Zaburi 78 – NEN & KJV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Zaburi 78:1-72

Zaburi 78

Mungu Na Watu Wake

Utenzi wa Asafu.

178:1 Kut 19:5; Kum 32:29; Isa 51:4; 55:3Enyi watu wangu, sikieni mafundisho yangu,

sikilizeni maneno ya kinywa changu.

278:2 Za 49:4; Mt 13:35Nitafungua kinywa changu kwa mafumbo,

nitazungumza mambo yaliyofichika, mambo ya kale:

378:3 Za 44:1; Amu 6:13yale ambayo tuliyasikia na kuyajua,

yale ambayo baba zetu walituambia.

478:4 Kut 12:26; Yos 4:6, 7; Kum 4:9; 11:19; 32:7; Za 71:18; 26:7; 71:17Hatutayaficha kwa watoto wao;

tutakiambia kizazi kijacho

matendo yastahiliyo sifa ya Bwana,

uweza wake, na maajabu aliyoyafanya.

578:5 Za 19:7; 81:5; 147:19Aliagiza amri kwa Yakobo

na akaweka sheria katika Israeli,

ambazo aliwaamuru baba zetu

wawafundishe watoto wao,

678:6 Za 22:31; 102:18ili kizazi kijacho kizijue,

pamoja na watoto ambao watazaliwa,

nao pia wapate kuwaeleza watoto wao.

778:7 Kum 6:12; 5:29Ndipo wangeweka tumaini lao kwa Mungu,

nao wasingesahau matendo yake,

bali wangalizishika amri zake.

878:8 2Nya 30:7; Kut 32:9; 23:21; Kum 21:18; Isa 30:9; 65:2Ili wasifanane na baba zao,

waliokuwa kizazi cha ukaidi na uasi,

ambao roho zao hazikuwa na uaminifu kwake,

ambao roho zao hazikumwamini.

978:9 Za 78:57; 1Nya 12:2; Hos 7:16; Amu 20:39Watu wa Efraimu, ingawa walijifunga pinde,

walikimbia siku ya vita.

1078:10 Yos 7:10; 2Fal 17:15; Kut 16:28; Yer 11:8Hawakulishika agano la Mungu

na walikataa kuishi kwa sheria yake.

1178:11 Za 106:13; Isa 17:10; Yer 2:32Walisahau aliyokuwa ameyatenda,

maajabu aliyokuwa amewaonyesha.

1278:12 Neh 9:17; Za 106:22; Kut 11:9; Hes 13:22; Mwa 32:3; Isa 19:11Alitenda miujiza machoni mwa baba zao,

huko Soani, katika nchi ya Misri.

1378:13 Kut 14:21, 22; 15:8; Za 66:6; 136:13Aliigawanya bahari akawapitisha,

alifanya maji yasimame imara kama ukuta.

1478:14 Kut 13:21; Za 105:39Aliwaongoza kwa wingu mchana

na kwa nuru kutoka kwenye moto usiku kucha.

1578:15 Hes 20:11; 1Kor 10:4; Kut 17; 6; Za 105:41; Isa 41:18Alipasua miamba jangwani

na akawapa maji tele kama bahari,

1678:16 Kum 9:21alitoa vijito kutoka kwenye jabali lililochongoka,

akayafanya maji yatiririke kama mito.

1778:17 Za 78:32Lakini waliendelea kutenda dhambi dhidi yake,

wakiasi jangwani dhidi ya Aliye Juu Sana.

1878:18 Kut 15:24; 17:2; 1Kor 10:9; Hes 11:4Kwa makusudi walimjaribu Mungu,

wakidai vyakula walivyovitamani.

1978:19 Hes 11:4; 21:5Walinena dhidi ya Mungu, wakisema,

“Je, Mungu aweza kuandaa meza jangwani?

2078:20 Hes 20:11; Kut 17:6Alipopiga mwamba, maji yalitoka kwa nguvu,

vijito vikatiririka maji mengi.

Lakini je, aweza kutupa chakula pia?

