以賽亞書 41 – CCBT & NEN

Chinese Contemporary Bible (Traditional)

以賽亞書 41:1-29

上帝是以色列的幫助

1上帝說:「眾海島啊,

要在我面前安靜!

讓眾民重新拿出勇力,

讓他們前來說話,

讓我們一起來理論。

2「誰使一人從東方興起?

誰憑公義把他召到跟前?

誰把列國交給他,

使他征服列國的君王,

用刀將他們化為塵土,

用弓將他們淪為風吹的碎稭?

3他追趕他們,

安然走過從未踏足之路。

4誰成就了這事?

誰在太初就掌管歷史的方向?

是我耶和華,

我太初就在那裡,

末了也在那裡。

5「眾海島看見我的作為就害怕,

地極也顫抖,

他們都上前來,

6彼此幫助,

互相勉勵說,『要剛強!』

7工匠鼓勵銀匠,

打磨的勉勵打砧的,

說,『打得好!』

他們用釘子把偶像釘牢,免得搖晃。

8「然而,以色列啊,你是我的僕人;

雅各啊,你是我揀選的,

是我朋友亞伯拉罕的後裔。

9我把你從地極帶來,

從遙遠的角落召來。

我對你說,『你是我的僕人,

我揀選了你,沒有丟棄你。

10我是你的上帝,我必與你同在,

你不用驚慌也不用害怕。

我必賜你力量,幫助你,

用我公義的右手扶持你。』

11「看啊,向你發怒的人必抱愧蒙羞;

與你為敵的人都要滅亡,

歸於無有。

12你尋找與你相爭的人,

卻找不到;

與你爭戰的人必歸於無有。

13因為我是你的上帝耶和華,

我必拉著你的右手對你說,

『不要怕,我必幫助你。』

14「如蛆如蟲的雅各啊,以色列人啊,不要怕!

我耶和華必幫助你。

以色列的聖者是你的救贖主。

15看啊,我要使你成為一具簇新、

帶許多利齒的打穀器。

你要打爛高山,

使丘陵碎如糠秕。

16你要簸它們,讓風吹散它們,

讓狂風捲走它們。

但你要以耶和華為喜樂,

以色列的聖者為榮耀。

17「貧窮困苦的人找不到水喝,

他們口乾舌燥。

但我耶和華必應允他們的呼求,

我——以色列的上帝不會撇棄他們。

18我要使光禿的山嶺上江河奔流,

山谷中泉水湧流;

我要使沙漠變成水塘,

使乾地冒出泉水。

19我要在曠野栽香柏樹、

皂莢樹、番石榴樹和橄欖樹。

我要在沙漠種松樹、杉樹和黃楊樹。

20人一看就知道,

一想就明白,

這是耶和華親手成就的,

以色列的聖者創造的。」

21耶和華對偶像說:

「陳明你們的理由。」

雅各的王說:

「拿出你們的證據吧。」

22告訴我們將要發生的事,

給我們說說以前發生的事,

我們好思想,以便明白事情的結局。

向我們宣告將來的事,

23告訴我們以後會發生什麼,

好叫我們知道你們是神明。

不論降福降禍,顯顯身手吧,

好叫我們一同驚懼!

24看啊,你們實在算不得什麼,

你們所做的毫無意義,

拜你們的人真是可憎!

25「我使一人從北方興起,

他來了,

他在東方求告我的名。

他必把掌權者像灰泥一樣踏在腳下,

像窯匠踩泥一樣踐踏。

26誰從太初就宣告這事,讓我們知道呢?

誰預先講明這事,讓我們說他能未卜先知呢?

誰也沒有說過,

誰也沒有預言過,

誰也沒有聽見你們說過什麼。

27是我首先把這件事告訴錫安

我要給耶路撒冷一個報好消息的使者。

28我看了看,沒有出謀劃策的。

我問話,沒有一個回答。

29看啊,它們全是假的,

毫無作為,虛空如風。

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Isaya 41:1-29

Msaidizi Wa Israeli

141:1 Za 37:7; Isa 48:16; 50:8; Hab 2:20; Zek 2:13; Isa 11:11; 1Sam 2:4“Nyamazeni kimya mbele zangu, enyi visiwa!

