Zaburi 91:1-6
Zaburi 91
91:1 Kut 33:2; Isa 49:2; Mao 4:20; Za 63:7Yeye akaaye mahali pa salama pake Yeye Aliye Juu Sana,
atadumu katika uvuli wake Mwenyezi.
91:2 Za 9:9; 91:9; 2Sam 22:2, 3Nitasema kumhusu Bwana, “Yeye ndiye kimbilio langu na ngome yangu,
Mungu wangu, ambaye ninamtumaini.”
91:3 Za 124:7; Mit 6:5; 1Fal 8:37Hakika yeye ataniokoa na mtego wa mwindaji,
na maradhi ya kuambukiza ya kuua.
91:4 Za 61:4; 17:8; 35:2; Rum 2:12; Kum 32:10; Isa 27:3; 31:5; Zek 12:8Atakufunika kwa manyoya yake,
chini ya mbawa zake utapata kimbilio,
uaminifu wake utakuwa ngao na kinga yako.
91:5 Ay 5:21; 5:19; Mit 3:23; Isa 43:2Hutaogopa vitisho vya usiku,
wala mshale urukao mchana,
wala maradhi ya kuambukiza
yanayonyemelea gizani,
wala tauni iharibuyo adhuhuri.