提摩太前书 6 – CCB & NEN

Chinese Contemporary Bible (Simplified)

提摩太前书 6:1-21

1做奴仆的要全心尊重自己的主人,免得上帝的名和我们的教导被人亵渎。 2若主人是基督徒,做奴仆的不可因为同是信徒就不尊敬自己的主人,反而要更好地服侍他,因为这些接受服侍的人是信徒,是主所爱的。你要教导这些事并勉励众人。

异端与贪财

3如果有人传的教义不符合我们主耶稣基督纯正的道和敬虔的教导, 4他就是狂妄自大、一无所知。这种人专好问难,争辩字句,结果引起嫉妒、纷争、毁谤和猜忌, 5使那些思想败坏、失去真理的人争论不休,甚至把敬虔当作生财之道。 6其实敬虔和知足才是真正的财富, 7因为我们空手来到世上,也要空手离开。 8只要有吃有穿,就该知足。 9那些渴望发财的人却陷入诱惑、网罗和许多愚蠢有害的欲望中,以致落入败坏和灭亡中。 10贪财是万恶之根,有人因为贪财就离弃了信仰,结果饱尝种种锥心般的痛苦。

保罗对提摩太的嘱咐

11但你这属上帝的人要远避这些事,要追求公义、敬虔、信心、爱心、忍耐和温柔, 12要为真道打美好的仗,要持定永生。你是为永生蒙召的,并在许多见证人面前做过美好的见证。 13在赐万物生命的上帝面前,也在向本丢·彼拉多做过美好见证的基督耶稣面前,我嘱咐你: 14要遵守这命令,做纯洁无瑕、无可指责的人,一直到我们的主耶稣基督再来。 15到了时候,配得称颂、独有权能的万王之王、万主之主要使基督显现。 16上帝是独一不朽的,住在人不能接近的光中,从来没有人见过祂,也没有人能够看见祂。愿尊贵和永远的权柄都归给祂。阿们!

17你要劝诫那些今世富足的人不要高傲,也不要冀望于靠不住的钱财,要信靠将万物厚赐给我们享用的上帝。 18你要劝他们多多行善、慷慨施舍、乐意助人。 19这样,他们可以为自己的将来奠定美好的基础,以便持守真正的生命。

20提摩太啊,你要持守所托付给你的,避开世俗的空谈和那些违背真理、似是而非的学问。 21有些自称有这种学问的人已经偏离了信仰。

愿恩典与你们同在!

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

1 Timotheo 6:1-21

Watumwa

16:1 1Pet 2:18; Tit 2:5-9Wale wote walio chini ya kongwa la utumwa inawapasa kuwahesabu mabwana zao kuwa wanastahili heshima yote, ili jina la Mungu lisitukanwe wala mafundisho yetu. 26:2 Efe 1:16; 1Tim 4:11Wale watumwa ambao wana mabwana waaminio, haiwapasi kupunguza heshima yao kwa sababu wao ni ndugu. Badala yake, wawatumikie hata vizuri zaidi, kwa sababu wale wanaonufaika na huduma yao ni waaminio, ambao ni wapenzi wao. Fundisha mambo haya na uwahimize kuyafuata.

Mafundisho Ya Uongo Na Utajiri Wa Kweli

36:3 1Tim 1:3-10Ikiwa mtu yeyote atafundisha mafundisho mapotovu wala hakubaliani na mafundisho manyofu ya Bwana wetu Yesu Kristo na yale ya utauwa, 46:4 2Tim 2:14huyo amejivuna wala hajui kitu chochote. Yeye amejaa tamaa ya mabishano na ugomvi kuhusu maneno ambavyo matokeo yake ni wivu na mapigano, maneno ya ukorofi, shuku mbaya, 56:5 Tit 1:15na kuzozana kusikokoma kati ya watu walioharibika akili zao, walioikosa kweli, na ambao hudhani kwamba utauwa ni njia ya kupata faida.

66:6 Flp 4:11; Ebr 13:5; 1Tim 4:8Lakini utauwa na kuridhika ni faida kubwa. 76:7 Ay 1:21; Za 49:17Kwa kuwa hatukuja humu duniani na kitu chochote, wala hatuwezi kutoka humu na kitu. 86:8 Mit 30:8; Ebr 13:5Lakini kama tuna chakula na mavazi, tutaridhika navyo. 96:9 Mit 15:27; 1Tim 3:7Lakini wale watu wanaotamani kuwa na mali kwa haraka huanguka kwenye majaribu, na wamenaswa na tamaa nyingi za kipumbavu zenye kudhuru, zinazowazamisha watu katika uharibifu na maangamizi. 106:10 Yak 5:19; 1Tim 3:3Kwa maana kupenda fedha ndiyo shina moja la maovu ya kila namna. Baadhi ya watu wakitamani fedha, wameiacha imani na kujichoma wenyewe kwa maumivu mengi.

Vitu Vizuri Vya Imani

116:11 2Tim 3:10-17Lakini wewe, mtu wa Mungu, yakimbie mambo haya yote. Fuata haki, utauwa, imani, upendo, saburi na upole. 126:12 1Kor 9:25-26; 1Tim 1:18; Flp 3:12Pigana vile vita vizuri vya imani. Shika uzima wa milele ambao ndio ulioitiwa ulipokiri ule ukiri mzuri mbele ya mashahidi wengi. 136:13 1Tim 1:11-17; Dan 2:47; Ufu 1:5Nakuagiza mbele za Mungu avipaye vitu vyote uhai, na mbele za Kristo Yesu ambaye alipokuwa anashuhudia mbele ya Pontio Pilato alikiri ukiri mzuri, 146:14 1The 3:13; 1Kor 1:7; 2Tim 1:10; 4:1, 8uishike amri hii bila dosari wala lawama mpaka kuja kwake Bwana wetu Yesu Kristo, 156:15 1Tim 1:11-17; Dan 2:47; Ufu 1:5ambaye Mungu atamleta kwa wakati wake mwenyewe: yeye ahimidiwaye, aliye peke yake Mtawala, Mfalme wa wafalme, na Bwana wa mabwana, 166:16 Yn 1:18yeye peke yake ambaye hapatikani na mauti, na anakaa katika nuru isiyoweza kukaribiwa, ambaye hakuna mwanadamu aliyemwona wala awezaye kumwona. Heshima na uweza una yeye milele. Amen.

176:17 Lk 12:20-21; 1Tim 4:10; Mdo 14:17Waagize wale ambao ni matajiri wa ulimwengu huu waache kujivuna, wala wasiweke tumaini lao katika mali ambayo si ya hakika, bali waweke tumaini lao katika Mungu ambaye hutupatia vitu vyote kwa wingi ili tuvifurahie. 186:18 1Tim 5:10; Rum 12:8-13Waagize watende mema, wawe matajiri katika matendo mema, pia wawe wakarimu na walio tayari kushiriki mali zao na wengine. 196:19 Mt 6:20Kwa njia hii watajiwekea hazina kama msingi kwa ajili ya wakati ujao na hivyo watajipatia uzima, yaani, ule uzima ambao ni wa kweli.

Maelekezo Ya Binafsi Na Maombi Ya Baraka

206:20 2Tim 1:12-14; 2:16-18Timotheo, linda kile kilichowekwa amana kwako. Epuka majadiliano yasiyo ya utauwa na mabishano ambayo kwa uongo huitwa elimu, 216:21 Kol 4:18ambayo wengine kwa kujidai kuwa nayo wameiacha imani.

Neema iwe nanyi. Amen.