民数记 9 – CCB & NEN

Chinese Contemporary Bible (Simplified)

民数记 9:1-23

逾越节

1以色列人离开埃及后第二年的一月,耶和华在西奈旷野对摩西说: 2以色列人要在指定的时间守逾越节, 3就是在一月十四日黄昏按照有关的律例和典章守逾越节。” 4于是,摩西吩咐以色列人守逾越节。 5一月十四日黄昏,以色列人照耶和华对摩西的吩咐,在西奈山守逾越节。

6可是,有几个人因碰到死尸而不洁净,不能在那天守逾越节,他们就来见摩西亚伦7说:“我们不过因碰到死尸而不洁净,为什么不准我们跟其他以色列人一起在指定的时间向耶和华献供物?” 8摩西说:“你们等一下,我要去听听耶和华对这事有什么吩咐。”

9耶和华对摩西说: 10“你把以下条例告诉以色列人。

“如果你们或你们的子孙中有人因为碰了死尸而不洁净,或是出了远门,可以改期为耶和华守逾越节。 11他们可以在二月十四日黄昏守逾越节,要配无酵饼和苦菜一起吃逾越节的羊羔。 12食物不可留到天明,也不可折断羊羔的一根骨头。要遵守逾越节的一切律例。 13如果有人是洁净的,又没有出远门,却不守逾越节,要将他从民中铲除。他不在指定的时间向耶和华献供物,就必须自负罪责。 14如果寄居在你们中间的外族人也想为耶和华守逾越节,他们也要遵守这些律例和典章。不论是外族人还是以色列人,都要遵守同样的律例。”

云彩遮盖会幕

15安放约柜的圣幕支起来那天,云彩遮盖了它。当晚,云彩整夜像火焰一般。 16之后,每天如此:白天云彩遮盖圣幕,晚上云彩像火。 17云彩什么时候从圣幕上升起,以色列人就启行;云彩在哪里停下来,以色列人就在哪里安营。 18他们无论启行还是安营,都遵照耶和华的吩咐。云彩在圣幕上停留多久,他们就安营多久。 19有时云彩在圣幕上停留多日,他们就遵照耶和华的吩咐安营多日。 20有时云彩在圣幕上只停留几天,他们就遵照耶和华的吩咐只安营几天。随后再照耶和华的吩咐启行。 21有时云彩整夜停留在圣幕上,到早晨才升起,他们就早晨才启行。不管白天黑夜,云彩一升起,他们就启行。 22不管是两天、一个月或是一年,只要云彩停留在圣幕上,以色列人就安营不动;云彩一升起,他们就启行。 23他们遵照耶和华的吩咐安营,也遵照耶和华的吩咐启行。他们遵行耶和华借摩西吩咐的话。

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Hesabu 9:1-23

Pasaka Huko Sinai

19:1 Hes 1:1; Kut 40:2Bwana akasema na Mose katika Jangwa la Sinai katika mwezi wa kwanza wa mwaka wa pili baada ya Waisraeli kutoka Misri. Akasema, 29:2 Kut 12:11; Hes 28:16; Ebr 10:1“Waamuru Waisraeli waadhimishe Pasaka katika wakati ulioamriwa. 39:3 Kut 12:2-11, 43-49; Law 23:5-8; Kum 16:1-8Adhimisheni wakati ulioamriwa, yaani wakati wa kuzama jua siku ya kumi na nne ya mwezi huu, kufuatana na desturi zake zote na masharti yake.”

49:4 Kut 12:11Hivyo Mose akawaambia Waisraeli waiadhimishe Pasaka, 59:5 Kut 12:6; Yos 5:10nao wakafanya hivyo kwenye Jangwa la Sinai wakati wa kuzama jua siku ya kumi na nne ya mwezi wa kwanza. Waisraeli wakafanya kila kitu kama vile Bwana alivyomwamuru Mose.

69:6 Law 5:3; 13:3; 21:11; Kut 18:15; Hes 27:2; Yn 18:28; Hes 6:6-7Lakini baadhi yao hawakuweza kuadhimisha Pasaka siku ile kwa sababu walikuwa najisi kwa taratibu za kiibada kwa ajili ya kugusa maiti. Kwa hiyo wakamwendea Mose na Aroni siku ile ile, 7wakamwambia Mose, “Tumekuwa najisi kwa sababu tumegusa maiti, lakini kwa nini tuzuiliwe kumtolea Bwana sadaka yake pamoja na Waisraeli wengine katika wakati ulioamriwa?”