Je, anaweza kuwapa watu wake nyama?”

2178:21 Hes 11:1Bwana alipowasikia, alikasirika sana,

moto wake ukawa dhidi ya Yakobo,

na ghadhabu yake ikawaka dhidi ya Israeli,

2278:22 Kum 1:32; Ebr 3:19; 3:10kwa kuwa hawakumwamini Mungu,

wala kuutumainia ukombozi wake.

2378:23 Mwa 7:11; Kum 28:12; 2Fal 7:2Hata hivyo alitoa amri kwa anga zilizo juu

na kufungua milango ya mbingu,

2478:24 Kut 16:4; Yn 6:31; Neh 9:15, 20; 1Kor 10:3akawanyeshea mana ili watu wale;

aliwapa nafaka ya mbinguni.

25Watu walikula mkate wa malaika,

akawatumia chakula chote ambacho wangeliweza kula.

2678:26 Hes 11:31Aliachia upepo wa mashariki kutoka kwenye mbingu

na kuuongoza upepo wa kusini kwa uwezo wake.

2778:27 Kut 16:13; Hes 11:31Aliwanyeshea nyama kama mavumbi,

ndege warukao kama mchanga wa pwani.

28Aliwafanya washuke ndani ya kambi yao,

kuzunguka mahema yao yote.

2978:29 Hes 11:20Walikula na kusaza,

kwa maana alikuwa amewapa kile walichotamani.

3078:30 Hes 11:33Kabla hawajamaliza kula walichokitamani,

hata kilipokuwa kingali bado vinywani mwao,

3178:31 Isa 10:16hasira ya Mungu ikawaka juu yao,

akawaua wale waliokuwa na nguvu zaidi miongoni mwao,

akiwaangusha vijana wa Israeli.

3278:32 Za 78:11, 17, 22Licha ya haya yote, waliendelea kutenda dhambi,

licha ya maajabu yake, hawakuamini.

3378:33 Hes 14:29, 35Kwa hiyo akamaliza siku zao katika ubatili

na miaka yao katika vitisho.

3478:34 Kum 4:29; Hos 5:15; Hes 5:15Kila mara Mungu alipowaua baadhi yao,

waliosalia walimtafuta,

walimgeukia tena kwa shauku.

3578:35 Mwa 49:24; Kum 9:26Walikumbuka kwamba Mungu alikuwa Mwamba wao,

kwamba Mungu Aliye Juu Sana alikuwa Mkombozi wao.

3678:36 Eze 33:31Lakini walimdanganya kwa vinywa vyao,

wakisema uongo kwa ndimi zao,

3778:37 Za 78:8; Mdo 8:21mioyo yao haikuwa thabiti kwake,

wala hawakuwa waaminifu katika agano lake.

3878:38 Kut 34:6; Neh 9:17; Za 25:11; 85:2; 86:15; 1Fal 21:29; Isa 1:25; 27:9; 48:9, 10; 30:18; Mik 7:18; Rum 2:4; Dan 11:35Hata hivyo alikuwa na huruma,

alisamehe maovu yao

na hakuwaangamiza.

Mara kwa mara alizuia hasira yake,

wala hakuchochea ghadhabu yake yote.

3978:39 Mwa 6:3; Isa 29:5; Ay 7:7; Yak 4:14; Yn 3:6Alikumbuka kwamba wao walikuwa nyama tu,

upepo upitao ambao haurudi.

4078:40 Kut 23:21; Za 95:8; 106:14; Efe 4:30Mara ngapi walimwasi jangwani

na kumhuzunisha nyikani!

4178:41 Kut 17:2; 2Fal 19:22; Za 71:22; 89:18Walimjaribu Mungu mara kwa mara,

wakamkasirisha yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli.

4278:42 Amu 3:7; Neh 9:17; Za 27:11Hawakukumbuka uwezo wake,

siku aliyowakomboa kutoka kwa mtesi,

4378:43 Kut 10:1; 3:20siku aliyoonyesha ishara zake za ajabu huko Misri,

maajabu yake huko Soani.

