Zekaria 1 – NEN & BPH

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Zekaria 1:1-21

Wito Wa Kumrudia Bwana

11:1 Ezr 4:24; 6:15; Mt 23:35; Lk 11:51; Neh 12:4Katika mwezi wa nane wa mwaka wa pili wa utawala wa Mfalme Dario, neno la Bwana lilimjia nabii Zekaria mwana wa Berekia, mwana wa Ido, kusema:

21:2 2Nya 36:16Bwana aliwakasirikia sana baba zako wa zamani. 31:3 Yak 4:8; Mal 3:7; Ay 22:2; Yer 25:5; Mik 7:19; Lk 15:20Kwa hiyo waambie watu: Hivi ndivyo Bwana Mwenye Nguvu Zote asemavyo: ‘Nirudieni mimi,’ asema Bwana Mwenye Nguvu Zote, ‘nami nitawarudia ninyi,’ asema Bwana Mwenye Nguvu Zote. 41:4 2Nya 7:14; 24:19; 36:15; Zek 7:7; 2Fal 17:13; Za 78:8; 106:6; Yer 6:17; 17:23; 23:22; Eze 20:18; 33:4; Isa 1:16-17; Yer 3:12; Eze 33:11; Hos 14:1; Mit 3:8-9; Mdo 3:19Msiwe kama baba zenu, ambao manabii waliotangulia waliwatangazia: Hivi ndivyo Bwana Mwenye Nguvu Zote asemavyo: ‘Geukeni, mziache njia zenu mbaya na matendo yenu maovu.’ Lakini hawakunisikiliza wala kufuata maelekezo yangu, asema Bwana. 5Wako wapi baba zako sasa? Nao manabii, je, wanaishi milele? 61:6 Isa 44:26; Kum 28:2; Dan 9:12; Hos 5:9; Yer 12:14-17; 39:16; 23:20; 44:17; Mao 2:17; Isa 55:1; Mao 1:18Je, maneno yangu na amri zangu nilizowaagiza manabii watumishi wangu, hayakuwapata baba zenu?”

“Kisha walitubu na kusema, ‘Bwana Mwenye Nguvu Zote ametutenda sawasawa na njia zetu na matendo yetu yalivyostahili, kama alivyokusudia kufanya.’ ”

Maono Ya Kwanza: Mtu Katikati Ya Miti Ya Mihadasi

7Katika siku ya ishirini na nne ya mwezi wa kumi na moja, yaani mwezi uitwao Shebati, katika mwaka wa pili wa utawala wa Mfalme Dario, neno la Bwana lilimjia nabii Zekaria mwana wa Berekia mwana wa Ido.

81:8 Ufu 6:4; Zek 6:2-7; Yos 5:13Wakati wa usiku nilipata maono, mbele yangu alikuwepo mtu akiendesha farasi mwekundu! Alikuwa amesimama katikati ya miti ya mihadasi kwenye bonde. Nyuma yake walikuwepo farasi wekundu, wa kikahawia na weupe.

91:9 Zek 4:1-5; 5:5; Dan 7:16Nikauliza, “Hivi ni vitu gani bwana wangu?”

Malaika aliyekuwa akizungumza na mimi akanijibu, “Nitakuonyesha kuwa ni nini.”

101:10 Zek 6:5-8; Za 91:11; Ebr 1:14Kisha yule mtu aliyesimama katikati ya miti ya mihadasi akaeleza, “Ni wale ambao Bwana amewatuma waende duniani kote.”

111:11 Isa 14:7; Mwa 16:7; Za 102:20Nao wakatoa taarifa kwa yule malaika wa Bwana, aliyekuwa amesimama katikati ya miti ya mihadasi, “Tumepita duniani kote na kukuta ulimwengu wote umepumzika kwa amani.”

121:12 Za 6:3; 40:11; Yer 40:5; 2Nya 36:21; Dan 9:2; Za 103:13; Ufu 6:10; Zek 7:5Kisha malaika wa Bwana akasema, “Bwana Mwenye Nguvu Zote, utazuia mpaka lini rehema kutoka Yerusalemu na miji ya Yuda, ambayo umeikasirikia kwa miaka hii sabini?” 131:13 Isa 35:4; Ay 15:11; Zek 4:1; Isa 40:1-2; Yer 29:10Kwa hiyo Bwana akazungumza maneno ya upole na ya kufariji kwa malaika aliyezungumza nami.

141:14 Isa 26:11; Yoe 2:18; Zek 8:2Kisha malaika yule aliyekuwa akizungumza nami akasema, “Tangaza neno hili: Hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote asemalo: ‘Nina wivu sana kwa ajili ya Yerusalemu na Sayuni, 151:15 Yer 48:11; 2Nya 28:9; Za 69:26; 123:3-4; Amo 1:11; Isa 47:6lakini nimeyakasirikia sana mataifa yanayojisikia kuwa yako salama. Nilikuwa nimewakasirikia Israeli kidogo tu, lakini mataifa hayo yaliwazidishia maafa.’

