Zaburi 36
Uovu Wa Mwanadamu
Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi mtumishi wa Bwana.
136:1 Ay 21:16; 23:15; Yer 2:19; 36:16, 24; Rum 3:18; Mit 8:13; Mwa 20:11; Mhu 12:3Kuna neno moyoni mwangu
kuhusu hali ya dhambi ya mwovu.
Hakuna hofu ya Mungu
mbele ya macho yake.
236:2 Kum 29:19Kwa kuwa machoni pake mwenyewe hujisifu mno
hata hawezi kugundua au kuichukia dhambi yake.
336:3 Yer 4:22; 13:23; Za 10:7; 5:6, 9; 43:1; 144:8, 11; 94:8; Ay 5:13; Isa 44:20; Amo 3:10Maneno ya kinywa chake ni maovu na ya udanganyifu,
ameacha kuwa mwenye hekima na kutenda mema.
436:4 Mik 2:1; Rum 12:9; Isa 65:2; Za 52:3Hata kitandani mwake hupanga hila mbaya,
hujitia katika njia ya dhambi
na hakatai lililo baya.
536:5 Za 89:1; 119:90; 108:4; 57:10; 89:2; 71:19; 103:11Upendo wako, Ee Bwana, unafika hadi mbinguni,
uaminifu wako hadi kwenye anga.
636:6 Za 5:8; 68:15; Mwa 1:2; Za 104:14; 7:11; 145:9; Neh 9:6; Rum 11:33; Ay 7:20; 11:8Haki yako ni kama milima mikubwa,
hukumu zako ni kama kilindi kikuu.
Ee Bwana, wewe huwahifadhi
mwanadamu na mnyama.
736:7 Za 6:4; 17:8; 57:1; 91:4; Rut 2:12Upendo wako usiokoma
ni wa thamani mno!
Watu wakuu na wadogo
hujificha uvulini wa mbawa zako.
836:8 Za 65:4; 23:2; 63:5; Yer 31:12, 14; Ufu 22:1; Isa 25:6; Ay 20:17Wanajifurahisha katika wingi nyumbani mwako,
nawe utawanywesha katika mto wa furaha zako.
936:9 Isa 12:3; 2:5; 9:2; 60:1, 19; Yer 2:13; Zek 13:1; Yn 1:4; 4:10, 14; Ufu 21:6; Mdo 26:18; Efe 5:8; Kol 1:13; 1Pet 2:9; Mit 10:11; 16:22; Za 87:7; 4:6; 27:1; 76:4; 104:2Kuwa pamoja nawe ni kijito cha uzima,
katika nuru yako twaona nuru.
1036:10 Yer 31:3; 9:24; 22:16; Za 7:10; 11:2; 94:15; 125:4Dumisha upendo wako kwa wale wanaokujua wewe,
haki yako kwa wale walio wanyofu wa moyo.
1136:11 Za 71:4; 140:4Mguu wa mwenye kiburi usije dhidi yangu,
wala mkono wa mwovu usinifukuze.
1236:12 Za 18:38Angalia jinsi watenda mabaya walivyoanguka:
wametupwa chini, hawawezi kuinuka!
Salmo 36
Al director musical. De David, el siervo del Señor.
1Dice el pecador:
«Ser impío lo llevo en el corazón».36:1 Dice el … corazón» (lectura probable); Oráculo del pecado al malvado en medio de mi corazón (TM).
No hay temor de Dios
delante de sus ojos.
2Cree que merece alabanzas
y no halla aborrecible su pecado.
3Sus palabras son inicuas y engañosas;
ha perdido el buen juicio
y la capacidad de hacer el bien.
4Aun en su lecho trama hacer el mal;
se aferra a su mal camino
y persiste en la maldad.
5Tu amor, Señor, llega hasta los cielos;
tu fidelidad alcanza las nubes.
6Tu justicia es como las altas montañas;36:6 las altas montañas. Alt. las montañas de Dios.
tus juicios, como el gran océano.
Tú, Señor, cuidas de hombres y animales;
7¡cuán precioso, oh Dios, es tu gran amor!
Todo ser humano halla refugio
a la sombra de tus alas.
8Se sacian de la abundancia de tu casa;
les das a beber de tu río de deleites.
9Porque en ti está la fuente de la vida,
y en tu luz podemos ver la luz.
10Extiende tu amor a los que te conocen,
y tu justicia a los rectos de corazón.
11Que no me aplaste el pie del orgulloso,
ni me desarraigue la mano del impío.
12Ved cómo fracasan los malvados:
¡caen a tierra, y ya no pueden levantarse!