Zaburi 139 – NEN & JCB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Zaburi 139:1-24

Zaburi 139

Mungu Asiyeweza Kukwepwa

Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi.

1139:1 Za 17:3; 44:21; Rum 8:27Ee Bwana, umenichunguza

na kunijua.

2139:2 2Fal 19:27; Za 94:11; Mit 24:12; Yer 12:3Unajua ninapoketi na ninapoinuka;

unatambua mawazo yangu tokea mbali.

3139:3 2Fal 19:27; Ay 31:4Unafahamu kutoka kwangu na kulala kwangu;

unaelewa njia zangu zote.

4139:4 Ebr 4:13Kabla neno halijafika katika ulimi wangu,

wewe walijua kikamilifu, Ee Bwana.

5139:5 1Sam 25:16; Za 32:10; 34:7; 125:2Umenizunguka nyuma na mbele;

umeweka mkono wako juu yangu.

6139:6 Za 131:1; Rum 11:33Maarifa haya ni ya ajabu mno kwangu,

ni ya juu sana kwangu kuyafikia.

7139:7 Yer 23:24Niende wapi nijiepushe na Roho yako?

Niende wapi niukimbie uso wako?

8139:8 Kum 30:12-15; Amo 9:2-3; Ay 17:13Kama nikienda juu mbinguni, wewe uko huko;

nikifanya vilindi139:8 Vilindi ina maana ya Kuzimu, ambayo ni Sheol kwa Kiebrania. kuwa kitanda changu,

wewe uko huko.

9Kama nikipanda juu ya mbawa za mapambazuko,

kama nikikaa pande za mbali za bahari,

10139:10 Za 23:3; 108:6; Isa 41:10hata huko mkono wako utaniongoza,

mkono wako wa kuume utanishika kwa uthabiti.

11Kama nikisema, “Hakika giza litanificha

na nuru inayonizunguka iwe usiku,”

12139:12 Ay 34:22; Dan 2:22hata giza halitakuwa giza kwako,

usiku utangʼaa kama mchana,

kwa kuwa giza ni kama nuru kwako.

13139:13 Za 119:73; Ay 10:11; Isa 44:2, 24; 46:3; 49:5; Yer 1:5Kwa maana wewe ndiwe uliyeumba utu wangu wa ndani;

uliniunga pamoja tumboni mwa mama yangu.

14Ninakusifu kwa sababu nimeumbwa

kwa namna ya ajabu na ya kutisha;

kazi zako ni za ajabu,

ninajua hayo kikamilifu.

15139:15 Mhu 11:5; Ay 10:11; Za 63:9Umbile langu halikufichika kwako,

nilipoumbwa mahali pa siri.

Nilipoungwa pamoja kwa ustadi katika vilindi vya nchi,

16139:16 Ay 33:29; Za 90:12macho yako yaliniona kabla mwili wangu haujakamilika.

Siku zangu zote ulizonipangia

ziliandikwa katika kitabu chako

kabla haijakuwepo hata moja.

17139:17 Za 92:5; Ay 5:9Tazama jinsi yalivyo ya thamani mawazo yako kwangu, Ee Mungu!

Jinsi jumla yake ilivyo kubwa!

18139:18 Za 40:5; 3:5; Ay 29:18Kama ningezihesabu,

zingekuwa nyingi kuliko mchanga.

Niamkapo,

bado niko pamoja nawe.

19139:19 Za 5:6; 6:8; 59:2; Isa 11:4Laiti ungewachinja waovu, Ee Mungu!

Ondokeni kwangu, ninyi wamwaga damu!

20139:20 Za 65:7; Kum 5:11; Ay 21:14-15; Yud 15Wanazungumza juu yako wakiwa na kusudi baya,

adui zako wanatumia vibaya jina lako.

21139:21 2Nya 19:2; Za 31:6; 26:5; 119:113Ee Bwana, je, nisiwachukie wanaokuchukia?

Nisiwachukie sana wanaoinuka dhidi yako?

22139:22 Mt 5:43Sina kitu zaidi ya chuki dhidi yao,

ninawahesabu ni adui zangu.

23139:23 Ay 31:6; 1Sam 16:7; 1Nya 29:17; Za 7:9; Mit 17:3; Yer 11:20; Ufu 2:23Ee Mungu, nichunguze, uujue moyo wangu,

nijaribu na ujue mawazo yangu.

24139:24 Yer 25:5; 36:3; Za 5:8; 23:2; 143:10Uone kama kuna njia iletayo machukizo ndani yangu,

uniongoze katika njia ya milele.

Japanese Contemporary Bible

詩篇 139:1-24

139

1主よ。あなたは私の心の奥底まで探り、

どんなささいなことも見のがされません。

2私の立つのも座るのも、すべてご存じです。

遠くからでも、私の心をすべて読み取られます。

3あなたは、私の進む道もご存じで、

どこで休息をとるべきかも教えてくださいます。

どんなときも、私の居場所もご存じです。

4そして、口を開く前から、

私が何を言いたいかも見抜いておられます。

5あなたは私の前を行き、後ろからも来られます。

あなたは私に、祝福の御手を置いてくださいます。

6このようなことはあまりにも栄光にあふれ、

すばらしい話なので、

ほんとうだとは信じがたいほどです。

7あなたの視界から逃れることは決してできません。

身を隠すことも不可能です。

8天まで昇ろうと、あなたはそこにおられ、

死者の世界まで降りて行っても、

あなたはそこで待っておられるのです。

9朝風に乗って、地の果てまで飛んで行っても、

10あなたの力強い腕は、私を導き、支えてくださいます。

11私が暗闇にまぎれ込もうとしても、

夜は私を照らし出す光となるのです。

12暗闇も、神から隠れることはできません。

神から見れば、暗闇も光も同じようなものなのです。

13神は、精巧に私の体のすべての器官を造り、

母の胎内で組み立ててくださいました。

14こんなにも複雑かつ緻密に

仕上げてくださったことを感謝します。

想像することもできないくらい、すばらしいことです。

あなたのわざは驚くべきもので、

私にはとうてい、理解することはできません。

15だれも立ち入ることのできない場所で

私が組み立てられた時、あなたはそこにおられました。

16生まれる前から、まだ呼吸を始める前から、

あなたの目は私に注がれ、

私の生涯にわたるご計画も、

練り上げられていたのです。

17-18主よ。

あなたが私をかた時も忘れずにいてくださることは、

ほんとうにたいせつな事実です。

あなたは一日に、数えきれないほど何度も、

私のことを思い起こしてくださいます。

眠っているときも、朝までずっと、

私のことを考えていてくださるのです。

19悪者どもは必ず、主の御手にかかって滅びます。

血に飢えた者どもよ、すみやかに消え失せるがよい。

20彼らはあなたの御名を汚し、横柄な態度をとっています。

なんと愚かなことでしょう。

21主よ。あなたを憎む者どもを、

この私が憎まずにいられましょうか。

心を痛めずにいられましょうか。

22私は彼らを憎みます。

あなたの敵は私の敵だからです。

23ああ神よ。

私の心を探り、内面を調べ上げてください。

24あなたを悲しませるようなものがあるなら、

教えてください。

私が永遠のいのちへの道からそれないように

お導きください。