民数记 10 – CCB & NEN

Chinese Contemporary Bible (Simplified)

民数记 10:1-36

银号

1耶和华对摩西说: 2“你要用银子打造两支号,用来招聚会众和发出拔营的号令。 3吹响两支号时,全体会众要聚集到你那里,即会幕门口。 4如果只吹响一支号,担任首领的以色列各族长要聚集到你那里。 5如果吹响拔营的号令,在东面扎营的就要启行; 6第二次吹响拔营号令时,在南面扎营的就要启行。拔营号令是启行的信号。 7但吹号招聚会众时,不要用拔营号令。 8做祭司的亚伦子孙要负责吹号,这是世代不变的律例。 9当你们在自己的土地上跟敌人作战时,要吹号,你们的上帝耶和华必眷顾你们,救你们脱离敌人。 10在节期和朔日10:10 朔日”即每月初一。这些欢乐的日子献燔祭和平安祭的时候,你们要吹号,好在你们的上帝面前蒙眷顾。我是你们的上帝耶和华。”

离开西奈山

11第二年的二月二十日,云彩从安放约柜的圣幕上升起, 12以色列人就从西奈旷野启行,直到云彩停在巴兰旷野时才停下来。 13这是他们初次照耶和华借摩西的吩咐启行。

14犹大旗下的营队率先出发,率领犹大支派的是亚米拿达的儿子拿顺15率领以萨迦支派的是苏押的儿子拿坦业16率领西布伦支派的是希伦的儿子以利押17然后,圣幕被拆下,革顺米拉利的子孙抬着圣幕出发。 18随后出发的是吕便旗下的营队,率领吕便支派的是示丢珥的儿子以利苏19率领西缅支派的是苏利沙代的儿子示路蔑20率领迦得支派的是丢珥的儿子以利雅萨

21随后出发的是哥辖人,他们抬着圣物前行。在他们到达之前,圣幕应已支好。 22随后出发的是以法莲旗下的营队,率领以法莲支派的是亚米忽的儿子以利沙玛23率领玛拿西支派的是比大苏的儿子迦玛列24率领便雅悯支派的是基多尼的儿子亚比但

25殿后的是旗下的营队,率领支派的是亚米沙代的儿子亚希以谢26率领亚设支派的是俄兰的儿子帕结27率领拿弗他利支派的是以南的儿子亚希拉28这是以色列各营队拔营前行的次序。

29摩西对岳父流珥之子米甸何巴说:“我们就要动身前往耶和华应许给我们的地方,祂曾说要把那地方赐给我们。请你跟我们一起去吧,我们必厚待你,耶和华已经应许要赐福给以色列人。” 30何巴说:“我不去了,我要回到我的家乡和亲族那里。” 31摩西说:“请不要离开我们。你熟悉旷野,可以做我们的向导,告诉我们在哪里扎营。 32如果你跟我们同去,我们一定与你分享耶和华赐给我们的福气。”

33以色列人离开耶和华的山,走了三天的路程,期间耶和华的约柜一直在队伍的前头,为他们寻找安营之地。 34他们拔营前行的时候,白天总有耶和华的云彩在他们上面。 35每当约柜出发的时候,摩西就说:“耶和华啊,求你兴起,击溃你的敌人,使恨你的人逃窜。” 36约柜停下来的时候,他就说:“耶和华啊,求你回到以色列的千万人中。”

