路加福音 2 – CCBT & NEN

Chinese Contemporary Bible (Traditional)

路加福音 2:1-52

耶穌降生伯利恆

1那時,凱撒奧古斯都頒下諭旨,命羅馬帝國的人民都辦理戶口登記。 2這是第一次戶口登記,正值居里紐敘利亞總督。 3大家都回到本鄉辦理戶口登記。 4約瑟因為是大衛家族的人,就從加利利拿撒勒鎮趕到猶太地區大衛的故鄉伯利恆5要和已許配給他、懷著身孕的瑪麗亞一起登記。 6他們抵達目的地時,瑪麗亞產期到了, 7便生下第一胎,是個兒子。她用布把孩子裹好,安放在馬槽裡,因為旅店沒有房間了。

牧羊人和天使

8當晚,伯利恆郊外有一群牧羊人正在看守羊群。 9忽然,主的天使向他們顯現,主的榮光四面照著他們,他們非常害怕。 10天使對他們說:「不要怕!我告訴你們一個有關萬民的大喜訊, 11今天在大衛的城裡有一位救主為你們降生了,祂就是主基督! 12你們將看見一個嬰孩包著布躺在馬槽裡,這就是給你們的記號。」

13忽然,有一大隊天軍出現,與那天使一同讚美上帝說:

14「在至高之處,

願榮耀歸於上帝!

在地上,

願平安臨到祂所喜悅的人!」

15眾天使離開他們升回天上之後,牧羊人便商議說:「我們現在去伯利恆,察看一下主剛才告訴我們的那件事吧!」 16他們就連忙進城,找到了瑪麗亞約瑟以及躺在馬槽裡的嬰孩。 17他們看過之後,就把天使告訴他們有關這嬰孩的事傳開了。 18聽見的人都對牧羊人的話感到驚訝。

19瑪麗亞把這些事牢記在心裡,反覆思想。 20牧羊人在歸途中不斷地將榮耀歸於上帝,讚美祂,因為他們的所見所聞跟天使告訴他們的一樣。

奉獻聖嬰

21在第八天,嬰孩接受了割禮,祂的名字叫耶穌,是瑪麗亞懷孕前天使取的。

22摩西律法規定的潔淨期滿後,約瑟瑪麗亞把嬰孩帶到耶路撒冷去獻給主, 23因為主的律法規定:必須把長子分別出來獻給主。 24他們又按照主的律法獻上祭物,即一對斑鳩或兩隻雛鴿。 25耶路撒冷有一位公義敬虔、有聖靈同在的人名叫希緬,他一直期待著以色列的安慰者到來。 26聖靈曾啟示他:他去世前必能親眼看見主所立的基督。

27一天,他受聖靈感動進入聖殿,看見約瑟瑪麗亞抱著嬰孩耶穌進來,要依照律法的規定為祂行奉獻禮, 28就把祂抱過來,稱頌上帝說:

29「主啊,現在你的話已經成就,

可以讓你的奴僕安然離世了,

30因為我已親眼看到你的救恩,

31就是你為萬民所預備的救恩。

32這救恩是啟示外族人的光,

也是你以色列子民的榮耀。」

33約瑟瑪麗亞聽見這番話,感到驚奇。 34希緬給他們祝福後,就對孩子的母親瑪麗亞說:「看啊,這孩子必使以色列許多人跌倒、許多人興起。祂將成為眾人攻擊的對象, 35好叫許多人的心思意念暴露出來,你自己則會心如刀割。」

36-37亞設支派中有一位八十四歲高齡的女先知名叫亞拿,是法內利的女兒,婚後七年便開始守寡,之後一直住在聖殿裡,禁食禱告,日夜事奉上帝。 38正在那時,她也前來感謝上帝,並把耶穌的事報告給所有盼望耶路撒冷蒙救贖的人。

