羅馬書 15 – CCBT & NEN

Chinese Contemporary Bible (Traditional)

羅馬書 15:1-33

我為人人

1我們堅強的人要扶助軟弱的人,分擔他們的重擔,不該只顧自己的喜好。 2我們每個人都應該為他人著想,建造他人的生命。 3因為基督並沒有專顧自己,正如聖經上說:「辱駡你之人的辱駡都落在我身上。」 4從前寫在聖經上的話都是為了教導我們,使我們靠著忍耐和聖經的鼓勵而有盼望。 5但願賜忍耐和鼓勵的上帝給你們合一的心去效法基督耶穌的榜樣, 6使你們一起同聲頌贊上帝——我們主耶穌基督的父。

7所以,你們應該像基督接納你們一樣彼此接納,使上帝得榮耀。 8你們要知道,基督為了上帝的真理成為猶太15·8 猶太」希臘文是「受割禮之人」。的僕人,好實現上帝對猶太人祖先們的應許, 9使外族人也因祂的憐憫而將榮耀歸給上帝。正如聖經上說:

「因此,我要在列邦中讚美你,

歌頌你的名。」

10又說:

「外族人啊,

你們當與主的子民一同歡樂。」

11又說:

「萬邦啊,你們當讚美主!

萬民啊,你們當頌讚祂!」

12以賽亞先知也說:

「將來耶西的根要興起,

祂要統治外族,

外族人都要仰望祂。」

13願使人有盼望的上帝,因為你們信祂,將諸般的喜樂和平安充滿你們的心,使你們藉著聖靈的能力充滿盼望!

福音特使

14弟兄姊妹,我知道你們充滿良善,知識全備,能彼此勸導。 15但我仍放膽寫信提醒你們幾件事,因為我蒙上帝賜恩, 16在外族人中作基督耶穌的僕人和上帝福音的祭司,好叫外族人藉著聖靈得以聖潔,可以作上帝喜悅的祭物。 17因此,我在基督耶穌裡以事奉上帝為榮。 18-19別的事我不敢提,只有一件是我津津樂道的,就是基督藉著我的言語行為,用神蹟奇事和聖靈的大能叫外族人順服,使我把基督的福音從耶路撒冷一路傳到了以利哩古。 20我立志只去從未聽過基督之名的地方傳福音,免得我建造在別人的根基上。 21正如聖經上說:「對祂毫無所聞的,將要看見;未曾聽過的,將要明白。」

保羅計劃去羅馬

22因此,我一直受到攔阻,不能到你們那裡。 23但如今福音傳遍了這一帶,況且我幾年來一直盼望去你們那裡, 24所以我想去西班牙的途中路過你們那裡,稍作停留,享受與你們的相聚之樂,然後由你們資助我上路。 25但現在我要去耶路撒冷服侍當地的聖徒, 26因為馬其頓亞該亞的教會欣然捐出了財物給耶路撒冷的窮困聖徒。 27這固然是他們慷慨解囊,但也可以說是他們該還的債。外族人既然分享了猶太聖徒屬靈的福分,現在以物質報答他們也是應該的。 28等我辦完這件事,將捐款交付他們之後,我就會途經你們那裡去西班牙29我知道我去的時候,必會把基督豐盛的祝福帶給你們。

30弟兄姊妹,我藉著我們主耶穌基督和聖靈所賜的愛心,懇求你們與我一同竭力禱告,為我祈求上帝, 31使我脫離猶太地區不信之人的迫害,叫耶路撒冷的聖徒樂意接受我帶去的捐款, 32並使我按照上帝的旨意歡然去與你們相聚,一同重新得力。

33願賜平安的上帝常與你們同在。阿們!

