申命记 28 – CCB & NEN

Chinese Contemporary Bible (Simplified)

申命记 28:1-68

遵守诫命蒙祝福

1“你们若全心顺服你们的上帝耶和华,谨遵祂今天借我吩咐你们的一切诫命,祂必使你们超越天下万国。 2你们若听从你们的上帝耶和华的话,以下的福气必临到你们,追随你们。

3“无论你们住在城里还是乡村,都必蒙福。

4“你们必子孙昌盛,五谷丰登,牛羊成群。

5“你们的篮子和揉面盆都必蒙福。

6“你们必出入平安。

7“耶和华必使来犯之敌败在你们面前、溃不成军、四散逃命。

8“耶和华必使你们凡事蒙福、五谷满仓。你们的上帝耶和华必在祂赐给你们的土地上赐福你们。

9“你们若遵守你们上帝耶和华的诫命,遵行祂的旨意,祂必按自己的誓言使你们成为祂圣洁的子民。 10天下万民将看出你们是耶和华的子民,并惧怕你们。

11“在耶和华向你们祖先起誓要赐给你们的土地上,祂必使你们子孙昌盛、牛羊成群、五谷丰登。 12耶和华要为你们打开天上美好的仓库,使你们风调雨顺、凡事蒙福。你们必借贷给多国,却无需向别国借贷。 13-14你们若听从你们的上帝耶和华借我今天吩咐你们的诫命,谨慎遵行,毫不偏离,也不随从、供奉别的神明,祂必使你们做首不做尾,居上不居下。

违背诫命受咒诅

15“你们若不听从你们的上帝耶和华,不谨遵祂今天借我吩咐你们的一切诫命和律例,祂必使以下的咒诅临到你们。

16“无论你们住在城里还是乡村,都必受咒诅。

17“你们的篮子和揉面盆都必受咒诅。

18“妇女所生的,土地所产的,牛羊所生的都必受咒诅。

19“你们出入都必受咒诅。

20“因为你们背弃耶和华,祂要使你们凡事受咒诅、混乱不堪、饱受责罚,直到你们被毁灭,迅速灭亡。

21“祂要使瘟疫紧紧跟随你们,直到你们在将要占领的土地上被灭绝。

22“祂要使你们遭受痨病、热症、疟疾、炙热、刀剑、干旱和霉烂之灾,直到你们灭亡。

23“祂要使你们头顶的天如铜,脚下的地如铁。

24“祂要使雨水变为尘土,降在你们身上,直到你们灭亡。

25“祂要使你们被敌人击败、溃不成军、四散逃命,下场令天下万国惊惧。 26你们的尸体要成为飞禽走兽的食物,必无人赶走它们。

27“祂要使你们患埃及的脓疮、肿瘤和癣疥,无药可治。

28“祂要使你们发疯、失明、心智错乱。

29“你们必在大白天摸索,就像盲人在黑暗中摸索一样,你们的道路必不得亨通,你们要终日受人欺压抢掠,无人搭救。

30“你们聘了妻子,别人必占有她;你们盖了房屋,必不能住在里面;你们栽种葡萄园,必吃不到园中的出产。

31“你们必看着自己的牛被宰杀却吃不到肉,自己的驴被抢走后一去不还,自己的羊被敌人掳走却无人搭救, 32自己的儿女被外族人掳走,你们终日望眼欲穿,却无能为力。

33“与你们素不相识的民族必吃光你们土地的出产和劳碌所得,你们必常受欺压, 34以致眼前的一切令你们发疯。

35“耶和华要使你们从头到脚长满毒疮,无药可治。

36“耶和华要带你们和你们的王到一个你们和你们祖先都不知道的国家,你们要在那里供奉木石神像。

37“在耶和华驱逐你们去的列国,你们的下场将很可怕,受尽嘲笑和讥讽。

38“你们种的多,却收的少,因为庄稼必被蝗虫吃掉。

39“你们栽种、修剪葡萄园,却吃不到葡萄,也喝不到葡萄酒,因为葡萄必被虫子吃掉。

40“你们境内长满橄榄树,却没有橄榄油抹身,因为橄榄必未熟先落。

41“你们生儿育女,却留不住一个,因为他们必被掳走。

42“蝗虫要吃光你们的树木和地上的出产。

43“你们中间的外族人要日益兴旺,你们却要日渐衰微。

44“他们要借贷给你们,你们却不能借贷给他们。他们要做首,你们要做尾。

45“如果你们不听你们上帝耶和华的话,不遵守祂吩咐你们的诫命和律例,这些咒诅都必临到你们、追赶你们,直到毁灭你们。 46这些咒诅要永远成为你们和你们子孙的警戒和征兆。 47如果你们在富足时不心甘情愿地事奉你们的上帝耶和华, 48你们必失去所有,饥饿干渴、赤身裸体地侍奉耶和华派来攻击你们的敌人。祂要把铁轭加在你们的颈上,直到消灭你们。

