پيدايش 47 – PCB & NEN

Persian Contemporary Bible

پيدايش 47:1-31

1يوسف به حضور فرعون رفت و به او خبر داد و گفت: «پدرم و برادرانم با گله‌ها و رمه‌ها و هر آنچه كه داشته‌اند از كنعان به اينجا آمده‌اند، و الان در جوشن هستند.» 2او پنج نفر از برادرانش را که با خود آورده بود، به فرعون معرفی كرد.

3فرعون از آنها پرسيد: «شغل شما چيست؟»

گفتند: «ما هم مثل اجدادمان چوپان هستيم. 4آمده‌ايم در مصر زندگی كنيم، زيرا در كنعان به علت قحطی شديد برای گله‌های ما چراگاهی نيست. التماس می‌كنيم به ما اجازه دهيد در جوشن ساكن شويم.»

5‏-6فرعون به يوسف گفت: «حال كه پدرت و برادرانت به اينجا آمده‌اند، هر جايی را كه می‌خواهی به آنها بده. بگذار در جوشن كه بهترين ناحيهٔ مصر است ساكن شوند. اگر افراد شايسته‌ای بين آنها هست، آنها را بر گله‌های من نيز بگمار.»

7سپس يوسف، پدرش يعقوب را نزد فرعون آورد، و يعقوب فرعون را بركت داد. 8فرعون از يعقوب پرسيد: «چند سال از عمرت می‌گذرد؟»

9يعقوب جواب داد: «صد و سی سال دارم و سالهای عمرم را در غربت گذرانده‌ام. عمرم كوتاه و پر از رنج بوده است و به سالهای عمر اجدادم كه در غربت می‌زيستند، نمی‌رسد.»

10يعقوب پيش از رفتن، بار ديگر فرعون را بركت داد.

11آنگاه يوسف چنانكه فرعون دستور داده بود بهترين ناحيهٔ مصر، يعنی ناحيهٔ رعمسيس را برای پدر و برادرانش تعيين كرد و آنها را در آنجا مستقر نمود، 12و يوسف برحسب تعدادشان خوراک كافی در اختيار آنها گذاشت.

قحطی

13قحطی روز‌به‌روز شدت می‌گرفت به طوری كه همه مردم مصر و كنعان گرسنگی می‌كشيدند. 14يوسف تمام پولهای مردم مصر و كنعان را در مقابل غله‌هايی كه خريده بودند، جمع كرد و در خزانه‌های فرعون ريخت. 15وقتی پولِ مردم تمام شد، نزد يوسف آمده، گفتند: «ديگر پولی نداريم كه به عوض غله بدهيم. به ما خوراک بده. نگذار از گرسنگی بميريم.»

16يوسف در جواب ايشان گفت: «اگر پول شما تمام شده، چارپايان خود را به من بدهيد تا در مقابل، به شما غله بدهم.» 17آنها چاره‌ای نداشتند جز اين كه چهار پايان خود را به يوسف بدهند تا به ايشان نان بدهد. به اين ترتيب در عرض يک سال، تمام اسبها و الاغها و گله‌ها و رمه‌های مصر از آنِ فرعون گرديد.

18سال بعد، آنها بار ديگر نزد يوسف آمده، گفتند: «ای سَروَر ما، پول ما تمام شده و تمامی گله‌ها و رمه‌های ما نيز از آن تو شده است. ديگر چيزی برای ما باقی نمانده جز خودمان و زمينهايمان. 19نگذار از گرسنگی بميريم؛ نگذار زمينهايمان از بين بروند. ما و زمينهايمان را بخر و ما با زمينهايمان مالِ فرعون خواهيم شد. به ما غذا بده تا زنده بمانيم و بذر بده تا زمينها باير نمانند.»

20پس يوسف تمامی زمين مصر را برای فرعون خريد. مصريان زمينهای خود را به او فروختند، زيرا قحطی بسيار شديد بود. 21به اين طريق مردمِ سراسر مصر غلامان فرعون شدند. 22تنها زمينی كه يوسف نخريد، زمين كاهنان بود، زيرا فرعون خوراک آنها را به آنها می‌داد و نيازی به فروش زمين خود نداشتند.

23آنگاه يوسف به مردم مصر گفت: «من شما و زمينهای شما را برای فرعون خريده‌ام. حالا به شما بذر می‌دهم تا رفته در زمينها بكاريد. 24موقع برداشت محصول، يک پنجم آن را به فرعون بدهيد و بقيه را برای كشت سال بعد و خوراک خود و خانواده‌هايتان نگاه داريد.»

