Исаия 65 – NRT & NEN

New Russian Translation

Исаия 65:1-25

Суд и спасение

1– Я открылся тем, кто не спрашивал Меня;

Я найден теми, кто не искал Меня.

Народу, не призывавшему Мое имя,

Я сказал: «Я здесь, Я здесь».

2Весь день Я простирал руки Мои

к народу упрямому,

что ходит путями недобрыми,

по собственным умыслам –

3к народу, что постоянно оскорбляет Меня

прямо в лицо,

принося жертвы в садах65:3 Речь идет о жертвах, которые приносили во время языческих обрядов плодородия.

и возжигая благовония на кирпичных жертвенниках65:3 Возжигая благовония на кирпичных жертвенниках – вавилоняне возжигали благовония во славу «господина небес» на глиняных жертвенниках (см. Иер. 19:13).;

4что сидит в гробницах

и ночи проводит в тайных местах;

что ест свинину и держит в горшках похлебку из нечистого мяса65:4 См. Лев. 11:7.;

5что говорит: «Держись подальше, не приближайся ко мне;

я для тебя слишком свят».

Они – как дым для Моих ноздрей,

огонь, что горит весь день.

6Вот что написано предо Мной:

не смолчу, но воздам сполна,

сполна Я воздам им

7и за ваши грехи, и за грехи ваших отцов, –

говорит Господь. –

Так как они возжигали благовония на горах

и оскорбляли Меня на холмах,

Я отмерю им полную плату

за прежние их дела.

8Так говорит Господь:

– Когда в виноградной грозди еще остается сок,

тогда говорят: «Не губи ее,

в ней еще есть польза»,

так поступлю и Я ради Моих слуг:

всех Я не погублю.

9Я произведу потомков от Иакова,

и от Иуды – тех, кто будет владеть Моими горами;

унаследует их Мой избранный народ,

будут там жить Мои слуги.

10Шарон65:10 Шарон – богатая растительностью долина, которая располагалась на берегу Средиземного моря, к западу от горы Кармил. станет пастбищем для овец,

а долина Ахор65:10 Ахор – долина к западу от Иерихона (см. Нав. 7:24; Ос. 2:15). – местом отдыха для волов

народа Моего, который Меня взыскал.

11Но вас, оставляющих Господа,

забывающих Мою святую гору,

накрывающих стол для Гада, божества удачи,

наполняющих приправленным вином чаши

для Мени, божества судьбы, –

12вас обреку Я мечу;

все вы пойдете на бойню,

потому что Я звал, а вы не отвечали,

Я говорил, а вы не слушали.

Вы творили зло у Меня на глазах

и предпочли то, что Мне неугодно.

13Поэтому так говорит Владыка Господь:

– Слуги Мои будут есть,

а вы будете голодать;

слуги Мои будут пить,

а вы будете жаждать;

14слуги Мои будут радоваться,

а вы будете постыжены;

слуги Мои будут петь от радости в сердце,

а вы будете кричать от сердечных мук

и стенать от сокрушения духа.

15Имя свое вы оставите Моим избранным,

чтобы те использовали его как проклятие;

Владыка Господь предаст вас смерти,

но слугам Своим даст Он другое имя.

16Всякий в стране, призывающий благословение на себя,

Богом истины будет благословляться;

всякий в стране, приносящий клятву,

Богом истины будет клясться.

Прежние горести позабудутся

и скроются с Моих глаз.

Новое небо и новая земля

17– Вот, Я творю новое небо и новую землю;

не пребудет в памяти прежнее

и на ум не придет.

18Радуйтесь же и ликуйте вовеки о том,

что Я творю!

Я сделаю Иерусалим местом ликования,

а народ его наполню радостью!

19Сам Я возликую об Иерусалиме

и возрадуюсь о Моем народе.

Звуков плача и вопля

не будет в нем больше слышно.

20Никогда больше в нем не будет младенца,

что жил бы лишь несколько дней,

или старца, что не проживал бы свой век целиком;

тот, кто умрет столетним,

будет считаться юношей,

а кто не достигнет65:20 Или: «а грешник, достигший». ста лет,

будет считаться проклятым.

21Они будут строить дома и жить в них,

сажать виноградники и есть их плоды.

22Не будут они больше строить дома,

чтобы жил в них другой,

не будут более сажать,

чтобы другой ел.

Потому что дни Моего народа

сравняются с днями дерева:

избранные Мои будут наслаждаться

плодами своего труда.

23Они не будут трудиться напрасно

и рожать детей на беду;

они будут народом, благословенным Господом –

они и с ними их потомки.

24Прежде чем воззовут они, Я отвечу;

пока еще будут говорить, Я услышу.

25Волк и ягненок будут кормиться вместе,

и лев, как вол, будет есть сено,

а для змеи пыль будет пищей.