49“耶和华要使一国从遥远的地极兴起,他们要如鹰飞来袭击你们。你们不懂他们的语言。 50他们面目狰狞,不尊重年老的,也不怜悯年少的。 51他们要吃光你们的牛羊、五谷、新酒和油,直到消灭你们。 52在你们的上帝耶和华所赐给你们的土地上,他们要把你们围困在各个城邑中,直到你们所依赖的高大坚固的城墙都倒塌。

53“当你们被敌人围困、陷入绝境时,你们必吃自己的亲生骨肉——你们的上帝耶和华赐给你们的儿女。 54-55因为被敌人困在城中,饥饿难熬,连你们中间最温柔体贴的男人也要独自吞吃子女的肉,不肯分给自己的兄弟、爱妻和剩下的儿女。 56-57因为被敌人困在城中,饥饿难熬,连你们中间最温柔、娇嫩得连脚也不肯踏在地上的妇女,都要偷偷吃掉自己生的婴儿和胎胞,不肯分给所爱的丈夫和子女。

58“如果你们不谨遵这书上所写的一切律法,不敬畏你们的上帝耶和华那荣耀、可畏的名, 59祂必使你们及子孙遭遇严重而长久的灾难和疾病, 60使你们所惧怕的埃及人的疾病都降在你们身上,缠扰你们, 61还使一切未记在这律法书上的疾病和灾难降在你们身上,直到消灭你们。 62如果你们不听从你们的上帝耶和华的话,即使你们的人数多如天上的星,也将所剩无几。 63正如耶和华喜欢赐福你们,使你们人丁兴旺,祂也同样会不惜消灭你们,使你们在将要占领的土地上灭亡。

64“耶和华要把你们分散到天下万邦,你们要在那里供奉祖祖辈辈素不认识的木石神像。 65你们在万邦中将不得安宁,没有落脚之地,耶和华必使你们胆战心惊、目光呆滞、精神颓废。 66你们必惴惴不安,昼夜恐惧,生死难料。 67你们必看见可怕之事,以致心中充满恐惧,早上盼望天黑,晚上盼望天亮。 68耶和华必沿着我曾说你们再不会走的路线,用船把你们送回埃及。你们将在那里卖身做敌人的仆婢,却无人买。”

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Kumbukumbu 28:1-68

Baraka Za Utiifu

(Walawi 26:3-13; Kumbukumbu 7:12-24)

128:1 Kum 15:5; Law 26:3; Hes 24:7; Kum 26:19; Kut 15:26; Za 106:3; 111:10; Isa 1:19; 3:10; Yer 11:4; 12:16; 1Nya 14:2; Rum 2:10Kama ukimtii Bwana Mungu wako kwa bidii na kufuata amri zake zote ninazokupa leo kwa bidii, Bwana Mungu wako atakuweka juu ya mataifa yote katika dunia. 228:2 Yer 32:24; Zek 1:6Baraka hizi zote zitakuja juu yako na kukupata, kama ukimtii Bwana Mungu wako:

328:3 Za 144:15; Mwa 39:5; Za 128:1-4Utabarikiwa mjini na utabarikiwa mashambani.

428:4 Mwa 49:25; Kum 8:18; Mit 10:22; 1Tim 4:8Utabarikiwa uzao wa tumbo lako, na mazao ya nchi yako na wanyama wako wachanga wa kufugwa, yaani ndama wa makundi yako ya ngʼombe, na wana-kondoo wa makundi yako.

5Kapu lako na vyombo vyako vya kukandia vitabarikiwa.

628:6 Za 121:8Utabarikiwa uingiapo na utabarikiwa utokapo.

728:7 2Nya 6:34; Law 26:8, 17Bwana atasababisha adui wainukao dhidi yako kushindwa mbele yako. Watakujia kwa njia moja lakini watakimbia mbele yako kwa njia saba.

