Zaburi 112 – NEN & JCB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Zaburi 112:1-10

Zaburi 112112 Zaburi hii imetungwa kila mstari ukianzia na herufi ya alfabeti ya Kiebrania zikifuatana tangu Aleph (A) hadi Taw (T); zote ni 22.

Baraka Za Mwenye Haki

1112:1 Za 33:2; 103:1; 150:1; 1:1, 2; Ay 1:8; Za 103:11; 115:13; 128:1; 1:2; 119:14, 16, 47, 92Msifuni Bwana.

Heri mtu yule amchaye Bwana,

mtu yule apendezwaye sana na amri zake.

2112:2 Za 25:13; 37:26; 128:2-4Watoto wake watakuwa wenye uwezo katika nchi,

kizazi cha watu waadilifu kitabarikiwa.

3112:3 Kum 8:18; Za 37:6; 111:3Nyumbani mwake kuna mali na utajiri,

haki yake hudumu milele.

4112:4 Za 18:28; 5:12Hata gizani nuru humzukia mtu mwadilifu,

yule mwenye rehema, huruma na haki.

5112:5 Za 37:21, 26; Lk 6:35Mema yatamjia mtu yule aliye mkarimu na mwenye kukopesha bila riba,

anayefanya mambo yake kwa haki.

6112:6 Za 15:5; 55:22; Mit 10:7; Mhu 2:16Hakika hatatikisika kamwe,

mtu mwenye haki atakumbukwa milele.

7112:7 Za 57:7; 108:1; 28:7; 56:3-4; Isa 12:2Hataogopa habari mbaya,

moyo wake ni thabiti, ukimtegemea Bwana.

8112:8 Za 3:6; 27:1; 54:7; 56:11; Mit 1:33; Isa 12:2Moyo wake ni salama, hatakuwa na hofu,

mwishoni ataona ushindi dhidi ya adui zake.

9112:9 Lk 19:8; Mdo 9:36; 2Kor 9:9; Za 111:3; 75:10Ametawanya vipawa vyake kwa ukarimu akawapa maskini;

haki yake hudumu milele;

pembe yake itatukuzwa kwa heshima.

10112:10 Za 86:17; 34:21; 37:12; Mt 8:12; Ay 8:13Mtu mwovu ataona na kuchukizwa,

atasaga meno yake na kutoweka,

kutamani kwa mtu mwovu kutaishia patupu.

Japanese Contemporary Bible

詩篇 112:1-10

112

1ハレルヤ。

主を信じて従う人は、

言い表せないほどの祝福を受けます。

心から、神のことばのとおりにする人は幸せです。

2正しい人は、子どもたちにまで祝福が受け継がれます。

その子らは至る所で尊敬を集めます。

3正しい人は資産にも恵まれ、

善行をたたえられるでしょう。

4たとえ、暗闇の力に巻き込まれたとしても、

すぐに輝くばかりの光に照らされるでしょう。

主はあわれみ深く、親切です。

5公平な取り引きをする人には、万事がうまく運びます。

6このような人は、事態が思わしくなくなっても、

動じたりしません。

周囲の人々は、

神が彼をいつも目にかけておられるのを見て、

深い感銘を受けるのです。

7彼は悪い知らせを受けても恐れず、

今度は何が起こるかと、不安になることもありません。

主に見放されるわけがないと、

信じきっているからです。

8それゆえ、何事も恐れず、

冷静に敵の顔を見つめることができるのです。

9彼は物惜しみしたりせず、

貧しい人に気前よく与えます。

その善行は、いつまでも忘れられず、

人々の尊敬を集めます。

10これを見たひねくれ者は、怒りに震えますが、

歯ぎしりしながら、逃げ出すしかありません。

望みが消え去ったからです。