Не будут ни вредить, ни разрушать

на всей святой горе Моей, –

говорит Господь.

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Isaya 65:1-25

Hukumu Na Wokovu

165:1 Rum 10:20; Efe 2:12-13; Rum 9:30; Za 22:27; Hos 1:10; Rum 9:24-26; Isa 43:7“Nilijifunua kwa watu wale ambao hawakuniulizia.

Nimeonekana na watu wale ambao hawakunitafuta.

Kwa taifa lile ambalo halikuliita Jina langu,

nilisema, ‘Niko hapa, niko hapa.’

265:2 Za 78:8; Rum 10:21; Za 81:11-12; Mit 24:2; Isa 66:18Mchana kutwa nimeinyoosha mikono yangu

kwa watu wakaidi,

wanaokwenda katika njia ambazo si nzuri,

wafuatao mawazo yao wenyewe:

365:3 Isa 1:29; Law 17:5; Ay 1:11; Yer 41:5; Eze 23:41; Yer 44:17taifa ambalo daima hunikasirisha

machoni pangu,

wakitoa dhabihu katika bustani

na kufukiza uvumba juu ya madhabahu za matofali;

465:4 Law 11:7; Isa 8:19; Law 19:31; Kum 18:11watu waketio katikati ya makaburi

na kukesha mahali pa siri,

walao nyama za nguruwe,

nazo sufuria zao zina mchuzi wa nyama zilizo najisi,

565:5 Za 40:4; Lk 7:39; Yud 19; Mt 9:11; Lk 18:9-12; Mit 10:26wasemao, ‘Kaa mbali; usinikaribie,

kwa maana mimi ni mtakatifu mno kwako!’

Watu wa aina hiyo ni moshi katika pua zangu,

ni moto uwakao mchana kutwa.

665:6 2Nya 6:23; Kum 32:34; Za 50:3; Yer 16:18; Lk 6:38; Isa 59:18; Za 79:12; Eze 9:10“Tazama, jambo hili hubakia limeandikwa mbele zangu:

sitanyamaza, bali nitalipiza kwa ukamilifu;

nitalipiza mapajani mwao:

765:7 Kut 20:5; Yer 32:18; Law 26:39; Isa 22:14; Mit 10:24; Isa 10:12; 57:7dhambi zenu na dhambi za baba zenu,”

asema Bwana.

“Kwa sababu walitoa dhabihu za kuteketezwa juu ya milima

na kunichokoza mimi juu ya vilima,

nitawapimia mapajani mwao

malipo makamilifu kwa matendo yao ya zamani.”

865:8 Isa 5:2; 54:17; Kut 4:22; Yer 3:4; Isa 29:16; Rum 9:20-21; Ay 10:3Hili ndilo asemalo Bwana:

“Kama vile divai mpya ingali bado inapatikana

katika kishada cha zabibu,

nao watu husema, ‘Usikiharibu,

kwa kuwa bado kuna kitu kizuri ndani yake,’

hivyo ndivyo nitakavyofanya kwa ajili ya watumishi wangu;

sitawaangamiza wote.

965:9 Isa 45:19; Hes 34:13; Amo 9:11-15; Isa 32:18; Yer 50:19Nitawaleta wazao kutoka kwa Yakobo,

na kutoka kwa Yuda wale watakaomiliki milima yangu,

nao watu wangu wateule watairithi,

nako huko wataishi watumishi wangu.

1065:10 1Nya 27:29; Hos 2:15; Mdo 9:35; Yos 7:26; Isa 35:2; Yer 31:12; Eze 34:13-14Sharoni itakuwa malisho

kwa ajili ya makundi ya kondoo,

na Bonde la Akori mahali pa kupumzikia

kwa makundi ya ngʼombe,

kwa ajili ya watu wangu wanaonitafuta.

1165:11 Eze 23:41; Yer 19:4; 1Kor 10:21; Kum 29:24-25; 32:15; Yer 2:13; 19:4“Bali kwenu ninyi mnaomwacha Bwana

na kuusahau mlima wangu mtakatifu,

ninyi mnaoandaa meza kwa ajili ya Bahati,65:11 Bahati alikuwa mungu wa Wakaldayo ambaye pia alijulikana kama Gadi.

na kujaza mabakuli ya mvinyo uliochanganywa

kwa ajili ya Ajali,65:11 Ajali au Meni alikuwa mungu wa majaliwa.

1265:12 Mit 1:24-25; Yer 7:27; 2Nya 36:15-16; Yer 13:11; Isa 1:20; 30:25; Mik 5:15nitawaagiza mfe kwa upanga,

nanyi nyote mtainama chini ili kuchinjwa;

kwa kuwa niliwaita lakini hamkuitika,

nilisema lakini hamkusikiliza.