828:8 Kum 15:4Bwana ataagiza baraka juu ya ghala zako na juu ya kila kitu utakachogusa kwa mkono wako. Bwana Mungu wako atakubariki katika nchi anayokupa.

928:9 Kut 19:6; Law 26:3; Kum 7:6Bwana atakufanya kuwa taifa lake takatifu, kama alivyokuahidi kwa kiapo, kama ukishika maagizo ya Bwana Mungu wako na kwenda katika njia zake. 1028:10 Hes 6:27; 1Fal 8:43; Yer 25:29; Dan 9:18; 2Nya 7:14Kisha mataifa yote ya dunia wataona kuwa unaitwa kwa jina la Bwana, nao watakuogopa. 1128:11 Kum 30:9; Mwa 30:27; Mit 10:22Bwana atakupa kustawi kwa wingi, katika tunda la uzao wa tumbo lako, katika wanyama wachanga wa mifugo yako na katika mazao ya ardhi yako, katika nchi aliyowaapia baba zako kuwapa.

1228:12 Ay 38:22; Za 135:7; Yer 10:13; 51:16; Za 65:11; 58:10; Yer 31:12; Law 26:4; 1Fal 8:35-36; 18:1; Za 104:13; Isa 5:6; 30:23; 32:20; 61:9; 65:23; Yer 32:38-41; Mal 3:12; Law 25:19; Kum 15:3-6; Eze 34:26Bwana atafungua mbingu, ghala zake za baraka, kukupa mvua kwa majira yake na kubariki kazi zako zote za mikono yako. Utakopesha mataifa mengi lakini hutakopa kwa yeyote. 1328:13 Yer 11:6; Kum 26:19Bwana atakufanya kichwa, wala si mkia. Kama utazingatia maagizo ya Bwana Mungu wako ninayokupa siku hii ya leo na kuyafuata kwa bidii, daima utakuwa juu, kamwe hutakuwa chini. 1428:14 Kum 5:32; Yos 1:7Usihalifu amri zangu zozote ninazokupa leo, kwa kwenda kuume au kushoto, kwa kufuata miungu mingine na kuitumikia.

Laana Kwa Kutokutii

(Walawi 26:14-46)

1528:15 1Fal 9:6; 2Nya 7:19; Kum 27:26; 27:26; Yos 23:15; 2Nya 12:5; Dan 9:11; Mal 2:2Hata hivyo, kama hutamtii Bwana Mungu wako na kuzishika kwa bidii amri zake zote na maagizo ninayokupa leo, laana hizi zote zitakuja juu yako na kukupata:

16Utalaaniwa mjini na utalaaniwa mashambani.

17Kapu lako na chombo chako cha kukandia kitalaaniwa.

1828:18 Isa 3:1; Hab 3:17Uzao wa tumbo lako utalaaniwa, mazao ya ardhi yako, ndama wa makundi yako ya ngʼombe na wana-kondoo wa makundi yako.

19Utalaaniwa uingiapo na utokapo.

2028:20 Law 26:16; Yer 42:18; Mal 2:2; 3:9; 4:6; Za 39:11; 76:6; 80:16; Isa 17:13; 51:20; 54:9; 66:15; Eze 5:15; Kum 4:26; Kut 32:22Bwana ataleta laana juu yako, fadhaa na kukaripiwa katika kila kitu unachokigusa kwa mkono wako, mpaka uwe umeharibiwa na kuangamizwa ghafula kwa ajili ya maovu uliyoyafanya kwa kumwacha yeye. 2128:21 Law 26:25; Hes 14:12; Yer 24:10; Amo 4:10Bwana atakupiga kwa magonjwa mpaka akuangamize kutoka nchi unayoingia kuimiliki. 2228:22 Kum 32:24; Law 26:16; 2Fal 8:1; Ay 12:15; Za 105:16; Yer 14:1; Hag 1:11; Mal 3:9; Hag 2:17; Law 26:25; Kum 4:26; Amo 4:9Bwana atakupiga kwa magonjwa ya kudhoofisha, kwa homa na kuwashwa, hari na kwa ukame, kutu na kuwa na uchungu ambavyo vitakupiga mpaka uangamie.

2328:23 Law 26:19Anga juu yako itakuwa shaba, na ardhi chini yako itakuwa chuma. 2428:24 Law 26:19; Kum 11:17; 1Fal 8:35; 17:1; Isa 5:6; Yer 14:1; Hag 1:10Bwana atafanya mvua ya nchi yako kuwa mavumbi na mchanga; vitakujia kutoka angani mpaka uangamie.