4478:44 Kut 7:20, 21; Za 105:29; 78:45Aligeuza mito yao kuwa damu,

hawakuweza kunywa maji kutoka vijito vyao.

4578:45 Kut 8:2, 6, 24; Za 105Aliwapelekea makundi ya mainzi yakawala,

na vyura wakawaharibu.

4678:46 Nah 3:15; Kut 10:13Aliruhusu tunutu kuharibu mimea yao,

mazao yao kwa nzige.

4778:47 Za 105:32; 147:17; Kut 9:23Aliharibu mizabibu yao kwa mvua ya mawe

na mikuyu yao kwa mvua iliyochangamana na theluji.

4878:48 Kut 9:25Aliwaachia mifugo yao mvua ya mawe,

akayapiga makundi ya wanyama wao kwa radi.

4978:49 Kut 15:7; Mwa 19:13; 1Kor 10:10; Rum 2:8Aliwafungulia hasira yake kali,

ghadhabu yake, hasira na uadui,

na kundi la malaika wa kuharibu.

50Aliitengenezea njia hasira yake,

hakuwaepusha na kifo,

bali aliwaachia tauni.

5178:51 Mwa 9:12; Kut 12:12; Za 135:8; 105:23; 106:22Aliwapiga wazaliwa wote wa kwanza wa Misri,

matunda ya kwanza ya ujana katika mahema ya Hamu.

5278:52 Ay 21:11; Za 28:9; 77:20Lakini aliwatoa watu wake kama kundi,

akawaongoza kama kondoo kupitia jangwani.

5378:53 Kut 14:28; 15:7; Za 106:10Aliwaongoza salama, wala hawakuogopa,

bali bahari iliwameza adui zao.

5478:54 Kut 15:17; Za 44:3Hivyo akawaleta hadi kwenye mpaka wa nchi yake takatifu,

hadi nchi ya vilima ambayo mkono wake wa kuume ulikuwa umeitwaa.

5578:55 Za 44:2; Kum 1:38; Yos 13:7; Mdo 13:19Aliyafukuza mataifa mbele yao,

na kuwagawia nchi zao kama urithi,

aliwakalisha makabila ya Israeli katika makao yao.

56Lakini wao walimjaribu Mungu,

na kuasi dhidi ya Yeye Aliye Juu Sana,

wala hawakuzishika sheria zake.

5778:57 2Nya 30:7; Za 78:9; Eze 20:27; Hos 7:16Kama baba zao, hawakuwa thabiti wala waaminifu,

wakawa wasioweza kutegemewa

kama upinde wenye kasoro.

5878:58 Amu 2:12; Law 26:30; Kut 20:4; Kum 12:2; 5:8; 32:21; Hes 33:51Wakamkasirisha Mungu kwa mahali pao pa juu pa kuabudia miungu,

wakachochea wivu wake kwa sanamu zao.

5978:59 Za 55:19; Law 26:28; Hes 32:14; Kum 32:19; Ebr 4:13Wakati Mungu alipowasikia, alikasirika sana,

akamkataa Israeli kabisa.

6078:60 Yos 18:1; Eze 8:6; 1Sam 4:11; Yer 7:12Akaiacha hema ya Shilo,

hema aliyokuwa ameiweka katikati ya wanadamu.

6178:61 Amu 18:30; 1Sam 4:12; Za 132:8; 1Sam 4:17Akalipeleka Sanduku la nguvu zake utumwani,

utukufu wake mikononi mwa adui.

6278:62 Kum 28:25; 1Sam 10:1Aliachia watu wake wauawe kwa upanga,

akaukasirikia sana urithi wake.

6378:63 1Fal 4:32; Yer 7:32; 16:9; 25:10; Hes 11:1Moto uliwaangamiza vijana wao,

na wanawali wao hawakuimbiwa nyimbo za arusi,

6478:64 Ay 27:15; 1Sam 4:17makuhani wao waliuawa kwa upanga,

wala wajane wao hawakuweza kulia.

