استر 1 – PCB & NEN

Persian Contemporary Bible

استر 1:1‏-22

ملكه وشتی بركنار می‌شود

1‏-3خشايارشا، پادشاه پارس، بر سرزمين پهناوری سلطنت می‌كرد كه از هند تا حبشه را در بر می‌گرفت و شامل ۱۲۷ استان بود.

او در سال سوم سلطنت خود، در كاخ سلطنتی شوش جشن بزرگی بر پا نمود و تمام بزرگان و مقامات مملكتی را دعوت كرد. فرماندهان لشكر پارس و ماد همراه با اميران و استانداران در اين جشن حضور داشتند. 4در طی اين جشن كه شش ماه طول كشيد، خشايارشا تمام ثروت و شكوه و عظمت سلطنت خود را به نمايش گذاشت.

5پس از پايان جشن، خشايارشا برای تمام كسانی كه در شوش زندگی می‌كردند، فقير و غنی، ميهمانی هفت روزه‌ای در باغ كاخ سلطنتی ترتيب داد. 6محل ميهمانی با پرده‌هايی از كتان سفيد و آبی تزيين شده بود. اين پرده‌ها با ريسمانهای سفيد و ارغوانی كه داخل حلقه‌های نقره‌ای قرار داشتند از ستونهای مرمر آويزان بود. تختهای طلا و نقره روی سنگفرشهايی از سنگ سماک، مرمر، صدف مرواريد و فيروزه قرار داشت. 7از كرم پادشاه، شراب شاهانه فراوان بود و در جامهای طلايی كه شكلهای گوناگون داشت، صرف می‌شد. 8پادشاه به پيشخدمتهای دربار دستور داده بود ميهمانان را در نوشيدن آزاد بگذارند، پس ايشان به دلخواه خود، هر قدر كه می‌خواستند شراب می‌نوشيدند.

9در همان هنگام، ملكه وشتی هم برای زنان دربار ضيافتی ترتيب داده بود.

10در آخرين روز ميهمانی، پادشاه كه از باده‌نوشی سرمست شده بود، هفت خواجهٔ حرمسرا يعنی مهومان، بزتا، حربونا، بغتا، ابغتا، زاتر و كركس را كه خادمان مخصوص او بودند احضار كرد. 11او به آنان دستور داد ملكه وشتی را كه بسيار زيبا بود با تاج ملوكانه به حضورش بياورند تا زيبايی او را به مقامات و مهمانانش نشان دهد. 12اما وقتی خواجه‌سرایان فرمان پادشاه را به ملكه وشتی رساندند، او از آمدن سرباز زد. پادشاه از اين موضوع بسيار خشمناک شد؛ 13‏-14اما پيش از آنكه اقدامی كند، اول از مشاوران خود نظر خواست، چون بدون مشورت با آنها كاری انجام نمی‌داد. مشاوران او مردانی دانا و آشنا به قوانين و نظام دادگستری پارس بودند و پادشاه به قضاوت آنها اعتماد داشت. نام اين دانشمندان كرشنا، شيتار، ادماتا، ترشيش، مرس، مرسنا و مموكان بود. اين هفت نفر جزو مقامات عالی رتبهٔ پارس و ماد و از اميران ارشد مملكتی بودند. 15خشايارشا از ايشان پرسيد: «در مورد ملكه وشتی چه بايد كرد؟ زيرا از فرمان پادشاه كه به او ابلاغ شده، سر باز زده است. قانون چه مجازاتی برای چنين شخصی تعيين كرده است؟»

16مموكان خطاب به پادشاه و اميران دربار گفت: «ملكه وشتی نه فقط به پادشاه بلكه به اميران دربار و تمام مردم مملكت اهانت كرده است. 17هر زنی كه بشنود ملكه وشتی چه كرده است، او نيز از دستور شوهرش سرپيچی خواهد كرد. 18وقتی زنانِ اميرانِ دربارِ پارس و ماد بشنوند كه ملكه چه كرده، آنان نيز با شوهرانشان چنين خواهند كرد و اين بی‌احترامی و سركشی به همه جا گسترش خواهد يافت. 19بنابراين، اگر پادشاه صلاح بدانند، فرمانی صادر كنند تا در قوانين ماد و پارس كه هرگز تغيير نمی‌كند ثبت گردد و بر طبق آن فرمان، ملكه وشتی ديگر به حضور پادشاه شرفياب نشود. آنگاه زن ديگری كه بهتر از او باشد به جای وی به عنوان ملكه انتخاب شود. 20وقتی اين فرمان در سراسر اين سرزمين پهناور اعلام شود آنگاه در همه جا شوهران، هر مقامی كه داشته باشند، مورد احترام زنانشان قرار خواهند گرفت.»

21پيشنهاد مموكان مورد پسند پادشاه و اميران دربار واقع شد و خشايارشا مطابق صلاحديد او عمل كرد 22و به تمام استانها، هر يک به خط و زبان محلی، نامه فرستاده، اعلام داشت كه هر مرد بايد رئيس خانهٔ خود باشد.