2528:25 1Sam 4:10; Za 78:62; Law 26:17; 2Nya 29:8; 30:7; Yer 15:4; 24:9; 26:6; 29:18; 44:12; Eze 23:46Bwana atakufanya ushindwe mbele ya adui zako. Utawajia kwa njia moja lakini utawakimbia mbele yao kwa njia saba, nawe utakuwa kitu cha kuchukiza kwa falme zote za dunia. 2628:26 Mwa 40:19; Za 79:2; Isa 18:6; Yer 7:33; 12:9; 15:2; 16:4; 19:7; 34:20Mizoga yenu itakuwa chakula cha ndege wa angani na wanyama wa nchi, wala hapatakuwepo mtu yeyote wa kuwafukuza. 2728:27 Kum 7:15; 1Sam 5:6Bwana atakupiga kwa majipu ya Misri na kwa vidonda vitokavyo usaha na kuwashwa, ambako huwezi kuponywa. 28Bwana atakupiga kwa wazimu, upofu na kuchanganyikiwa kwa akili. 2928:29 Mwa 19:11; Kut 10:21; Ay 5:14; 12:25; 24:13; 38:15; Isa 59:10; Amu 3:9; 2Fal 13:5; Es 4:14; Isa 19:20; 43:11; Hos 13:4; Oba 1:21Wakati wa adhuhuri utapapasapapasa huku na huko kama mtu kipofu katika giza. Hutafanikiwa katika lolote ufanyalo; siku baada ya siku utaonewa na kunyangʼanywa, wala hakuna yeyote atakayekuokoa.

3028:30 Ay 31:10; Isa 65:22; Amo 5:11; Yer 12:13; 8:10Utaposa mke, lakini mtu mwingine atakutana naye kimwili. Utajenga nyumba, lakini hutaishi ndani yake. Utapanda shamba la mizabibu, lakini hutakula matunda yake. 31Ngʼombe wako atachinjwa mbele ya macho yako lakini hutakula nyama yake. Punda wako atachukuliwa kwa nguvu kutoka kwako wala hatarudishwa. Kondoo wako watapewa adui zako, wala hakuna mtu yeyote wa kuwaokoa. 32Wanao na binti zako watatolewa kwa mataifa mengine, nawe utayachosha macho yako ukiwatazamia siku baada ya siku, hutakuwa na nguvu kuinua mkono. 3328:33 Yer 5:15-17; Eze 25:4Taifa usilolijua watakula mazao ya nchi yako na taabu ya kazi yako, hutakuwa na chochote, bali kuonewa kikatili siku zako zote. 34Vitu utakavyoviona kwa macho yako vitakufanya wazimu. 3528:35 Kum 7:15; Ufu 16:2; Ay 2:7; 7:5; 13:28; 30:17; Isa 1:6Bwana atayapiga magoti yako na miguu yako kwa majipu yenye maumivu makali yasiyoponyeka, yakienea kutoka nyayo za miguu yako hadi utosini.

3628:36 1Sam 12:25; Kum 4:27; 2Fal 24:14; 25:7-11; 2Nya 33:11; 36:21; Ezr 5:12; Yer 15:14; 16:13; 27:20; 29:1-9; 52:28; Mao 1:3; Kum 4:28Bwana atakupeleka wewe na mfalme uliyemweka juu yako uende kwenye taifa ambalo hukulijua wewe wala baba zako. Huko utaabudu miungu mingine, miungu ya miti na mawe. 3728:37 Yer 42:18; Eze 5:15; Za 22:7; 39:8; 44:13; 64:8; Yer 18:16; 48:27; Mik 6:16; 2Nya 7:20; Ezr 9:7; Yer 44:8; 1Fal 9:7; Za 44:14; Yer 19:8; 24:9; 25:9, 18; 29:18; Mao 2:15Utakuwa kitu cha kuchukiza, tena kitu cha kudharauliwa na kudhihakiwa kwa mataifa yote huko Bwana atakakokupeleka.