6578:65 Za 44:23; Isa 42:13Ndipo Bwana alipoamka kama vile kuamka usingizini,

kama vile mtu aamkavyo kutoka kwenye bumbuazi la mvinyo.

6678:66 1Sam 5:6Aliwapiga na kuwashinda adui zake,

akawatia katika aibu ya milele.

6778:67 Yer 7:15; Hos 9:13; 12:1Ndipo alipozikataa hema za Yosefu,

hakulichagua kabila la Efraimu,

6878:68 Hes 1:7; Kut 15:17; Za 68:16; 108:8lakini alilichagua kabila la Yuda,

Mlima Sayuni, ambao aliupenda.

6978:69 Za 15:1; 1Fal 6:1Alijenga patakatifu pake kama vilele,

kama dunia ambayo aliimarisha milele.

7078:70 1Sam 16:1Akamchagua Daudi mtumishi wake

na kumtoa kwenye mazizi ya kondoo.

7178:71 Mwa 37:2; Za 28:9; 2Sam 5:2; 1Nya 11:2; Mik 5:2-4; Zek 11:4Kutoka kuchunga kondoo alimleta

kuwa mchungaji wa watu wake Yakobo,

wa Israeli urithi wake.

7278:72 1Fal 9:4; Mwa 17:1Naye Daudi aliwachunga kwa uadilifu wa moyo,

kwa mikono ya ustadi aliwaongoza.

King James Version

Psalms 78:1-72

Maschil of Asaph.

1Give ear, O my people, to my law: incline your ears to the words of my mouth.78.1 Maschil…: or, A Psalm for Asaph to give instruction

2I will open my mouth in a parable: I will utter dark sayings of old:

3Which we have heard and known, and our fathers have told us.

4We will not hide them from their children, shewing to the generation to come the praises of the LORD, and his strength, and his wonderful works that he hath done.

5For he established a testimony in Jacob, and appointed a law in Israel, which he commanded our fathers, that they should make them known to their children:

6That the generation to come might know them, even the children which should be born; who should arise and declare them to their children:

7That they might set their hope in God, and not forget the works of God, but keep his commandments:

8And might not be as their fathers, a stubborn and rebellious generation; a generation that set not their heart aright, and whose spirit was not stedfast with God.78.8 that…: Heb. that prepared not their heart

9The children of Ephraim, being armed, and carrying bows, turned back in the day of battle.78.9 carrying: Heb. throwing forth

10They kept not the covenant of God, and refused to walk in his law;

11And forgat his works, and his wonders that he had shewed them.

12Marvellous things did he in the sight of their fathers, in the land of Egypt, in the field of Zoan.

13He divided the sea, and caused them to pass through; and he made the waters to stand as an heap.

14In the daytime also he led them with a cloud, and all the night with a light of fire.

15He clave the rocks in the wilderness, and gave them drink as out of the great depths.

16He brought streams also out of the rock, and caused waters to run down like rivers.

17And they sinned yet more against him by provoking the most High in the wilderness.

18And they tempted God in their heart by asking meat for their lust.

19Yea, they spake against God; they said, Can God furnish a table in the wilderness?78.19 furnish: Heb. order

20Behold, he smote the rock, that the waters gushed out, and the streams overflowed; can he give bread also? can he provide flesh for his people?

21Therefore the LORD heard this, and was wroth: so a fire was kindled against Jacob, and anger also came up against Israel;

22Because they believed not in God, and trusted not in his salvation:

23Though he had commanded the clouds from above, and opened the doors of heaven,

24And had rained down manna upon them to eat, and had given them of the corn of heaven.

25Man did eat angels’ food: he sent them meat to the full.78.25 Man…: or, Every one did eat the bread of the mighty

26He caused an east wind to blow in the heaven: and by his power he brought in the south wind.78.26 to blow: Heb. to go

27He rained flesh also upon them as dust, and feathered fowls like as the sand of the sea:78.27 feathered…: Heb. fowl of wing

28And he let it fall in the midst of their camp, round about their habitations.