Mataifa na wafanye upya nguvu zao!

Wao na wajitokeze, kisha waseme,

tukutane pamoja mahali pa hukumu.

241:2 2Sam 22:43; Isa 40:24; Yer 51:11; Ezr 1:2; Isa 44:28; Yer 50:3; 25:9“Ni nani aliyemchochea mmoja kutoka mashariki,

akimwita katika haki kwa utumishi wake?

Huyatia mataifa mikononi mwake,

na kuwatiisha wafalme mbele zake.

Huwafanya kuwa mavumbi kwa upanga wake,

huwafanya makapi yapeperushwayo na upepo kwa upinde wake.

341:3 Dan 8:4Huwafuatia na kuendelea salama,

katika njia ambayo miguu yake haijawahi kupita.

441:4 Isa 48:12; Ufu 22:13; Mdo 15:18; Isa 43:7; Kum 32:29Ni nani aliyefanya jambo hili na kulitimiliza,

akiita vizazi tangu mwanzo?

Mimi, Bwana, ni wa kwanza

nami nitakuwa pamoja na wa mwisho:

mimi Bwana ndiye.”

541:5 Eze 26:17-18; Kum 30:4; Isa 11:11-12Visiwa vimeliona na kuogopa,

miisho ya dunia inatetemeka.

Wanakaribia na kuja mbele,

641:6 Isa 1:6kila mmoja humsaidia mwingine

na kusema kwa ndugu yake, “Uwe hodari!”

741:7 Isa 40:19; 44:13; Yer 30:3-5Fundi humtia moyo sonara,

yeye alainishaye kwa nyundo

humhimiza yeye agongeaye kwenye fuawe,

Humwambia yeye aunganishaye, “Ni kazi njema.”

Naye huikaza sanamu kwa misumari ili isitikisike.

841:8 Mwa 18:19; Isa 29:22; Neh 9:7; 2Nya 20:7; Yak 2:23; Isa 63:16; Za 136:22“Lakini wewe, ee Israeli, mtumishi wangu,

Yakobo, niliyemchagua,

ninyi wazao wa Abrahamu rafiki yangu,

941:9 Isa 37:16; Kum 7:6; Isa 20:3; 11:12nilikuchukua toka miisho ya dunia,

nilikuita kutoka pembe zake za mbali.

Nilisema, ‘Wewe ni mtumishi wangu’;

nimekuchagua, wala sikukukataa.

1041:10 Kum 3:22; Rum 8:3; Isa 49:8; Yer 30:10; 46:27-28; Ay 40:14; Za 18:35Hivyo usiogope, kwa maana niko pamoja nawe;

usifadhaike, kwa maana mimi ni Mungu wako.

Nitakutia nguvu na kukusaidia;

nitakutegemeza kwa mkono wa kuume wa haki yangu.

1141:11 Isa 17:12; 54:17; Kut 23:22; Isa 29:8; Zek 12:3; Yer 2:3; Isa 29:23“Wote walioona hasira dhidi yako

hakika wataaibika na kutahayarika,

wale wakupingao

watakuwa kama vile si kitu, na kuangamia.

1241:12 Za 37:35-36; Isa 34:12; Ay 7:8; Isa 29:20; 17:14Ingawa utawatafuta adui zako,

hutawaona.

Wale wanaopigana vita dhidi yako

watakuwa kama vile si kitu kabisa.

1341:13 Za 73:23; Isa 42:6; 45:1; 51:18Kwa maana Mimi ndimi Bwana, Mungu wako,

nikushikaye mkono wako wa kuume

na kukuambia, Usiwe na hofu,

nitakusaidia.

1441:14 Ay 4:19; Za 22:6; Kut 15:13; Ay 19:23; Isa 1:27Usiogope, ee Yakobo uliye mdudu,

ee Israeli uliye mdogo,

kwa kuwa Mimi mwenyewe nitakusaidia,” asema Bwana,

Mkombozi wako, yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli.

1541:15 Ay 41:30; Mik 4:13; Isa 21:10; Kut 19:18; Yer 9:10; Eze 33:28“Tazama, nitakufanya chombo cha kupuria,

kipya na chenye makali, chenye meno mengi.