39約瑟瑪麗亞辦完了主的律法規定的一切事之後,就回到他們的家鄉——加利利拿撒勒40耶穌漸漸長大,身心強健,充滿智慧,上帝的恩典與祂同在。

少年耶穌聖殿論道

41約瑟瑪麗亞每年都上耶路撒冷去過逾越節。 42耶穌十二歲那年,跟父母照例上去過節。 43節期完了,約瑟瑪麗亞便啟程回家,他們並不知道少年耶穌仍然留在耶路撒冷44還以為祂跟在同行的人中間。他們走了一天的路後,才開始在親戚朋友中找祂, 45結果沒有找到,只好回到耶路撒冷46三天後,他們才在聖殿裡找到耶穌,祂正和教師們坐在一起,一邊聽一邊問問題。 47祂的知識和對答令聽見的人感到驚奇。 48約瑟瑪麗亞看見耶穌在那裡,大為驚奇。

瑪麗亞對祂說:「兒子,你為什麼這樣對我們呢?你父親和我急得到處找你!」

49耶穌對他們說:「你們為什麼找我呢?難道你們不知道我應該在我父的家嗎?」 50但他們不明白祂在講什麼。

51於是,耶穌隨父母回到拿撒勒,並順從他們。瑪麗亞把這一切事牢記在心。 52耶穌漸漸長大,智慧與日俱增,越來越受上帝和人們的喜愛。

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Luka 2:1-52

Kuzaliwa Kwa Yesu

(Mathayo 1:18-25)

12:1 Lk 3:1; Mt 22:17; 24:14Siku zile Kaisari Augusto alitoa amri kwamba watu wote waandikishwe katika ulimwengu wa Kirumi. 22:2 Mdo 21:3; Mt 4:24; Mdo 15:23, 41(Orodha hii ndiyo ya kwanza iliyofanyika wakati Krenio alikuwa mtawala wa Shamu2:2 Shamu inamaanisha Syria.). 3Kila mtu alikwenda kuandikishwa katika mji wake alikozaliwa.

42:4 Yn 7:42Hivyo Yosefu akapanda kutoka mji wa Nazareti ulioko Galilaya kwenda Uyahudi, mpaka Bethlehemu, mji wa Daudi, kwa sababu yeye alikuwa wa ukoo na wa nyumba ya Daudi. 52:5 Lk 1:27; Mt 1:16Alikwenda huko kujiandikisha pamoja na Maria, ambaye alikuwa amemposa naye alikuwa mjamzito. 6Wakiwa Bethlehemu, wakati wa Maria wa kujifungua ukawa umetimia, 72:7 Mt 1:25naye akamzaa mwanawe, kifungua mimba. Akamfunika nguo za kitoto na kumlaza katika hori ya kulia ngʼombe, kwa sababu hapakuwa na nafasi katika nyumba ya wageni.

Wachungaji Na Malaika

8Katika eneo lile walikuwako wachungaji waliokuwa wakikaa mashambani, wakilinda makundi yao ya kondoo usiku. 92:9 Lk 1:11; Mdo 5:19Ghafula tazama, malaika wa Bwana akawatokea, nao utukufu wa Bwana ukawangʼaria kotekote, wakaingiwa na hofu. 102:10 Mt 14:27Lakini malaika akawaambia: “Msiogope. Kwa maana tazama nawaletea habari njema za furaha itakayokuwa kwa watu wote. 112:11 Yn 3:17; Rum 11:14; Mdo 3:20; 9:22Leo katika mji wa Daudi kwa ajili yenu amezaliwa Mwokozi, ndiye Kristo2:11 Kristo maana yake ni Masiya, yaani Aliyetiwa mafuta. Bwana. 122:12 1Sam 10:7; Za 86:17Hii ndiyo itakayokuwa ishara kwenu: Mtamkuta mtoto mchanga amefunikwa nguo za kitoto na kulazwa katika hori ya kulia ngʼombe.”

