尼希米記 2 – CCBT & NEN

Chinese Contemporary Bible (Traditional)

尼希米記 2:1-20

尼希米返回耶路撒冷

1亞達薛西王二十年尼散月2·1 尼散月」即希伯來曆的一月,陽曆是三月中旬到四月中旬。,酒呈到王面前後,我端起酒遞給王。在王面前,我一向沒有愁容。 2王問我:「你沒有病,為什麼面帶愁容?一定是心中煩惱。」我非常害怕。 3我對王說:「願王萬歲!我祖墳所在的城邑已成廢墟,城門也被燒毀,我怎能不面帶愁容?」 4王問我:「你有什麼要求?」我向天上的上帝禱告後, 5回答說:「如果王認為好,如果僕人在王面前蒙恩,請王派我到猶大,重建我祖墳所在的城邑。」 6當時王后坐在王的旁邊,王問我:「你要去多久?什麼時候回來?」我告訴王一個日期,王欣然批准。 7我又說:「如果王認為好,求王賜我詔書,通知河西省長准我經過前往猶大8求王再發一道詔書,通知管理王室園林的亞薩,吩咐他供給我木材,用來做聖殿堡壘的門梁及建造城牆和我住的房子。」王批准了我的請求,因為我的上帝施恩幫助我。

9王派將領率騎兵沿途護送我。到了河西省長那裡,我把王的詔書交給他們。 10和倫參巴拉和官長亞捫多比雅聽到有人來幫以色列人謀求好處,非常不悅。

尼希米視察耶路撒冷的城牆

11我到了耶路撒冷,在那裡住了三天, 12然後在夜間起來,帶著幾個人出去。上帝感動我要為耶路撒冷做的事,我沒有告訴任何人。除了我騎的牲口外,我們沒有帶其他牲口。 13我穿過谷門,朝龍泉的方向走到糞廠門,在那裡察看耶路撒冷倒塌的城牆和被燒毀的城門。 14我又往前走到泉門和王池,我騎的牲口無法通過那裡, 15我就乘夜沿溪而上,察看城牆,然後轉身取道谷門回城。 16官員不知道我到過哪裡,做過何事,因為我還沒有向猶太人、祭司、貴族、官員和其他要參與這工程的人透露我的計劃。

17後來我對他們說:「你們都看到了我們的困境。耶路撒冷已成廢墟,城門也被燒毀。來吧,讓我們重建耶路撒冷的城牆,免得我們再受凌辱。」 18然後,我把我的上帝怎樣施恩幫助我以及王對我說的話都告訴了他們。他們就說:「我們起來重建城牆吧!」於是他們開始做這善工。 19和倫參巴拉和官長亞捫多比雅,以及阿拉伯基善聽說後,就譏笑我們,藐視我們,說:「你們在做什麽?想要背叛王嗎?」 20我回答他們說:「天上的上帝必使我們亨通,我們身為祂僕人,要起來重建這城牆,但你們在耶路撒冷無份、無權、無業。」

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Nehemia 2:1-20

Artashasta Amtuma Nehemia Yerusalemu

12:1 Ezr 4:7; 7:1Katika mwezi wa Nisani2:1 Nisani (Abibu) ni mwezi wa kwanza katika kalenda ya Kiyunani; katika kalenda yetu ni Machi/Aprili. mwaka wa ishirini wa utawala wa Mfalme Artashasta, wakati divai ilipoletwa kwake, niliichukua na kumpa mfalme. Sikuwahi kuonekana mwenye huzuni mbele yake kabla ya hapo. 22:2 Mit 15:13Basi mfalme akaniuliza, “Kwa nini uso wako unaonekana una huzuni wakati wewe si mgonjwa? Jambo hili si kitu kingine bali ni huzuni ya moyo.”

Niliogopa sana, 32:3 1Fal 1:13; Dan 3:9; 5:10; Za 137:6lakini nikamwambia mfalme, “Mfalme na aishi milele! Kwa nini uso wangu usiwe na huzuni wakati mji walipozikwa baba zangu umebaki magofu, na malango yake yameteketezwa kwa moto?”

42:4 1Sam 1:13; Mit 3:6Mfalme akaniambia, “Je, haja yako ni gani?”

Ndipo nikaomba kwa Mungu wa mbinguni, 5na nikamjibu mfalme, “Kama ikimpendeza mfalme, na kama mtumishi wako amepata kibali machoni pake, anitume kule mji wa Yuda, mahali baba zangu walipozikwa, ili niweze kuujenga upya.”