Utaipura milima na kuiponda

na kuvifanya vilima kuwa kama makapi.

1641:16 Yer 51:2; Isa 45:25; 60:19; Dan 2:35; Yer 15:7; Isa 25:9; Mk 1:24Utaipepeta, nao upepo utaichukua,

dhoruba itaipeperushia mbali.

Bali wewe utajifurahisha katika Bwana

na katika utukufu wa yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli.

1741:17 Isa 43:20; 35:7; 30:19“Maskini na wahitaji wanatafuta maji,

lakini hayapo,

ndimi zao zimekauka kwa kiu.

Lakini Mimi Bwana nitawajibu,

Mimi, Mungu wa Israeli, sitawaacha.

1841:18 Isa 30:25; 43:19; Ay 38:26; Isa 35:7; 2Fal 3:17Nitaifanya mito itiririke juu ya vilima vilivyo kame,

nazo chemchemi ndani ya mabonde.

Nitaligeuza jangwa liwe mabwawa ya maji,

nayo ardhi iliyokauka kuwa chemchemi za maji.

1941:19 Isa 60:13; Kut 25:10-13; Isa 37:24; 44:14Katika jangwa nitaotesha

mwerezi, mshita, mhadasi na mzeituni.

Nitaweka misunobari, mivinje na misanduku

pamoja huko nyikani,

2041:20 Ay 12:9; Isa 4:5ili kwamba watu wapate kuona na kujua,

wapate kufikiri na kuelewa,

kwamba mkono wa Bwana umetenda hili,

kwamba yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli ndiye alilifanya.”

2141:21 Isa 43:14; 44:6Bwana asema, “Leta shauri lako.

Toa hoja yako,” asema Mfalme wa Yakobo.

2241:22 Isa 48:14; 65:17; Yn 13:19; Isa 43:9; 45:21“Leteni sanamu zenu zituambie

ni nini kitakachotokea.

Tuambieni mambo ya zamani yalikuwa nini,

ili tupate kuyatafakari

na kujua matokeo yake ya mwisho.

Au tutangazieni mambo yatakayokuja,

2341:23 Kum 18:22; Isa 44:7-8; Yer 10:5; Isa 43:5; 2Fal 19:26tuambieni ni nini kitakachotokea baadaye,

ili tupate kujua kuwa ninyi ni miungu.

Fanyeni jambo lolote zuri au baya,

ili tupate kutishika na kujazwa na hofu.

2441:24 Isa 37:19; 1Kor 8:4; Za 115:8; 1Sam 12:21; Isa 48:8Lakini ninyi ni zaidi ya bure kabisa,

na kazi zenu hazifai kitu kabisa;

yeye awachaguaye ni chukizo sana.

2541:25 Yer 51:48; Nah 3:14; 2Sam 22:43; Yer 50:9“Nimemchochea mtu mmoja kutoka kaskazini,

naye yuaja, mmoja toka mawio ya jua aliitaye Jina langu.

Huwakanyaga watawala kana kwamba ni matope,

kama mfinyanzi akanyagavyo udongo wa kufinyangia.

2641:26 Hab 2:18-19; 1Fal 18:26; Isa 52:6Ni nani aliyenena hili tokea mwanzoni, ili tupate kujua,

au kabla, ili tuweze kusema, ‘Alikuwa sawa’?

Hakuna aliyenena hili,

hakuna aliyetangulia kusema hili,

hakuna yeyote aliyesikia maneno kutoka kwenu.

2741:27 Isa 48:3, 16; 40:9Nilikuwa wa kwanza kumwambia Sayuni,

‘Tazama, wako hapa!’

Nilimpa Yerusalemu mjumbe wa habari njema.

2841:28 Eze 22:30; Za 22:11; Isa 40:13-14; 50:2; 59:16; 64:7; Yer 25:4Ninatazama, lakini hakuna yeyote:

hakuna yeyote miongoni mwao awezaye kutoa shauri,

hakuna yeyote wa kutoa jibu wakati ninapowauliza.

2941:29 Yer 5:13; 1Sam 12:21; Isa 37:19Tazama, wote ni ubatili!

Matendo yao ni bure;

vinyago vyao ni upepo mtupu na machafuko.