彌迦書 4 – CCBT & NEN

Chinese Contemporary Bible (Traditional)

彌迦書 4:1-13

耶路撒冷的將來

1在末後的日子,

耶和華殿所在的山必超乎群山,

高過眾嶺,

萬民都要歸向它。

2多國的民都要前來,說:

「來吧,讓我們登耶和華的山,

雅各之上帝的殿。

祂必指示我們當行的路,

我們也要遵行祂的道。」

因為訓誨必出於錫安

耶和華的話語必來自耶路撒冷

3祂要在各民族中施行審判,

為遠方的強國斷定是非。

他們要把刀劍鑄成犁頭,

把矛槍打成鐮刀。

國與國之間不再動刀槍,

也不再學習戰爭。

4人人都安然坐在自己的葡萄樹和無花果樹下,

不再擔驚受怕。

這是萬軍之耶和華親口說的。

5萬民都遵從自己的神明,

但我們要永遠遵從我們的上帝耶和華。

6耶和華說:

「到那日,我要聚集瘸腿的,

招聚被擄的和被我懲罰的。

7我要使瘸腿的成為餘民,

讓被擄的成為強國。

耶和華要在錫安山做王治理他們,

從那時直到永遠。

8「你這羊群的瞭望塔,

錫安4·8 」希伯來文是「女子」,可能是對錫安的暱稱,下同4·13的堅壘啊!

從前的國權——

耶路撒冷城的王位必重新歸你。」

9現在你為何大聲哭喊?

是因為你沒有王嗎?

難道你的謀士都死了嗎,

以致你像分娩的婦人一樣痛苦不堪?

10錫安的百姓啊,

你們要像分娩的婦人一樣輾轉呻吟,

因為你們現在要離開這城,

住在荒野,被擄到巴比倫

在那裡,你們將得到解救;

在那裡,耶和華必從敵人手中救贖你們。

11現在許多國家一起來攻擊你們,說:

「願錫安遭蹂躪,

我們要看著錫安被毀滅。」

12他們卻不知道耶和華的心意,

也不明白祂的計劃。

祂聚集他們是要懲罰他們,

像把禾捆堆積在麥場一樣。

13耶和華說:

錫安城啊,

起來打穀吧!

我要給你鐵角,

我要給你銅蹄。

你要打碎列國,

將他們的不義之財獻給耶和華,

把他們的財富獻給普天下的主。」

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Mika 4:1-13

Mlima Wa Bwana

(Isaya 2:2-4)

14:1 Za 48:1; 86:9; Zek 8:3; Isa 2:2; Dan 2:35; 2:44; Eze 17:22; Yer 3:17; 31:12Katika siku za mwisho

mlima wa Hekalu la Bwana utaimarishwa

kama mlima mkuu miongoni mwa milima yote;

utainuliwa juu ya vilima,

na watu wa mataifa watamiminika humo.

24:2 Yer 31:6; Yn 6:45; Eze 20:40; Zek 2:11; 14:16; Isa 54:13; Za 25:8-9; 119:171Mataifa mengi yatakuja na kusema,

“Njooni, twendeni mlimani mwa Bwana,

kwenye nyumba ya Mungu wa Yakobo.

Atatufundisha njia zake,

ili tuweze kuenenda katika mapito yake.”

Sheria itatoka Sayuni,

neno la Bwana litatoka Yerusalemu.

34:3 Isa 2:4; 11:4; Yoe 3:10; Hos 2:18; Za 72:7; Zek 8:20-22; 9:10; Za 46:9Atahukumu kati ya mataifa mengi,

na ataamua migogoro ya mataifa

yenye nguvu na yaliyo mbali.

Watafua panga zao ziwe majembe,

na mikuki yao kuwa miundu ya kukata matawi.

Taifa halitainua upanga dhidi ya taifa jingine,

wala hawatajifunza vita tena.

44:4 1Fal 4:25; Law 26:6; Eze 39:26; Isa 1:20; 36:16; Yer 31:10; Zek 3:10Kila mtu ataketi chini ya mzabibu wake

na chini ya mtini wake,

wala hakuna mtu atakayewaogopesha,

kwa kuwa Bwana Mwenye Nguvu Zote amesema.

54:5 2Fal 17:29; Mdo 14:16; Yos 24:14-15; Isa 26:8; Yer 2:11; Zek 10:12Mataifa yote yanaweza kutembea

katika jina la miungu yao;

sisi tutatembea katika jina la Bwana

Mungu wetu milele na milele.

Mpango Wa Bwana

64:6 Yer 31:8; Isa 56:8; Za 147:2; 106:47; Eze 34:13, 16; 37:21; Sef 3:19“Katika siku hiyo,” asema Bwana,

“nitawakusanya walemavu;

nitawakusanya walio uhamishoni

na wale niliowahuzunisha.

74:7 Yoe 2:32; Mik 2:12; Isa 9:6; Mwa 12:2; Dan 2:44; 7:14; Ufu 11:15; Lk 1:33Nitawafanya walemavu kuwa mabaki,

wale waliofukuzwa kuwa taifa lenye nguvu.

Bwana atatawala juu yao katika Mlima Sayuni

kuanzia siku hiyo na hata milele.

84:8 Isa 1:26; Zek 9:9Lakini kuhusu wewe, ee mnara wa ulinzi wa kundi,

ee ngome ya Binti Sayuni,

milki ya awali itarudishwa kwako,

ufalme utakuja kwa Binti Yerusalemu.”

94:9 Yer 8:19; 30:6; 48:41; Mwa 3:16Kwa nini sasa unalia kwa nguvu:

kwani huna mfalme?

Je, mshauri wako amekufa, hata maumivu yakukamate

kama ya mwanamke

aliye na utungu wa kuzaa?

104:10 Kum 21:10; 2Fal 20:18; Isa 43:14; 48:20Gaagaa kwa utungu, ee Binti Sayuni,

kama mwanamke mwenye utungu wa kuzaa,

kwa kuwa sasa ni lazima uuache mji

ukapige kambi uwanjani.

Utakwenda Babeli;

huko utaokolewa.

Huko Bwana atakukomboa

kutoka mikononi mwa adui zako.

114:11 Mao 2:16; Oba 1:12; Mik 7:8Lakini sasa mataifa mengi

yamekusanyika dhidi yako.

Wanasema, “Mwache anajisiwe,

macho yetu na yatazame Sayuni kwa furaha!”

124:12 Mwa 50:20; Isa 55:8; Rum 11:33-34Lakini hawayajui

mawazo ya Bwana;

hawauelewi mpango wake,

yeye awakusanyaye kama miganda

kwenye sakafu ya kupuria.

134:13 Isa 21:10; 23:18; 45:1; Ufu 21:24; Dan 2:44“Inuka upure, ee Binti Sayuni,

kwa kuwa nitakupa pembe za chuma;

nitakupa kwato za shaba

na utavunja vipande vipande mataifa mengi.”

Utatoa mapato yao waliopata kwa udanganyifu kwa Bwana,

utajiri wao kwa Bwana wa dunia yote.