25آنها گفتند: «تو در حق ما خوبی كرده‌ای و جان ما را نجات داده‌ای، بنابراين غلامان فرعون خواهيم بود.»

26پس يوسف در تمامی سرزمين مصر مقرر نمود كه از آن به بعد، هر ساله يک پنجم از تمامی محصول به عنوان ماليات به فرعون داده شود. محصول زمينهای كاهنان مشمول اين قانون نبود. اين قانون هنوز هم به قوت خود باقی است.

27پس بنی‌اسرائيل در سرزمين مصر در ناحيهٔ جوشن ساكن شدند و بر تعداد و ثروت آنها پيوسته افزوده می‌شد. 28يعقوب بعد از رفتن به مصر، هفده سال ديگر زندگی كرد و در سن صد و چهل و هفت سالگی درگذشت. 29او در روزهای آخر عمرش، يوسف را نزد خود خواند و به او گفت: «دستت را زير ران من بگذار و سوگند ياد كن كه مرا در مصر دفن نكنی. 30بعد از مردنم جسد مرا از سرزمين مصر برده، در كنار اجدادم دفن كن.»

يوسف به او قول داد كه اين كار را بكند.

31يعقوب گفت: «برايم قسم بخور كه اين كار را خواهی كرد.» وقتی يوسف برايش قسم خورد، يعقوب خدا را شكر كرد و با خيال راحت در بسترش دراز كشيد.

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Mwanzo 47:1-31

Yakobo Ambariki Farao

147:1 Mwa 46:31Yosefu akaenda na kumwambia Farao, “Baba yangu na ndugu zangu wamekuja kutoka nchi ya Kanaani wakiwa na makundi yao ya kondoo, mbuzi na ngʼombe, pamoja na kila kitu walicho nacho, nao sasa wapo huko Gosheni.” 2Akachagua ndugu zake watano na kuwaonyesha kwa Farao.

347:3 Mwa 46:33Farao akawauliza hao ndugu zake, “Kazi yenu ni nini?”

Wakamjibu, “Watumishi wako ni wachunga mifugo, kama vile baba zetu walivyokuwa.” 447:4 Mwa 46:34Pia wakamwambia Farao, “Tumekuja kukaa huku kwa muda mfupi, kwa sababu njaa ni kali huko Kanaani, na mifugo ya watumishi wako haina malisho. Kwa hiyo sasa, tafadhali uruhusu watumishi wako wakae huko Gosheni.”

5Farao akamwambia Yosefu, “Baba yako na ndugu zako wamekuja kwako, 647:6 Kut 18:21nayo nchi ya Misri ipo mbele yako, uwakalishe baba yako na ndugu zako katika sehemu iliyo bora kupita zote katika nchi. Na waishi Gosheni. Kama unamfahamu yeyote miongoni mwao mwenye uwezo maalum, waweke wawe wasimamizi wa mifugo yangu.”

747:7 2Sam 14:22Ndipo Yosefu akamleta Yakobo baba yake na kumtambulisha mbele ya Farao. Baada ya Yakobo kumbariki Farao, 8Farao akamuuliza, “Je una umri gani?”

947:9 Mwa 25:7Naye Yakobo akamwambia Farao, “Siku za miaka ya kusafiri kwangu ni miaka 130. Miaka yangu imekuwa michache na ya taabu, wala haikufikia miaka ya kusafiri ya baba zangu.” 1047:10 Mwa 47:7Kisha Yakobo akambariki Farao, naye akaondoka mbele ya uso wake.

1147:11 Hes 33:3, 5Ndipo Yosefu akawakalisha baba yake na ndugu zake katika nchi ya Misri na kuwapa milki katika sehemu bora sana ya nchi, wilaya ya Ramesesi, kama Farao alivyoelekeza. 1247:12 Mwa 45:11Pia Yosefu akampa baba yake, na ndugu zake na wote wa nyumbani mwa baba yake vyakula, kwa kulingana na hesabu ya watoto wao.

Uongozi Wa Yosefu Wakati Wa Njaa

1347:13 Mwa 12:10Hata hivyo, hapakuwepo chakula katika sehemu yote kwa kuwa njaa ilikuwa kali sana; Misri na Kanaani zote zikaharibiwa kwa sababu ya njaa. 1447:14 Kut 7:23Yosefu akakusanya fedha zote zilizopatikana kutoka mauzo ya nafaka huko Misri na Kanaani, akazileta kwenye jumba la kifalme la Farao. 1547:15 Kut 16:3Fedha za watu wa Misri na Kanaani zilipokwisha, Wamisri wote wakamjia Yosefu na kumwambia, “Tupatie chakula. Kwa nini tufe mbele ya macho yako? Fedha zetu zimekwisha.”

