Zaburi 109 – NEN & NIV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Zaburi 109:1-31

Zaburi 109

Lalamiko La Mtu Aliyeko Kwenye Shida

Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi.

1109:1 Kut 15:2; Yer 17:14; Ay 34:29; Za 83:1Ee Mungu, ambaye ninakusifu,

usiwe kimya,

2109:2 Za 43:1; 52:4kwa maana watu waovu na wadanganyifu

wamefungua vinywa vyao dhidi yangu;

wasema dhidi yangu

kwa ndimi za udanganyifu.

3109:3 Za 69:4; 35:7; 35:7, 10; Yn 15:25; 1Sam 19:4, 5Wamenizunguka kwa maneno ya chuki,

wananishambulia bila sababu.

4109:4 Za 69:13; 141:5Wanachonilipa badala ya urafiki wangu ni kunishtaki,

lakini mimi ninawaombea.

5109:5 Mwa 44:4; Za 38:20Wananilipiza mabaya kwa mema,

chuki badala ya urafiki wangu.

6109:6 1Nya 21:1; Ay 1:6; Zek 3:1Agiza mtu mwovu ampinge,

mshtaki109:6 Mshtaki hapa maana yake ni Shetani. asimame mkono wake wa kuume.

7109:7 Za 1:5; Mit 28:9; Zek 3:1Anapohukumiwa, apatikane na hatia,

nayo maombi yake yamhukumu.

8109:8 Ay 15:32; Mdo 1:20Siku zake za kuishi na ziwe chache,

nafasi yake ya uongozi ichukuliwe na mtu mwingine.

9109:9 Kut 22:24; Yer 18:21Watoto wake na waachwe yatima,

mke wake na awe mjane.

10109:10 Mwa 4:12Watoto wake na watangetange wakiomba,

na wafukuzwe kwenye magofu ya nyumba zao.

11109:11 Hes 14:3; Isa 1:7; 6:11; 36:1; Mao 5:2; Neh 5:3; Ay 20:18; 18:9Mtu anayemdai na ateke vyote alivyo navyo,

matunda ya kazi yake yatekwe nyara na wageni.

12109:12 Ay 5:4Asiwepo mtu yeyote wa kumtendea mema

wala wa kuwahurumia yatima wake.

13109:13 Za 21:10; 9:5; 37:28; Hes 14:12; Mit 10:7; Ay 18:19Uzao wake na ukatiliwe mbali,

majina yao yafutike katika kizazi kifuatacho.

14109:14 Kut 20:5Maovu ya baba zake na yakumbukwe

mbele za Bwana,

dhambi ya mama yake

isifutwe kamwe.

15109:15 Za 90:8; Kut 17:14; Kum 32:26; Ay 18:17Dhambi zao na zibaki daima mbele za Bwana,

ili apate kukatilia mbali kumbukumbu lao duniani.

16109:16 Ay 20:19; Za 35:10; 34:18Kwa maana kamwe hakuweza kutenda wema,

bali alimfukuza mnyonge na mhitaji,

aliwafanyia jeuri wahitaji na waliovunjika moyo.

17109:17 Mit 28:27; Mt 7:2Alipenda kulaani,

nayo laana ikampata;

hakupenda kubariki,

kwa hiyo baraka na ikae mbali naye.

18109:18 Za 10:7; Hes 5:22Alivaa kulaani kama vazi lake,

nayo laana ikamwingia mwilini mwake kama maji,

kwenye mifupa yake kama mafuta.

19109:19 Za 109:29; 73:6; Eze 7:27Na iwe kama joho alilozungushiwa,

kama mshipi aliofungiwa daima.

20109:20 Kut 32:34; Za 54:5; 94:23; 7:10; Isa 3:11; 2Tim 4:14Haya na yawe malipo ya Bwana kwa washtaki wangu,

kwa wale wanaoninenea mabaya.

21109:21 Kut 9:16; Za 3:7; 23:3; 69:16Lakini wewe, Ee Bwana Mwenyezi,

unitendee wema kwa ajili ya jina lako,

uniokoe kwa wema wa pendo lako.

