wakalichukua Sanduku la Mungu mabegani mwao wakitumia mipiko, kama vile Mose alivyoamuru sawasawa na neno la Bwana.

1615:16 Ezr 2:41; Neh 11:23; Amo 6:5; Ay 21:12; Za 68:25; 1Nya 6:31; 13:8; Za 33:2Daudi akawaambia viongozi wa Walawi kuwaweka ndugu zao waimbaji ili waimbe nyimbo za shangwe, wakiwa na vyombo vya uimbaji: zeze, vinubi na matoazi.

1715:17 1Nya 6:33-44Basi Walawi wakawaweka Hemani mwana wa Yoeli; kutoka miongoni mwa ndugu zake, Asafu mwana wa Berekia; kutoka miongoni mwa ndugu zao Wamerari, Ethani mwana wa Kushaiya; 1815:18 2Sam 6:10; 1Nya 26:4-5hawa ndio waliochaguliwa kuwa wasaidizi wao: Zekaria, Yaazieli, Shemiramothi, Yehieli, Uni, Eliabu, Benaya, Maaseya, Matithia, Elifelehu, Mikneya, pamoja na mabawabu Obed-Edomu na Yehieli.

1915:19 1Nya 16:12-13; 29:26Waimbaji Hemani, Asafu na Ethani walichaguliwa kupiga matoazi ya shaba; 20Zekaria, Azieli, Shemiramothi, Yehieli, Uni, Eliabu, Maaseya na Benaya walikuwa wapiga zeze kufuatana na sauti ya alamothi,15:20 Huenda ni aina ya uimbaji. 21na Matithia, Elifelehu, Mikneya, Obed-Edomu, Yehieli na Azazia walikuwa wapiga vinubi, wakiongozwa kwa kufuata sauti ya sheminithi.15:21 Huenda ni aina ya uimbaji. 22Kenania kiongozi wa Walawi alikuwa msimamizi wa uimbaji; huu ndio uliokuwa wajibu wake kwa sababu alikuwa stadi katika hilo.

23Berekia na Elikana walikuwa mabawabu kwa ajili ya Sanduku. 2415:24 2Nya 5:12; Hes 10:8; 2Nya 29:26; Za 81:3Shebania, Yoshafati, Nethaneli, Amasai, Zekaria, Benaya na Eliezeri, makuhani, walikuwa wapiga tarumbeta mbele ya Sanduku la Mungu. Obed-Edomu na Yehiya waliwekwa pia kuwa mabawabu wa Sanduku.

2515:25 2Sam 16:12-13; 2Nya 5:2; Yer 3:16; Kum 12:7, 18; Ezr 6:16Basi Daudi pamoja na wazee wa Israeli na majemadari wa vikosi vya elfu wakaenda ili kulipandisha Sanduku la Agano la Bwana kutoka nyumba ya Obed-Edomu kwa shangwe. 2615:26 Ay 42:8; Hes 23:1-4, 29Kwa sababu Mungu alikuwa amewasaidia Walawi waliokuwa wanalichukua Sanduku la Agano la Bwana, mafahali saba na kondoo dume saba walitolewa dhabihu. 27Basi Daudi alikuwa amevaa joho la kitani safi, kama walivyokuwa wamevaa Walawi wote waliokuwa wanalichukua lile Sanduku, waimbaji nao walivaa vivyo hivyo, pamoja na Kenania aliyekuwa anaongoza nyimbo za waimbaji. Daudi alivaa pia kisibau cha kitani safi. 2815:28 Kut 19:13; 1Nya 13:8Hivyo Israeli wote wakalipandisha Sanduku la Agano la Bwana kwa shangwe, wakipiga pembe za kondoo dume, tarumbeta, matoazi, wakipiga zeze na vinubi.

2915:29 2Sam 6:16; Mdo 2:13Sanduku la Agano la Bwana lilipokuwa linaingia katika Mji wa Daudi, Mikali binti Sauli akachungulia dirishani. Naye alipomwona Mfalme Daudi akicheza na kusherehekea, akamdharau moyoni mwake.

Chinese Contemporary Bible (Traditional)

歷代志上 15:1-29

約櫃被運到耶路撒冷

1大衛大衛城為自己建造宮殿,並為上帝的約櫃預備地方,支搭帳篷。 2大衛說:「除了利未人以外,誰也不可抬上帝的約櫃,因為耶和華只揀選他們抬上帝的約櫃,永遠事奉祂。」

3大衛召集以色列人到耶路撒冷,要把耶和華的約櫃抬到他所預備的地方。 4大衛又召集了亞倫的子孫和利未人: 5哥轄的後代烏列族長和他的一百二十個族人; 6米拉利的後代亞帥雅族長和他的二百二十個族人; 7革順的後代約珥族長和他的一百三十個族人; 8以利撒番的後代示瑪雅族長和他的二百個族人; 9希伯崙的後代以列族長和他的八十個族人; 10烏薛的後代亞米拿達族長和他的一百一十二個族人。

11大衛召來撒督亞比亞他兩位祭司以及利未烏列亞帥雅約珥示瑪雅以列亞米拿達12對他們說:「你們是利未人的族長,你們和你們的族人都要潔淨自己,好將以色列的上帝耶和華的約櫃抬到我所預備的地方。 13先前你們沒有抬約櫃,我們也沒有按規矩求問我們的上帝耶和華,以致祂向我們發怒。」 14於是祭司和利未人就潔淨自己,好將以色列的上帝耶和華的約櫃抬上來。 15利未人按照耶和華藉摩西頒佈的命令,用杠把上帝的約櫃抬在肩上。

16大衛又吩咐利未人的族長去派他們的族人做歌樂手,伴著琴瑟和鈸的樂聲歡唱。 17於是,利未人指派約珥的兒子希幔和他的親族比利迦的兒子亞薩,以及他的親族米拉利的後代古沙雅的兒子以探18協助他們的親族有撒迦利雅雅薛示米拉末耶歇烏尼以利押比拿雅瑪西雅瑪他提雅以利斐利戶彌克尼雅,以及守門的俄別·以東耶利

19歌樂手希幔亞薩以探負責敲銅鈸, 20撒迦利雅雅薛示米拉末耶歇烏尼以利押瑪西雅比拿雅負責鼓瑟,調用高音。 21瑪他提雅以利斐利戶彌克尼雅俄別·以東耶利亞撒西雅負責帶領彈琴,調用低音。 22利未人的族長基拿尼雅善於歌唱,是歌樂手的領班。 23比利迦以利加拿負責看守約櫃。 24祭司示巴尼約沙法拿坦業亞瑪賽撒迦利雅比拿亞以利以謝負責在上帝的約櫃前吹號,俄別·以東耶希亞也負責看守約櫃。

25大衛以色列的長老以及千夫長去俄別·以東家,高高興興地將耶和華的約櫃抬上來。 26耶和華上帝恩待抬約櫃的利未人,他們就獻上七頭公牛和七隻公羊為祭物。 27大衛和抬約櫃的利未人、歌樂手及其領班基拿尼雅都穿上細麻衣,大衛還穿上細麻布的以弗得。 28以色列人把耶和華的約櫃抬了上來,一路上歡呼吹角、鳴號、敲鈸、鼓瑟、彈琴,大聲奏樂。 29耶和華的約櫃進大衛城的時候,掃羅的女兒米甲從窗戶往外看,看見大衛王在興高采烈地跳舞,心裡就輕視他。