Mlitenda maovu machoni pangu,

nanyi mkachagua mambo yale yanayonichukiza.”

1365:13 Isa 1:19; Ay 18:12; Lk 6:25; Isa 33:16; 60:5; 44:9Kwa hiyo hili ndilo asemalo Bwana Mwenyezi:

“Watumishi wangu watakula,

lakini ninyi mtaona njaa;

watumishi wangu watakunywa

lakini ninyi mtaona kiu;

watumishi wangu watafurahi,

lakini ninyi mtaona haya.

1465:14 Isa 15:2; Lk 13:28; Za 109:28; Sef 3:14-20; Yak 5:13; Mt 8:12Watumishi wangu wataimba

kwa furaha ya mioyo yao,

lakini ninyi mtalia

kutokana na uchungu wa moyoni,

na kupiga yowe kwa sababu

ya uchungu wa roho zenu.

1565:15 Hes 5:27; Mdo 11:26; Zek 8:13; Za 102:8; Mwa 32:28; Ufu 2:17Mtaliacha jina lenu

kuwa laana kwa watu wangu waliochaguliwa;

Bwana Mwenyezi atawaua ninyi,

lakini watumishi wake atawapa jina jingine.

1665:16 Za 31:5; Ufu 3:14; Isa 19:18; Kum 29:19; Ay 11:16; Za 63:11Yeye aombaye baraka katika nchi

atafanya hivyo kwa Mungu wa kweli;

yeye aapaye katika nchi

ataapa kwa Mungu wa kweli.

Kwa kuwa taabu za zamani zitasahaulika

na kufichwa kutoka machoni pangu.

Mbingu Mpya Na Dunia Mpya

1765:17 2Kor 5:17; 2Pet 3:13; Yer 3:16; Ufu 7:17; Isa 41:22; 43:18“Tazama, nitaumba

mbingu mpya na dunia mpya.

Mambo ya zamani hayatakumbukwa,

wala hayatakuja akilini.

1865:18 Kum 32:43; Za 98:1-9; Isa 25:9; Ufu 21:2Lakini furahini na kushangilia daima

katika hivi nitakavyoumba,

kwa kuwa nitaumba Yerusalemu uwe wa kupendeza,

nao watu wake wawe furaha.

1965:19 Isa 35:10; 62:5; Ufu 7:17; Kum 30:9; Isa 25:8Nami nitaifurahia Yerusalemu

na kuwafurahia watu wangu;

sauti ya maombolezo na ya kilio

haitasikika humo tena.

2065:20 Mwa 15:15; Mhu 8:12; Zek 8:4; Isa 11:8; Mwa 5:1-32“Kamwe hatakuwepo tena ndani yake

mtoto mchanga atakayeishi siku chache tu,

au mzee ambaye hataishi akatimiza miaka yake.

Yeye atakayekufa akiwa na umri wa miaka mia moja

atahesabiwa kwamba ni kijana tu,

yeye ambaye hatafika miaka mia moja,

atahesabiwa kuwa amelaaniwa.

2165:21 Isa 32:18; 2Fal 19:29; Eze 28:26; Isa 61:4; 37:30; Amo 9:14Watajenga nyumba na kuishi ndani yake;

watapanda mashamba ya mizabibu na kula matunda yake.

2265:22 Za 92:12-14; 21:4; 91:16; Kum 28:30; Isa 14:1Hawatajenga nyumba, nao watu wengine waishi ndani yake,

au kupanda mazao na wengine wale.

Kwa kuwa kama zilivyo siku za mti,

ndivyo zitakavyokuwa siku za watu wangu,

wateule wangu watafurahia kwa siku nyingi

kazi za mikono yao.

2365:23 Mwa 12:2; Kum 28:3-12; Mdo 2:39; Hos 9:12; Isa 49:4; 1Kor 15:58; Yer 3:4Hawatajitaabisha kwa kazi bure,

wala hawatazaa watoto ili wapatwe na majanga,

kwa kuwa watakuwa taifa lililobarikiwa na Bwana,

wao na wazao wao pamoja nao.

2465:24 Dan 9:20-23; 10:12; Mt 6:8; Isa 55:6; Ay 8:6; Zek 10:6; Isa 30:19Kabla hawajaita, nitajibu,

nao wakiwa katika kunena, nitasikia.

2565:25 Mwa 3:14; Rum 16:20; Mik 7:17; Isa 11:6; Dan 2:35; Ay 40:15; 5:23; Isa 2:4Mbwa mwitu na mwana-kondoo watalisha pamoja,

naye simba atakula nyasi kama maksai,

lakini mavumbi yatakuwa chakula cha nyoka.

Hawatadhuru wala kuharibu

katika mlima wangu mtakatifu wote,”

asema Bwana.