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Esta 1:1-22

Malkia Vashti Aondolewa

11:1 Ezr 4:16; Es 9:30Hili ndilo lililotokea wakati wa utawala wa Mfalme Ahasuero, yule aliyetawala juu ya majimbo mia na ishirini na saba tangu Bara Hindi hadi Kushi.1:1 Kushi hapa ina maana ya Ethiopia. 2Wakati huo Mfalme Ahasuero alitawala katika kiti chake cha enzi katika ngome ya mji wa Shushani. 31:3 1Fal 3:15Katika mwaka wa tatu wa utawala wake, alifanya karamu kwa ajili ya wakuu wake wote pamoja na maafisa. Akawaalika viongozi wa jeshi wa Uajemi na Umedi, wana wa wafalme na wakuu wa majimbo.

4Kwa siku zote 180 mfalme alionyesha utajiri mwingi wa ufalme wake, fahari na utukufu wa enzi yake. 51:5 Amu 14:17; 2Fal 21:18Siku hizo zilipopita, mfalme alifanya karamu kwa muda wa siku saba, katika bustani ya ndani katika jumba la kifalme, kwa ajili ya watu wote kuanzia mdogo hadi mkubwa, waliokuwa katika ngome ya mji wa Shushani. 61:6 Eze 23:41; Amo 3:12; 6:4Bustani ilikuwa na mapazia ya kitani nyeupe na buluu, yaliyofungiwa kamba za kitani nyeupe na kitambaa cha zambarau, kwenye pete za fedha juu ya nguzo za marmar. Kulikuwepo viti vya dhahabu na vya fedha vilivyokuwa vimewekwa kwenye ile sakafu iliyotengenezwa kwa mawe ya rangi, marmar, lulumizi na mawe mengine ya thamani. 7Vyombo vya dhahabu vilitumika kwa watu kunywea mvinyo, kila kimoja tofauti na kingine, naye mfalme akatoa mvinyo kwa wingi kwa kadiri ya ukarimu wake. 8Kwa amri ya mfalme kila mgeni aliruhusiwa kunywa alichotaka, kwa kuwa mfalme alitoa maagizo kwa watumishi wote wa kuhudumu mvinyo kumhudumia kila mtu kwa jinsi alivyotaka.

9Malkia Vashti pia akawafanyia wanawake karamu katika jumba la kifalme la Mfalme Ahasuero.

101:10 Rut 3:7; Dan 5:1-4Siku ya saba, wakati Mfalme Ahasuero alikuwa amesisimka roho yake kwa mvinyo, aliamuru matowashi saba waliokuwa wakimhudumia, yaani, Mehumani, Biztha, Harbona, Bigtha, Abagtha, Zethari na Karkasi, 11kumleta Malkia Vashti mbele ya mfalme akiwa amevaa taji lake la kifalme, ili aonyeshe uzuri wake kwa watu na wakuu, kwa kuwa alikuwa ni mzuri wa kupendeza. 121:12 Mwa 39:19; Mit 19:12Lakini wakati watumishi walipotoa amri ya mfalme, Malkia Vashti alikataa kuja. Ndipo mfalme alighadhibika, na hasira yake ikawaka.

131:13 1Nya 12:32Kwa kuwa ilikuwa desturi ya mfalme kupata ushauri kwa wataalamu katika mambo ya sheria na haki, alizungumza na watu wenye busara, ambao walijua nyakati, 14nao waliokuwa karibu na mfalme ni Karshena, Shethari, Admatha, Tarshishi, Meresi, Marsena na Memukani, wakuu saba wa Uajemi na Umedi waliokuwa na nafasi ya pekee kwa mfalme nao walikuwa na vyeo vya juu kabisa katika utawala wake.

15Mfalme akauliza, “Kulingana na sheria, Malkia Vashti anapaswa kutendewa nini? Malkia hakutii amri ya Mfalme Ahasuero ambayo matowashi walimpelekea.”

16Kisha Memukani akajibu mbele ya mfalme na wakuu, “Malkia Vashti si kwamba amemkosea mfalme tu bali pia amewakosea wakuu wote na watu wa himaya yote ya Mfalme Ahasuero. 17Kwa maana tendo hili la malkia litajulikana kwa wanawake wote, kwa hiyo watawadharau waume zao na kusema, ‘Mfalme Ahasuero aliagiza Malkia Vashti aletwe mbele yake, lakini alikataa.’ 18Leo hii wanawake wa wakuu wa Uajemi na Umedi ambao wamesikia juu ya tabia ya malkia watawatendea wakuu wote wa mfalme vivyo hivyo. Hapatakuwepo na mwisho wa dharau na magomvi.

191:19 Es 8:6; Dan 6:8, 12“Kwa hiyo, kama itampendeza mfalme, atoe amri ya kifalme na iandikwe katika sheria ya Uajemi na Umedi, ambayo haitabadilika, kwamba Vashti kamwe asije tena mbele ya Mfalme Ahasuero. Pia mfalme na atoe hiyo nafasi yake ya umalkia kwa mwanamke mwingine aliye bora kumliko yeye. 20Kisha mbiu hii ya mfalme itakapotangazwa katika himaya yake iliyo kubwa sana, wanawake wote watawaheshimu waume zao, kuanzia mdogo hadi mkubwa.”

21Mfalme na wakuu wake walipendezwa na shauri hili, hivyo basi mfalme akafanya kama Memukani alivyopendekeza. 221:22 Neh 13:24Alipeleka barua katika sehemu zote za ufalme wake, kwa kila jimbo kwa maandishi yake mwenyewe na kwa kila watu katika lugha yao wenyewe, akitangaza kwa msemo wa kila watu kwamba inampasa kila mwanaume kuwa mtawala wa nyumba yake mwenyewe.