132:13 Dan 7:10; Mwa 28:12; 32:12; Za 103:20, 21; 148:2; Ebr 1:14; Ufu 5:11Ghafula pakawa na jeshi kubwa la mbinguni pamoja na huyo malaika wakimsifu Mungu wakisema,

142:14 Isa 9:6; Rum 5:1“Atukuzwe Mungu juu mbinguni,

na duniani iwe amani kwa watu aliowaridhia.”

15Hao malaika walipokwisha kuondoka na kwenda zao mbinguni, wale wachungaji wakasemezana wao kwa wao, “Twendeni Bethlehemu tukaone mambo haya ya ajabu yaliyotukia, ambayo Bwana ametuambia habari zake.”

162:16 Lk 2:7Hivyo wakaenda haraka Bethlehemu, wakawakuta Maria na Yosefu na yule mtoto mchanga akiwa amelala katika hori la kulia ngʼombe. 172:17 Lk 2:10-12Walipomwona yule mtoto, wakawaeleza yale waliyokuwa wameambiwa kuhusu huyo mtoto. 18Nao wote waliosikia habari hizi wakastaajabia yale waliyoambiwa na wale wachungaji wa kondoo. 192:19 Lk 2:51Lakini Maria akayaweka mambo haya yote moyoni mwake na kuyatafakari. 202:20 Mt 9:8Wale wachungaji wakarudi, huku wakimtukuza Mungu na kumsifu kwa ajili ya mambo yote waliyokuwa wameambiwa na kuyaona.

212:21 Lk 1:31, 59Hata zilipotimia siku nane, ulikuwa ndio wakati wa kumtahiri mtoto, akaitwa Yesu, jina alilokuwa amepewa na malaika kabla hajatungwa mimba.

Yesu Apelekwa Hekaluni

222:22 Law 12:2-8Ulipotimia wakati wa utakaso wake Maria kwa mujibu wa Sheria ya Mose, basi Yosefu na Maria walimpeleka mtoto Yerusalemu, ili kumweka wakfu kwa Bwana 232:23 Kut 2:12-15; Hes 3:13(kama ilivyoandikwa katika Sheria ya Bwana, kwamba, “Kila mtoto wa kiume kifungua mimba atawekwa wakfu kwa Bwana”), 242:24 Law 12:8na pia kutoa dhabihu kulingana na yale yaliyonenwa katika Sheria ya Bwana: “Hua wawili au makinda mawili ya njiwa.”

252:25 Lk 16:6; 23:51; Isa 52:9Basi alikuwako huko Yerusalemu mtu mmoja jina lake Simeoni, ambaye alikuwa mwenye haki na mcha Mungu, akitarajia faraja ya Israeli, na Roho Mtakatifu alikuwa juu yake. 262:26 Za 89:48; Ebr 11:5Roho Mtakatifu alikuwa amemfunulia kuwa hatakufa kabla hajamwona Kristo wa Bwana. 272:27 Mwa 46:30; Flp 1:23; Lk 2:22Simeoni, akiwa ameongozwa na Roho Mtakatifu, alikwenda Hekaluni. Wazazi walipomleta mtoto Yesu ili kumfanyia kama ilivyokuwa desturi ya Sheria, 28ndipo Simeoni akampokea mtoto mikononi mwake na kumsifu Mungu, akisema:

292:29 Mdo 2:24“Bwana Mwenyezi, kama ulivyoahidi,

sasa wamruhusu mtumishi wako

aende zake kwa amani.

302:30 Isa 40:5; Lk 3:6; Isa 52:10Kwa maana macho yangu yameuona wokovu wako,

31ulioweka tayari machoni pa watu wote,

322:32 Isa 49:6; Mdo 26:23nuru kwa ajili ya ufunuo kwa watu wa Mataifa

na kwa ajili ya utukufu kwa watu wako Israeli.”