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Warumi 15:1-33

Usijipendeze Mwenyewe, Bali Wapendeze Wengine

115:1 Rum 14:1; 1The 5:14Sisi tulio na nguvu, hatuna budi kuchukuliana na kushindwa kwa wale walio dhaifu wala si kujipendeza nafsi zetu wenyewe. 215:2 1Kor 10:33Kila mmoja wetu inampasa kumpendeza jirani yake kwa mambo mema, ili kumjenga katika imani. 315:3 2Kor 8:9; Za 69:9Kwa maana hata Kristo hakujipendeza mwenyewe, bali kama ilivyoandikwa: “Matukano yao wale wanaokutukana wewe yalinipata mimi.” 415:4 Rum 4:23, 24; 1Kor 10:11; 9:9, 10; 10:11; 2Tim 3:16, 17Kwa maana kila kitu kilichoandikwa zamani, kiliandikwa kutufundisha, ili kwamba kwa saburi na faraja tunayopata katika Maandiko tuwe na tumaini.

515:5 2Kor 13:11; Efe 4:3Mungu atoaye saburi na faraja, awajalie ninyi roho ya umoja miongoni mwenu mnapomfuata Kristo Yesu, 615:6 Ufu 1; 6; Za 34:3; Mdo 4:24, 32ili kwa moyo mmoja mpate kumtukuza Mungu aliye Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo.

Injili Sawa Kwa Wayahudi Na Kwa Watu Wa Mataifa

715:7 Rum 14:1; 5:2Karibishaneni ninyi kwa ninyi kama Kristo alivyowakaribisha ninyi ili kumletea Mungu utukufu. 815:8 Mt 15:24; Mdo 3:25, 26; 2Kor 1:20Kwa maana nawaambia kwamba, Kristo amekuwa mtumishi kwa wale waliotahiriwa ili kuonyesha kweli ya Mungu na kuthibitisha zile ahadi walizopewa baba zetu wa zamani, 915:9 Rum 3:29; Mt 9:8; 2Sam 22:50; Za 18:49pia ili watu wa Mataifa wamtukuze Mungu kwa rehema zake. Kama ilivyoandikwa:

“Kwa hiyo nitakutukuza katikati ya watu wa Mataifa;

nitaliimbia sifa jina lako.”

1015:10 Kum 32:43Tena yasema,

“Enyi watu wa Mataifa, furahini

pamoja na watu wa Mungu.”

1115:11 Za 117:1Tena,

“Msifuni Bwana, ninyi watu wa Mataifa wote,

na kumwimbia sifa, enyi watu wote.”

1215:12 Ufu 5:5; Isa 11:10; Mt 12:21Tena Isaya anasema,

“Shina la Yese litachipuka,

yeye atakayeinuka ili kutawala juu ya mataifa.

Watu wa Mataifa watamtumaini.”

1315:13 Rum 14:17; 1Kor 4:20Mungu wa tumaini awajaze ninyi furaha yote na amani katika kumwamini, ili mpate kujawa na tumaini tele kwa nguvu ya Roho Mtakatifu.

Paulo Mhudumu Wa Watu Wa Mataifa

1415:14 Efe 5:9; 2Pet 1:12Ndugu zangu, mimi mwenyewe ninasadiki kwamba mmejaa wema na ufahamu wote, tena mnaweza kufundishana ninyi kwa ninyi. 1515:15 Rum 12:3; 1:5; 12:3; Gal 1:15; Efe 3:7, 8Nimewaandikia kwa ujasiri vipengele kadha wa kadha katika waraka huu kama kuwakumbusha tena kwa habari ya ile neema Mungu aliyonipa, 1615:16 Mdo 9:5; Rum 11:13; 1:1; Isa 66:20ili kuwa mhudumu wa Kristo Yesu kwa watu wa Mataifa nikiwa na huduma ya kikuhani ya kutangaza Injili ya Mungu, ili watu wa Mataifa wapate kuwa dhabihu inayokubaliwa na Mungu, iliyotakaswa na Roho Mtakatifu.