1647:16 Mwa 47:18, 19Yosefu akawaambia, “Basi leteni mifugo yenu, nitawauzia chakula kwa kubadilisha na mifugo yenu, kwa kuwa fedha zenu zimekwisha.” 1747:17 Kut 14:9Kwa hiyo wakaleta mifugo yao kwa Yosefu, naye akawapa chakula kwa kubadilishana na farasi zao, kondoo na mbuzi zao, ngʼombe na punda zao. Katika mwaka huo wote Yosefu akawapa chakula kwa kubadilishana na mifugo yao yote.

18Mwaka ule ulipokwisha, wakamjia mwaka uliofuata na kumwambia, “Hatuwezi kuficha ukweli mbele za bwana wetu kwamba, kwa kuwa fedha zetu zimekwisha na wanyama wetu ni mali yako, sasa hakuna chochote kilichosalia kwa ajili ya bwana wetu isipokuwa miili yetu na ardhi yetu. 19Kwa nini tuangamie mbele ya macho yako, sisi pamoja na nchi yetu? Utununue sisi pamoja na ardhi yetu ili kubadilishana kwa chakula. Nasi pamoja na nchi yetu tutakuwa watumwa wa Farao. Tupe sisi mbegu ili tuweze kuishi wala tusife, nchi yetu isije ikawa ukiwa.”

2047:20 Mwa 12:10Kwa hiyo Yosefu akamnunulia Farao nchi yote ya Misri. Wamisri, mmoja baada ya mwingine, waliuza mashamba yao, kwa sababu njaa ilikuwa kali sana kwao. Nchi ikawa mali ya Farao, 21naye Yosefu akawafanya watu watumike kama watumwa, kuanzia upande mmoja wa Misri hadi upande mwingine. 2247:22 Kum 14:28-29Hata hivyo, hakununua nchi ya makuhani, kwa sababu walikuwa wanapata mgawo wao wa kawaida kutoka kwa Farao, nao walikuwa na chakula cha kuwatosha kutokana na mgawo waliopewa na Farao. Hii ndiyo sababu hawakuuza ardhi yao.

2347:23 Neh 5:3Yosefu akawaambia watu, “Kwa vile nimewanunua ninyi pamoja na nchi yenu leo kuwa mali ya Farao, hapa kuna mbegu kwa ajili yenu ili mweze kuziotesha. 2447:24 Mwa 41:34Lakini wakati mazao yatakapokuwa tayari, mpeni Farao sehemu ya tano. Sehemu hizo nne zitakazobaki mtaziweka kama mbegu kwa ajili ya mashamba na kwa ajili ya chakula chenu wenyewe na cha watu wa nyumbani mwenu na watoto wenu.”

2547:25 Mwa 32:5Wakamwambia, “Umeokoa maisha yetu. Basi na tupate kibali mbele ya macho ya bwana wetu; tutakuwa watumwa wa Farao.”

2647:26 Mwa 41:34Basi Yosefu akaiweka iwe sheria kuhusu nchi ya Misri, ambayo inatumika mpaka leo, kwamba, sehemu ya tano ya mazao ni mali ya Farao. Ni nchi ya makuhani tu ambayo haikuwa ya Farao.

2747:27 Mwa 1:22Basi Waisraeli wakaishi Misri katika nchi ya Gosheni. Wakapata mali huko wakastawi na kuongezeka kwa wingi sana.

2847:28 Za 105:23Yakobo akaishi Misri miaka kumi na saba, nayo miaka ya maisha yake ilikuwa 147. 2947:29 Mwa 24:32Wakati ulipokaribia wa Israeli kufa, akamwita mwanawe Yosefu na kumwambia, “Kama nimepata kibali machoni pake, weka mkono wako chini ya paja langu na uniahidi kuwa utanifanyia fadhili na uaminifu. Usinizike Misri, 3047:30 Yos 24:32lakini nitakapopumzika na baba zangu, unichukue kutoka Misri, ukanizike walipozikwa.”

Yosefu akamwambia, “Nitafanya kama unavyosema.”

3147:31 Amu 15:12Akamwambia, “Niapie.” Ndipo Yosefu akamwapia, naye Israeli akaabudu, akiwa ameegemea juu ya kichwa cha fimbo yake.