Zekaria 6 – NEN & NIRV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Zekaria 6:1-15

Maono Ya Nane: Magari Manne Ya Vita

16:1 2Fal 2:12Nikatazama juu tena: nikaona mbele yangu magari manne ya vita yakija kutoka kati ya milima miwili, milima ya shaba! 26:2 Ufu 6:5; Zek 1:8Gari la kwanza lilivutwa na farasi wekundu, la pili lilivutwa na farasi weusi, 36:3 Ufu 6:2la tatu lilivutwa na farasi weupe na gari la nne lilivutwa na farasi wa madoadoa ya kijivu, wote wenye nguvu. 46:4 Zek 5:10Nikamuuliza malaika aliyekuwa akizungumza nami, “Hawa ni nani bwana wangu?”

56:5 Eze 37:9; Mt 24:31; Yos 3:11; Za 68:17; Ebr 1:7; 1:7, 14; Dan 7:10; Lk 1:19Malaika akanijibu, “Hizi ni roho nne za mbinguni zisimamazo mbele ya uwepo wa Bwana wa dunia yote, zinatoka kwenda kufanya kazi yake. 66:6 Yer 1:14Gari linalovutwa na farasi weusi linaelekea katika nchi ya kaskazini, la farasi weupe linaelekea magharibi na la farasi wa madoadoa ya kijivu linaelekea kusini.”

76:7 Isa 43:6; Mwa 13:17Wakati hao farasi wenye nguvu walipokuwa wakitoka, walikuwa wakijitahidi kwenda duniani kote. Akasema, “Nenda duniani kote!” Kwa hiyo wakaenda duniani kote.

86:8 Mhu 10:4; Eze 5:13; 24:13; Zek 1:10Kisha akaniita, “Tazama, wale wanaokwenda kuelekea nchi ya kaskazini wamepumzisha Roho yangu katika nchi ya kaskazini.”

Taji Kwa Ajili Ya Yoshua

9Neno la Bwana likanijia kusema: 106:10 Ezr 2:1; 7:14-16; Yer 28:6“Chukua fedha na dhahabu kutoka kwa watu waliohamishwa, yaani Heldai, Tobia na Yedaya ambao wamefika kutoka Babeli. Siku iyo hiyo nenda nyumbani kwa Yosia mwana wa Sefania. 116:11 Kut 28:36; Za 21:3; 1Nya 6:15; Ezr 2:2; 3:2; Zek 3:1Chukua fedha na dhahabu utengeneze taji, nawe uiweke kichwani mwa kuhani mkuu Yoshua, mwana wa Yehosadaki. 126:12 Isa 4:2; Eze 17:22; Ezr 3:8-10; Zek 4:6-9; Isa 9:6; Mik 5:5; Yer 23:5; 33:15; Zek 13:7; Mk 15:39; Lk 1:78; Yn 1:45; Za 80:15-17; Efe 2:20; Ebr 2:9Umwambie, hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote: ‘Huyu ndiye mtu ambaye jina lake ni Tawi, naye atachipua kutoka mahali pake na kujenga Hekalu la Bwana. 136:13 Za 110:4; 21:5Ni yeye atakayejenga Hekalu la Bwana, naye atavikwa utukufu na ataketi kumiliki katika kiti cha enzi naye atakuwa kuhani katika kiti chake cha enzi. Hapo patakuwa amani kati ya hao wawili.’ 146:14 Kut 28:12; Mk 14:9Taji itatolewa kwa Heldai, Tobia, Yedaya na Heni mwana wa Sefania kama kumbukumbu ndani ya Hekalu la Bwana. 156:15 Efe 2:13; Isa 60:10; Zek 2:9-11; Isa 58:12; Yer 7:23Wale walio mbali sana watakuja na kusaidia kulijenga Hekalu la Bwana, nanyi mtajua ya kwamba Bwana Mwenye Nguvu Zote amenituma kwenu. Hili litatokea ikiwa mtamtii Bwana Mungu wenu kwa bidii.”

New International Reader’s Version

Zechariah 6:1-15

A Vision of Four Chariots

1I looked up again and saw four chariots. They were coming out from between two mountains. The mountains were made out of bronze. 2The first chariot was pulled by red horses. The second one had black horses. 3The third had white horses. And the fourth had spotted horses. All the horses were powerful. 4I asked the angel who was talking with me, “Sir, what are these?”

5The angel answered, “The four spirits of heaven. They are going out to serve the Lord of the whole world. 6The chariot pulled by the black horses is going toward the north country. The one with the white horses is going toward the west. And the one with the spotted horses is going toward the south.”

7The powerful horses went out. They were in a hurry to go all over the earth. The angel said, “Go all through the earth!” So they did.

8Then the Lord called out to me, “Look! The horses going toward the north have given my Spirit rest in the north country.”

A Crown Is Given to Joshua

9A message from the Lord came to me. His angel said, 10“Get some silver and gold from Heldai, Tobijah and Jedaiah. They have just come back from Babylon. On that same day go to Josiah’s house. He is the son of Zephaniah. 11Use the silver and gold to make a crown. Set it on the head of Joshua the high priest. He is the son of Jozadak. 12Give Joshua a message from the Lord who rules over all. He says, ‘Here is the man whose name is the Branch. He will branch out and build my temple. 13That is what he will do. He will be dressed in majesty as if it were his royal robe. He will sit as king on his throne. He will also be a priest there. So he will combine the positions of king and priest in himself.’ 14The crown will be given to Heldai, Tobijah, Jedaiah and Zephaniah’s son Hen. The crown will be kept in the Lord’s temple. It will remind everyone that the Lord’s promises will come true. 15Those who are far away will come to Jerusalem. They will help build the Lord’s temple. Then his people will know that the Lord who rules over all has sent me to them. It will happen if they are careful to obey the Lord their God.”