วิวรณ์ 4 – TNCV & NEN

Thai New Contemporary Bible

วิวรณ์ 4:1-11

พระที่นั่งในสวรรค์

1หลังจากนั้นข้าพเจ้ามองไปเห็นประตูหนึ่งเปิดไว้ในสวรรค์ต่อหน้าข้าพเจ้า และพระสุรเสียงคล้ายเสียงแตรซึ่งข้าพเจ้าได้ยินเมื่อตอนต้นนั้นตรัสแก่ข้าพเจ้าว่า “ขึ้นมาที่นี่เถิด เราจะสำแดงสิ่งที่ต้องเกิดขึ้นหลังจากนี้แก่เจ้า” 2ทันใดนั้นข้าพเจ้าก็อยู่ในพระวิญญาณและตรงหน้าข้าพเจ้ามีพระที่นั่งตั้งอยู่ในสวรรค์ มีผู้หนึ่งประทับบนพระที่นั่งนั้น 3ผู้ประทับอยู่นั้นทรงโอ่อ่าตระการตาดั่งเพชรนิลจินดา สายรุ้งดุจมรกตล้อมรอบพระที่นั่ง 4รายรอบพระที่นั่งนั้นมีอีกยี่สิบสี่ที่นั่งซึ่งมีผู้อาวุโสยี่สิบสี่คนนั่งอยู่ ทุกคนนุ่งห่มขาว สวมมงกุฎทองคำบนศีรษะ 5มีฟ้าแลบแวบวาบ เสียงฟ้าคำรนครืนๆ จากพระที่นั่งนั้น ตรงหน้าพระที่นั่งมีคบเพลิงเจ็ดอันลุกโชติช่วงอยู่คือวิญญาณทั้งเจ็ด4:5 หรือพระวิญญาณทั้งเจ็ดของพระเจ้า 6และหน้าพระที่นั่งมีสิ่งซึ่งคล้ายทะเลแก้วใสเหมือนแก้วผลึก

บริเวณตรงกลางรอบพระที่นั่งมีสิ่งมีชีวิตสี่ตนซึ่งมีดวงตาเต็มไปหมดทั้งด้านหน้าและด้านหลัง 7ตนแรกคล้ายสิงโต ตนที่สองคล้ายวัว ตนที่สามมีใบหน้าคล้ายคน ตนที่สี่คล้ายนกอินทรีที่กำลังบิน 8สิ่งมีชีวิตทั้งสี่นี้ แต่ละตนมีหกปีกและมีดวงตาทั่วไปหมดแม้แต่ใต้ปีก ต่างร้องขานทั้งวันทั้งคืนไม่หยุดว่า

“บริสุทธิ์ บริสุทธิ์ บริสุทธิ์

คือองค์พระผู้เป็นเจ้าพระเจ้าผู้ทรงฤทธิ์

ผู้ทรงดำรงอยู่ในอดีตและดำรงอยู่ในปัจจุบัน

และจะเสด็จมา”

9ทุกครั้งที่สิ่งมีชีวิตทั้งสี่ถวายพระสิริ พระเกียรติ และคำขอบพระคุณแด่พระองค์ผู้ประทับบนพระที่นั่ง ผู้ทรงดำรงอยู่ตลอดกาล 10ผู้อาวุโสทั้งยี่สิบสี่คนก็หมอบกราบพระองค์ผู้ประทับบนพระที่นั่งนั้น นมัสการพระองค์ผู้ทรงดำรงอยู่ตลอดกาล พวกเขาวางมงกุฎของตนลงหน้าพระที่นั่งนั้นและทูลว่า

11“ข้าแต่องค์พระผู้เป็นเจ้าและพระเจ้าของเรา

พระองค์ทรงสมควรที่จะรับพระสิริ

พระเกียรติและเดชานุภาพ

เพราะพระองค์ได้ทรงสร้างสรรพสิ่ง

และโดยพระดำริของพระองค์ สิ่งเหล่านี้ได้ถูกสร้างขึ้น

และเป็นอยู่”

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Ufunuo 4:1-11

Kiti Cha Enzi Kilichoko Mbinguni

14:1 Ufu 1:10; 11:12; 1:19Baada ya mambo hayo nilitazama, nami nikaona mbele yangu mlango uliokuwa wazi mbinguni. Nayo ile sauti niliyokuwa nimeisikia hapo mwanzo ikisema nami kama tarumbeta ikasema, “Njoo, huku, nami nitakuonyesha yale ambayo hayana budi kutokea baada ya haya.” 24:2 1Fal 22:19; Ufu 20:11Ghafula nilikuwa katika Roho, na hapo mbele yangu kilikuwepo kiti cha enzi mbinguni, kikiwa kimekaliwa na mtu. 34:3 Eze 1:28Aliyekuwa amekikalia alikuwa anaonekana kama yaspi na akiki. Kukizunguka kile kiti cha enzi palikuwa na upinde wa mvua ulioonekana kama zumaridi.

44:4 Ufu 11:16; 3:4-5Kukizunguka hicho kiti cha enzi palikuwa na viti vingine vya enzi ishirini na vinne, na juu ya hivyo viti walikuwa wameketi wazee ishirini na wanne. Walivaa mavazi meupe, na walikuwa na taji za dhahabu vichwani mwao. 54:5 Kut 19:16; Zek 4:2; Ufu 1:4Kwenye kile kiti cha enzi palikuwa panatoka miali ya umeme wa radi, ngurumo na sauti za radi. Mbele ya kiti cha enzi, taa saba zilikuwa zinawaka. Hizi ndizo roho saba4:5 Roho saba za Mungu hapa inamaanisha Roho wa Mungu katika ukamilifu wa utendaji wake. za Mungu. 64:6 Ufu 15:2; Eze 1:5-10Pia mbele ya kiti cha enzi palikuwa na kile kilichoonekana kama bahari ya kioo, iliyokuwa angavu kama bilauri.

Katikati, kukizunguka kile kiti cha enzi, kulikuwa na viumbe wanne wenye uhai, wakiwa wamejawa na macho mbele na nyuma. 74:7 Eze 10:14Kiumbe wa kwanza mwenye uhai alikuwa kama simba, wa pili alikuwa kama ngʼombe dume, wa tatu alikuwa na uso kama wa mwanadamu, na wa nne alikuwa kama tai anayeruka. 84:8 Isa 6:2-3; Ufu 1:4-8Kila mmoja wa hawa viumbe wanne wenye uhai alikuwa na mabawa sita, na kujawa na macho pande zote hadi chini ya mabawa. Usiku na mchana hawaachi kusema:

“Mtakatifu, Mtakatifu, Mtakatifu,

ni Bwana Mungu Mwenyezi,

aliyekuwako, aliyeko na atakayekuja.”

94:9 Za 47:8Kila mara viumbe hao wanne wenye uhai wanapomtukuza, kumheshimu na kumshukuru yeye aketiye kwenye kile kiti cha enzi, tena aishiye milele na milele, 104:10 Kum 33:3wale wazee ishirini na wanne huanguka mbele zake aketiye kwenye kiti cha enzi na kumwabudu yeye aliye hai milele na milele. Huziweka taji zao mbele ya kiti cha enzi, wakisema:

114:11 Ufu 1:6; 10:6“Bwana wetu na Mungu wetu,

wewe unastahili kupokea utukufu

na heshima na uweza,

kwa maana ndiwe uliyeviumba vitu vyote,

na kwa mapenzi yako viliumbwa

na vimekuwako.”