3828:38 Law 26:20; Za 129:7; Isa 5:10; Yer 12:13; Hos 8:7; Mik 6:15; Hag 1:6-9; 2:16; Kut 10:4; 10:15; Yoe 1:4Utapanda mbegu nyingi katika shamba lakini utavuna haba, kwa sababu nzige watazila. 3928:39 Law 10:9; Yoe 1:4; 2:25; Mal 3:11; Isa 5:10; 17:10-11; Sef 1:13Utapanda mashamba ya mizabibu na kuyapalilia, lakini hutakunywa divai yake wala hutakusanya zabibu, kwa sababu wadudu watazila. 4028:40 Yer 11:16; Mik 6:15Utakuwa na mizeituni katika nchi yako yote, lakini hutatumia hayo mafuta yake, kwa sababu zeituni zitapukutika. 41Utakuwa na wana na binti lakini hawatakuwa nawe, kwa sababu watachukuliwa mateka. 4228:42 Amu 6:5; 7:12; Yer 46:23Makundi ya nzige yatavamia miti yako yote na mazao ya nchi yako.

43Mgeni anayeishi miongoni mwako atainuka juu zaidi na zaidi kuliko wewe, lakini wewe utashuka chini zaidi na zaidi. 4428:44 Kum 26:19Yeye atakukopesha, lakini wewe hutamkopesha. Yeye atakuwa kichwa, lakini wewe utakuwa mkia.

4528:45 Kut 15:9; Kum 4:25-26Laana hizi zote zitakuja juu yako. Zitakufuatia na kukupata mpaka uangamizwe, kwa sababu hukumtii Bwana Mungu wako, na kuzishika amri zake na maagizo yake aliyokupa. 4628:46 Hes 16:38; Za 71:7; Isa 8:18; 20:3; Eze 5:15; Zek 3Zitakuwa ishara na ajabu kwako na kwa wazao wako milele. 4728:47 Kum 10:12; Law 23:20; Neh 9:35; 9:35-37Kwa sababu hukumtumikia Bwana Mungu wako kwa furaha na kwa moyo wakati wa kufanikiwa kwako, 4828:48 Yer 14:3; Mao 4:4; Yer 28:13-14; Mwa 49:8; Isa 47:6; Yer 27:12; 28:14; Mt 11:29kwa hiyo katika njaa na kiu, katika uchi na umaskini wa kutisha, utawatumikia adui ambao Bwana atawatuma dhidi yako. Yeye ataweka nira ya chuma shingoni mwako hadi amekwisha kukuangamiza.

4928:49 Law 26:44; Isa 5:26-30; 7:18-20; 39:3; Yer 4:16; 5:15; 6:22; 25:32; 31:8; Hab 1:6; 2Sam 1:23; Yer 4:13; 48:40; 49:22; Mao 4:19; Eze 17:3; Hos 8:1; Mwa 11:7; 1Kor 14:21Bwana ataleta taifa dhidi yako kutoka mbali, kutoka miisho ya dunia, kama tai ashukiavyo mawindo chini, taifa ambalo hutaijua lugha yake, 5028:50 Isa 47:6taifa lenye uso mkali lisilojali wazee wala kuwahurumia vijana. 5128:51 Za 4:7; Isa 36:17; Hag 1:11; Hes 18:12; Amu 6:428:51 Isa 1:7; 62:8; Yer 5:15-17Watakula wadogo wa mifugo yako na mazao ya nchi yako mpaka umeangamia. Hawatakuachia nafaka, divai mpya au mafuta, wala ndama wowote wa kundi lako au wana-kondoo wa kundi lako mpaka umekuwa magofu. 5228:52 2Fal 6:24; Yer 10:18; Eze 1:10; Sef 1:14-17Nao wataizingira miji yote katika nchi yako mpaka kuta ndefu za ngome ambazo unazitegemea zimeanguka. Watazingira miji yote katika nchi ambayo Bwana Mungu wako anakupa.

5328:53 Law 26:29; 2Fal 6:28-29; Mao 2:20; 4:10; Yer 19:9Utakula uzao wa tumbo lako, nyama ya wana wako na binti zako ambao Bwana Mungu wako amekupa, kwa sababu ya mateso yale adui zako watakayokuletea wakati wa kukuzingira. 54Hata yule mtu muungwana sana na makini miongoni mwako hatakuwa na huruma kwa ndugu yake mwenyewe au kwa mke ampendaye au watoto wake waliosalia, 5528:55 2Fal 6:29naye hatampa hata mmoja wao nyama ya watoto wake ambao anawala. Kwa kuwa hakuna kitu kingine kilichosalia kwake katika mazingirwa makali ambayo adui yako watakuletea kwa miji yako yote. 5628:56 Isa 47:1; Mao 4:10Mwanamke ambaye ni muungwana sana na makini miongoni mwako, yaani ambaye ni makini sana na muungwana kiasi kwamba asingethubutu kugusa ardhi kwa wayo wa mguu wake, yeye atakuwa mchoyo kwa mume ampendaye na mwanawe mwenyewe au binti yake, 5728:57 Kum 28:53kondoo wa nyuma kutoka kwenye tumbo lake na watoto anaowazaa. Kwa kuwa anakusudia kuwala kwa siri wakati wa kuzingirwa na katika taabu zile ambazo adui yako atazileta juu yako na miji yako.

