Zaburi 80 – NEN & KJV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Zaburi 80:1-19

Zaburi 80

Maombi Kwa Ajili Ya Kuponywa Kwa Taifa

Kwa mwimbishaji. Mtindo wa “Yungiyungi za Agano.” Zaburi ya Asafu.

180:1 Kut 25:22; 1Sam 4:4; Za 77:20; 89:1; Kum 33:2Ee Mchungaji wa Israeli tusikie,

wewe umwongozaye Yosefu kama kundi;

wewe uketiye katika kiti cha enzi

katikati ya makerubi, angaza

280:2 Hes 2:18-24; Za 35:23; 54:1; 71:2; 109:26; 116:4; 119:94mbele ya Efraimu, Benyamini na Manase.

Uamshe nguvu zako,

uje utuokoe.

380:3 Za 71:20; 85:4; Yer 31:18; Mao 5:21; Hes 6:25; Za 80:7, 19; 1Fal 18:37Ee Mungu, uturejeshe,

utuangazie uso wako,

ili tuweze kuokolewa.

480:4 Za 74:10; Kum 29:20Ee Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote,

hata lini hasira yako itawaka na kufoka moshi

dhidi ya maombi ya watu wako?

580:5 Ay 3:24; Isa 30:20Umewalisha kwa mkate wa machozi,

umewafanya wanywe machozi bakuli tele.

680:6 Za 79:4Tumekuwa chanzo cha ugomvi kwa jirani zetu,

na adui zetu wanatudhihaki.

780:7 Za 80:3Ee Mungu Mwenye Nguvu Zote, uturejeshe;

utuangazie uso wako,

nasi tuweze kuokolewa.

880:8 Isa 5:1-2, 7; Yer 2:21; Mt 21:33-41; Kut 15:17; 23:28-30; Yos 13:6; Mdo 7:45; Eze 15:6Ulileta mzabibu kutoka Misri,

ukawafukuza mataifa, ukaupanda.

9Uliandaa shamba kwa ajili yake,

mizizi ikawa imara, ukajaza nchi.

10Milima ilifunikwa kwa kivuli chake,

matawi yake yakafunika mierezi mikubwa.

1180:11 Kut 23:31; Za 72:8Matawi yake yalienea mpaka Baharini,80:11 Huenda inamaanisha Bahari ya Mediterania.

machipukizi yake mpaka kwenye Mto.80:11 Yaani Mto Frati.

1280:12 Isa 5:5; 30:13; Za 89:40; Yer 39:8Mbona umebomoa kuta zake

ili wote wapitao karibu

wazichume zabibu zake?

1380:13 Yer 5:6Nguruwe mwitu wanauharibu

na wanyama wa kondeni hujilisha humo.

1480:14 Kum 26:15; Zek 1:12, 16, 17; Isa 63:15Turudie, Ee Mungu Mwenye Nguvu Zote!

Tazama chini kutoka mbinguni na uone!

Linda mzabibu huu,

1580:15 Isa 49:5mche ulioupanda kwa mkono wako wa kuume,

mwana uliyemlea

kwa ajili yako mwenyewe.

1680:16 Za 79:1; Kum 28:20Mzabibu wako umekatwa, umechomwa moto,

unapowakemea, watu wako huangamia.

1780:17 Ay 25:6; Za 89:21; 110:1; Kut 4:22; Dan 7:13, 14; Yn 5:21-27Mkono wako na utulie juu ya mtu aliyeko mkono wako wa kuume,

mwana wa mtu uliyemlea kwa ajili yako mwenyewe.

1880:18 Za 85:6; Isa 57:15; Hos 6:2Ndipo hatutakuacha tena,

utuhuishe, nasi tutaliitia jina lako.

1980:19 Hes 6:25; Za 27:4, 9Ee Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote, uturejeshe;

utuangazie uso wako,

ili tuweze kuokolewa.

King James Version

Psalms 80:1-19

To the chief Musician upon Shoshannim-eduth, A Psalm of Asaph.

1Give ear, O Shepherd of Israel, thou that leadest Joseph like a flock; thou that dwellest between the cherubims, shine forth.80.1 of: or, for

2Before Ephraim and Benjamin and Manasseh stir up thy strength, and come and save us.80.2 come…: Heb. come for salvation to us

3Turn us again, O God, and cause thy face to shine; and we shall be saved.

4O LORD God of hosts, how long wilt thou be angry against the prayer of thy people?80.4 be…: Heb. smoke

5Thou feedest them with the bread of tears; and givest them tears to drink in great measure.

6Thou makest us a strife unto our neighbours: and our enemies laugh among themselves.

7Turn us again, O God of hosts, and cause thy face to shine; and we shall be saved.

8Thou hast brought a vine out of Egypt: thou hast cast out the heathen, and planted it.

9Thou preparedst room before it, and didst cause it to take deep root, and it filled the land.

10The hills were covered with the shadow of it, and the boughs thereof were like the goodly cedars.80.10 goodly…: Heb. cedars of God

11She sent out her boughs unto the sea, and her branches unto the river.

12Why hast thou then broken down her hedges, so that all they which pass by the way do pluck her?

13The boar out of the wood doth waste it, and the wild beast of the field doth devour it.

14Return, we beseech thee, O God of hosts: look down from heaven, and behold, and visit this vine;

15And the vineyard which thy right hand hath planted, and the branch that thou madest strong for thyself.

16It is burned with fire, it is cut down: they perish at the rebuke of thy countenance.

17Let thy hand be upon the man of thy right hand, upon the son of man whom thou madest strong for thyself.

18So will not we go back from thee: quicken us, and we will call upon thy name.

19Turn us again, O LORD God of hosts, cause thy face to shine; and we shall be saved.