161:16 Zek 2:1-2; 8:3; Ay 38:5; Isa 12:1“Kwa hiyo, hivi ndivyo asemavyo Bwana: ‘Nitairudia Yerusalemu kwa rehema na huko nyumba yangu itajengwa tena. Nayo kamba ya kupimia itanyooshwa Yerusalemu,’ asema Bwana Mwenye Nguvu Zote.

171:17 Isa 14:1; 40:1; 54:8-10; 61:4; Ezr 9:9; Za 51:18; Isa 51:3; Zek 3:2“Endelea kutangaza zaidi kwamba: Hivi ndivyo asemavyo Bwana Mwenye Nguvu Zote: ‘Miji yangu itafurika tena ustawi na Bwana atamfariji tena Sayuni na kumchagua Yerusalemu.’ ”

Maono Ya Pili: Pembe Nne Na Mafundi Wanne

18Kisha nikatazama juu, na pale mbele yangu nikaona pembe nne! 191:19 Amo 6:13; Ezr 4:1; Hab 3:14Nikamuuliza yule malaika aliyekuwa akizungumza nami, “Ni nini hivi?”

Akanijibu, “Hizi ni zile pembe zilizowatawanya Yuda, Israeli na Yerusalemu.”

20Kisha Bwana akanionyesha mafundi wanne. 211:21 1Fal 22:11; Za 75:4, 10; Isa 54:16-17; Zek 12:9Nikauliza, “Hawa wanakuja kufanya nini?”

Akanijibu, “Hizi ndizo pembe zilizowatawanya Yuda ili asiwepo atakayeweza kuinua kichwa chake, lakini mafundi wamekuja kuzitia hofu na kuzitupa chini hizi pembe za mataifa ambayo yaliinua pembe zao dhidi ya nchi ya Yuda na kuwatawanya watu wake.”

Bibelen på hverdagsdansk

Zakariasʼ Bog 1:1-17

Et kald til folket om at vende om til Gud

1I den ottende måned i kong Dareios1,1 Dareios Hystaspes, konge i Persien fra 522-486 f.Kr. af Persiens andet regeringsår talte Herren til Israels folk gennem profeten Zakarias, der var søn af Berekja og barnebarn af Iddo:

2-4„Hør, hvad jeg, Herren den Almægtige, siger: Hvis I vil vende om og komme til mig, vil jeg komme jer i møde. Vær ikke som jeres forfædre, som jeg var nødt til at straffe hårdt. Jeg advarede dem gennem mine profeter om at vende om fra deres ugudelige levemåde og onde handlinger, men de nægtede at lytte til mig. 5Nu er de alle sammen borte, og profeterne er døde. 6Men det, jeg sagde til dem gennem mine tjenere, profeterne, gik i opfyldelse, og de måtte angrende erkende: ‚Herren straffede os for vores onde levevis og handlinger, akkurat som han sagde, at han ville!’ ”

Herren opmuntrer Israels folk

7Den 24. dag i den 11. måned1,7 Teksten tilføjer: „Shebat måned”. samme år, talte Herren til mig i et syn om natten. 8Jeg så en mand sidde på en rød hest mellem nogle myrtebuske i en kløft. Bag ham var der mange ryttere på røde, brune og hvide heste. 9Ved siden af mig stod en engel. „Hvad betyder alle de heste?” spurgte jeg englen. „Det vil du få at se!” svarede han.

10„Herren sendte dem ud for at inspicere hele jorden,” forklarede englen på den røde hest, 11der stod mellem myrtebuskene. Derefter aflagde de øvrige ryttere rapport: „Vi har været overalt på jorden, og alle vegne er der fred og ro.” 12Da sagde englen på den røde hest: „Almægtige Herre, i 70 år har du været vred på de landflygtige fra Jerusalem og Judas byer. Hvornår vil du gribe ind og vise dem barmhjertighed?”

13Herren talte nu til englen, som stod ved min side, 14hvorpå englen henvendte sig til mig og sagde: „Forkynd følgende budskab fra Herren, den Almægtige: ‚Jerusalem og Zions bjerg har en særlig plads i mit hjerte. 15Jeg er vred på de selvsikre, gudløse folkeslag, for selv om jeg brugte dem til at straffe mit folk, gik de alt for langt i deres skånselsløse opførsel. 16Derfor erklærer jeg, Herren: Jeg kommer Jerusalem i møde med barmhjertighed. Mit tempel skal genrejses, og hele Jerusalem skal genopbygges. Ja, siger jeg, Herren den Almægtige: 17Jeg vil igen velsigne Israels byer med velstand, trøste Jerusalems indbyggere og bosætte mig på Zions bjerg.’ ”