以賽亞書 40 – CCBT & NEN

Chinese Contemporary Bible (Traditional)

以賽亞書 40:1-31

上帝對祂子民的安慰

1你們的上帝說:

「你們要安慰我的子民。

2要溫柔地告訴耶路撒冷

她的苦難已經結束,

她的罪惡已經被除去。

她因自己的一切罪已受到耶和華加倍的懲罰40·2 她因自己的一切罪已受到耶和華加倍的懲罰」或譯「她的一切罪已得到耶和華雙倍的赦免」。。」

3聽啊,有人高喊:

「在曠野預備耶和華的道,

在沙漠修直我們上帝的路。

4一切山谷將被填滿,

大山小丘將被削平;

坎坷之地將變得平坦,

崎嶇的地面將成為平原。

5耶和華的榮耀必彰顯,

世人必一同看見。

這是耶和華親口說的。」

6有聲音說:「呼喊吧!」

我問道:「我呼喊什麼呢?」

那聲音說:「芸芸眾生盡如草,

榮華富貴像野地的花。

7耶和華吹一口氣,

草就枯乾,花也凋殘。

人類誠然像草。

8草必枯乾,花必凋殘,

唯有我們上帝的話永遠長存。」

9錫安報告好消息的人啊,

要登上高山!

耶路撒冷報告好消息的人啊,

要大聲宣告!

要提高聲音,不要懼怕!

要高聲對猶大的城邑說:

「你們的上帝來了!」

10看啊,主耶和華帶著能力來了,

祂的臂膀執掌王權;

祂帶著賞賜而來,

要酬勞祂的子民。

11祂像牧人一樣牧養自己的羊群,

用臂膀把羊羔聚在一起,

抱在懷中,

溫柔地引導母羊。

12誰曾用手心量海水?

誰曾用手掌度蒼天?

誰曾用升斗盛大地的塵土?

誰曾用秤稱高山,用天平稱丘陵?

13誰曾測度耶和華的心?

誰曾做祂的謀士指點祂?

14祂請教過誰?

誰教過祂正道?

誰教過祂知識?

誰指點過祂領悟之道?

15看啊,列國就像水桶中的一滴水,

又如天平上的塵埃。

祂舉起眾海島,好像捧起微塵。

16黎巴嫩的樹木不夠作獻祭的燃料,

林中的走獸也不夠作燔祭。

17萬國在祂面前都算不得什麼,

在祂看來不過是虛無。

18你們拿誰與上帝相比呢?

你們用什麼形像比作上帝呢?

19偶像是工匠製造的,

銀匠替它包上金子、打造銀鏈。

20買不起這種偶像的人就選一塊耐用的木頭,

找個精巧的工匠,

雕出一個可以站立不倒的偶像。

21難道你們不知道嗎?

難道你們沒有聽過嗎?

難道不是從起初就告訴過你們嗎?

難道從大地奠立根基以來,

你們一直沒有明白嗎?

22上帝的寶座設立在大地的圓圈之上,

地上的人類好像蚱蜢。

祂鋪展諸天,就像鋪展幔子、鋪展人居住的帳篷。

23祂使掌權者歸於無有,

使世上的審判官化為虛無。

24他們像草一樣剛被栽上,

剛被種上,

剛在土裡扎根,

上帝一口氣吹來,便都枯乾了,

暴風將他們像禾稭一樣吹去。

25那位聖者說:「你們拿誰與我相比,

使之與我同等呢?」

26你們向天舉目,

看看是誰創造了這萬象?

是誰把眾星一一領出來,

給它們取名?

祂的權柄和能力極大無比,

它們一個也不會少。

27雅各啊,你怎能說耶和華看不見你的遭遇呢?

以色列啊,你怎能說上帝並不顧念你的冤情呢?

28難道你不知道?

難道你沒有聽見過?

永恆的上帝耶和華——創造地極的主宰不會疲乏也不會困倦,

祂的智慧深不可測。

29祂賜疲乏的人能力,

給軟弱的人力量。

30即使青年也會疲乏困倦,

強壯的人也會踉蹌跌倒;

31但仰望耶和華的人必重新得力。

他們必像鷹一樣展翅高飛,

他們奔跑也不困倦,

他們行走也不疲乏。

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Isaya 40:1-31

Faraja Kwa Watu Wa Mungu

140:1 Zek 1:17; 2Kor 1:3; Sef 3:14-17; Yer 31:13; Isa 49:13; 57:18Wafarijini, wafarijini watu wangu,

asema Mungu wenu.