5828:58 Kum 31:24; Za 96:4; Yer 5:22; Mal 1:14; 2:5; 3:5, 16; 4:2; Kut 3:15; 6:3; Yos 7:9Kama hutafuata kwa bidii maneno yote ya sheria hii, ambayo yameandikwa katika kitabu hiki na kama hutalicha hili jina la fahari na la kutisha, yaani la Bwana Mungu wako, 5928:59 1Fal 9:7, 9; Mao 1:9, 12; 4:12; Dan 9:12; 2Nya 21:12-15Bwana ataleta mapigo ya kutisha juu yako na kwa wazao wako, maafa makali na ya kudumu, magonjwa mazito na ya kudumu. 6028:60 Kut 15:26Atakuletea juu yako magonjwa yote ya Misri yale uliyoyaogopa, nayo yataambatana nawe. 6128:61 Kum 29:21; 30:10; 31:26; Yos 1:8; 8:34; 23:6; 24:26; 2Fal 14:6; 22:8; 2Nya 17:9; 25:4; Neh 8:1, 18; Mal 4:4; Kum 4:25-26Pia Bwana atakuletea kila aina ya ugonjwa na maafa ambayo hayakuandikwa humu katika kitabu hiki cha sheria, mpaka utakapokuwa umeangamizwa. 6228:62 Mwa 22:17; Kum 4:27; 10:22; Law 26:22; Neh 9:23Ninyi ambao mlikuwa wengi kama nyota za angani mtaachwa wachache tu, kwa sababu hamkumtii Bwana Mungu wenu. 6328:63 Kum 30:9; Isa 62:5; 65:19; Yer 32:41; Sef 3:17; Mit 1:26; Mwa 6:7; Za 52:5; Yer 12:14; 31:28; 45:4Kama ilivyompendeza Bwana kuwafanya ninyi mstawi na kuongezeka kwa idadi, ndivyo itakavyompendeza kuwaharibu na kuwaangamiza ninyi. Mtangʼolewa kutoka nchi mnayoiingia kuimiliki.

6428:64 Kum 4:27; Ezr 9:7; Isa 6:12; Yer 32:23; 43:11; 52:27; Za 44:11; Neh 1:8; Yer 13:24; 18:17; 22:22; Kum 4:32; Yer 8:19; Kum 11:28; 32:17; Law 26:33Kisha Bwana atawatawanya miongoni mwa mataifa yote, kutoka mwisho mmoja wa dunia hadi mwingine. Huko mtaabudu miungu mingine, miungu ya miti na ya mawe, ambayo ninyi wala baba zenu hamkuijua. 6528:65 Mao 1:3; Ay 11:20; Law 26:16, 30; Hos 9:17Miongoni mwa mataifa hayo hamtapata raha wala mahali pa kupumzisha wayo wa mguu wenu. Huko Bwana atawapa mahangaiko ya mawazo, macho yaliyochoka kwa kungojea na moyo uliokata tamaa. 66Utaishi katika mahangaiko siku zote, ukiwa umejaa hofu usiku na mchana, wala hutakuwa kamwe na uhakika wa maisha yako. 6728:67 Ay 7:4Wakati wa asubuhi utasema hivi, “Laiti ingekuwa jioni!” Jioni utasema, “Laiti ingekuwa asubuhi,” kwa sababu ya hofu ile itakayojaza moyo wako na vitu vile macho yako yatakavyoviona. 6828:68 Kut 13:14; Yer 44:7; Hos 8:13; 9:3Bwana atawarudisha tena Misri kwa meli, safari niliyosema kamwe hamngeenda tena. Huko mtajiuza ninyi wenyewe kwa adui zenu kama watumwa wa kiume na wa kike, lakini hakuna yeyote atakayewanunua.