Zaburi 109 – NEN & HOF

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Zaburi 109:1-31

Zaburi 109

Lalamiko La Mtu Aliyeko Kwenye Shida

Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi.

1109:1 Kut 15:2; Yer 17:14; Ay 34:29; Za 83:1Ee Mungu, ambaye ninakusifu,

usiwe kimya,

2109:2 Za 43:1; 52:4kwa maana watu waovu na wadanganyifu

wamefungua vinywa vyao dhidi yangu;

wasema dhidi yangu

kwa ndimi za udanganyifu.

3109:3 Za 69:4; 35:7; 35:7, 10; Yn 15:25; 1Sam 19:4, 5Wamenizunguka kwa maneno ya chuki,

wananishambulia bila sababu.

4109:4 Za 69:13; 141:5Wanachonilipa badala ya urafiki wangu ni kunishtaki,

lakini mimi ninawaombea.

5109:5 Mwa 44:4; Za 38:20Wananilipiza mabaya kwa mema,

chuki badala ya urafiki wangu.

6109:6 1Nya 21:1; Ay 1:6; Zek 3:1Agiza mtu mwovu ampinge,

mshtaki109:6 Mshtaki hapa maana yake ni Shetani. asimame mkono wake wa kuume.

7109:7 Za 1:5; Mit 28:9; Zek 3:1Anapohukumiwa, apatikane na hatia,

nayo maombi yake yamhukumu.

8109:8 Ay 15:32; Mdo 1:20Siku zake za kuishi na ziwe chache,

nafasi yake ya uongozi ichukuliwe na mtu mwingine.

9109:9 Kut 22:24; Yer 18:21Watoto wake na waachwe yatima,

mke wake na awe mjane.

10109:10 Mwa 4:12Watoto wake na watangetange wakiomba,

na wafukuzwe kwenye magofu ya nyumba zao.

11109:11 Hes 14:3; Isa 1:7; 6:11; 36:1; Mao 5:2; Neh 5:3; Ay 20:18; 18:9Mtu anayemdai na ateke vyote alivyo navyo,

matunda ya kazi yake yatekwe nyara na wageni.

12109:12 Ay 5:4Asiwepo mtu yeyote wa kumtendea mema

wala wa kuwahurumia yatima wake.

13109:13 Za 21:10; 9:5; 37:28; Hes 14:12; Mit 10:7; Ay 18:19Uzao wake na ukatiliwe mbali,

majina yao yafutike katika kizazi kifuatacho.

14109:14 Kut 20:5Maovu ya baba zake na yakumbukwe

mbele za Bwana,

dhambi ya mama yake

isifutwe kamwe.

15109:15 Za 90:8; Kut 17:14; Kum 32:26; Ay 18:17Dhambi zao na zibaki daima mbele za Bwana,

ili apate kukatilia mbali kumbukumbu lao duniani.

16109:16 Ay 20:19; Za 35:10; 34:18Kwa maana kamwe hakuweza kutenda wema,

bali alimfukuza mnyonge na mhitaji,

aliwafanyia jeuri wahitaji na waliovunjika moyo.

17109:17 Mit 28:27; Mt 7:2Alipenda kulaani,

nayo laana ikampata;

hakupenda kubariki,

kwa hiyo baraka na ikae mbali naye.

18109:18 Za 10:7; Hes 5:22Alivaa kulaani kama vazi lake,

nayo laana ikamwingia mwilini mwake kama maji,

kwenye mifupa yake kama mafuta.

19109:19 Za 109:29; 73:6; Eze 7:27Na iwe kama joho alilozungushiwa,

kama mshipi aliofungiwa daima.

20109:20 Kut 32:34; Za 54:5; 94:23; 7:10; Isa 3:11; 2Tim 4:14Haya na yawe malipo ya Bwana kwa washtaki wangu,

kwa wale wanaoninenea mabaya.

21109:21 Kut 9:16; Za 3:7; 23:3; 69:16Lakini wewe, Ee Bwana Mwenyezi,

unitendee wema kwa ajili ya jina lako,

uniokoe kwa wema wa pendo lako.

22Maana mimi ni maskini na mhitaji,

moyo wangu umejeruhiwa ndani yangu.

23109:23 Ay 14:2Ninafifia kama kivuli cha jioni,

nimerushwa-rushwa kama nzige.

24109:24 Ebr 12:12; Ay 16:8; Za 35:13Magoti yangu yamelegea kwa kufunga,

mwili wangu umedhoofika na kukonda.

25109:25 Za 22:6; Ay 16:4; Mt 27:39; Mk 15:29; Isa 37:22Nimekuwa kitu cha kudharauliwa kwa washtaki wangu,

wanionapo, hutikisa vichwa vyao.

26109:26 Za 12:1; 119:86Ee Bwana, Mungu wangu nisaidie,

niokoe sawasawa na upendo wako.

27109:27 Ay 37:7Watu na wafahamu kuwa ni mkono wako,

kwamba wewe, Ee Bwana, umetenda hili.