240:2 Mwa 34:3; Isa 41:11-13; 49:25; Zek 9:12; Ufu 18:6; Yer 16:18; Law 26:4Sema na Yerusalemu kwa upole,

umtangazie

kwamba kazi yake ngumu imekamilika,

kwamba dhambi yake imefanyiwa fidia,

kwamba amepokea kutoka mkononi mwa Bwana

maradufu kwa ajili ya dhambi zake zote.

340:3 Isa 11:16; Mt 3:3; Mal 3:1; Mk 1:3; Isa 43:19; Yn 1:23Sauti ya mtu aliaye:

“Itengenezeni jangwani njia ya Bwana,

nyoosheni njia kuu nyikani

kwa ajili ya Mungu wetu.

440:4 Za 26:12; Yer 31:9; Isa 2:14; 49:11; 26:7; 45:2Kila bonde litainuliwa,

kila mlima na kilima kitashushwa;

penye mabonde patanyooshwa,

napo palipoparuza patasawazishwa.

540:5 Kut 16:7; Isa 58:14; Lk 3:4-6; Eze 36:23; Hes 14:21; Isa 59:19; Lk 2:20Utukufu wa Bwana utafunuliwa,

nao wanadamu wote watauona pamoja.

Kwa maana kinywa cha Bwana kimenena.”

640:6 Ay 14:2; Mwa 6:3; Isa 29:5Sauti husema, “Piga kelele.”

Nami nikasema, “Nipige kelele gani?”

“Wanadamu wote ni kama majani,

nao utukufu wao wote

ni kama maua ya kondeni.

740:7 Kut 15:10; Ay 41:21; Yos 8:12; Isa 15:6; Za 103:6; Eze 22:21Majani hunyauka na maua huanguka,

kwa sababu pumzi ya Bwana huyapuliza.

Hakika wanadamu ni majani.

840:8 1Pet 1:25; Isa 59:21; Mt 5:18; Za 119:89; Isa 5:24; Yak 1:10; Mit 19:21Majani hunyauka na maua huanguka,

lakini neno la Mungu wetu ladumu milele.”

940:9 Nah 1:15; Isa 25:9; Rum 10:15; Isa 41:27; 52:7-10; 1Kor 15:1-4Wewe uletaye habari njema Sayuni,

panda juu ya mlima mrefu.

Wewe uletaye habari njema Yerusalemu,

inua sauti yako kwa kupiga kelele,

inua sauti, usiogope;

iambie miji ya Yuda,

“Yuko hapa Mungu wenu!”

1040:10 Ufu 22:7; Isa 35:4; Za 44:3; Isa 9:6-7; Ufu 22:12; Mt 21:5; Isa 28:2Tazameni, Bwana Mwenyezi anakuja na nguvu,

nao mkono wake ndio utawalao kwa ajili yake.

Tazameni, ujira wake u pamoja naye,

nayo malipo yake yanafuatana naye.

1140:11 Za 28:9; Yn 10:11; Ebr 13:20; Mwa 48:15; Mik 5:4; Hes 12:11; Kum 26:19Huchunga kundi lake kama mchungaji wa mifugo:

Hukusanya wana-kondoo katika mikono yake

na kuwachukua karibu na moyo wake,

huwaongoza taratibu wale wanyonyeshao.

1240:12 Mit 30:4; Ebr 1:10-12; Ay 38:10; 12:15; Mit 16:11Ni nani aliyepima maji ya bahari

kwenye konzi ya mkono wake,

au kuzipima mbingu kwa shibiri40:12 Shibiri ni sawa na sentimita 20 au inchi 8. yake?

Ni nani aliyeyashika mavumbi ya dunia katika kikapu,

au kupima milima kwenye kipimio

na vilima kwenye mizani?

1340:13 Ay 15:8; 1Kor 2:16; Rum 11:34Ni nani aliyeyafahamu mawazo ya Bwana,

au kumfundisha akiwa kama mshauri wake?

1440:14 Ay 21:22; Kol 2:3; Ay 12:13; 34:13; Isa 55:9Ni nani ambaye Bwana ametaka shauri kwake ili kumwelimisha,

naye ni nani aliyemfundisha njia iliyo sawa?

Ni nani aliyemfundisha maarifa

au kumwonyesha mapito ya ufahamu?

1540:15 Za 62:9; Isa 2:22; Kum 9:21Hakika mataifa ni kama tone ndani ya ndoo,

ni kama vumbi jembamba juu ya mizani,

huvipima visiwa kana kwamba vilikuwa vumbi laini.

