以赛亚书 54 – CCB & NEN

Chinese Contemporary Bible (Simplified)

以赛亚书 54:1-17

主爱不移

1耶和华说:“不生育、未生养的妇人啊,要欢唱;

未曾生产的女子啊,

要高歌、欢呼;

因为没有丈夫的比有丈夫的儿女更多。

2要扩大你的帐篷,

尽量拉宽帐篷的幔子,

放长绳子,钉牢橛子。

3因为你要向左右扩展,

你的后裔要统治列国,

使荒凉的城邑重新有人居住。

4“不要惧怕,因为你不会再受羞辱;

不要怕,因为你不会再受凌辱。

你必忘记年轻时的羞辱,

不再想起寡居时的耻辱。

5因为造你的是你的丈夫,

祂名叫万军之耶和华;

救赎你的是以色列的圣者,

祂是普天下的上帝。

6耶和华要召你回来,

如同召一个遭遗弃、

心中忧伤的年轻妻子。

这是你的上帝说的。

7我丢弃了你片刻,

但我要怀着极大的怜悯接你回来。

8我盛怒之下暂时掩面不理你,

但我要以永远不变的慈爱怜悯你。

这是你的救赎主耶和华说的。

9“这就像挪亚的时代,

我怎样起誓不让挪亚时代的洪水再淹没大地,

我也照样起誓不再向你发怒,

也不再斥责你。

10大山可以挪开,

小山可以迁移,

但我的慈爱必不离开你,

我平安的约也不会更改。

这是怜悯你的耶和华说的。

11“困苦不堪、饱经风雨、

得不着安慰的城啊,

我要以彩石作你的地基,

用蓝宝石来建造你,

12用红宝石建你的城楼、

水晶造你的城门、

宝石建你的城墙。

13你的儿女都必受耶和华的训诲,

安享太平。

14你必因公义而坚立,

再不会受欺压,

也不会担惊受怕,

因为恐惧不会临近你。

15倘若有人来攻打你,

那必不是我的旨意。

攻打你的必然失败。

16看啊,是我造了扇旺炭火、

铸造合用兵器的铁匠,

是我造了毁灭者。

17为攻击你而造的兵器必不能奏效,

你必驳倒控告你的人。

这是耶和华众仆人的产业,

是我给他们的胜利54:17 胜利”或译“公义”。

这是耶和华说的。”

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Isaya 54:1-17

Utukufu Wa Baadaye Wa Sayuni

154:1 Isa 49:20; Gal 4:27; Mwa 21:6; Za 98:4; Isa 66:7; 49:20“Imba, ewe mwanamke tasa,

wewe ambaye kamwe hukuzaa mtoto;

paza sauti kwa kuimba, piga kelele kwa furaha,

wewe ambaye kamwe hukupata utungu;

kwa sababu watoto wa mwanamke aliyeachwa ukiwa ni wengi

kuliko wa mwanamke mwenye mume,”

asema Bwana.

254:2 Mwa 26:22; Isa 26:15; Kut 35:18; 39:40; Isa 49:19-20“Panua mahali pa hema lako,

tandaza mapazia ya hema lako uyaeneze mbali,

wala usiyazuie;

ongeza urefu wa kamba zako,

imarisha vigingi vyako.

354:3 Mwa 13:14; Isa 48:19; Ay 12:23; Isa 14:2; 60:4-11; 49:19Kwa maana utaenea upande wa kuume

na upande wa kushoto;

wazao wako watayamiliki mataifa

na kukaa katika miji yao iliyoachwa ukiwa.

454:4 Isa 30:10; Yoe 2:21; Isa 28:16; Mwa 30:23; Za 25:7; 119:39; Yer 22:21; Isa 47:8“Usiogope, wewe hutaaibika.

Usiogope aibu, wewe hutaaibishwa.

Wewe utasahau aibu ya ujana wako,

wala hutakumbuka tena mashutumu ya ujane wako.