1715:17 Flp 3:3; Ebr 2:17Kwa hiyo ninajisifu katika Kristo Yesu, kwenye utumishi wangu kwa Mungu. 1815:18 Mdo 15:12; Rum 1:15; 16:26Kwa maana sitathubutu kusema kitu chochote zaidi ya kile ambacho Kristo amefanya kwa kunitumia mimi katika kuwaongoza watu wa Mataifa wamtii Mungu kwa yale niliyosema na kufanya, 1915:19 Yn 4:48; Mdo 19:11; 22:17-21kwa nguvu za ishara na miujiza, kwa uweza wa Roho wa Mungu, hivyo kuanzia Yerusalemu hadi maeneo yote ya kandokando yake mpaka Iliriko, nimekwisha kuihubiri Injili ya Kristo kwa ukamilifu. 2015:20 2Kor 10:15, 16Hivyo ni nia yangu kuhubiri Habari Njema, si pale ambapo Kristo amekwisha kujulikana, ili nisije nikajenga juu ya msingi wa mtu mwingine. 2115:21 Isa 52:15Lakini kama ilivyoandikwa:

“Wale ambao hawajahubiriwa habari zake wataona,

nao wale ambao hawajazisikia watafahamu.”

2215:22 Rum 1:13Hii ndiyo sababu nimezuiliwa mara nyingi nisiweze kuja kwenu.

Paulo Apanga Kwenda Rumi

2315:23 Mdo 19:21; 24:17Lakini sasa kwa kuwa hakuna nafasi zaidi kwa ajili yangu katika sehemu hii, ninatamani kuja kwenu kama ambavyo nimekuwa na shauku kwa miaka mingi. 2415:24 Rum 15:28; 1Kor 16:6; Tit 3:1Nimekusudia kufanya hivyo nitakapokuwa njiani kwenda Hispania. Natarajia kuwaona katika safari yangu na kusafirishwa nanyi mpaka huko, baada ya kufurahia ushirika wenu kwa kitambo kidogo. 2515:25 Mdo 19:21; 24:17Sasa, niko njiani kuelekea Yerusalemu kwa ajili ya kuwahudumia watakatifu huko. 2615:26 Rum 16:9; 2Kor 1:11; Kol 4:12Kwa kuwa imewapendeza watu wa Makedonia na Akaya kufanya changizo kwa ajili ya maskini walioko miongoni mwa watakatifu huko Yerusalemu. 2715:27 1Kor 9:11; Rum 9:4; 11:17; Gal 6:6Imewapendeza kufanya hivyo, naam, kwani ni wadeni wao. Kwa maana ikiwa watu wa Mataifa wameshiriki baraka za rohoni za Wayahudi, wao ni wadeni wa Wayahudi, ili Wayahudi nao washiriki baraka zao za mambo ya mwilini. 2815:28 Flp 4:17; Rum 15:24Kwa hiyo baada ya kukamilisha kazi hii na kuhakikisha kuwa wamepokea kila kitu kilichokusanywa, nitapitia kwenu nikiwa njiani kwenda Hispania. 2915:29 Rum 1:10; 1:11Ninajua kwamba nitakapokuja kwenu, nitakuja na wingi wa baraka za Kristo.

3015:30 Gal 5:22; 2Kor 1:11; Kol 4:12Basi, ndugu zangu, nawasihi kwa Jina la Bwana wetu Yesu Kristo na kwa upendo wa Roho Mtakatifu, kujiunga nami katika taabu zangu mkiniombea kwa Mungu. 3115:31 2Kor 1:10; 2Tim 3:11Ombeni ili nipate kuokolewa mikononi mwa wale wasioamini walioko Uyahudi, na kwamba utumishi wangu upate kukubaliwa na watakatifu wa huko Yerusalemu, 3215:32 Mdo 18:21; Rum 1:10, 13; 1Kor 16:18ili kwa mapenzi ya Mungu niweze kuja kwenu kwa furaha, nami niburudishwe pamoja nanyi. 3315:33 2The 3:16Mungu wa amani na awe pamoja nanyi nyote. Amen.