33Naye Yosefu na mama yake mtoto wakastaajabu kwa yale yaliyokuwa yamesemwa kumhusu huyo mtoto. 342:34 Mt 12:46; Isa 8:14; Gal 5:11Kisha Simeoni akawabariki, akamwambia Maria mama yake, “Mtoto huyu amewekwa kwa makusudi ya kuanguka na kuinuka kwa wengi katika Israeli. Atakuwa ishara ambayo watu watanena dhidi yake, 352:35 Za 42:10; Yn 19:25ili mawazo ya mioyo mingi yadhihirike. Nao upanga utauchoma moyo wako.”

362:36 Mdo 21:9Tena alikuwako Hekaluni nabii mmoja mwanamke, jina lake Ana binti Fanueli, wa kabila la Asheri. Alikuwa mzee sana; naye alikuwa ameolewa na kuishi na mume kwa miaka saba tu, kisha mumewe akafa. 372:37 1Tim 5:9; Mdo 14:23Hivyo alikuwa mjane na umri wake ulikuwa miaka themanini na minne. Yeye hakuondoka humo Hekaluni usiku wala mchana, bali alikuwa akimwabudu Mungu, akifunga na kuomba. 382:38 Isa 52:9; Lk 24:21Wakati huo huo, Ana alikuja akaanza kusifu, akimshukuru Mungu na kusema habari za huyo mtoto kwa watu wote waliokuwa wakitarajia ukombozi wa Yerusalemu.

392:39 Mt 2:23Yosefu na Maria walipokuwa wamekamilisha mambo yote yaliyotakiwa na Sheria ya Bwana, walirudi mjini kwao Nazareti huko Galilaya. 402:40 Lk 2:52; 1:80Naye yule mtoto akakua na kuongezeka nguvu, akiwa amejaa hekima, na neema ya Mungu ilikuwa juu yake.

Kijana Yesu Hekaluni

412:41 Kut 23:15; Lk 22:8Kila mwaka Yosefu na Maria mama yake Yesu walikuwa na desturi ya kwenda Yerusalemu kwa ajili ya Sikukuu ya Pasaka. 42Yesu alipokuwa na umri wa miaka kumi na miwili, walipanda kwenda kwenye Sikukuu hiyo kama ilivyokuwa desturi. 432:43 Kut 12:18Baada ya Sikukuu kumalizika, wakati Yosefu na Maria mama yake walipokuwa wakirudi nyumbani, Yesu alibaki Yerusalemu lakini hawakutambua. 44Wao wakidhani kuwa yuko miongoni mwa wasafiri, walienda mwendo wa kutwa nzima. Ndipo wakaanza kumtafuta miongoni mwa jamaa zao na marafiki. 45Walipomkosa walirudi Yerusalemu ili kumtafuta. 46Baada ya siku tatu wakamkuta ndani ya Hekalu, akiwa ameketi katikati ya walimu wa sheria, akiwasikiliza na kuwauliza maswali. 472:47 Mt 7:28Wote waliomsikia walistaajabishwa na uwezo wake mkubwa wa kuelewa, na majibu aliyoyatoa. 482:48 Mt 12:46; Lk 3:23; 4:22Yosefu na Maria mama yake walipomwona walishangaa. Mama yake akamuuliza, “Mwanangu, mbona umetufanyia hivi? Tazama, mimi na baba yako tumekuwa tukikutafuta kwa wasiwasi mkubwa kila mahali.”

492:49 Yn 2:16Yesu akawaambia, “Kwa nini kunitafuta? Hamkujua kwamba imenipasa kuwa katika nyumba ya Baba yangu?”

502:50 Mk 9:32Lakini wao hawakuelewa maana ya lile alilowaambia.

512:51 Lk 2:19Ndipo akashuka pamoja nao hadi Nazareti, naye alikuwa mtiifu kwao. Lakini mama yake akayaweka moyoni mwake mambo haya yote. 522:52 Mit 3; 4; Lk 1:80Naye Yesu akakua katika hekima na kimo, akimpendeza Mungu na wanadamu.