29So they did eat, and were well filled: for he gave them their own desire;

30They were not estranged from their lust. But while their meat was yet in their mouths,

31The wrath of God came upon them, and slew the fattest of them, and smote down the chosen men of Israel.78.31 smote…: Heb. made to bow78.31 chosen…: or, young men

32For all this they sinned still, and believed not for his wondrous works.

33Therefore their days did he consume in vanity, and their years in trouble.

34When he slew them, then they sought him: and they returned and enquired early after God.

35And they remembered that God was their rock, and the high God their redeemer.

36Nevertheless they did flatter him with their mouth, and they lied unto him with their tongues.

37For their heart was not right with him, neither were they stedfast in his covenant.

38But he, being full of compassion, forgave their iniquity, and destroyed them not: yea, many a time turned he his anger away, and did not stir up all his wrath.

39For he remembered that they were but flesh; a wind that passeth away, and cometh not again.

40How oft did they provoke him in the wilderness, and grieve him in the desert!78.40 provoke: or, rebel against

41Yea, they turned back and tempted God, and limited the Holy One of Israel.

42They remembered not his hand, nor the day when he delivered them from the enemy.78.42 from…: or, from affliction

43How he had wrought his signs in Egypt, and his wonders in the field of Zoan:78.43 wrought: Heb. set

44And had turned their rivers into blood; and their floods, that they could not drink.

45He sent divers sorts of flies among them, which devoured them; and frogs, which destroyed them.

46He gave also their increase unto the caterpiller, and their labour unto the locust.

47He destroyed their vines with hail, and their sycomore trees with frost.78.47 destroyed: Heb. killed78.47 frost: or, great hailstones

48He gave up their cattle also to the hail, and their flocks to hot thunderbolts.78.48 gave…: Heb. shut up78.48 hot…: or, lightnings

49He cast upon them the fierceness of his anger, wrath, and indignation, and trouble, by sending evil angels among them.

50He made a way to his anger; he spared not their soul from death, but gave their life over to the pestilence;78.50 He made…: Heb. He weighed a path78.50 life…: or, beasts to the murrain

51And smote all the firstborn in Egypt; the chief of their strength in the tabernacles of Ham:

52But made his own people to go forth like sheep, and guided them in the wilderness like a flock.

53And he led them on safely, so that they feared not: but the sea overwhelmed their enemies.78.53 overwhelmed: Heb. covered

54And he brought them to the border of his sanctuary, even to this mountain, which his right hand had purchased.

55He cast out the heathen also before them, and divided them an inheritance by line, and made the tribes of Israel to dwell in their tents.

56Yet they tempted and provoked the most high God, and kept not his testimonies:

57But turned back, and dealt unfaithfully like their fathers: they were turned aside like a deceitful bow.

58For they provoked him to anger with their high places, and moved him to jealousy with their graven images.

59When God heard this, he was wroth, and greatly abhorred Israel:

60So that he forsook the tabernacle of Shiloh, the tent which he placed among men;

61And delivered his strength into captivity, and his glory into the enemy’s hand.

62He gave his people over also unto the sword; and was wroth with his inheritance.

63The fire consumed their young men; and their maidens were not given to marriage.78.63 given…: Heb. praised

64Their priests fell by the sword; and their widows made no lamentation.

65Then the Lord awaked as one out of sleep, and like a mighty man that shouteth by reason of wine.

66And he smote his enemies in the hinder parts: he put them to a perpetual reproach.

67Moreover he refused the tabernacle of Joseph, and chose not the tribe of Ephraim:

68But chose the tribe of Judah, the mount Zion which he loved.

69And he built his sanctuary like high palaces, like the earth which he hath established for ever.78.69 established: Heb. founded

70He chose David also his servant, and took him from the sheepfolds:

71From following the ewes great with young he brought him to feed Jacob his people, and Israel his inheritance.78.71 following: Heb. after

72So he fed them according to the integrity of his heart; and guided them by the skilfulness of his hands.