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Hesabu 10:1-36

Tarumbeta Za Fedha

1Bwana akamwambia Mose: 210:2 Hes 31:6; Neh 4:18; 12:35; Za 47:5; 98:6; 105:3; Yer 4:5; 19; 6:1; Hos 5:8; 8:1; Yoe 2:1“Tengeneza tarumbeta mbili za fedha ya kufua, uzitumie kwa kuita jumuiya pamoja na wakati wa kuvunja makambi ili kuondoka. 3Tarumbeta zote mbili zikipigwa, jumuiya yote itakusanyika mbele yako katika ingilio la Hema la Kukutania. 410:4 Kut 18:21; Hes 7:2Kama tarumbeta moja tu ikipigwa, viongozi, yaani wakuu wa koo za Israeli, ndio watakaokusanyika mbele yako. 5Wakati mlio wa kujulisha hatari ukipigwa, makabila yaliyo na makambi upande wa mashariki yataondoka. 6Ukisikika mlio wa pili wa jinsi hiyo, walioko kwenye makambi ya kusini wataondoka. Mlio huo wa kujulisha hatari utakuwa ishara ya kuondoka. 710:7 Yer 4:5; 6:1; Eze 33:3; Yoe 2:1; 1Kor 14:8Ili kukusanya kusanyiko, piga tarumbeta zote, lakini siyo kwa mlio wa kujulisha hatari.

810:8 Mwa 9:12; Hes 15:14; 35:29; Yos 6:4; 2Nya 13:12“Wana wa Aroni, makuhani, ndio watakaopiga hizo tarumbeta. Hili litakuwa agizo la kudumu kwa ajili yenu na kwa vizazi vijavyo. 910:9 Kut 3:9; Amu 2:18; 6:9; 1Sam 10:18; 2Fal 13:4; Za 106:42; Law 23:24; 2Nya 13:12; Mwa 8:1Wakati mtakapopigana vita katika nchi yenu wenyewe dhidi ya adui anayewaonea, piga tarumbeta kwa mlio wa kujulisha hatari. Ndipo utakumbukwa na Bwana Mungu wenu na kuokolewa kutoka kwa adui zenu. 1010:10 Hes 28:11; 1Sam 20:5, 24; 2Fal 4:23; 2Nya 8:13; Za 81:3; Isa 1:13; Eze 45:17; 46:6; Amo 8:5; Law 23:24; 1:3; 3:1; 11:44; Hes 6:14Pia nyakati za furaha yenu, yaani sikukuu zenu zilizoamriwa na sikukuu za Mwezi Mwandamo, mtapiga tarumbeta juu ya sadaka zenu za kuteketezwa na sadaka zenu za amani, nazo zitakuwa ukumbusho kwa ajili yenu mbele za Mungu wenu. Mimi ndimi Bwana, Mungu wenu.”

Waisraeli Waondoka Sinai

1110:11 Kut 38:21; 40:17; Hes 9:17Katika siku ya ishirini ya mwezi wa pili wa mwaka wa pili, wingu liliinuka kutoka juu ya maskani ya Ushuhuda. 1210:12 Mwa 14:6; Kum 1:1; 33:2; Kut 40:36; Hes 12:16; Hab 3:3Ndipo Waisraeli wakaondoka kutoka Jangwa la Sinai wakasafiri kutoka sehemu moja hadi nyingine mpaka wingu lilipotua katika Jangwa la Parani. 1310:13 Kum 1:6; Hes 2:34Waliondoka kwa mara ya kwanza kwa agizo la Bwana kupitia kwa Mose.

1410:14 Hes 1:52; 2:3-9; 1:7Vikosi vya kambi ya Yuda vilitangulia kwanza chini ya alama yao. Nashoni mwana wa Aminadabu alikuwa kiongozi wao. 1510:15 Law 24:11; Hes 1:8Nethaneli mwana wa Suari alikuwa kiongozi wa kabila la Isakari, 1610:16 Hes 2:7; 1:9naye Eliabu mwana wa Heloni alikuwa kiongozi wa kabila la Zabuloni. 1710:17 Hes 4:21-32Ndipo Maskani iliposhushwa, nao wana wa Gershoni na wana wa Merari ambao waliibeba wakaondoka.