22Maana mimi ni maskini na mhitaji,

moyo wangu umejeruhiwa ndani yangu.

23109:23 Ay 14:2Ninafifia kama kivuli cha jioni,

nimerushwa-rushwa kama nzige.

24109:24 Ebr 12:12; Ay 16:8; Za 35:13Magoti yangu yamelegea kwa kufunga,

mwili wangu umedhoofika na kukonda.

25109:25 Za 22:6; Ay 16:4; Mt 27:39; Mk 15:29; Isa 37:22Nimekuwa kitu cha kudharauliwa kwa washtaki wangu,

wanionapo, hutikisa vichwa vyao.

26109:26 Za 12:1; 119:86Ee Bwana, Mungu wangu nisaidie,

niokoe sawasawa na upendo wako.

27109:27 Ay 37:7Watu na wafahamu kuwa ni mkono wako,

kwamba wewe, Ee Bwana, umetenda hili.

28109:28 2Sam 16:12; Za 66:4; Isa 35:10; 51:11; 54:1; 65:14; Hes 22:12Wanaweza kulaani, lakini wewe utabariki,

watakaposhambulia wataaibishwa,

lakini mtumishi wako atashangilia.

29109:29 Za 35:26Washtaki wangu watavikwa fedheha,

na kufunikwa na aibu kama joho.

30109:30 Za 35:18Kwa kinywa changu nitamtukuza sana Bwana,

katika umati mkubwa nitamsifu.

31109:31 Za 16:8; 108:6Kwa maana husimama mkono wa kuume wa mhitaji,

kuokoa maisha yake kutoka kwa wale wanaomhukumu.

New International Version

Psalms 109:1-31

Psalm 109

For the director of music. Of David. A psalm.

1My God, whom I praise,

do not remain silent,

2for people who are wicked and deceitful

have opened their mouths against me;

they have spoken against me with lying tongues.

3With words of hatred they surround me;

they attack me without cause.

4In return for my friendship they accuse me,

but I am a man of prayer.

5They repay me evil for good,

and hatred for my friendship.

6Appoint someone evil to oppose my enemy;

let an accuser stand at his right hand.

7When he is tried, let him be found guilty,

and may his prayers condemn him.

8May his days be few;

may another take his place of leadership.

9May his children be fatherless

and his wife a widow.

10May his children be wandering beggars;

may they be driven109:10 Septuagint; Hebrew sought from their ruined homes.

11May a creditor seize all he has;

may strangers plunder the fruits of his labor.

12May no one extend kindness to him

or take pity on his fatherless children.

13May his descendants be cut off,

their names blotted out from the next generation.

14May the iniquity of his fathers be remembered before the Lord;

may the sin of his mother never be blotted out.

15May their sins always remain before the Lord,

that he may blot out their name from the earth.

16For he never thought of doing a kindness,

but hounded to death the poor

and the needy and the brokenhearted.

17He loved to pronounce a curse—

may it come back on him.

He found no pleasure in blessing—

may it be far from him.

18He wore cursing as his garment;

it entered into his body like water,

into his bones like oil.

19May it be like a cloak wrapped about him,

like a belt tied forever around him.

20May this be the Lord’s payment to my accusers,

to those who speak evil of me.

21But you, Sovereign Lord,

help me for your name’s sake;

out of the goodness of your love, deliver me.

22For I am poor and needy,

and my heart is wounded within me.

23I fade away like an evening shadow;

I am shaken off like a locust.

24My knees give way from fasting;

my body is thin and gaunt.

25I am an object of scorn to my accusers;

when they see me, they shake their heads.

26Help me, Lord my God;

save me according to your unfailing love.

27Let them know that it is your hand,

that you, Lord, have done it.

28While they curse, may you bless;

may those who attack me be put to shame,

but may your servant rejoice.

29May my accusers be clothed with disgrace

and wrapped in shame as in a cloak.

30With my mouth I will greatly extol the Lord;

in the great throng of worshipers I will praise him.

31For he stands at the right hand of the needy,

to save their lives from those who would condemn them.