出埃及記 6 – CCBT & NEN

Chinese Contemporary Bible (Traditional)

出埃及記 6:1-30

上帝應許拯救以色列人

1耶和華對摩西說:「你就要看見我怎樣用大能的手對付法老,那時他會讓以色列人走,甚至把他們趕出埃及!」 2上帝又對摩西說:「我是耶和華, 3我曾以全能上帝的身份向亞伯拉罕以撒雅各顯現,但沒有讓他們知道我的名字是耶和華。 4我向他們堅守所立的約,要把他們寄居的迦南賜給他們。 5我已聽見以色列人因受埃及人的奴役而發出的呼求,也想起了我的約。 6所以,你要轉告以色列人說,『我是耶和華。我要伸出臂膀重重地懲罰埃及,救贖你們脫離埃及人的轄制,脫離他們的奴役。 7我要接納你們做我的子民,我要做你們的上帝。這樣,你們就知道我是你們的上帝耶和華,曾救你們脫離埃及人的轄制。 8我必帶領你們進入我舉手起誓要給亞伯拉罕以撒雅各的那片土地,把它賜給你們作產業。我是耶和華。』」

9摩西把這番話轉告百姓,可是他們因為殘酷的勞役無比沮喪,不肯聽他的話。 10耶和華對摩西說: 11「你再去見法老,要他讓以色列人離開他的土地。」 12摩西卻說:「以色列人都不聽我的話,法老又怎麼肯聽我這拙口笨舌的人呢?」 13耶和華吩咐摩西亞倫回到以色列人和法老那裡,要他們領以色列人離開埃及

摩西和亞倫的族譜

14以下是以色列各宗族族長的名字:

以色列長子呂便的兒子是哈諾法路希斯崙迦米。這些是呂便的宗族。

15西緬的兒子是耶姆利雅憫阿轄雅斤瑣轄掃羅掃羅的母親是迦南人。這些是西緬的各宗族。

16利未的兒子依次是革順哥轄米拉利利未享年一百三十七歲。 17革順的兒子是立尼示每,二人各成宗族。 18哥轄的兒子是暗蘭以斯哈希伯崙烏薛哥轄享年一百三十三歲。 19米拉利的兒子是抹利姆示。這些是利未的各宗族。 20暗蘭娶了他父親的妹妹約基別,生了亞倫摩西暗蘭享年一百三十七歲。 21哥轄另一個兒子以斯哈生了可拉尼斐細基利22烏薛的兒子是米沙利以利撒反西提利23亞倫亞米拿達的女兒、拿順的妹妹以利沙巴結婚,生了拿答亞比戶以利亞撒以他瑪24可拉的兒子是亞惜以利加拿亞比亞撒,這些是可拉的各宗族。 25亞倫的兒子以利亞撒普鐵的一個女兒結婚,生了非尼哈。以上是利未各宗族的族長。

26正是亞倫摩西受耶和華之命,要按以色列人的宗族支派把他們帶出埃及27也是這二人要求埃及王法老讓他們把以色列人帶出埃及28那時,耶和華曾經在埃及摩西說: 29「我是耶和華,你要把我吩咐你的一切話告訴埃及法老。」 30摩西卻對耶和華說:「你看,我拙口笨舌,法老怎肯聽我的話?」

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Kutoka 6:1-30

16:1 Kut 3:20; 11:1; 12:31-39; Kum 5:15Kisha Bwana akamwambia Mose, “Sasa utaona kitu nitakachomfanyia Farao: Kwa sababu ya mkono wangu wenye nguvu atawaachia watu waende; kwa sababu ya mkono wangu wenye nguvu atawafukuza waondoke nchini mwake.”

26:2 Kut 3:14-15; 7:5; 8:22; 10:2; 12:12; 14:4, 18; 16:12; Law 11:44; 18:21; 20:7; Isa 41:20; 43:11; 49:23; 60:16; Eze 13:9; 25:17; 36:38; 37:6, 13; Yoe 2:27Pia Mungu akamwambia Mose, “Mimi ndimi Bwana. 36:3 Mwa 7:1; 2Sam 7:26; Za 48:10; 61:5; 68:4; 83:18; 99:3; Isa 52:6; Kut 3:14, 15; Yn 8:58Nilimtokea Abrahamu, Isaki na Yakobo kama Mungu Mwenyezi,6:3 Mungu Mwenyezi hapa ni jina la Kiebrania, El-Shaddai (yaani Mungu Mwenye utoshelevu wote). ingawa sikuwajulisha Jina langu, Yehova, Mimi mwenyewe sikujitambulisha kwao. 46:4 Mwa 6:18; 12:7; 15:18; 17:8; Mdo 7:5; Rum 4:13; Gal 3:16; Ebr 11:8-10Pia niliweka Agano langu nao kuwapa nchi ya Kanaani, ambako waliishi kama wageni. 56:5 Kut 2:23; Mdo 7:34; Mwa 9:15Zaidi ya hayo, nimesikia kilio cha huzuni cha Waisraeli ambao Wamisri wamewatia utumwani, nami nimelikumbuka Agano langu.