62:6 Neh 5:14; 13:6Kisha mfalme, na malkia akiwa ameketi karibu naye, akaniuliza, “Safari yako itachukua muda gani, nawe utarudi lini?” Ilimpendeza mfalme kunituma, kwa hiyo nikapanga muda.

72:7 Ezr 8:36Pia nikamwambia, “Kama ikimpendeza mfalme, naomba nipewe barua kwa watawala wa Ngʼambo ya Frati, ili wanipe ulinzi mpaka nifike Yuda. 82:8 Neh 3:7; Ezr 7:6; Neh 7:2; Mdo 7:10Naomba nipewe barua nipeleke kwa Asafu, mtunzaji wa msitu wa mfalme, ili anipe miti ya kutengeneza boriti kwa ajili ya malango ya ngome ya Hekalu, na ukuta wa mji, na makao yangu nitakapoishi.” Kwa kuwa mkono wenye neema wa Mungu wangu ulikuwa juu yangu, mfalme akanijalia ombi langu. 92:9 Ezr 8:22Basi nilienda kwa watawala wa Ngʼambo ya Frati na kuwapa barua za mfalme. Pia mfalme alikuwa ametuma maafisa wa jeshi na askari wapanda farasi pamoja nami.

102:10 Neh 2:10; 4:1, 7; 6:1-2, 5, 12, 14; 13:28; 4:3; 13:4-7; Es 10:3Sanbalati Mhoroni na Tobia afisa Mwamoni waliposikia juu ya jambo hili, waliudhika sana kwamba amekuja mtu kuinua ustawi wa Waisraeli.

Nehemia Akagua Kuta Za Yerusalemu

112:11 Mwa 40:13Nilienda Yerusalemu, na baada ya kukaa huko siku tatu, 12nikaondoka wakati wa usiku pamoja na watu wachache. Sikuwa nimemwambia mtu yeyote kile ambacho Mungu wangu alikuwa ameweka moyoni mwangu kufanya kwa ajili ya Yerusalemu. Hapakuwepo na mnyama yeyote pamoja nami isipokuwa yule niliyekuwa nimempanda.

132:13 2Nya 26:9; Neh 12:31; 3:13Nikatoka nje usiku kupitia Lango la Bondeni, kuelekea Kisima cha Joka na Lango la Samadi, nikikagua kuta za Yerusalemu zilizokuwa zimebomolewa, na malango yake yaliyokuwa yameteketezwa kwa moto. 142:14 Neh 12:37; 2Fal 18:17; 20:20Kisha nikaelekea mpaka Lango la Chemchemi na Bwawa la Mfalme, lakini hapakuwepo nafasi ya kutosha kwa ajili ya mnyama wangu kupita, 152:15 2Sam 15:23; Yer 31:40; Yn 18:1kwa hiyo nikapandia bondeni usiku nikikagua ukuta. Mwishoni nikarudi na kuingia tena kupitia Lango la Bondeni. 16Maafisa hawakujua nilikokwenda wala nilichokuwa nikifanya, kwa sababu mpaka sasa nilikuwa bado sijasema lolote kwa Wayahudi, wala makuhani, wala wakuu, wala maafisa, wala mtu yeyote ambaye angefanya kazi.

172:17 Za 102:16; Isa 30:13; 58:12; Eze 5:14; Neh 1:3Ndipo nilipowaambia, “Mnaona taabu tuliyo nayo: Yerusalemu imebaki magofu na malango yake yameteketezwa kwa moto. Njooni tujenge upya ukuta wa Yerusalemu, nasi hatutakuwa tena katika aibu hii.” 182:18 Ezr 5:5; 2Sam 2:7Pia niliwaambia kuhusu mkono wenye neema wa Mungu wangu uliokuwa juu yangu, na kile mfalme alichokuwa ameniambia.

Wakajibu, “Haya! Tuanze kujenga tena.” Kwa hiyo wakaanza kazi hii njema.

192:19 Neh 6:1-6; Za 44:13-16Lakini Sanbalati Mhoroni, Tobia afisa Mwamoni, na Geshemu Mwarabu waliposikia kuhusu jambo hili, walitudhihaki na kutucheka. Wakauliza, “Ni nini hiki mnachokifanya? Je, mnaasi dhidi ya mfalme?”

202:20 Ezr 4:3; Mdo 8:21; Rum 8:31Nikawajibu kwa kusema, “Mungu wa mbinguni atatufanikisha. Sisi watumishi wake tutaanza kujenga upya, lakini kwenu ninyi, hamna sehemu wala dai lolote wala kumbukumbu la haki katika Yerusalemu.”