554:5 Wim 3:3; Isa 41:14; 48:17; Rum 3:29; Hos 2:7-16; Za 149:2; Isa 51:13Kwa maana Muumba wako ndiye mume wako,

Bwana Mwenye Nguvu Zote ndilo jina lake,

yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli ni Mkombozi wako,

yeye anaitwa Mungu wa dunia yote.

654:6 Isa 49:14-21; 60:15; 62:4; Yer 44:2; Hos 1:10; Kut 20:14; Mal 2:14Bwana atakuita urudi

kana kwamba ulikuwa mke aliyeachwa na kuhuzunishwa rohoni;

kama mke aliyeolewa bado angali kijana

na kukataliwa,” asema Mungu wako.

754:7 Ay 14:13; Isa 26:20; 2Kor 4:17; Isa 27:8; Za 71:11; Isa 49:18“Kwa kitambo kidogo nilikuacha,

lakini kwa huruma nyingi nitakurudisha.

854:8 Isa 9:12; Yer 31:3; Za 92:2; Isa 26:20; Za 25:6; Isa 55:3; 63:7; Hos 2:19Katika ukali wa hasira

nilikuficha uso wangu kwa kitambo,

lakini kwa fadhili za milele

nitakuwa na huruma juu yako,”

asema Bwana Mkombozi wako.

954:9 Mwa 8:21; Mik 7:18; Eze 39:29; Isa 14:24; Kum 28:20; Isa 49:18“Kwangu mimi jambo hili ni kama siku za Noa,

nilipoapa kuwa maji ya Noa kamwe hayatafunika tena dunia.

Hivyo sasa nimeapa sitawakasirikia ninyi,

kamwe sitawakemea tena.

1054:10 Za 46:2; Ebr 12:27; Mwa 9:16; Kut 34:10; Ufu 6:14; Hes 25:12; Isa 55:7Ijapotikisika milima, na vilima viondolewe,

hata hivyo upendo wangu usiokoma kwenu hautatikisika,

wala agano langu la amani halitaondolewa,”

asema Bwana, mwenye huruma juu yenu.

1154:11 Isa 14:32; 29:6; 1Nya 29:2; Ufu 21:18; 21:19-20; Isa 26:18; 28:16; Kut 24:10“Ewe mji uliyeteswa, uliyepigwa kwa dhoruba na usiyetulizwa,

nitakujenga kwa almasi, nitaweka misingi yako kwa yakuti samawi.

1254:12 Ufu 21:21Nitafanya minara yako ya akiki,

malango yako kwa vito vingʼaavyo,

nazo kuta zako zote za vito vya thamani.

1354:13 Mik 4:2; Ebr 8:11; Law 26:6; Isa 11:9; 28:9; 48:18; Yn 6:45Watoto wako wote watafundishwa na Bwana,

nayo amani ya watoto wako itakuwa kuu.

1454:14 2Sam 7:10; Isa 9:4; 17:14; 26:2; Yer 30:20; Sef 3:17; Zek 9:8Kwa haki utathibitika:

Kuonewa kutakuwa mbali nawe;

hutaogopa chochote.

Hofu itakuwa mbali nawe;

haitakukaribia wewe.

1554:15 Isa 41:11-16Kama mtu yeyote akikushambulia,

haitakuwa kwa ruhusa yangu;

yeyote akushambuliaye

atajisalimisha kwako.

1654:16 Isa 44:12; 10:5; 13:5“Tazama, ni mimi niliyemuumba mhunzi,

yeye afukutaye makaa kuwa moto,

na kutengeneza silaha inayofaa kwa kazi yake.

Tena ni mimi niliyemwambia mharabu

kufanya uharibifu mwingi.

1754:17 Isa 29:8; Mdo 6:10; Isa 45:24-25; 41:11; 56:6-8; Zek 1:20-21; Isa 65:8-9Hakuna silaha itakayofanyizwa dhidi yako

itakayofanikiwa,

nawe utauthibitisha kuwa mwongo

kila ulimi utakaokushtaki.

Huu ndio urithi wa watumishi wa Bwana

na hii ndiyo haki yao itokayo kwangu,”

asema Bwana.