历代志下 8 – CCB & NEN

Chinese Contemporary Bible (Simplified)

历代志下 8:1-18

所罗门的功绩

1所罗门用二十年的时间兴建了耶和华的殿和他自己的王宫。 2他重修希兰送给他的城邑,让以色列人居住。

3所罗门去攻打哈马琐巴,并攻取了此城。 4他兴建旷野里的达莫以及哈马境内所有的储货城, 5把上伯·和仑与下伯·和仑建成有墙、有门、有闩的坚城, 6还建造巴拉、所有的储货城、屯车城、养马城和他想在耶路撒冷黎巴嫩及其统治的全境兴建的城邑。 7当时国中有人、亚摩利人、比利洗人、希未人和耶布斯人的后裔, 8以色列人没有灭绝他们。所罗门让他们服劳役,至今如此。 9所罗门王没有让以色列人服劳役,而是让他们做战士、将领、战车长和骑兵长。 10他还任命二百五十名监工负责监管工人。

11所罗门带法老的女儿离开大卫城,来到为她建造的宫中,因为所罗门说:“我的妻子不可住在以色列大卫的宫里,因为约柜所到之处都是圣洁的。”

12所罗门在门廊前他所筑的耶和华的坛上向耶和华献燔祭, 13并照摩西的规定,在安息日、朔日和每年特定的三个节期,即除酵节、七七节和住棚节献上当献的祭。

14所罗门照着他父亲大卫的吩咐,指派祭司分班供职,让利未人负责颂赞、辅助祭司尽每天的职责,还指派殿门守卫分班守门。这些都是上帝的仆人大卫规定的。 15他们没有违背大卫王就库房等工作对祭司和利未人的吩咐。

16从耶和华的殿奠基直到完工,所罗门所有的计划都已顺利完成。这样,耶和华的殿落成了。

17之后,所罗门前往以东地区靠海的以旬·迦别以禄18希兰派懂得航海的仆人乘船只与所罗门的仆人一同到俄斐,从那里为所罗门王运回十五吨黄金。

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

2 Nyakati 8:1-18

Shughuli Nyingine Za Solomoni

(1 Wafalme 9:10-28)

18:1 1Fal 9:10Miaka ishirini ilipopita, ambayo katika hiyo Solomoni alilijenga Hekalu la Bwana na jumba lake mwenyewe la kifalme, 2Solomoni akajenga tena vijiji vile ambavyo Hiramu alikuwa amempa, naye akawapa Waisraeli waishi humo. 38:3 Hes 13:21; 2Sam 8:2-3Kisha Solomoni akaenda Hamath-Soba na kuuteka. 48:4 1Fal 9:14Pia akajenga mji wa Tadmori katika jangwa na miji yote ya kuhifadhia vitu katika Hamathi. 58:5 Yos 10:10; 1Nya 7:24; Hes 13:21Akajenga tena Beth-Horoni ya Juu na Beth-Horoni ya Chini, miji yenye ngome, kuta, malango na makomeo. 68:6 Yos 15:11Solomoni pia akajenga Baalathi na miji yake yote ya kuhifadhia vitu, na miji kwa ajili ya magari yake na kwa ajili ya farasi wake, chochote alichotaka kujenga katika Yerusalemu, katika Lebanoni na katika nchi yote aliyotawala.

78:7 Mwa 15:18-21; 1Fal 9:20; Ezr 9:1; Mwa 10:15Watu wote waliosalia kutoka kwa Wahiti, Waamori, Waperizi, Wahivi na Wayebusi (haya mataifa hayakuwa Waisraeli), 88:8 1Fal 9:21; 2Nya 2:18yaani, wazao wao waliobakia katika nchi, ambao Waisraeli hawakuwa wamewaangamiza: hawa Solomoni akawalazimisha kuwa watumwa katika shokoa, kama ilivyo hadi leo. 98:9 Kut 19:5; Kum 23:19; Law 25:39; Gal 4:28-31Lakini Solomoni hakuwafanya Waisraeli watumwa kwa ajili ya kazi yake, bali walikuwa wapiganaji, majemadari, maafisa wake, majemadari wa magari yake ya vita na waendesha magari ya vita. 108:10 1Fal 5:16; 9:23; 2Nya 2:18Pia walikuwa maafisa wakuu wa Mfalme Solomoni, yaani, maafisa wakaguzi 250 waliosimamia watu.

118:11 1Fal 7:8; 9:24Solomoni akampandisha mke wake binti Farao kutoka Mji wa Daudi na kumleta jumba la kifalme alilokuwa amemjengea, kwa kuwa alisema, “Mke wangu hataishi katika jumba la kifalme la Daudi mfalme wa Israeli, kwa sababu mahali ambapo Sanduku la Bwana limefika ni patakatifu.”

128:12 1Fal 8:64; 1Nya 4:1Mfalme Solomoni akamtolea Bwana dhabihu za kuteketezwa juu ya madhabahu ya Bwana ambayo alikuwa ameijenga mbele ya ukumbi, 138:13 Kut 29:38; Hes 28:3-9; Kut 23:14-16; Kum 16:16; 1Fal 9:25kulingana na mahitaji ya kila siku kwa ajili ya sadaka zilizoamriwa na Mose kwa ajili ya Sabato, Mwezi Mwandamo na sikukuu nyingine tatu za mwaka, yaani, Sikukuu ya Mikate Isiyotiwa Chachu, Sikukuu ya Majuma na Sikukuu ya Vibanda. 148:14 1Nya 24:1; 9:17; Neh 12:24, 36, 45; 1Nya 23:6; 2Sam 23:2; 2Nya 5:11; 31:2; 1Nya 25:1; 26:1Kwa kushika maagizo ya Daudi baba yake, aliweka migawanyo ya makuhani kwa ajili ya kazi zao, nao Walawi kuongoza kusifu na kusaidia makuhani kufuatana na mahitaji ya kila siku. Pia akaweka mabawabu katika migawanyo kwa ajili ya malango mbalimbali, kwa sababu hili ndilo Daudi mtu wa Mungu alilokuwa ameagiza. 15Nao hawakuziacha amri za mfalme alizoamuru makuhani au Walawi katika jambo lolote, ikiwa ni pamoja na zile za hazina.

16Kazi yote ya Mfalme Solomoni ilifanyika kuanzia siku msingi wa Hekalu la Bwana ulipowekwa mpaka kukamilika kwake. Kwa hiyo Hekalu la Bwana likamalizika kujengwa.

178:17 Kum 2:8; 2Fal 14:22; 1Fal 9:26Ndipo Solomoni akaenda Esion-Geberi na Elathi katika pwani ya Edomu. 188:18 1Fal 9:27; Isa 13:12; 2Nya 9:9; Mwa 10:29; Ay 22:24Naye Hiramu alimpelekea meli zilizoongozwa na maafisa wake mwenyewe, watu waliokuwa na ujuzi wa baharini. Hawa watu pamoja na wale wa Solomoni wakasafiri kwa bahari mpaka Ofiri, wakaleta kutoka huko talanta 450 za dhahabu, ambazo walimkabidhi Mfalme Solomoni.