1810:18 Hes 2:16; 2:10-16; 1:5Vikosi vya kambi ya Reubeni vilifuata, chini ya alama yao. Elisuri mwana wa Shedeuri alikuwa kiongozi wao. 19Shelumieli mwana wa Surishadai aliongoza kikosi cha kabila la Simeoni, 2010:20 Hes 1:14naye Eliasafu mwana wa Deueli aliongoza kikosi cha kabila la Gadi. 2110:21 Hes 2:17; 4:20Kisha Wakohathi wakaondoka, wakichukua vitu vitakatifu. Maskani ilikuwa isimamishwe kabla wao hawajafika.

2210:22 Hes 2:24; 1:10Vikosi vya kambi ya Efraimu vilifuata, chini ya alama yao. Elishama mwana wa Amihudi alikuwa kiongozi wao. 23Gamalieli mwana wa Pedasuri aliongoza kikosi cha kabila la Manase, 2410:24 Hes 1:11naye Abidani mwana wa Gideoni alikuwa kiongozi wa kikosi cha kabila la Benyamini.

2510:25 Hes 2:31; 1:12; Yos 6:9Mwishowe, kama kikosi cha nyuma cha ulinzi wa vikosi vyote, vikosi vya kambi ya Dani viliondoka chini ya alama yao. Ahiezeri mwana wa Amishadai alikuwa kiongozi wao. 26Pagieli mwana wa Okrani aliongoza kikosi cha kabila la Asheri, 27naye Ahira mwana wa Enani aliongoza kikosi cha kabila la Naftali. 2810:28 Za 80:1; Wim 6:10Huu ndio ulikuwa utaratibu wa kuondoka wa vikosi vya Waisraeli walipokuwa wanaondoka.

2910:29 Amu 4:11; Kut 2:18; 3:1; Mwa 12:7; 15:14Basi Mose akamwambia Hobabu mwana wa Reueli, Mmidiani, mkwewe Mose, “Tunaondoka kwenda mahali ambapo Bwana amesema ‘Nitawapa ninyi mahali hapo.’ Twende pamoja nasi tutakutendea mema, kwa maana Bwana ameahidi mambo mema kwa Israeli.”

3010:30 Mt 21:29; Kut 18:27Akajibu, “Hapana, sitakwenda; nitarudi kwenye nchi yangu mwenyewe na watu wangu mwenyewe.”

3110:31 Ay 29:15Lakini Mose akasema, “Tafadhali usituache. Wewe unajua mahali ambapo yatupasa kupiga kambi jangwani, nawe unaweza kuwa macho yetu. 3210:32 Kut 12:48; Kum 10:18; Za 22:27-31; 67:5-7Ikiwa utafuatana nasi, tutashirikiana nawe mema yoyote tutakayopewa na Bwana.”

3310:33 Kum 1:33; 10:8; 31:9; Yos 3:3; Amu 20:27; 2Sam 15:24; Yer 31:2Hivyo waliondoka kutoka mlima wa Bwana, nao wakasafiri kwa siku tatu. Sanduku la Agano la Bwana liliwatangulia kwa zile siku tatu ili kuwatafutia mahali pa kupumzika. 3410:34 Hes 9:15-23; Kut 13:21; Neh 9:12, 19Wingu la Bwana lilikuwa juu yao wakati wa mchana walipoondoka kambini.

3510:35 2Nya 6:41; Za 17:13; 44:26; 94:2; 132:8; Amu 5:31; 2Sam 2:1; Za 68:1; 92:9; Kum 5:9; 7:10; Isa 17:12-14; 59:18Wakati wowote Sanduku lilipoondoka, Mose alisema,

“Ee Bwana, inuka!

Watesi wako na watawanyike;

adui zako na wakimbie mbele zako.”

3610:36 Isa 52:8; 63:17; Mwa 15:5; 26:4; Kum 1:10; 10:22; Neh 9:23Wakati wowote Sanduku liliposimama, alisema,

“Ee Bwana, rudi,

kwa maelfu ya Waisraeli wasiohesabika.”