Zaburi 80 – NEN & CST

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Zaburi 80:1-19

Zaburi 80

Maombi Kwa Ajili Ya Kuponywa Kwa Taifa

Kwa mwimbishaji. Mtindo wa “Yungiyungi za Agano.” Zaburi ya Asafu.

180:1 Kut 25:22; 1Sam 4:4; Za 77:20; 89:1; Kum 33:2Ee Mchungaji wa Israeli tusikie,

wewe umwongozaye Yosefu kama kundi;

wewe uketiye katika kiti cha enzi

katikati ya makerubi, angaza

280:2 Hes 2:18-24; Za 35:23; 54:1; 71:2; 109:26; 116:4; 119:94mbele ya Efraimu, Benyamini na Manase.

Uamshe nguvu zako,

uje utuokoe.

380:3 Za 71:20; 85:4; Yer 31:18; Mao 5:21; Hes 6:25; Za 80:7, 19; 1Fal 18:37Ee Mungu, uturejeshe,

utuangazie uso wako,

ili tuweze kuokolewa.

480:4 Za 74:10; Kum 29:20Ee Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote,

hata lini hasira yako itawaka na kufoka moshi

dhidi ya maombi ya watu wako?

580:5 Ay 3:24; Isa 30:20Umewalisha kwa mkate wa machozi,

umewafanya wanywe machozi bakuli tele.

680:6 Za 79:4Tumekuwa chanzo cha ugomvi kwa jirani zetu,

na adui zetu wanatudhihaki.

780:7 Za 80:3Ee Mungu Mwenye Nguvu Zote, uturejeshe;

utuangazie uso wako,

nasi tuweze kuokolewa.

880:8 Isa 5:1-2, 7; Yer 2:21; Mt 21:33-41; Kut 15:17; 23:28-30; Yos 13:6; Mdo 7:45; Eze 15:6Ulileta mzabibu kutoka Misri,

ukawafukuza mataifa, ukaupanda.

9Uliandaa shamba kwa ajili yake,

mizizi ikawa imara, ukajaza nchi.

10Milima ilifunikwa kwa kivuli chake,

matawi yake yakafunika mierezi mikubwa.

1180:11 Kut 23:31; Za 72:8Matawi yake yalienea mpaka Baharini,80:11 Huenda inamaanisha Bahari ya Mediterania.

machipukizi yake mpaka kwenye Mto.80:11 Yaani Mto Frati.

1280:12 Isa 5:5; 30:13; Za 89:40; Yer 39:8Mbona umebomoa kuta zake

ili wote wapitao karibu

wazichume zabibu zake?

1380:13 Yer 5:6Nguruwe mwitu wanauharibu

na wanyama wa kondeni hujilisha humo.

1480:14 Kum 26:15; Zek 1:12, 16, 17; Isa 63:15Turudie, Ee Mungu Mwenye Nguvu Zote!

Tazama chini kutoka mbinguni na uone!

Linda mzabibu huu,

1580:15 Isa 49:5mche ulioupanda kwa mkono wako wa kuume,

mwana uliyemlea

kwa ajili yako mwenyewe.

1680:16 Za 79:1; Kum 28:20Mzabibu wako umekatwa, umechomwa moto,

unapowakemea, watu wako huangamia.

1780:17 Ay 25:6; Za 89:21; 110:1; Kut 4:22; Dan 7:13, 14; Yn 5:21-27Mkono wako na utulie juu ya mtu aliyeko mkono wako wa kuume,

mwana wa mtu uliyemlea kwa ajili yako mwenyewe.

1880:18 Za 85:6; Isa 57:15; Hos 6:2Ndipo hatutakuacha tena,

utuhuishe, nasi tutaliitia jina lako.

1980:19 Hes 6:25; Za 27:4, 9Ee Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote, uturejeshe;

utuangazie uso wako,

ili tuweze kuokolewa.

Nueva Versión Internacional (Castilian)

Salmo 80:1-19

Salmo 80

Al director musical. Sígase la tonada de «Los lirios del pacto». Salmo de Asaf.

1Pastor de Israel,

tú que guías a José como a un rebaño,

tú que reinas entre los querubines, ¡escúchanos!

¡Resplandece 2delante de Efraín, Benjamín y Manasés!

¡Muestra tu poder, y ven a salvarnos!

3Restáuranos, oh Dios;

haz resplandecer tu rostro sobre nosotros,

y sálvanos.

4¿Hasta cuándo, Señor Dios Todopoderoso,

arderá tu ira contra las oraciones de tu pueblo?

5Por comida, le has dado pan de lágrimas;

por bebida, lágrimas en abundancia.

6Nos has hecho motivo de contienda

para nuestros vecinos;

nuestros enemigos se burlan de nosotros.

7Restáuranos, oh Dios Todopoderoso;

haz resplandecer tu rostro sobre nosotros,

y sálvanos.

8De Egipto trajiste una vid;

expulsaste a los pueblos paganos, y la plantaste.

9Le limpiaste el terreno,

y ella echó raíces y llenó la tierra.

10Su sombra se extendía hasta las montañas,

su follaje cubría los más altos cedros.

11Sus ramas se extendieron hasta el Mediterráneo

y sus renuevos hasta el Éufrates.

12¿Por qué has derribado sus muros?

¡Todos los que pasan le arrancan uvas!

13Los jabalíes del bosque la destruyen,

los animales salvajes la devoran.

14¡Vuélvete a nosotros, oh Dios Todopoderoso!

¡Asómate a vernos desde el cielo

y brinda tus cuidados a esta vid!

15¡Es la raíz que plantaste con tu diestra!

¡Es el vástago que has criado para ti!

16Tu vid está derribada, quemada por el fuego;

a tu reprensión perece tu pueblo.80:16 Tu vid … tu pueblo (lectura probable); Haz que perezcan, a tu reprensión, / los que la queman y destruyen (TM).

17Bríndale tu apoyo al hombre de tu diestra,

al ser humano80:17 ser humano. Lit. hijo de hombre. que para ti has criado.

18Nosotros no nos apartaremos de ti;

reavívanos, e invocaremos tu nombre.

19Restáuranos, Señor Dios Todopoderoso;

haz resplandecer tu rostro sobre nosotros,

y sálvanos.