66:6 Kut 3:8, 19-20; 12:17, 51; 15:13; 16:6; 20:2; 29:46; Law 22:33; 26:13; Kum 6:12; 7:8; 9:26; Za 9:16; 19:14; 34:22; 74:2; 77:15; 81:10; 105:27; 136:11; Yer 2:6; 15:21; 31:11; 50:34; Hos 13:4; Amo 2:10; Mik 6:4; 1Nya 17:21; Isa 29:22; 35:9; 44:23; 48:20; Mdo 13:17“Kwa hiyo, waambie Waisraeli: ‘Mimi ndimi Bwana, nami nitawatoa mtoke katika kongwa la Wamisri. Nitawaweka huru mtoke kuwa watumwa wao, nami nitawakomboa kwa mkono ulionyooshwa pamoja na matendo makuu ya hukumu. 76:7 Mwa 17:7; Kut 34:9; Eze 11:19-20; 39:6; Rum 9:4; 1Fal 20:13, 28; Isa 43:10; Yoe 3:17Nitawatwaa mwe watu wangu mwenyewe, nami nitakuwa Mungu wenu. Ndipo mtajua kuwa mimi ndimi Bwana Mungu wenu, niliyewatoa chini ya kongwa la Wamisri. 86:8 Mwa 12:7; 14:22; Kut 3:8; Yer 11:5; Eze 20:6; Ufu 10:5-6; Za 136:21-22; Law 18:21Nami nitawaleta mpaka nchi niliyoapa kwa mkono ulioinuliwa kumpa Abrahamu, Isaki na Yakobo. Nitawapa iwe milki yenu. Mimi ndimi Bwana.’ ”

96:9 Mwa 34:30; Kut 2:23Mose akawaarifu Waisraeli jambo hili, lakini hawakumsikiliza kwa sababu ya maumivu makuu ya moyoni na utumwa wa kikatili.

10Ndipo Bwana akamwambia Mose, 116:11 Kut 3:18“Nenda, mwambie Farao mfalme wa Misri awaachie Waisraeli waondoke nchini mwake.”

126:12 Kut 3:18; 4:10Lakini Mose akamwambia Bwana, “Ikiwa Waisraeli hawatanisikiliza, kwa nini yeye Farao anisikilize mimi, ambaye huzungumza kwa kigugumizi?”

Orodha Ya Jamaa Ya Mose Na Aroni

136:13 Kut 3:10Ndipo Bwana akanena na Mose na Aroni kuhusu Waisraeli na Farao mfalme wa Misri, naye akawaamuru wawatoe Waisraeli kutoka Misri.

146:14 Kut 13:3; Hes 1:1; 26:4; Mwa 29:32Hawa walikuwa wakuu wa jamaa zao:

Wana wa Reubeni mzaliwa wa kwanza wa kiume wa Israeli walikuwa Hanoki, Palu, Hesroni na Karmi. Hawa walikuwa ndio koo za Reubeni.

156:15 Mwa 29:33Wana wa Simeoni walikuwa Yemueli, Yamini, Ohadi, Yakini, Sohari na Shauli mwana wa mwanamke Mkanaani. Hawa walikuwa ndio koo za Simeoni.

166:16 Mwa 29:34; 46:11; Hes 3:17; Yos 21:7; 1Nya 6:1, 16Haya ndiyo majina ya wana wa Lawi kufuatana na orodha zao: Gershoni, Kohathi na Merari. Lawi aliishi miaka 137.

176:17 Hes 3:18; 1Nya 6:17Wana wa Gershoni kwa koo, walikuwa Libni na Shimei.

186:18 Hes 3:19, 27; 1Nya 6:18; 23:12Wana wa Kohathi walikuwa Amramu, Ishari, Hebroni na Uzieli. Kohathi aliishi miaka 133.

196:19 1Nya 6:19; 23:21; Hes 3:20, 33Wana wa Merari walikuwa Mahli na Mushi.

Hizi ndizo zilizokuwa koo za Lawi kufuatana na orodha zao.

206:20 Kut 2:1-2; 1Nya 23:13; Hes 26:59Amramu akamwoa Yokebedi, shangazi yake, ambaye alimzalia Aroni na Mose. Amramu aliishi miaka 137.

216:21 1Nya 6:38Wana wa Ishari walikuwa Kora, Nefegi na Zikri.

226:22 Law 10:4; Hes 3:30; 2Nya 29:13Wana wa Uzieli walikuwa Mishaeli, Elisafani na Sithri.

236:23 Rut 4:19-20; 1Nya 2:10; 6:3; 24:1; Hes 2:3; 3:2, 32; 4:28; 16:37-39; 26:60; Kum 10:6; Kut 24:1; Law 10:1-6; 10:12-16Aroni akamwoa Elisheba binti wa Aminadabu ndugu yake Nashoni, naye akamzalia Nadabu, Abihu, Eleazari na Ithamari.

246:24 Hes 16:1; 1Nya 6:22, 37Wana wa Kora walikuwa Asiri, Elikana na Abiasafu. Hawa walikuwa ndio koo za Kora.

256:25 Hes 25:7; 31:6; Yos 24:33; Za 106:30Eleazari mwana wa Aroni akamwoa mmoja wa binti za Putieli, naye akamzalia Finehasi.

Hawa walikuwa ndio wakuu wa jamaa za Walawi, ukoo kwa ukoo.

266:26 Kut 3:10; 7:4; 12:17, 41, 51Hawa walikuwa Aroni na Mose wale wale ambao Bwana aliwaambia, “Watoeni Waisraeli katika nchi ya Misri kwa vikosi vyao.” 27Ndio hao hao waliozungumza na Farao mfalme wa Misri kuhusu kuwatoa Waisraeli Misri. Ilikuwa ni huyo Mose na huyo Aroni.

Aroni Kuzungumza Badala Ya Mose

28Bwana aliponena na Mose huko Misri, 29akamwambia, “Mimi ndimi Bwana. Mwambie Farao mfalme wa Misri kila kitu nikuambiacho.”

306:30 Kut 3:11Lakini Mose akamwambia Bwana, “Kwa kuwa mimi huzungumza kwa kigugumizi, Farao atanisikiliza mimi?”