28109:28 2Sam 16:12; Za 66:4; Isa 35:10; 51:11; 54:1; 65:14; Hes 22:12Wanaweza kulaani, lakini wewe utabariki,

watakaposhambulia wataaibishwa,

lakini mtumishi wako atashangilia.

29109:29 Za 35:26Washtaki wangu watavikwa fedheha,

na kufunikwa na aibu kama joho.

30109:30 Za 35:18Kwa kinywa changu nitamtukuza sana Bwana,

katika umati mkubwa nitamsifu.

31109:31 Za 16:8; 108:6Kwa maana husimama mkono wa kuume wa mhitaji,

kuokoa maisha yake kutoka kwa wale wanaomhukumu.

Hoffnung für Alle

Psalm 109:1-31

Herr, bestrafe meine Feinde!

1Ein Lied von David.

Mein Gott, ich lobe dich! Bitte schweige doch nicht!

2Rücksichtslos gehen gottlose Menschen gegen mich vor,

sie reißen ihren Mund auf und verleumden mich.

3Sie bedrängen mich mit hasserfüllten Worten

und bekämpfen mich ohne jeden Grund.

4Meine Freundschaft beantworten sie mit Feindschaft,

ich aber bete weiter zu dir.

5Mit Bosheit zahlen sie mir heim, was ich ihnen Gutes tue;

meiner Liebe setzen sie nur Hass entgegen.

6O Herr, lass einen Ankläger gegen meinen Feind auftreten,

der so ungerecht und gewissenlos ist wie er selbst.

Schicke doch jemanden, der mit ihm ins Gericht geht!109,6 Möglicherweise zitiert der Beter in den Versen 6‒19 die Verwünschungen seiner Gegner. Dann müsste der Abschnitt eingeleitet werden mit: »Sie sagen: Ein Ankläger soll gegen ihn auftreten.«

7Wenn das Urteil gefällt wird, soll er schuldig gesprochen werden.

Selbst sein Gebet rechne ihm als Sünde an!

8Er soll nicht mehr lange leben,

und seine Stellung soll ein anderer bekommen.

9Seine Kinder sollen zu Waisen werden,

und seine Frau soll als Witwe zurückbleiben.

10Ruhelos sollen seine Kinder umherirren und betteln,

ihr Elternhaus lass zu einer Ruine verfallen.

11Seine Gläubiger mögen seinen Besitz an sich reißen,

und Fremde sollen rauben, was er sich erworben hat.

12Niemand soll sein Andenken in Ehren halten

und mit seinen verwaisten Kindern Mitleid haben.

13Seine Nachkommen sollen ausgerottet werden,

schon in der nächsten Generation möge ihr Name erlöschen.

14Der Herr soll niemals das Unrecht vergessen,

das die Vorfahren meines Feindes begingen,

und auch die Schuld seiner Mutter soll nicht vergeben werden!

15Die Sünden aller seiner Vorfahren

sollen dem Herrn stets vor Augen stehen,

doch an sie selbst soll niemand mehr denken!

16Denn dieser Mensch dachte nicht daran, anderen Gutes zu tun.

Die Armen und Hilflosen verfolgte er,

und die Niedergeschlagenen trieb er in den Tod.

17Er liebte es, andere zu verfluchen –

nun soll der Fluch ihn selbst treffen!

Er hasste es, andere zu segnen –

darum bleibe der Segen von ihm fern!

18Das Fluchen wurde ihm zur Gewohnheit,

er hüllte sich darin ein wie in einen Mantel.

Aber nun wird sein Fluch gegen ihn selbst wirksam:

Er dringt in ihn ein wie Wasser, das man trinkt,

und wie Öl, mit dem man sich einreibt.

19Er soll ihn bedecken wie ein Gewand

und ihn für immer einschnüren wie ein enger Gürtel!

20Ja, Herr, damit strafe alle meine Feinde,

alle, die mich so gehässig verleumden!

21Herr, mein Gott, tritt für mich ein, es geht doch um deine Ehre!

Rette mich, denn auf deine Gnade ist Verlass!

22Ich bin niedergeschlagen und hilflos,

im tiefsten Herzen verletzt.

23Mein Leben gleicht einem Schatten am Abend,

der bald in der Dunkelheit verschwindet.

Ich bin wie eine Heuschrecke, die man vom Arm abschüttelt.

24Vom vielen Fasten zittern mir die Knie,

ich bin nur noch Haut und Knochen.

25Für meine Feinde bin ich zum Gespött geworden;

wenn sie mich sehen, schütteln sie den Kopf.

26Hilf mir, Herr, und rette mich,

denn du bist doch ein gnädiger Gott!

27Herr, lass meine Feinde erkennen,

dass du es bist, der alles so gefügt hat!

28Mögen sie mich auch verwünschen – du wirst mich segnen!

Sollen sie doch angreifen – sie werden dabei scheitern!

Zuletzt werde ich, dein Diener, mich freuen.

29Schimpf und Schande sollen über meine Ankläger kommen,

sie sollen sie einhüllen wie ein Mantel!

30Immer wieder will ich dem Herrn danken,

in aller Öffentlichkeit will ich ihn loben.

31Er steht dem Wehrlosen zur Seite

und rettet ihn vor denen, die seinen Tod fordern.