89:8 Kut 18:15; Law 24:12; Hes 15:34; 27:5, 21; Za 85:8; Yn 7:17; Efe 1:9, 18; Ebr 3:5-6Mose akawajibu, “Ngojeni mpaka nitafute kile Bwana anachoagiza kuwahusu ninyi.”

9Ndipo Bwana akamwambia Mose, 109:10 2Nya 30:2“Waambie Waisraeli: ‘Wakati mmoja wenu au wazao wenu wanapokuwa najisi kwa sababu ya maiti au wakiwa safarini, hata hivyo wanaweza kuadhimisha Pasaka ya Bwana. 119:11 Kut 12:6-8; 2Nya 30:2, 15Wataiadhimisha wakati wa kuzama jua siku ya kumi na nne ya mwezi wa pili. Watamla mwana-kondoo, pamoja na mkate usiotiwa chachu, na mboga chungu. 129:12 Kut 12:8, 10, 43, 46; Yn 19:36Wasibakize chochote hadi asubuhi wala wasivunje mifupa ya mwana-kondoo. Wakati wanapoadhimisha Pasaka, hawana budi kufuata masharti yote. 139:13 Mwa 17:14; Kut 12:15; Law 17:4; Ebr 12:25; Hes 5:31; Gal 3:10; Ebr 10:26Lakini kama mtu ni safi kwa taratibu za kiibada naye hayuko safarini, asipoadhimisha Pasaka, mtu huyo hana budi kukatiliwa mbali na watu wake kwa sababu hakutoa sadaka ya Bwana kwa wakati ulioamriwa. Mtu huyo atawajibika kubeba matokeo ya dhambi yake.

149:14 Kut 12:19, 43-49“ ‘Mgeni anayeishi miongoni mwenu ambaye anataka kuadhimisha Pasaka ya Bwana, lazima afanye hivyo kwa kufuata desturi na masharti. Lazima masharti yawe sawasawa kwa mgeni na mzawa.’ ”

Wingu La Moto Juu Ya Maskani

(Kutoka 40:34-38)

159:15 Kut 38:21; 26:30; 33:16; 13:21; 40:34Katika siku hiyo ambayo Maskani, Hema la Ushuhuda, iliposimamishwa, wingu liliifunika. Kuanzia jioni mpaka asubuhi wingu lililokuwa juu ya Maskani lilionekana kama moto. 169:16 Kut 40:38; Kum 1:33; Neh 9:12Hivyo ndivyo lilivyoendelea kuwa; wingu liliifunika wakati wa mchana, na usiku lilionekana kama moto. 179:17 Kut 40:36-38; 1Kor 10:1; Za 78:14; Isa 49:10; Yn 10:4; Hes 9:21; Kut 13:21, 22Wakati wowote wingu lilipoinuka kutoka juu ya Hema, nao Waisraeli waliondoka; mahali popote wingu liliposimama, Waisraeli walipiga kambi. 189:18 Kut 40:37Kwa amri ya Bwana Waisraeli waliondoka, na kwa amri yake walipiga kambi. Kwa muda wote wingu liliposimama juu ya Maskani, Waisraeli walibaki wamepiga kambi.

199:19 Law 8:35; Kut 40:37Wakati wingu lilipobaki juu ya Maskani kwa muda mrefu, Waisraeli walitii amri ya Bwana nao hawakuondoka. 209:20 Za 48:14; Mit 3:5-6Wakati mwingine wingu lilikuwa juu ya Maskani kwa siku chache tu; kwa amri ya Bwana wangelipiga kambi na kisha kwa amri yake wangeliondoka. 219:21 Mt 28:20Wakati mwingine wingu lilikuwepo kuanzia jioni mpaka asubuhi tu, na lilipoinuka asubuhi, nao waliondoka. Ikiwa ni mchana au usiku, wakati wowote wingu lilipoinuka, waliondoka. 22Ikiwa wingu lilikaa juu ya Maskani kwa siku mbili au mwezi au mwaka, Waisraeli wangebaki wamepiga kambi na hawakuondoka; lakini lilipoinuka, wangeondoka.

239:23 Za 73:24; 107:7; Isa 63:14Kwa amri ya Bwana walipiga kambi, na kwa amri ya Bwana waliondoka. Walitii amri ya Bwana, kufuatana na agizo lake kupitia Mose.