1640:16 Mik 6:7; Ebr 10:5-9; Isa 37:24; Za 50:9-11Lebanoni hautoshi kwa moto wa madhabahuni,

wala wanyama wake hawatoshi kwa sadaka za kuteketezwa.

1740:17 Isa 30:28; Ay 12:19; Isa 29:7; Dan 4:35; Isa 37:19Mbele yake mataifa yote ni kama si kitu,

yanaonekana yasio na thamani

na zaidi ya bure kabisa.

1840:18 Mdo 17:29; Kut 8:10; Kum 4:15; 1Sam 2:2Basi, utamlinganisha Mungu na nani?

Utamlinganisha na kitu gani?

1940:19 Kut 20:4; Zek 10:2; Yer 10:3-4; Isa 31:7; 37:19; 42:17; Hab 2:18Kwa habari ya sanamu, fundi huisubu,

naye mfua dhahabu huifunika kwa dhahabu

na kuitengenezea mikufu ya fedha.

2040:20 Isa 44:19; 5:3Mtu aliye maskini sana asiyeweza kuleta sadaka kama hii

huuchagua mti usiooza.

Humtafuta fundi stadi

wa kusimamisha sanamu ambayo haitatikisika.

2140:21 Mdo 14:17; Rum 1:19; Isa 48:13; 51:13; 2Fal 19:25Je, hujui?

Je, hujasikia?

Je, hujaambiwa tangu mwanzo?

Je, hujafahamu tangu kuumbwa kwa dunia?

2240:22 Hes 13:33; Ay 22:14; 36:29; 2Nya 6:18; Isa 48:13; Ay 26:7Anakaa kwenye kiti cha enzi juu ya duara ya dunia,

nao watu wakaao ndani yake ni kama panzi.

Huzitandaza mbingu kama chandarua,

na kuzitandaza kama hema la kuishi.

2340:23 Ay 12:18; Isa 34:12; Za 107:40; Amo 2:3Huwafanya wakuu kuwa si kitu,

na kuwashusha watawala wa dunia hii kuwa kitu bure.

2440:24 2Sam 22:16; Isa 11:4; Ay 5:3; 8:12; 18:16; 24:24; Isa 41:2, 16Mara baada ya kupandwa,

mara baada ya kutiwa ardhini,

mara baada ya kutoa mizizi yao ardhini,

ndipo huwapulizia nao wakanyauka,

nao upepo wa kisulisuli

huwapeperusha kama makapi.

2540:25 Kum 4:15; Mdo 17:24-29; 1Nya 16:25; Isa 37:23“Utanilinganisha mimi na nani?

Au ni nani anayelingana nami?” asema yeye Aliye Mtakatifu.

2640:26 Za 89:11-13; 2Fal 17:16; Neh 9:6; Isa 34:16; 51:6; Ay 9:4; Efe 1:19Inueni macho yenu mtazame mbinguni:

Ni nani aliyeumba hivi vyote?

Ni yeye aletaye nje jeshi la nyota moja baada ya nyingine

na kuziita kila moja kwa jina lake.

Kwa sababu ya uweza wake mkuu na nguvu zake kuu,

hakuna hata mojawapo inayokosekana.

2740:27 Ay 6:29; Lk 18:7-8; Ay 27:2Kwa nini unasema, ee Yakobo,

nanyi ee Israeli, kulalamika,

“Njia yangu imefichwa Bwana asiione,

Mungu wangu hajali shauri langu?”

2840:28 Kum 33:27; Za 90:2; Rum 11:33; Isa 37:16; 44:12; Za 147:5Je wewe, hufahamu?

Je wewe, hujasikia?

Bwana ni Mungu wa milele,

Muumba wa miisho ya dunia.

Hatachoka wala kulegea,

wala hakuna hata mmoja

awezaye kuupima ufahamu wake.

2940:29 Isa 57:19; Yer 31:25; Mwa 18:14; Za 68:35; 119:28Huwapa nguvu waliolegea

na huongeza nguvu za wadhaifu.

3040:30 Isa 9:17; Yer 9:21; Isa 5:27Hata vijana huchoka na kulegea,

nao vijana wanaume hujikwaa na kuanguka,

3140:31 2Fal 6:33; Kut 19:4; Ebr 12:1-3; Mao 3:25; 2Kor 4:8-10, 16; Za 37:9; Isa 30:18bali wale wamtumainio Bwana

atafanya upya nguvu zao.

Watapaa juu kwa mbawa kama tai;

watapiga mbio wala hawatachoka,

watatembea kwa miguu wala hawatazimia.