Zaburi 108 – NEN & HTB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Zaburi 108:1-13

Zaburi 108

Kuomba Msaada Dhidi Ya Adui

(Zaburi 57:7-11; 60:5-12)

Wimbo. Zaburi ya Daudi.

1108:1 Za 112:7; 119:30, 112; 18:49Ee Mungu, moyo wangu ni thabiti;

nitaimba na kusifu kwa moyo wangu wote.

2108:2 Ay 21:12Amka, kinubi na zeze!

Nitayaamsha mapambazuko.

3Nitakusifu wewe, Ee Bwana, katikati ya mataifa;

nitaimba habari zako, katikati ya jamaa za watu.

4108:4 Hes 14:18; Kum 7:9; Kut 34:6; Za 36:5; Mik 7:18-20Kwa maana upendo wako ni mkuu, ni juu kuliko mbingu;

uaminifu wako unazifikia anga.

5108:5 Za 8:1; 57:5Ee Mungu, utukuzwe juu ya mbingu,

utukufu wako na uenee duniani kote.

6108:6 Ay 40:14Tuokoe na utusaidie kwa mkono wako wa kuume,

ili wale uwapendao wapate kuokolewa.

7108:7 Za 89:35; 68:35; 102:19; Mwa 12:6; 33:17Mungu amenena kutoka patakatifu pake:

“Nitaigawa Shekemu kwa ushindi

na kulipima Bonde la Sukothi.

8108:8 Za 78:68; Mwa 49:10Gileadi ni yangu, Manase ni yangu,

Efraimu ni kofia yangu ya chuma,

nayo Yuda ni fimbo yangu ya utawala.

9108:9 Mwa 19:37; 2Sam 8:1, 13-14Moabu ni sinia langu la kunawia,

juu ya Edomu natupa kiatu changu;

nashangilia kwa kushindwa kwa Ufilisti.”

10108:10 Za 60:9Ni nani atakayenipeleka hadi mji wenye ngome?

Ni nani atakayeniongoza hadi nifike Edomu?

11108:11 Za 44:9Ee Mungu, si ni wewe uliyetukataa sisi,

na hutoki tena na majeshi yetu?

12108:12 Isa 10:3; 30:3, 5; 31:3; Yer 2:36; 17:7; Za 118:8; 146:3Tuletee msaada dhidi ya adui,

kwa maana msaada wa mwanadamu haufai kitu.

13108:13 Za 44:5; Isa 22:5; 63:3, 6; 25:10; Mao 1:15; Mal 4:3; Ufu 14:9Kwa msaada wa Mungu tutapata ushindi,

naye atawaponda adui zetu.

Het Boek

Psalmen 108:1-14

1Een psalm van David.

2Ik voel mij veilig en rustig bij U, mijn God!

Ik verlang ernaar voor U lofliederen te zingen.

3Vooruit, harp en citer!

Nog voor de zon opkomt, wil ik al spelen.

4In tegenwoordigheid van alle volken, Here,

wil ik U prijzen en eren.

Voor vreemde volken wil ik psalmen over U zingen.

5Uw goedheid en liefde zijn onmetelijk,

zij gaan hoger dan het blauw van de hemel.

Uw trouw is net zo min op te meten

als de afstand tot de wolken.

6Maak Uzelf maar groot

tot in alle hemelen, mijn God.

Uw macht en majesteit

zullen over de hele wereld worden gezien.

7Wilt U ons antwoorden?

Wilt U ons de overwinning bezorgen,

zodat uw volgelingen worden bevrijd?

8God heeft in zijn heilige woning gesproken

en ik juich over zijn antwoord.

Ik zal Sichem verdelen

en het dal van Sukkot opmeten.

9Gilead en Manasse zijn van mij

en Efraïm is mijn helm.

Juda is de staf waarmee ik regeer.

10Moab is mijn wasbak,

Edom vertrap ik met mijn sandalen

en over Filistea triomfeer ik.

11Wie brengt mij naar de versterkte vesting?

Wie begeleidt mij naar Edom?

12U bent het, o God,

U die ons eerst had verstoten.

Wilt U, o God, optrekken met onze legers?

13Help ons tegen de vijand,

want hulp van mensen stelt niets voor.

14Met de hulp van God

kunnen wij dapper strijden,

Hij zal onze vijanden verslaan.